Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Lisu ni kiboko aisee anapendwa na Watanzania kweli kweli kama anavyosema yeye..
Mtu yupo ndani harafu watu wamejaa hivyo kwenye kesi yake si balaa hilo.
 
Good News.
Mlinzi wa Mhe Tundu Lissu Ameachiwa muda huu hapa Central Police Mbeya alikokuwa akishikiliwa. Ikumbukwe alipelekwa Mkoa wa Songwe na usiku wa leo alirudishwa Mbeya.
1770733681000.jpg
 
Kesho mapema sana tukutane Mahakama Kuu kwenye kesi ya Mhe. Lissu💪🏿✌🏿📌🔨
 
KUTOKA UKUMBI WA MAHAKAMA KUU

Waandishi wa Habari wapo wa kutosha sana ndani ya Ukumbi wa Mahakama.

Muda huu ameingia Makamu Mwenyekiti wa Chama Mhe. John Heche pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Chama Dr. Rugemeleza Nshala.

Ameingia pia Naibu Katibu Mkuu wa Chama, Amani Golugwa. Tunasubiri

Leo nawaona Mawakili wa Mhe. Tundu Lissu wapo wakutosha pia.

Nimemuona.

1. Dr. Nshala
2. Hekima Mwasipu
3. Edson Kilatu
4. Faraji Mangula
5. Frednand Makore
6. Deogratias Mahinyila
7. Michael Lugina
8. Ikoti Lissu

Na wengine ngoja niendelee kutafuta majina yao hapa.

Mawakili wa Serikali pia nao naona wanaingia sasa muda huu saa nne kamili asubuhi, hawa jamaa huwa wanaingia kiboss sana.

Muda wowote Mahakama itaanza maana nimeona Makarani wa Mahakama wameanza kupanga vitu kule juu sehemu za Majaji.

Kesi imechelewa lisaa limoja zaidi mbele.
 
Hiki ndo kizimba cha mashaidi wa kificho pamoja na Mahakama kuhairisha kesi jana ili kirekebishwe ila mpaka muda huu naona kipo vile vile hakuna kilichobadilishwa.
1770887889251.jpg
 
Back
Top Bottom