Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

TAARIFA KUTOKA GEREZA LA UKONGA KWA MHE. LISSU

Ni kwamba kwasasa Mhe. Lissu anaendelea vizuri kiafya.

Jumatatu yani Mei 25, 2026 atakuwepo katika kesi ya Chadema ya mgawanyo wa mali, ameomba Wanachama pamoja na wafuasi wa CHADEMA wahudhurie Makahama Kuu siku hiyo ili kufuatilia kesi hiyo.

Lakini pia kesi yake ya mchongo ya UHAINI itaendelea kuanzia JUNE 11, 2026.

#FreeTunduLissu
1779645404297.jpg
 
"Msiogope kwani, Hakuna jambo baya zaidi ya yale ambayo tayari tumeyapitia linaloweza kutupata". Tundu Lissu, 25/05/2026.
1779807094965.jpg
 
Mbeya wala kiapo cha kupambana hadi Tundu Lissu aachiwe, katiba mpya ipatikane, na ccm iondoke madarakani.

Sikiliza kiapo hiki mbele ya polisi mbeya wameapa kwa maisha yao!

#KatibaMpyaNiSasa #october29samiaaliuwanduguzetu #kataawahuni #freelissu #TUTAKUWEPO


View: https://www.facebook.com/share/v/1Gz12tEyjm/
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kipaumbele na nguvu zake zote kwa sasa zimeelekezwa katika mapambano ya kisiasa yenye lengo la kukiondoa madarakani Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa njia za kidemokrasia.

Kauli hiyo imetolewa leo, Alhamisi ya Mei 28, 2026, na Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Tanzania Bara, Amani Golugwa, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye viunga vya Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam.

Golugwa ametoa msimamo huo wa chama chake muda mfupi tu baada ya Mahakama Kuu kutoa uamuzi wa kuifuta rasmi na kuiondoa mahakamani kesi ya madai iliyokuwa inahusu usawa wa mgawanyo wa mali na rasilimali za chama hicho kati ya Tanzania Bara na Zanzibar.

Kiongozi huyo alieleza kuwa kukamilika kwa shauri hilo kunakipa chama fursa ya kuweka kando migogoro ya ndani na kujikita katika mikakati mikuu ya kuelekea uchaguzi, akisisitiza kuwa muundo wa uendeshaji wa CHADEMA unabaki kuwa imara na wenye mrengo wa kitaifa.

"Kazi kubwa iliyopo mbele yetu kwa sasa ni kupambana kuiondoa CCM madarakani kwa njia ya kidemokrasia," alikaririwa Golugwa akionyesha kuwa chama hicho kikuu cha upinzani kimejipanga upya kimkakati mara baada ya kushinda hatua hiyo ya kisheria mahakamani.
1779971637375.jpg
 
MAHAKAMA YA RUFAA KUSIKIKIZA KESI DHIDI YA MHE. LISSU, June 11,2026:

Mahakama ya Rufaa itasikiliza maombi ya Mkurugenzi wa mashitaka nchini dhidi ya Mwenyekiti wa Chama Taifa, Mhe Tundu Antipas Lissu Alhamisi ya tarehe 11 June, 2026.

Haya ni yale maombi ya Jamhuri ambayo waliyapeleka baada ya Mahakama kuu kukubali pingamizi la Mhe Lissu dhidi ya maombi ya Serikali kuraka kuongeza maelezo ya nyongeza ya shahidi.

Jopo la Majaji 3 wa Mahakama ya Rufaa wamepangwa ambao ni, Mhe Mwalija, Mhe Jaji Muruke na Mhe Jaji Khamisi.

Hakikisha ujumbe huu umewafikia kwa wingi marafiki wa Demokrasia na Haki.

Gaston Shundo Garubindi
Mkurungenzi wa Sheria wa CHADEMA HQ
1780199461742.jpg
 
#BREAKING: JUKWAA LA MAJAJI AFRIKA LASISITIZA KESI YA LISSU KUAMULIWA KWA HARAKA
Jukwaa la Majaji na Wanasheria wa Afrika (AJJF) imeitaka Mahakama ya Tanzania kuharakisha mashauri ya jinai dhidi ya kiongozi wa upinzani Tundu Lissu, ikionya kuwa ucheleweshaji wa kesi unaweza kudhoofisha imani ya umma kwa taasisi za haki.

Katika taarifa yake, AJJF ilibainisha kuwa mashauri yanayomhusisha mwanasiasa maarufu huvutia uangalizi wa kitaifa na kimataifa, hivyo uwazi na kasi ya uendeshaji ni muhimu.

Jukwaa hilo lilionya kuwa “haki ikicheleweshwa inaweza kuathiri imani ya umma kwa mahakama na mfumo mpana wa utoaji haki.”

AJJF ilisisitiza kuwa uamuzi wa haraka na wa kuaminika unahudumia maslahi ya mtuhumiwa na ya Serikali, huku ukilinda uthabiti wa demokrasia.

Pia ilihimiza mahakama za Tanzania kutekeleza wajibu wao wa kikatiba kwa uhuru na weledi, kuhakikisha mashauri yanaheshimu viwango vya haki ya kusikilizwa na kuimarisha imani ya wananchi kwa utawala wa kikatiba.
1780420884545.jpg
 
Mtoto wa Lissu ametinga Senate kupambania Baba yake. Ni moto juu ya moto!
IMG-20260605-WA0015.jpg
IMG-20260605-WA0014.jpg
 
Siku ya jana, mtoto wa Mhe. Lissu, Augustino Tundu Lissu aliungana na Dada Tausi Likokola Liberatus Mwang'ombe na Emanuel Katili walifika Washington, DC ofisini kwa Congressman, Joe Wilson kwa ajili ya kufanya mazungumzo juu ya uvunjifu wa haki za binadamu na za kuabudu ulio fanywa na chama cha majambazi
 
Back
Top Bottom