Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 187

Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi ASP Geofrey Lutufye.

Mhe. Lissu: Mnajifanya mapolisi mnawasingizia watu vitu vya bure haya itakushangaza hao mliowakamata baada ya kesi yao kuisha ni mashahidi wa kesi hii?

ASP Geofrey Lutufye : Hainishangazi.

Mhe. Lissu: haikushangazi kwasababu huo ndio utaratibu wenu mapolisi wa Tanzania.

Mhe. Lissu: Au unabisha nikufungulie ripoti ya Jaji Mkuu Othman Chande amesema mnawafungulia watu makosa ya uongo.

Sasa nikuulize swali lingine, umewahi kuona video mimi nikiwa nazungumza habari za huo uchaguzi mkuu?

ASP Geofrey Lutufye : amekaa kimya

Mhe. Lissu: Unajua kwanini nimeshitakiwa kwa Uhaini ASP geofrey lutufye? Unajua sababu.

ASP Geofrey Lutufye : Sababu ya ile kauli uliyotoa.

Mhe. Lissu: Ipi hiyo?

ASP Geofrey Lutufye : Ulisema utazuia uchaguzi wa mwaka 2025.

Mhe. Lissu: Ndio nakuuliza uliiona hiyo video?

ASP Geofrey Lutufye : Sikumbuki.

Mhe. Lissu: Hawa ndio kesho watakuwa ma RPC siku inayofuata utashangaa anakuwa IGP,

Sina maswali mengine Waheshimiwa majaji.

Watu wanasonya tu hapa.

Anasimama Wakili wa Serikali Renatus Mkude kwa ajili ya Re-examination

Maelezo yako uliandika kama nani?

ASP Geofrey Lutufye : Kama shahidi.

Wakili: Unalizungumziaje kuhusu kujiandika mwenyewe?

ASP Geofrey Lutufye : naweza kujiandika mwenyewe au kuandikwa.

Renatus Mkude: Sina swali lingine. Re Examination imeishia hapo.

Jaji anamruhusu Shahidi.

Shahidi anatoka akiwa ameshika kipaza sauti.

Jaji Ndunguru: Unasahau maji yako hapo.

Shahidi: Hapana siyataki tena.

Jaji: Basi turudishie hiyo MIC tafadhali.

Anairudisha na kutoka nje akiwa anatikisa kichwa.

Watu wanacheka.😂😂😂

Kesi inaahirishwa watu wakale.

Tutaendelea baada ya lisaa limoja.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
Sasa shahidi kama huyu hata maji hataki tena na kakimbia na kipaza😆😆😆Jamaa aliona hela yake ngumu kwa kweli. Si lazima kazi ngumu ihusishe kazi za nguvu au mwili tu ila hata akili kuna kazi ni ngumu sana..Mfano ni kuwa shahidi wa hii kesi ya Lisu. Unakaririshwa maelezo hafu unakutana na maswali hukukaririshwa majibu ndo unaondoka na kipaza sauti au unajibu hujui kitu hujaandika kwenye maelezo😅😅Let it be!!
 
#Pichani

Huyu aliyeshika 🎤 ndo Shahidi wetu wa leo Coplo Vicent yeye kasema hajui PGO wala sheria yoyote ambayo imeandikwa kwa lugha ya Kingereza.

Anasema yeye ni mpelelezi, anakamata watu kwa amri ya Polisi tu hata kama hajui wamekosa nini.😂😂😂View attachment 3546383
Anadhalilisha wenye vitambi mbinuko na kaunda suti😅
 
Huyu shahidi p9 ana jeuri sana lakini hakumbuki alichoandika kwenye maelezo anajichanganya kumbe ndo wale wanaoandikiwa maelezo kituoni yaani kituko tupu kwanza nyie mmewahi kuona samsung 8 pro? 😂😂😂 nachoka sana

#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 210

Anaendelea Mhe. Lissu na Cross Examination.

Mhe. Lissu: Waheshimiwa Majaji naomba shahidi apewe kielelezo D13

Mhe Lissu: Jana kwenye ushahidi wako uliulizwa unaishi wapi na ukasema unaishi katika Halmashauri ya Mbeya, kweli si kweli?

Shahidi wa kificho P9 : Kweli.

Mhe. Lissu: Naomba uangalie maelezo yako, nenda palipo andikwa makazi usome pameandikwa makazi yako wapi?

Shahidi wa kificho P9: Pameandiwa Mwakibete.

Mhe. Lissu: Kwenye mstari wa kwanza kabisa sema palivoandikwa hapo? Kwamba unaishi?

Shahidi wa kificho P9 : Pameandikwa Mwakibete lakin nilihojiwa Mbeya.

Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama unafahamu kwamba haya maeneo huwa yanatangazwa kwenye gazeti la serikali na waziri wa TAMISEMI

Shahidi wa kificho P9 : sifahamu

Mhe. Lissu: Umeonyesha gazeti la Serikali linaloonyesha Mwakibete ni Mbeya,?

Shahidi wa kificho P9; Hapana.

Mhe. Lissu: unafikri unaandika andika tu unaingizwa chaka na mapolisi na wewe unaandika tu.

Mhe. Lissu: Uliulizwa unafanya shughuli gani na ulisema unafanya kazi ya fundi umeme na kazi zako unafanya katika Halmashauri ya Mbeya, kweli si kweli?

Shahidi wa kificho P9 : Kweli

Mhe. Lissu: Angalia maelezo yako unafanya kazi gani?

Shahidi wa kificho P9 : Mkulima

Mhe. Lissu: Kazi ni mkulima hapa unajifanya fundi umeme, lugha gongana.

Watu wanacheka: 😂😂😂😂

Mhe. Lissu: nyie Waha wa kigoma wajanja sana nyie na mimi napenda watu wajanja kama wewe.

Mhe. Lissu: Uliulizwa unakumbuka kitu gani kilikukuta 2024, ukasema nilivutiwa na sera za CHADEMA na nikawanafatilia matangazo, mikutano n.k haya sasa soma maelezo yako mjanja wa Jiji la Mbeya…😁

Mhe. Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji hayo maelezo uliyosoma hapo kama yapo na ulivyosema jana

Shahidi wa kificho P9 : Hayapo

Mhe. Lissu : Uliandika kwa mapolisi wakakupuuza wakaandika ya kwao.

Mhe. Lissu: Katika matukio mengi uliyofatilia ulitaja matembezi ya yaliyoongozwa na Lissu yalianzia Uyole, na Heche Isanga, mwambie jaji kama Mhe. Heche yupo katika maelezo kayo

Shahidi wa kificho P9: Nilieleza ni Mnyika sio Heche.

Mhe. Lissu: Jana ulisema Heche alianzia Isanga, unataka niwasumbue majaji wakusomee ulichokisema??

Shahidi wa kificho P9: inawezekana nilikosea

Mhe. Lissu: Kazi yangu ni kukamata watu waongo kama wewe.

Shahidi wa kificho P9 : Hiyo unasema ww

Mhe. Lissu: ndio nasema.

Mhe. Lissu: Ulisema mnamo tarehe 3 April 2025 ukiwa nyumbani kwako wakati unaperuzi mitandao kupitia simu yako aina ya Samsung 8 pro, kweli au si kweli?

Shahidi wa kificho P9 : kweli

Mhe. Lissu: Angalia maelezo yako waeleze majaji kama kuna mahala popote ulikua unaangalia mitandao kupitia aina ya Samsung 8 pro.

Shahidi wa kificho P9: hayajaandikwa.

Mhe. Lissu: Asante, mmeuzwa na mapolisi.

Mhe. Lissu: Ulisema kwamba uliingia kwenye mtandao wa instagram na ili uweze kuimgia instagram lazima uwe na simu janja, account na bundle, hayo maneno yapo au hayapo.

Shahidi wa kificho P9 : hayapo.

Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako jana ulisema wakati unaingia kwenye instagram uliona video ya Tundu lissu na ukasema huo mtandao umeusahau.

Shahidi wa kificho P9 : Ndio nimeusahau.

Mhe. Lissu: Kama umesahau inamaana, kwenye maelezo yako utakua umeandika.

Shahidi wa kificho P9: Sasa wewe unaniuliza mambo waliyoniuliza mawakili.

Mhe. Lissu: Jibu swali langu. Unanifundisha namna ya kukuhoji?

Shahidi wa kificho P9 : Ndio hakuna

Mhe. Lissu: Uliulizwa muonekano wa Tundu Lissu, ukasema alikua ukumbini alivaa kombati za kaki za chadema na tshirt nyeusi na bendera ya taifa na rangi za CHADEMA, kweli si kwei?

Shahidi wa kificho P9 : Kweli

Mhe. Lissu: Sasa waeleze waheshimiwa majaji kama yapo katika maelezo yako.

Shahidi wa kificho P9 : Hakuna

Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako jana uliulizwa alisema atauzuiaje ukasema tutafanya vurugu na kuuvuruga uchaguzi huo.

Shahidi wa kificho P9: Kweli

Part 211 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
1771604389919.jpg
 
Wana JF kuna mahali tulipitiwa na kujisahau.. Tulipaswa kuwa na mada maalum ya Tundu Antipas Lissu.

Mwanasheria nguli, mwanaharakati wa haki za binadamu na sasa mfungwa wa kisiasa wa kesi ya uhaini na mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani Tanganyika

Ana historia yake maalum .. Ana mengi mazuri ya kiwango kaifanyia Tanganyika.. TUMUENZI SASA. NI WAKATI WAKEView attachment 3381742
(7,029) Historia fupi ya maisha ya shule ya Tundu Lissu | JamiiForums Historia fupi ya maisha ya shule ya Tundu Lissu
Namsikiliza Lissu akiwa mahakamani navyoona akijisimamia dhidi ya Jopo kubwa la Mawakili wa Serikali na bado anaonekana amewa Outsmart.

Lissu ni kiumbe ktk Viumbe Adimu
 
Huyu shahidi p9 ana jeuri sana lakini hakumbuki alichoandika kwenye maelezo anajichanganya kumbe ndo wale wanaoandikiwa maelezo kituoni yaani kituko tupu kwanza nyie mmewahi kuona samsung 8 pro? 😂😂😂 nachoka sana

#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 210

Anaendelea Mhe. Lissu na Cross Examination.

Mhe. Lissu: Waheshimiwa Majaji naomba shahidi apewe kielelezo D13

Mhe Lissu: Jana kwenye ushahidi wako uliulizwa unaishi wapi na ukasema unaishi katika Halmashauri ya Mbeya, kweli si kweli?

Shahidi wa kificho P9 : Kweli.

Mhe. Lissu: Naomba uangalie maelezo yako, nenda palipo andikwa makazi usome pameandikwa makazi yako wapi?

Shahidi wa kificho P9: Pameandiwa Mwakibete.

Mhe. Lissu: Kwenye mstari wa kwanza kabisa sema palivoandikwa hapo? Kwamba unaishi?

Shahidi wa kificho P9 : Pameandikwa Mwakibete lakin nilihojiwa Mbeya.

Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama unafahamu kwamba haya maeneo huwa yanatangazwa kwenye gazeti la serikali na waziri wa TAMISEMI

Shahidi wa kificho P9 : sifahamu

Mhe. Lissu: Umeonyesha gazeti la Serikali linaloonyesha Mwakibete ni Mbeya,?

Shahidi wa kificho P9; Hapana.

Mhe. Lissu: unafikri unaandika andika tu unaingizwa chaka na mapolisi na wewe unaandika tu.

Mhe. Lissu: Uliulizwa unafanya shughuli gani na ulisema unafanya kazi ya fundi umeme na kazi zako unafanya katika Halmashauri ya Mbeya, kweli si kweli?

Shahidi wa kificho P9 : Kweli

Mhe. Lissu: Angalia maelezo yako unafanya kazi gani?

Shahidi wa kificho P9 : Mkulima

Mhe. Lissu: Kazi ni mkulima hapa unajifanya fundi umeme, lugha gongana.

Watu wanacheka: 😂😂😂😂

Mhe. Lissu: nyie Waha wa kigoma wajanja sana nyie na mimi napenda watu wajanja kama wewe.

Mhe. Lissu: Uliulizwa unakumbuka kitu gani kilikukuta 2024, ukasema nilivutiwa na sera za CHADEMA na nikawanafatilia matangazo, mikutano n.k haya sasa soma maelezo yako mjanja wa Jiji la Mbeya…😁

Mhe. Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji hayo maelezo uliyosoma hapo kama yapo na ulivyosema jana

Shahidi wa kificho P9 : Hayapo

Mhe. Lissu : Uliandika kwa mapolisi wakakupuuza wakaandika ya kwao.

Mhe. Lissu: Katika matukio mengi uliyofatilia ulitaja matembezi ya yaliyoongozwa na Lissu yalianzia Uyole, na Heche Isanga, mwambie jaji kama Mhe. Heche yupo katika maelezo kayo

Shahidi wa kificho P9: Nilieleza ni Mnyika sio Heche.

Mhe. Lissu: Jana ulisema Heche alianzia Isanga, unataka niwasumbue majaji wakusomee ulichokisema??

Shahidi wa kificho P9: inawezekana nilikosea

Mhe. Lissu: Kazi yangu ni kukamata watu waongo kama wewe.

Shahidi wa kificho P9 : Hiyo unasema ww

Mhe. Lissu: ndio nasema.

Mhe. Lissu: Ulisema mnamo tarehe 3 April 2025 ukiwa nyumbani kwako wakati unaperuzi mitandao kupitia simu yako aina ya Samsung 8 pro, kweli au si kweli?

Shahidi wa kificho P9 : kweli

Mhe. Lissu: Angalia maelezo yako waeleze majaji kama kuna mahala popote ulikua unaangalia mitandao kupitia aina ya Samsung 8 pro.

Shahidi wa kificho P9: hayajaandikwa.

Mhe. Lissu: Asante, mmeuzwa na mapolisi.

Mhe. Lissu: Ulisema kwamba uliingia kwenye mtandao wa instagram na ili uweze kuimgia instagram lazima uwe na simu janja, account na bundle, hayo maneno yapo au hayapo.

Shahidi wa kificho P9 : hayapo.

Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako jana ulisema wakati unaingia kwenye instagram uliona video ya Tundu lissu na ukasema huo mtandao umeusahau.

Shahidi wa kificho P9 : Ndio nimeusahau.

Mhe. Lissu: Kama umesahau inamaana, kwenye maelezo yako utakua umeandika.

Shahidi wa kificho P9: Sasa wewe unaniuliza mambo waliyoniuliza mawakili.

Mhe. Lissu: Jibu swali langu. Unanifundisha namna ya kukuhoji?

Shahidi wa kificho P9 : Ndio hakuna

Mhe. Lissu: Uliulizwa muonekano wa Tundu Lissu, ukasema alikua ukumbini alivaa kombati za kaki za chadema na tshirt nyeusi na bendera ya taifa na rangi za CHADEMA, kweli si kwei?

Shahidi wa kificho P9 : Kweli

Mhe. Lissu: Sasa waeleze waheshimiwa majaji kama yapo katika maelezo yako.

Shahidi wa kificho P9 : Hakuna

Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako jana uliulizwa alisema atauzuiaje ukasema tutafanya vurugu na kuuvuruga uchaguzi huo.

Shahidi wa kificho P9: Kweli

Part 211 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.View attachment 3546641
Shahidi P11 aliivyoenda kumkamata Shahidi P9 harafu akasema amemaliza Ushahidi, Majaji wakashangaa ndio ushahidi gani sasa huu😆😆😆
 
Mhe. Lissu: Uliulizwa unafanya shughuli gani na ulisema unafanya kazi ya fundi umeme na kazi zako unafanya katika Halmashauri ya Mbeya, kweli si kweli?

Shahidi wa kificho P9 : Kweli

Mhe. Lissu: Angalia maelezo yako unafanya kazi gani?

Shahidi wa kificho P9 : Mkulima

Mhe. Lissu: Kazi ni mkulima hapa unajifanya fundi umeme, lugha gongana.
Hawakufanyuwa rehersal ya kutosha
 
Kuendelea kumshikilia Tundu Lissu kunazidisha dhuluma na kuathiri zaidi hadhi ya Tanzania, ndani na kimataifa.

Matukio ya Oktoba 29 yaliashiria mojawapo ya sura mbaya zaidi katika historia ya taifa. Kutoweka kwa nguvu, mmomonyoko wa nafasi za kiraia, na kuzorota kwa uhuru wa kimsingi kumeharibu sana sifa ya Tanzania. Ukweli usemwe- ukweli huu umevuta hisia za kimataifa na kuharibu taswira ya nchi ambayo hapo awali ilichukuliwa kama taifa la amani.

Sifa na amani ya Tanzania haitarejeshwa kwa ukimya au ukandamizaji. Watarejeshwa kupitia ukweli, uwajibikaji, na haki.
1771914919190.jpg
 
Ngoma Nzito! UN imezitaka mamlaka za Tanzania:
1. Kumwachia huru Mheshimiwa Lissu mara moja bila masharti
2. Kumlipa fidia na stahiki kwa kifungo kisicho halali
3. Kuchukua hatua za kurekebisha mifumo ya kisheria inayoruhusu kukiukwa
kwa haki za msingi.

CHADEMA
1771923438142.jpg
 
#UPDATES_KUTOKA_MAHAKAMA_KUU

Muda huu ni saa sita nayo dakika 17 kesi ya mchongo ya uhaini dhidi ya Mhe. Lissu bado haijaanza na Mawakili wa Serikali hawaonekani.

Tetesi kutoka kwa msiri wetu zinasema wanapigiwa simu hawapokei na wengine wamezima simu.

Mawakili wa Serikali wamechimba. Majaji na Mahakama imeachwa solemba, haya mambo yanashangaza kabisa.

Jamhuri kama hii kesi imewashinda waiondoe au wakae na Lissu Gerezani bila kesi kuendelea tujue moja maana hapo awali leo Walisema wanahitaji lisaa limoja kutafakari muda huu yamefika masaa mawili. Hawaonekani na hawajulikani walipo.

Unaambiwa hakuna anayefanikiwa kuwapata Mawakili wa Serikali na hawajulikani wameenda wapi?

Sijui ndio kufuata maagizo kutoka juu.😂😂😂😂

Haya ni maajabu na ni mambo yanayoshangaza sana.
IMG-20260224-WA0009.jpg
 
IMG-20260224-WA0010.jpg

JAMBO LA KUSHANGAZA MAHAKAMANI.

Muda huu wameingia wasaidizi na walinzi wa Majaji wamechukua Computer na vifaa vya Mahakama wameondoka navyo.

Inaonekana muda huu kesi haiwezi kuendelea maana wanaondoa kila kitu Mahakamani.

Taarifa tuliyonayo Mawakili wa Serikali hawajaonekana na hawajarudi Mahakamani so muda huu Karani amesimama hapa na kusema kuwa kuna jambo limejitokeza anaenda kutafuta ufafanuzi kwa Msajili wa Mahakama atarudi kuleta mrejesho.

Kwahiyo tupo njiapanda hatujui kinachoendelea hadi sasa.

Kesi imewashinda wanalazimisha ni aibu kwa Mahakama kuiamuru Jamhuri kuwa ilete Mashahidi baada ya lisaa limoja kwasasa ni masaa mawili yanaelekea matatu hakuna kinachoendelea.

Mawakili wa Serikali wanaamua kesi iendelee au isiendelee.

Vituko, Vichekesho na Maajabu.

Tunaendelea tuone mwisho wa hizi drama zao.

Wako Muhabarishaji,
Hilda Newton.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 224

Majaji wameingia muda huu saa nane Kamili Mchana.

Wanaandika pale juu.

Mheshimiwa Lissu ameingia na kuteta jambo na Dr. Nshala tunamsikia anasema waende kokote watakapotaka kwenda tutakutana nao huko. Sasa sijui ni wapi anamaanisha.

Anasimama Renatus Mkude Wakili wa Serikali kwa niaba ya jopo la Mawakili wa Serikali tunaomba radhi kwani tulifikiri tungetumia lisaa limoja.

Mchana huu nipo na Ajuaye, Thawabu Issa na Cathbert Mbiringe. Kwa wote tunawakilisha jamhuri na Mshitakiwa yupo.

Shauri lilipangwa kuendelea na mashahidi. Lakini tumetafakari na tunaitafsiri kwa mujibu wa kifungu cha 6 cha Appellate Jurisdiction Act na kanuni ya 65(1) ya kanuni za Mahakama ya Rufani.

Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) anatoa taarifa ya kuwasilisha taarifa ya mapitio (revision)

Hapa kwanza anakosea Mapitio ni Review alipaswa kusema Marejeo ndio Revision sijui kasoma wapi nae huyu jamaa.😂😂😂

Anaendelea hapa Renatus Mkude, kuwa Notice of motion hiyo imeambatanishwa na kiapo cha Cathbert Mbiringe Wakili wa Serikali ambayo taarifa hii ya kutoa notice kwenda Mahakama ya Rufani imesainiwa leo Tar. 24/02/2026.

Na kupokelewa kwa mifumo ya kielektroniki inayotambulika na Mahakama na kusajili kama. CRIMINAL REVISION NO. 7203216/2026 imepokelewa na Mahakama ya Rufani Tanzania hapa Dar es salaam.

Ambalo chimbuko lake ni Criminal Sessions No. 19605/2025 ambayo iko mbele yenu Waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu. (Ndunguru, Karyemaha, Kiwonde)

Kwa kuwa shahidi wetu aliyekuwa anafuata ACP Mahamba tuliyemuombea notice additional substamce of evidence na ikakataliwa.

Ni Rai yetu kwamba kwa kuwa shauri hili limeshapokelewa Mahakama ya Rufani haiwezi kusimama ili kuweza kutoa nafasi kwa shauri husika huko Mahakama ya Rufani kuweza kuamuliwa.

Ni hayo tu kwa sasa.

Tunamsubiri Mh. Lissu atajibu nini?

Mhe. Lissu anaanza.

Baada ya kuzikiliza wasilisho la upande wa Mashitaka nina haya ya kusema.

1. Kwa vile mimi nipo gerezani na wanajua nataka wanipatie hiyo nakala ya Notice of Motion waliyofile niweze kuiona.

2. Ninafahamu na ninatumaini na wao wanajua kwamba kwa mujibu wa kifungu cha 8(2)(d) cha Sheria ya Mamlaka ya Rufaa ambacho wamekitaja (Appellate Jurisdiction Act) wanafahamu kwamba hakiruhusu rufaa wala mapitio wala marejeo ya maamuzi ya Mahakama ambayo hayamalizi shauri la msingi. (Interlocutory decisions) sina shaka na wao wanalifahamu hilo.

3. Waheshimiwa Majaji siwaombi mtoe uamuzi wowote kuhusu hili ninalolisema.

Nataka iwe kwenye record kwamba nafahamu na naamini upande wa mashitaka wanafahamu lengo la kupeleka ombi la marejeo Mahakama ya rufani na wanafahamu hairuhusiwi ni kurefusha mashauri haya ili niendelee kukaa Gerezani. Ni hilo tu.

Kwamba tupeleke Mahakama ya Rufani ili huyu mbaya wao ambae ni mimi aendelee kukaa Gerezani.

Kwa vile wananipeleka kwe ye Mahakama ya Rufani nataka niwaeleze kuwa nitawafuata huko huko naenda kuwashughulikia huko huko.

Kama ambavyo kesi yao is dead on arrival najua hata hii revision yao pia imeshakufa.

Tutarudi hapa yakiisha huko ya Mahakama ya rufani tutarejea hapa na nitawashughulikia tukirudi.

Jambo la Mwisho Mawakili wangu wametaka kunipa nyaraka hapa lakini siwezi kupewa hadi nyie mseme.

Sijui wanaogopa nini watu wa magereza nisipewe huo uamuzi hapo ni makaratasi tu.

Naambiwa ni hukumu kutoka huko Umoja Wa Mataifa lakini Magereza wanaogopa nisipewe.

Tena ni uamuzi unaohusiana na mimi kuwepo Gerezani. Tatizo liko wapi?

Jaji anasema uko wapi? Umepelekwa wameuona wamesema wape Mawakili wa Serikali.

Wako wanasoma hapa Mawakili wa Serikali huo uamuzi.

Anasimama Renatus Mkude anasema mimi ni member wa working group za UN Human Rights Council.

Jaji: Tumesema apewe au asipewe?

Renatus Mkude: Apewe tu.

Part 225 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba Repost yako.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 225

Mhe. Lissu anaendelea hapa.

Kama mtakumbuka nilisema ninavyoishi Ukonga, siruhusiwi kuonana na Mawakili wangu in private.

Mnaruhusiwa kutembelea Magereza naomba mliangalie na hili kama itawapendeza inawapa Mamlaka ya kutoa mapendekezo na mamlaka za Magereza kurekebisha masuala yanayohusu wafungwa kama haya niliyosema.

Ni muhimu kwamba kuwasiliana na washauri wangu wa kisheria ilindwe kama sheria inavyosema bila kusikilizwa na maafisa wa Magereza.

Ni hayo tu Waheshimiwa

Mhe. Tundu Lissu amemaliza na amekaa sasa.

Majaji wanaandika hapa.

Anasimama Renatus Mkude kuwa tutampatia hizi nyaraka ndani ya siku 14 tutampatia.

Hili la masuala ya utawala wa mambo ya magereza kwa mujibu wa kifungu cha 16 cha National Prosecution Act na sisi ofisi ya DPP tutatembelea ili kuhakisha kunakuwa na fair trial.

Wameombwa Majaji anasema DPP ataenda eti huko Magereza kuangalia haki za Mtuhumiwa. Uongo uongo uongo. Hawana hata aibu hawa jamaa.

Majaji wanaandika baada ya kusikia
 
‼️🚨TUNDU LISSU AMEVUNJIWA HAKI ZAKE LUKUKI NA SERIKALI IMEKIUKA MAKUNDI 4 KATI YA 5 YA UMINYWAJIBWA HAKI KWA MUJIBU WA UMOJA WA MATAIFA‼️
Maamuzi ya Kikosi Kazi cha @UmojaWaMataifa imeeleza wazi kuwa:
Tundu Antiphas Mughwai Lissu kunyimwa uhuru wake ni kinyume na vifungu vya 2, 3, 7, 9, 10, 11, 19, 20 na 21 vya Azimio la Haki za Binadamu la Ulimwengu na vifungu vya 2, 9, 14, 19, 21, 22, 25 na 26 vya mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa, ni kinyume cha sheria ya kimataifa na hivyo ukiukwaji huu umefikia viwango kuwekwa ndani ya makundi ya I, II, III na V ya makosa ya mataifa
Sasa haya makundi au viwango yaani Category ni yapi? Nimeyatafsiri ili wapumbavu waliopo ndani ya mfumo waelewe UZITO wa maamuzi haya!
Maelezo ya Category
Category I (kiwango/kundi ) - hii ni wakati ni wazi haiwezekani kuwepo na kutumika msingi wowote wa kisheria unaohalalisha mhusika kunyimwa uhuru (kama vile mtu anapowekwa kizuizini baada ya kukamilika kwa kifungo chake au licha ya sheria ya msamaha inayomhusu)
Category II -inatokea wakati kunyimwa uhuru kunatokana na kuminywa kwa haki au uhuru unaohakikishwa na vifungu vya 7, 13, 14, 18, 19, 20 na 21 vya Azimio la Haki za Binadamu la Ulimwengu na, kwa kadiri Mataifa Wanachama yanavyohusika, na vifungu vya 12, 18, 19, 21, 22, 25, 26 na 27 vya Mkataba kuhusu haki za kisiasa na kiraia ;
Category III - hutokea pale ambapo serikali haifuati kwa jumla au kwa sehemu kanuni za kimataifa zinazohusiana na haki ya kesi ya haki, ilivyoainishwa katika Azimio la Haki za Binadamu la Ulimwengu na katika vyombo husika vya kimataifa vinavyokubaliwa na Mataifa husika, ni jambo la uzito kiasi cha kupelekea kunyimwa uhuru kuwa jambo la kiholela.
Category V - pale ambapo kunyimwa uhuru kunamaanisha ukiukaji wa sheria za kimataifa kwa misingi ya ubaguzi, kulingana na kuzaliwa, asili ya kitaifa, kikabila au kijamii, lugha, dini, hali ya kiuchumi, maoni ya kisiasa au mengine, jinsia, mwelekeo wa kijinsia, ulemavu au hali nyingine yoyote, ambayo inalenga au inaweza kusababisha kupuuza usawa wa wanadamu.
@judiciarytanzania mjipange #FreeTunduLissu
1771958412115.jpg
1771958412115.jpg
 
Back
Top Bottom