Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 182

Mhe. Lissu anaendelea na maswali ya Dodoso

Mhe. Lissu: haya hayo ndio maelezo yako?

Shahidi wa kificho P8: Haya ndio maelezo yangu nayatambua. Yana sahihi yangu.

Mhe. Lissu: Amemsomea maelezo yake yote. Anamuuliza hayo ndio maelezo yako kama nilivyosoma?

Shahidi wa kificho P8: Bila shaka.

Mhe. Lissu: Bila shaka nini?

Shahidi wa kificho P8: umesoma sahihi.

Mhe. Lissu: Anamsomea maeneo ambayo atamuhoji kumkanusha.

Anamuorodheshea hapa.

Mh. Lissu amemaliza kumsomea hayo maeneo anamuuliza je ungependa maelezo yako yapokelewe Mahakamani kama ushahidi?

Shahidi wa kificho P8: Sina Pingamizi.

Jaji: Mawakili mnasemaje wa Serikali?

Renatus Mkude: Hatuna pingamizi kabisa.

Mhe. Lissu: Waheshimiwa naomba apewe D7.

Mhe. Lissu: Sasa swali langu la kwanza kuhusu simu yako nioneshe uliposema kwenye maelezo

Shahidi wa kificho P8: Hakuna

Mhe. Lissu: Kuna mahali umesema chochote kuhusu simu?

Shahidi wa kificho P8: Hakuna.

Mhe. Lissu: ni kweli umesema ulikuwa na account ya youtube?

Shahidi wa kificho P8: Ni kweli

Mhe. Lissu: Na onyesha sasa wapi kwenye maelezo kua uliona hiyo video.

Shahidi wa kificho P8 : Kimya

Mhe. Lissu: Unasema Lissu alisema tunapaswa kufanya uasi dhidi ya Serikali?

Shahidi wa kificho P8: nilisema.

Mhe. Lissu: Tuonyeshe kwenye maelezo yako

Shahidi wa kificho P8: Huko hakuna.

Mhe. Lissu: Umetuambia habari za kupelekwa kwa Rashid kutoa maelezo.

Tuambie zipo wapi kwenye maelezo?

Shahidi wa kificho P8: Hakuna.

Mhe. Lissu: Je ulipelekwa kwa RCO na kuwekwa mahabusu kama ulivyosema?

Shahidi wa kificho P8: Ni sahihi.

Mhe. Lissu: Tuoneshe hayo kwenye maelezo yako?

Shahidi wa kificho P8: Hakuna.

Mhe. Lissu: Haya uliyosema leo Mahakamani unaamini ni muhimu ndio maana umeyasema leo?

Shahidi wa kificho P8: Sahihi.

Mhe. Lissu: Nitakosea nikisema haukuyasema Polisi kwasababu hukuamini ni muhimu wao kuyajua?

Shahidi wa kificho P8: utakosea.

Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama wakati unatoa ushahidi ulitoa sababu.

Shahidi wa kificho P8: Naweza kuzitoa sasa hivi.

Mhe. Lissu: Huu sio muda wake we kaa nazo hizo sababu zako.

Mhe. Lissu: umesema kukinukisha hivi nilisema maana yake?

Shahidi wa kificho P8: Ndio ulisema maana yake ni kufanya uasi

Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama umewasilisha hiyo video mahakamani.

Shahidi wa kificho P8: Sijawasilisha.

Mhe. Lissu: Soma kwa sauti kilichosababisha mimi kukuhamasisha

Shahidi wa kificho P8: Nisomeeee.

Mhe. Lissu: P8 amesema nilichukia wizi wa uchaguzi wa CCM kwenye uchaguzi na sisi wanachama hatukubaliani na mambo ya hovyo na ndio maana tunapinga.

Mhe. Lissu: Haya ni yako?

Shahidi wa kificho P8: We uliza swali hayo mengine ni siri yangu.

Watu wanacheka.😂😂😂

Mhe. Lissu: Jibu swali sasa.

Shahidi wa kificho P8: ndio hivyo yakwangu.

Mhe. Lissu: Umesema ulikuwa unasubiri kauli yangu baada ya ile hotuba.

Shahidi wa kificho P8: Ni kweli.

Mhe. Lissu: Sasa baada ya kuona hiyo video hadi leo kama umewahi kuiona hiyo kauli ya Lissu?

Shahidi wa kificho P8: Hajatoa hadi leo maana ni muhalifu.

Watu wanacheka tena.😂😂

Mhe. Lissu: umesema ulivyosikia kauli yangu ukapata hamasa ukaanza kutekeleza uasi?

Shahidi wa kificho P8: Ndio

Mhe. Lissu: Kwahiyo ulijiongeza hata kabla sijatoa kauli.

Shahidi wa kificho P8: sikujiongeza lakini ndio hivyo.

Mhe. Lissu: Sasa wewe ni mwanachama wangu inabidi nisikutese hapa ngoja nimalizie uondoke.

Shahidi wa kificho P8: Mimi sio mwanachama wako kwani wewe unaona haya ni mazuri, Mimi sikuwahi kutegemea kama siku moja nitafika hapa.

Watu wanacheka sana.😂😂😂

Mhe. Lissu: Je umewahi kuwasiliana tena na Polisi kuanzia tarehe 22/04 hadi sasa?

Shahidi wa kificho P8: Sijawasiliana na Polisi hadi leo labda walivyoniambia tu nije kutoa ushahidi.

Part 183 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 188

Mahakama imerejea.

Majaji wameingia muda huu saa tisa.

Mhe. Tundu Lissu yupo.

Cha ajabu Mawakili wa Serikali hawapo. Mh. Lissu ameuliza Jamhuri imekimbia.

Watu wanacheka.😂😂😂

Majaji wako pale mbele.

Hakuna kinachoendelea muda huu.

Sasa wanaingia baada ya kuwaweka Majaji dakika kama 20 hivi.

Anasimama Renatus Mkude anasema Waheshimiwa Majaji tunaomba radhi kwa kuchelewa kwa niaba ya wenzangu naomba mtusamehe.

Tunae shahidi mwingine tunaomba kuendelea.

Majaji wanaandika kidogo

Shahidi anayefuata ni P4 na ataongozwa na Wakili Winiwa Kasawa.

Huyu ni Shahidi anayelindwa sasa Winiwa anajiandaa kuja kumuhoji P4 ambae ni Shahidi wa 10 wa Jamhuri.

Jaji anamuuliza una miaka mingapi?

Shahidi wa kificho P4: 29

Jaji: Dini yako?

Shahidi wa kificho P4 : Mkristo.

Jaji: Haya muapisheni.

Anaapishwa hapa P4

Wakili: Wewe ni mkazi wa wapi?

Shahidi wa kificho P4 : Arusha.

Wakili: unajishughulisha na nini:

Shahidi wa kificho P4 : Dereva Bajaji.

Wakili: unafanyia wapi hizo bajaji?

Shahidi wa kificho P4 : Kwa Mrombo.

Wakili: Unakumbuka nini tarehe 03/04/2025

Shahidi wa kificho P4 : Nakumbuka tarehe hiyo majira ya saa sita mchana nikiwa natoka nyumbani nilifika mahali nikasimama mahali kusubiri wateja.

Nikawa naperuzi kwenye simu yangu nikaingia kwenye mtandao wa Youtube. Nikakutana na habari za Mwenyekiti wa Chadema. Anaitwa Tundu Lissu

Wakili: nini kiliendelea?

Shahidi wa kificho P4 : Akawa anaelezea kuwa amejipanga kuzuia uchaguzi.

Wakili: Kingine nini uliona?

Shahidi wa kificho P4 : Alisema watakinukisha maana hawana imani na Uchaguzi. Kwani hata Majaji ni vibaraka wa CCM.

Wakili: ikawaje?

Shahidi wa kificho P4 : alisema hawana imani na tume ya Uchaguzi kwani imevuruga uchaguzi mdogo wa 2024 kwahiyo hawana imani na tume.

Wakili: nini kingine?

Shahidi wa kificho P4 : Hata Polisi wanashiriki kuiba kura.

Wakili: ikawaje sasa?

Shahidi wa kificho P4 : Maneno yale yalini convice kusapoti alichokuwa anakisema.

Wakili: Nini kingine kiliendelea?

Shahidi wa kificho P4 : Abiria wangu walifika niliwapeleka kwa Mrombo na baadae kijiweni.

Wakili: Nini kilikuwa kimeku convice?

Shahidi: Maneno ya kwamba tutafanya uasi, tutakinukisha na hivyo vyombo vyote kuwa hawezi kuviamini.

Wakili: Yalikushawishi nini?

Shahidi wa kificho P4 : Hali ya maisha ni ngumu sana ndio maana nikashawishika.

Wakili: Kingine je?

Shahidi wa kificho P4 : Nikarudi kwa Mrombo pale maana nilikuwa nimeshawapeleka wateja wangu.

Wakili: Nini kikaendelea?

Shahidi wa kificho P4 : Walikuwa wanasimuliana pale kijiweni kuhusu Mwenyekiti wa Chadema alivyokuwa anazungumza pale kijiwe cha Bajaji.

Wakili: nini kikaendelea?

Shahidi wa kificho P4 : Watu wengi walikuwa wanaunga mkono wanasema bora kinuke ili unafuu wa maisha upatikane.

Mhe. Lissu: Waheshimiwa Wana kasi wawe taratibu.

Wakili: Nilikuuliza akina nani hao?

Shahidi wa kificho P4 : madereva bajaji wenzangu na mwenye kiduka pembeni.

Wakili: ikawaje?

Shahidi wa kificho P4 : Nilishangaa Polisi wametuvamia na kila mtu akakimbia ila nikakamatwa Mimi na Mwenzangu ambae ni P7. Tukapelekwa kituo cha Murieti na Baadae Central Mjini.

Wakili: Ikawaje?

Shahidi wa kificho P4 : Tukaambiwa pale Polisi kuwa tunazuia Uchaguzi. Tukawekwa ndani.

Wakili: nini kilifuata?

Shahidi wa kificho P4 : Tuliandikwa maelezo tukawekwa ndani.

Wakili: Ikawaje tena?

Shahidi wa kificho P4 : Wakaja mdogo wangu na Dada angu kuniwekea dhamana.

Wakili: Walijuaje?

Shahidi wa kificho P4 : Tulikamatwa watu wakiwa wanatuona. Walituwekea dhamana na Polisi walitupa utaratibu wa kwenda kuripoti kila siku.

Part 189 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 191

Jaji Ndunguru anawaita upande wa Serikali kwa ajili ya Re-Examination

Wakili wa Serikali anasema hawatakuwa na maswali.

Jaji Ndunguru : Shahidi sasa uende tumemalizana.

Shahidi anasepa.

Renatus Mkude: Tunae shahidi P7 tunaomba yeye aendeleee kesho asubuhi.

Majaji wanaandika kidogo pale juu.

Kesi inaahirishwa hadi kesho asubuhi maana muda umeisha inakaribia saa 11 jioni.

So tutaendelea kesho, Mungu akitujalia uzima.🙏
 
#Pichani

Huyu aliyeshika 🎤 ndo Shahidi wetu wa leo Coplo Vicent yeye kasema hajui PGO wala sheria yoyote ambayo imeandikwa kwa lugha ya Kingereza.

Anasema yeye ni mpelelezi, anakamata watu kwa amri ya Polisi tu hata kama hajui wamekosa nini.😂😂😂
1771540909898.jpg
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 187

Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi ASP Geofrey Lutufye.

Mhe. Lissu: Mnajifanya mapolisi mnawasingizia watu vitu vya bure haya itakushangaza hao mliowakamata baada ya kesi yao kuisha ni mashahidi wa kesi hii?

ASP Geofrey Lutufye : Hainishangazi.

Mhe. Lissu: haikushangazi kwasababu huo ndio utaratibu wenu mapolisi wa Tanzania.

Mhe. Lissu: Au unabisha nikufungulie ripoti ya Jaji Mkuu Othman Chande amesema mnawafungulia watu makosa ya uongo.

Sasa nikuulize swali lingine, umewahi kuona video mimi nikiwa nazungumza habari za huo uchaguzi mkuu?

ASP Geofrey Lutufye : amekaa kimya

Mhe. Lissu: Unajua kwanini nimeshitakiwa kwa Uhaini ASP geofrey lutufye? Unajua sababu.

ASP Geofrey Lutufye : Sababu ya ile kauli uliyotoa.

Mhe. Lissu: Ipi hiyo?

ASP Geofrey Lutufye : Ulisema utazuia uchaguzi wa mwaka 2025.

Mhe. Lissu: Ndio nakuuliza uliiona hiyo video?

ASP Geofrey Lutufye : Sikumbuki.

Mhe. Lissu: Hawa ndio kesho watakuwa ma RPC siku inayofuata utashangaa anakuwa IGP,

Sina maswali mengine Waheshimiwa majaji.

Watu wanasonya tu hapa.

Anasimama Wakili wa Serikali Renatus Mkude kwa ajili ya Re-examination

Maelezo yako uliandika kama nani?

ASP Geofrey Lutufye : Kama shahidi.

Wakili: Unalizungumziaje kuhusu kujiandika mwenyewe?

ASP Geofrey Lutufye : naweza kujiandika mwenyewe au kuandikwa.

Renatus Mkude: Sina swali lingine. Re Examination imeishia hapo.

Jaji anamruhusu Shahidi.

Shahidi anatoka akiwa ameshika kipaza sauti.

Jaji Ndunguru: Unasahau maji yako hapo.

Shahidi: Hapana siyataki tena.

Jaji: Basi turudishie hiyo MIC tafadhali.

Anairudisha na kutoka nje akiwa anatikisa kichwa.

Watu wanacheka.😂😂😂

Kesi inaahirishwa watu wakale.

Tutaendelea baada ya lisaa limoja.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
Yaani shahidi anaulizwa aliiona video anajibu sikumbuki😅😅😅Yaan video za kina Arnord au Rambo tunazikumbuka kipindi ambacho ni wadogo miaka ya 80s, Tv ni mbili au moja mtaa mzima na tunazikumbuka..jitu la miaka 30s linasema halikumbuki tukio la kuangalia video ya ndani ya mwaka tu na ni video muhim sababu ni ya kesi ya uhaini. Ushahidi wa kitoto sana cause haulingani na uhalisia! Na kwanini mashahidi wengi ni bodaboda na ushahidi wao ni kuperuzi Youtube? Kwa uharisia bodaboda wengi hawaperuzi Youtube,wengi ni IG,Titock au facebook. Youtube kwa watu wa kawaida wengi wanaingia kwa kusudi la kutafuta( Searching) na si kupitapita tu bila mpangilio. Mashahidi wengi husema walipaki vyombo vyao wakawa wanapitapita huko Youtube ndo wakakutana na video za Mh.Lissu kuhamasisha uasi😆😆😆uzuri wamekaririshwa kwamba ukishindwa kueleza sema sikumbuki au sijui. Ila kwa muktadha wa kawaida hata sisi tusiojua sheria vzuri kwa kutumia busara tu, hamna mashahidi hapo!!
 
Back
Top Bottom