Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Leo naambiwa shahidi wa siri ni Yericko? 🤣 ila watanzania mkimchoka mtu analo!
Anyway hiki kizimba mbona ka kibanda cha kuku?
Aisee!
Mashahidi nasikia wanaingia mitini mmoja baada ya mwingine 😆 chezeya Lissu!
#FreeTunduLissu #LissuSioMhaini #LissuHanaHatia
#SamiaMustGo
1770922465754.jpg
 
Basi bhana leo wakati shahidi wa kificho anatoa ushahidi wake alipewa desa akawa anasoma asa Mawakili wa Serikali walimuandikia aseme simu aliyotumia kutizama video ya Kukinukisha ni Sony Experia au Galaxy yeye akasema alitumia simu aina ya Sony Xperia Galaxy .😂😂😂😂
 
Kuna mtu kananiambia, Hilda unashangaa hawa watu kumnyima Mhe. Lissu chakula,

Umesahau kwamba baada ya watu kupigwa risasi Oktoba 29 ni hawa hawa waliamuru majeruhi wa risasi wapelekwe Mochwari.😤
 
Wakati tunaendelea na updates za kesi ya Uhaini dhidi ya Mhe. Lissu

Huyu ndo Shahidi wa kificho siku ya leo kwenye kesi ya Uhaini ya Mhe. Lissu.

Watu wa maeneo ya Songea mjini bila shaka mnamfahamu, mwambieni aache kutumika.

Haya tuendelee na updates
1770975899554.jpg
1770975896392.jpg
 
Brother @⁨Unknown user⁩
Nilisoma Hii Nikiwa Na Hasira Kali Sana Nikajikuta Nacheka Kwa Sauti Mpaka Nitasema eeeee mbona Nipo Mwenye 👇👇👇

Hon, LISSU, Anauliza Maswali Shahidi.
Sasa waeleze Majaji ilikuaje ukabadilika Kuwa Mtuhumiwa Wa Kupanga njama za Kufanya Maandamano Na Leo ukawa Shahidi?

P6, Anajibu!
Hata Mimi Sijui Nini kilitokea🤣🤣

Hon, LISSU, Polisi Walikwambia Ukiwa Shahidi Kwenye Kesi Hii watakufutia mashitaka Yako si Ndio?

Anajibu Shahidi P6.
Hapana Mheshimiwa we Acha Tu🤣🤣

Hapana Hakuna Kesi Ni Kutumia Raslimali Za Umma Bure
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 172

Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi wa kificho P6.

Mhe. Lissu: Mhe. Jaji naomba shahidi ajibu maswali yangu.

Jaji: Hebu muulize tena.

Mhe. Lissu: Hayo maneno ya simu infinix smart 8 yapo au hayapo?

Shahidi wa kificho P6: sifahamu.

Jaji: Nafikiri lengo lako mshitakiwa ni ku empeach credibility ya shahidi kwahiyo akisema hafahamu wakati kielelezo kipo na sisi Mahakama tutakipitia. Basi acha aendelee kusema hafahamu.

Mhe. Lissu: Maneno kwamba ulikuwa na bando la kuingia youtube hebu tuoneshe kwenye maelezo yako hapo?

Shahidi wa kificho P6: Yapo.

Mhe. Lissu: Tuonyeshe.

Shahidi wa kificho P6: Majira ya saa nne niliona mtandao wa youtube hotuba ya Tundu Lissu.

Mhe. Lissu: Swali langu ni ulikuwa na bando la internet.

P6: Hayo hayapo.

Lissu: Kumbe una akili unaelewa. Tukienda hivi itakuwa vizuri. Haya tuendeleee.

Ulisema uliingia katika mtandao ya Jambo TV?

P6: Nilisema niliingia kwenye account.

Lissu: Hivyo hivyo account eheee yapo kwenye maelezo yako?

Shahidi wa kificho P6: Hayapo.

Mhe. Lissu: Umeeleza kwamba wakati nahutubia huo Mkutano nilisema maneno kwamba yeyote atakayekuwa nasi tutaenda nae na asiyetaka tutamuacha, yapo kwenye maelezo?

Shahidi wa kificho P6: Hayapo.

Mhe.Lissu: Ulisema nilisema kuwa kama kuna anayetaka kugombea udiwani asahau na anayetaka kugombea ubunge asahau, hayo nayo yapo kwenye maelezo yako?

Shahidi wa kificho P6: Polisi nilitoa ila hapa kwenye maandishi sioni.

Mhe. Lissu: Ahsante, Polisi ni waongo wamekuibia maneno yako, tuendelee.

Haya umesema nilisema maneno No Reforms, No Election, haya ni maneno yangu kweli nimeyasema sana.

Shahidi wa kificho P6: hayo sikusema. nilisema bila mabadiliko hakuna uchaguzi.

Mhe. Lissu: Basi twende na hayo hayo, yapo kwenye maelezo au hayapo?

Shahidi wa kificho P6: Hayo maneno siyaoni kwenye maelezo.

Mhe. Lissu: Turudi kwenye simu kwenye maelezo yako yote Polisi nataka uniambie ulisema kama ulikuwa na simu popote pale? Nataka unioneshe humo kwenye maelezo yako?

Shahidi wa kificho P6: nilisema nimejiunga na magroup ya whatsapp kwahiyo maana yake ni simu.

Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama maneno ya bendera za taifa na Chadema yapo kwenye maelezo yako?

Shahidi wa kificho P6: Hayapo.

Mhe.Lissu: Kwamba nilivaa kombati za Kaki nayo pia yapo humo kwenye maelezo?

Shahidi wa kificho P6: Maelezo siyaoni.

Mhe. Lissu: Umemuelezea mtu anaitwa Essau Chiza pia anaitwa Mwamba wa Kigoma sasa tuoneshe Mwamba wa Kigoma kama yapo?

Shahidi wa kificho P6: Hayapo.

Mhe. Lissu: Ulisema Essau ni Katibu sehemu nyingine ni Mwenyekiti kipi ni kipi?

Shahidi wa kificho P6: Mimi sijasema hivyo.

Mhe. Lissu: Sasa wewe leta hayo maelezo nikuoneshe, anamsomea aliposema Mwenyekiti na aliposema ni Katibu.

Shahidi wa kificho P6: Mimi sikusema hivyo watakuwa mapolisi ndio walikosea.

Mhe. Lissu: Pole kwa kuingizwa chaka na mapolisi.

Shahidi wa kificho P6: Ahsante sana.

Watu wanacheka.😂😂😂

Mhe. Lissu: Ulisema ulivyohamasika kufanya vurugu tuoneshe hizo habari nazo kwenye maelezo yako?

Shahidi wa kificho P6: anasoma mambo tofauti kabisa.

Mhe. Lissu: Wewe ulihamasika kwamba utazuia uchaguzi kwa kukinukisha ndio nayataka yapo?

Shahidi wa kificho P6: Mimi binafsi maneno ya Mwenyekiti wa Chama yalinihamasisha na kupata moyo wa kijasiri na kunipa hamasa ya kuvuruga uchaguzi mkuu 2025 kwa kukinukisha.

Mhe. Lissu: Ohoo Hongera sana kumbe wewe na mimi letu lilikuwa moja ila Mwenzangu uko kizimba cha shahidi nashangaaa. Haya tuendelee lakini.

Part 173 itaendelea kwenye post inayofuata

Naomba repost yako.
 
Akiwa ndani anachafua hali ya hewa, akiwa nje anaichafua hali ya hewa.
Lissu ni noumar sana.
 

Attachments

  • 1771210286535.jpg
    1771210286535.jpg
    17.8 KB · Views: 8
Back
Top Bottom