#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 184
Wakili wa Serikali anaendelea kumuongoza shahidi
Jaji: Endeleeni
Wakili: Eheee kikaendelea nini?
ASP Geofrey Lutufye: Nilivyowakuta wale vijana waliokuwa wanakula njama nikawaambia wako chini ya Ulinzi.
Jaji: Hiyo MIC ameshikaje mbona hasikiki?
Wakili: ikawaje shahidi?
ASP Geofrey Lutufye: Tuliwakamata P4 na P7 ambao walikuwa wameanza kukimbia baada ya hapo nilitoa maekekezo wapelekwe kituo cha Polisi Murieti, hao askari ni wanne, kituo cha Murieti kipo Mkoa wa Arusha.
Wakili: Nini kiliendelea?
ASP Geofrey Lutufye: Sisi tuliendelea kuwatafuta waliokuwepo pale lakini hatukufanikiwa kuwakamata.
Wakili: Nini kingine kiliendelea?
ASP Geofrey Lutufye: Waliacha Bajaji zao tukazichukua na kuzipeleka kituo cha Polisi Murieti na mbili zilikuwa za wale watuhumiwa tuliowakamata.
Wakili: Nini kiliendelea?
ASP Geofrey Lutufye: Majira ya saa moja ndio tulizipeleka hizo Bajaji kituo cha Polisi Murieti.
Wakili: Kituo cha Polisi Murieti nini kiliendelea?
ASP Geofrey Lutufye: Ulipata maelekezo kutoka kwa kaimu mkuu wa upelelezi Arusha.
Maelekezo hayo yalinitaka niwapeleke ofisi za mkuu wa upelelezi Arusha, tukiwa njiani tunawapeleka P4 na P7 niliwahoji kwamba kwanini mnahusika kula njama kutaka uchaguzi mkuu wa 2025 usifanyike?
Wakili: Ikawaje?
ASP Geofrey Lutufye: Wote walikiri kuwa wanamuunga mkono Mwenyekiti wa Chadema Tundu Lissu kutokana na ile kauli yake aliyoitoa kwenye Mtandao kuwa atazuia Uchaguzi, ataleta uchochezi na atakinukisha.
Wakili: Nini kiliendelea?
ASP Geofrey Lutufye: Tuliwafikisha Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha majira ya saa mbili.
Wakili: Nini kiliendelea?
ASP Geofrey Lutufye: Nilipewa maelekezo tena nifungue jalada la Uchunguzi, nilifungua jalada hilo ambalo ni ARS/D/CID/B/40/2025.
Wakili: Kikaendelea nini?
ASP Geofrey Lutufye: Nikapewa maelekezo tena na Kaimu Mkuu wa Upelelezi Arusha yakinitaka niwahoji watuhumiwa hao kwa kuchukuliwa maelezo yao.
Wakili: Nini kiliendelea?
ASP Geofrey Lutufye: Mimi niliwaa asign maaskari wengine wa RCO wawachukue maelezo na mimi nikaendelea na majukumu mengine.
Wakili: Kingine kilichoendleea?
ASP Geofrey Lutufye: Niliandika maelezo yangu Tarehe 18/04/2025.
Renatus Mkude, Wakili wa Serikali. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji kwa shahidi huyu.
Watu wanaangalia usoni wanacheka.😂
Jaji Ndunguru: Maswali ya Dodoso
Mhe. Lissu anasimama: Shahidi naomba nikuulize maswali na ujibu maswali yangu kwa kadri nitakavyokuuliza.
Sasa waeleze majaji, Huko Polisi mnakojifunzia hizi kazi huwa mnafundishwa kuwa waongo?
ASP Geofrey Lutufye: Hatufundishwi kuwa waongo.
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama huwa mnafundishwa mnapotoa ushahidi mahakamani kuongeza maneno ambayo hayapo?
ASP Geofrey Lutufye: Hatufundishwi.
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama huko Polisi mnafundishwa kutokuwa na heshima?
ASP Geofrey Lutufye: Sio kweli
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama huko Polisi mnafundishwa watu wasio na maadili?
ASP Geofrey Lutufye: Sio kweli
Mhe. Lissu: Sio kweli nini sasa?
ASP Geofrey Lutufye: Tunafundishwa kuwa watu wenye maadili.
Mhe. Lissu: Unafahamu kitu kinaitwa PGO?
ASP Geofrey Lutufye: Amekaa kimya kidogo, PGO naifahamu mimi.
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama ni sahihi au sio sahihi kwamba PGO inasema askari wanapaswa kuwa weledi kwenye kazi zao?
ASP Geofrey Lutufye: Ni kweli inasema hivyo.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kwa mujibu wa PGO Polisi wanatakiwa kuwa waaminifu. Anamsomea PGO hapa. Wasiwe mafisadi na wawe wakweli
ASP Geofrey Lutufye: Ni kweli.
MheLissu: Hii PGO leo tutacheza nayo sana. Umesema uliandika maelezo yako Polisi?
ASP Geofrey Lutufye: Ni kweli niliandika na naweza kuyatambua.
Mhe. Lissu: Mheshimiwa Jaji naomba apewe maelezo yake.
Anatafutiwa na kupewa hapa.
ASP Geofrey Lutufye: Haya ndio maelezo uliyoandika Tarehe 18/04 mwaka jana.
Part 185 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.