Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

"Hakuna njia rahisi ya kuelekea kwenye uhuru wa kweli, na wengi wetu tutapitia kwenye bonde la uvuli wa mauti, lakini MSIOGOPE, tutashinda".- Mhe. Tundu Lissu.
1770506545085.jpg
 
Kesi ya Uongo ya Mwenyekiti wetu inaendelea Februari 09. Watesi wetu wanamshikilia Mwenyekiti wetu tangu Juni 10, 2025, sasa ni miezi minane Mwenyekiti yupo gerezani. Sote tupige kelele na kuchukua hatua Mwenyekiti aachiwe huru kwani sio Mhaini.
#LissuSioMhaini
1770510368440.jpg
 
Kuna siri kubwa sana nyuma ya nateso ya Tundu Lissu ila kwa kifupi ni Lissu ni mvumilivu, mstahamilivu lakini si mnyonge wala si mwoga wala hakubali kuonewa! Hekima yake imemweka katika vitabu vya historia vya Ulimwengu na amekuwa chanzo cha anguko la CCM! Kuna siku mtanielewa!


By standing firm, @TunduALissu has inspired an entire generation to stand up and fight. He forced Samia to make mistakes that effectively means the end of CCM! This could also signal the end of the Union.
20260209_061054.jpg
 
Naomba Repost Yako kwa MIAMBA hii @TunduALissu na @HecheJohn .
Kesho LISSU anaenda Kutoa Elimu ya SHERIA huku HECHE akitoa Elimu ya URAIA
20260209_061435.jpg
.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 155

Naomba nimalizie kwa upande wetu wa Serikali na tumuachie mwenzetu aweze kujibu na kuwasilisha Rejoinder yake.

Jaji anawauliza mmemaliza Upande wa Mashitaka.

Wanajibu wamemaliza.

Mhe. Lissu anajiandaa kufanya rejoinder hapa.

Anasimama Mh. Lissu.

Nawashukuru Waheshimiwa Majaji.

Nimesikiliza hoja za Majibu ya Mawakili wa Serikali na nitajibu kama zilivyoletwa na Wakili wa Serikali.

Hoja ya kuhusu kizimba maalumu cha mashahidi. Swali nililouliza je hicho kizimba kinaendana na matakwa ya sheria?

Sheria inasema kizimba ni eneo ambalo sisi wengine haturuhusiwi kumuona shahidi ila nyie majaji pia mnayo macho ya kuona.

Upo msemo wa kilatin unasema Res Ipsa Loquitour, maana yake mambo yanajisemea yenyewe kama yalivyo.

Hivyo hicho sio kizimba cha mashahidi kwa mujibu wa kanuni.

Huyo shahidi haonekani na Mahakama.

Kwahiyo haihitaji maneno mengi na hizo sio kizimba lilichozungumzwa na sheria.

Jambo lingine ni kwamba je Mahakama iliyotoa ulinzi wa mashahidi ilijumuisha na kizimba hicho?

Jibu lake ni kwamba ruling ya Jaji Mtembwa walisema ilindwe kwa kutumia kizimba, Haikusema hayo yote.

Waheshimiwa Majaji Wakili wa serikali amerudia kifungu cha 6(c) za ulinzi wa mashahidi.

Kwamba mahakama inaweza kueleza utaratibu wa kutumika kwa kutumia kizimba cha mashahidi.

Sasa DPP lazima aombe namna gani anataka kulinda mashahidi.

DPP hakuomba namna ya kulinda mashahidi kwa kutumia kizimba cha mashahidi.

Walichoomba ni majina yasionekane na vingine na Jaji aliwapa walichokitaka.

Haya ya vizimba yametokea hapa, hawawezi kupewa ambacho hawakuomba.

Pia Kanuni ya 5(1) inasema amri ya ulinzi inatolewa kwa shahidi ambae amebainishwa sasa kama Shahidi hajabainishwa kwa lolote Mahakama inajuaje anayepaswa kulindwa ni nani?

Hawakubainisha Majina kwa Mahakama wakapata amri hiyo ya uongo na leo hawaonekani hapa Mahakamani, watatoaje ushahidi watu WASIOJULIKANA.

kicheko kidogo hapa. 😂

Hivyo mnachoombwa hapa ni kwamba kwenye kesi ya Uhaini ambayo adhabu yake ni kifo, hamumfahamu, humumuoni isipokuwa kwao na wao wanaita hiyo HAKI.

Nilisema kwenye hoja yangu ya msingi na haijajibiwa na utaratibu huo ni wa Star Chamber Court karne ya 16 ndio wanataka mahakama kuu ya Tanzania zitumie utaratibu wa giza au kwenye kesi yoyote ile nyingine.

Justice must seen to be done.

Mambo ya gizani hayo na haki gizani sio Haki.

Anaendelea Mh. Lissu.

Huyu Wakili wa Serikali anasema Mahakama ifanye rejea kwenye uamuzi wa Jaji Mtembwa. Nina majibu mawili hapo.

1. Hoja yangu inalenga kulinda integrity ya uamuzi wa Jaji Mtembwa. Wapewe majina ya bandia na maelezo yao yasitolewe kwenye nyaraka. Tukiruhusu mambo ya kizimba ambayo hayakusemwa na Jaji Mtembwa ndio tunataka kuyarekebisha.

2. Kwani ni kosa gani kubadilisha uamuzi wa Jaji mtembwa iwapo kuna sababu za msingi za kuubadilisha. Kanuni ya 8 inasema amri ya ulinzi inaweza kufutwa, kubadilishwa na Mahakama kwa utashi wake au kufuatia kuna mabadiliko ya hali fulani toka amri kutolewa.

Hakuna aliyekuwa anayajua mambo yote haya, tumekuja kuyajulia hapa na kwa vile tumeyajua leo kwa mujibu wa kanuni ya 8 inasema yanawezekana kutokea mambo yakabadilisha hali basi atoe ushahidi wake hapo kizimbani tumuone wote.

Narudia tena amri ya Jaji mtembwa haijataja kizimba lakini pia hakutajwa huyo.

Jambo lingine ni kwamba amri za ulinzi zipo 16 kwenye kanuni na wao waliomba amri nne tu.

Sasa Katuga amatuambia Mahakama inaweza tu kuongeza hizo amri za ulinzi wa mashahidi kwa kadri itakavyoona.

Hiyo haitakuwa Mahakama sasa kama ikifanya hivyo.

Part 156 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba Repost yako.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 155

Naomba nimalizie kwa upande wetu wa Serikali na tumuachie mwenzetu aweze kujibu na kuwasilisha Rejoinder yake.

Jaji anawauliza mmemaliza Upande wa Mashitaka.

Wanajibu wamemaliza.

Mhe. Lissu anajiandaa kufanya rejoinder hapa.

Anasimama Mh. Lissu.

Nawashukuru Waheshimiwa Majaji.

Nimesikiliza hoja za Majibu ya Mawakili wa Serikali na nitajibu kama zilivyoletwa na Wakili wa Serikali.

Hoja ya kuhusu kizimba maalumu cha mashahidi. Swali nililouliza je hicho kizimba kinaendana na matakwa ya sheria?

Sheria inasema kizimba ni eneo ambalo sisi wengine haturuhusiwi kumuona shahidi ila nyie majaji pia mnayo macho ya kuona.

Upo msemo wa kilatin unasema Res Ipsa Loquitour, maana yake mambo yanajisemea yenyewe kama yalivyo.

Hivyo hicho sio kizimba cha mashahidi kwa mujibu wa kanuni.

Huyo shahidi haonekani na Mahakama.

Kwahiyo haihitaji maneno mengi na hizo sio kizimba lilichozungumzwa na sheria.

Jambo lingine ni kwamba je Mahakama iliyotoa ulinzi wa mashahidi ilijumuisha na kizimba hicho?

Jibu lake ni kwamba ruling ya Jaji Mtembwa walisema ilindwe kwa kutumia kizimba, Haikusema hayo yote.

Waheshimiwa Majaji Wakili wa serikali amerudia kifungu cha 6(c) za ulinzi wa mashahidi.

Kwamba mahakama inaweza kueleza utaratibu wa kutumika kwa kutumia kizimba cha mashahidi.

Sasa DPP lazima aombe namna gani anataka kulinda mashahidi.

DPP hakuomba namna ya kulinda mashahidi kwa kutumia kizimba cha mashahidi.

Walichoomba ni majina yasionekane na vingine na Jaji aliwapa walichokitaka.

Haya ya vizimba yametokea hapa, hawawezi kupewa ambacho hawakuomba.

Pia Kanuni ya 5(1) inasema amri ya ulinzi inatolewa kwa shahidi ambae amebainishwa sasa kama Shahidi hajabainishwa kwa lolote Mahakama inajuaje anayepaswa kulindwa ni nani?

Hawakubainisha Majina kwa Mahakama wakapata amri hiyo ya uongo na leo hawaonekani hapa Mahakamani, watatoaje ushahidi watu WASIOJULIKANA.

kicheko kidogo hapa. 😂

Hivyo mnachoombwa hapa ni kwamba kwenye kesi ya Uhaini ambayo adhabu yake ni kifo, hamumfahamu, humumuoni isipokuwa kwao na wao wanaita hiyo HAKI.

Nilisema kwenye hoja yangu ya msingi na haijajibiwa na utaratibu huo ni wa Star Chamber Court karne ya 16 ndio wanataka mahakama kuu ya Tanzania zitumie utaratibu wa giza au kwenye kesi yoyote ile nyingine.

Justice must seen to be done.

Mambo ya gizani hayo na haki gizani sio Haki.

Anaendelea Mh. Lissu.

Huyu Wakili wa Serikali anasema Mahakama ifanye rejea kwenye uamuzi wa Jaji Mtembwa. Nina majibu mawili hapo.

1. Hoja yangu inalenga kulinda integrity ya uamuzi wa Jaji Mtembwa. Wapewe majina ya bandia na maelezo yao yasitolewe kwenye nyaraka. Tukiruhusu mambo ya kizimba ambayo hayakusemwa na Jaji Mtembwa ndio tunataka kuyarekebisha.

2. Kwani ni kosa gani kubadilisha uamuzi wa Jaji mtembwa iwapo kuna sababu za msingi za kuubadilisha. Kanuni ya 8 inasema amri ya ulinzi inaweza kufutwa, kubadilishwa na Mahakama kwa utashi wake au kufuatia kuna mabadiliko ya hali fulani toka amri kutolewa.

Hakuna aliyekuwa anayajua mambo yote haya, tumekuja kuyajulia hapa na kwa vile tumeyajua leo kwa mujibu wa kanuni ya 8 inasema yanawezekana kutokea mambo yakabadilisha hali basi atoe ushahidi wake hapo kizimbani tumuone wote.

Narudia tena amri ya Jaji mtembwa haijataja kizimba lakini pia hakutajwa huyo.

Jambo lingine ni kwamba amri za ulinzi zipo 16 kwenye kanuni na wao waliomba amri nne tu.

Sasa Katuga amatuambia Mahakama inaweza tu kuongeza hizo amri za ulinzi wa mashahidi kwa kadri itakavyoona.

Hiyo haitakuwa Mahakama sasa kama ikifanya hivyo.

Part 156 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba Repost yako.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 156

Anaendelea Mhe. Lissu

Kifungu cha 282 cha CPA amekisoma Katuga hapa kwamba Mahakama inaweza ku regulate taratibu zake wakati wa kutekeleza wajibu wake wa jinai.

Msifungwe sana na hizi kanuni maana mnaweza kuregulate procedure zenu.

Sasa kifungu cha 282 sio kichaka cha kujificha ili kukiuka sheria na taratibu zilizowekwa wazi.

Utaratibu wa kulinda mashahidi umewekwa wazi kifungu cha 194 cha CPA na kanuni za ulinzi wa mashahidi.

Huu mualiko wa kwamba muache sheria inasemaje mtafute busara zenu nawashauri msikubali huu mwaliko wa Katuga wa kudharau sheria.

Anaendelea Mhe. Lissu.

Wakili wa Serikali anasema Haki itatendeka tu hata kama shahidi haonekani.

Sheria inasema amri yoyote ya kulinda mashahidi haipaswi kuathiri haki ya kusikilizwa kwa usawa.

Shahidi ambae wao wanamfahamu mimi simfahamu, wao wanamfahamu jina na taarifa zote mimi sifahamu kuna usawa hapo?

Mahakama itaeleza hatua za kulinda mashahidi kwa usawa wa pande zote.

Hiki wanachoomba kinakiuka kanuni ya 6(2) ya kanuni za kuficha mashahidi.

Waheshimiwa Majaji yote niliyosema nimeyazungumza kwa kulinganisha na Katiba ya Tanzania na sheria za Afrika na Dunia kote.

Nilieleza kwa kina namna sheria zote za kimataifa zimezungumzia suala hili ila wao hawajajibu hata moja.

Hawajajibu kwasababu hayajibiki Waheshimiwa majaji, na hayajibiki kwasababu ni ya kweli. Tuishie hapo.

Kuhusu kanuni kutumika retrospectively, imesemwa na Katuga kwamba kanuni zote za utaratibu zinatumika retrospectively.

Sasa waheshimiwa majaji kanuni za procedure ambazo haziathiri haki zina retrospective effect.

Kanuni za procedure zinapoathiri haki haziwezi kutumika retrospective.

Angalieni ukurasa wa 11 na 12 wa Hukumu aliyoleta Katuga inasema if the legislation affect substantive right it should not operate retrospective.

Sasa hapa tunajadili right to be heard na kanuni hizi mshitakiwa hawezi kumjua shahidi kuanzia majina na vingine.

Kanuni hizi zina affect substantive right.

Kanuni zinakiuka haki zangu za Kikatiba hatuwezi kuziacha hivi zilivyo zikatumika kama wao wanaona ni jambo dogo wamlete shahidi wao hadharani hapa tumenyane nae waone.

Anaendelea Mhe Lissu.

Hizi kanuni zenu mlitunga kwa ajili yangu na matakwa ya kisheria yanakataa.

Sio mnamkamata mtu, mnamfungulia kesi halafu baadae ndio mnaenda kutunga kanuni kwamba tumtungie sheria gani?

Wamepitisha hizo sheria zao ili waje kunishitaki nazo, hilo haliwezekani kabisa.

Huyu Katuga anapenda sana kusema mimi naitishia Mahakama labda hajui nashitakiwa kwa kosa gani?

Nisipojitetea kwa nguvu zangu zote itakuwaje?

If i dont defend myself to the best of my ability itakuwaje?

Nisipoibua yote haya consequences ni adhabu ya kifo.

Maisha ni matamu i am not ready yet to die kama kuna la kusema nitasema tu.

Nitatishaje majaji wa Mahakama Kuu niko Gerezani miezi 10 ila ninachotaka Majaji muyatizame mambo haya kwa kuangalia uzito wa kesi hii.

Naomba kumalizia kwa kusema yafuatayo:

Kwamba ile kesi ya Mahakama Kuu iliyokuwa mbele ya Jaji Mkwizu, Waheshimiwa Majaji mtajiridhisha wenyewe mtakaposoma hiyo kesi mtaona kwamba hiyo kesi haikuwa inahusu uhalali wa hizi kanuni, haikuwa inahusu uhalali wa mashahidi kutoa ushahidi kwa kificho. In fact iliishia kwenye PO (Pingamizi la awali) Jaji hakutaka kusikiliza.

Sasa imeletwa hapa ili iweje? Haina uhusiano wowote na constitutionality ya kanuni na suala la shahidi kutoa ushahidi.

Wameleta hapa ili muone kuwa walishinda hiyo kesi. Hawana kingine cha maana. In fact ilikuwa ni kesi ya cyber crime na sio kesi hii ya uhaini.

Naomba mtafakari hoja zangu na mkubali shahidi asiruhusiwe kutoa ushahidi kwenye hilo box kwasababu zote ambazo nimezieleza.

Nataka Majaji mumuone shahidi na mimi ambae wanasema ni muhaini nataka nimuone, nimuhoji na anijibu.

Part 157 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba Repost yako.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Leo February 9, 2026

Last time tuliishia Part 150 so leo tutaendelea na-;

Part 151.

Ameingia Mheshimiwa Lissu, zimepigwa kelele nyingi sana hapa Mahakamani ni kelele za Rais! Rais! Rais!

Mhe. Lissu amepiga kombati ya kaki, ameingia kwa vibe sana.

Amebeba makabrasha yake, mavifurushi mengi sana ya vitabu.

Imepigwa sauti ya Courttttt ikiwa na ukali watu hawanyamazi wanaendelea na minong'ono fulani ya kushangilia.

Wameingia Majaji na kuketi eneo lao.

Jaji anasema tuendelee

Karani anasoma namba ya shauri.

Anasimama Renatus Mkude wakili wa Serikali Mkuu, yuko na Ajuaye, Nasoro Katuga, Cathbert Mbiringe, Thawabu Issa wanawakilisha upande wa Jamhuri na Mshitakiwa Tundu Lissu yupo.

Leo tumekuja kujibu hoja za Tundu Lissu kama yeye atakuwa tayari, sisi upande wa Serikali tuko tayari Waheshimiwa Majaji.

Mhe. Lissu anaulizwa uko tayari?

Anasema niko tayari lakini nahitaji kuzungumza mambo yaingie kwenye rekodi za Mahakama.

Niwatakie heri ya Mwaka Mpya nyie Majaji, Mawakili wa Serikali na wote waliopo hapo.

Maswala mawili kati ya matatu ninayotaka kuzungumza nitasema kwasababu kifungu cha 11(1)(2) cha sheria ya magereza nyie majaji ni visiting justices kule magereza.

Majaji wanaodhuru magereza mna wajibu wa kuhakikisha magereza yanaendeshwa kwa mujibu wa sheria na wafungwa iwe wamehukumiwa au mahabusu kama mimi wanapata treatment kwa mujibu wa Sheria.

Na kwa mujibu wa kifungu hicho mna mamlaka ya kutoa maelekezo na mapendekezo kuhusu treatment ya wafungwa na mahabusu.

Sisi tunaoishi huko magerezani tumepewa Haki kwa mujibu wa kifungu cha 48 cha sheria hiyo kuwaeleza juu ya mambo yalivyo na tunavyotendewa huko magereza.

Jambo la 1 ni kuhusu haki ya mfungwa kuwasiliana na Mawakili wake.

Wafungwa wana haki ya kufanya mawasiliano na mawakili au washauri wa kisheria bila kusikilizwa na maafisa wa magereza Kanuni ya 13 ya kanuni za uendeshaji wa magereza GN. NO. 60/1987. (Prison Management Regulations)

Kanuni inasema kila mfungwa atapewa fursa ya kuwasiliana na mwanasheria wake na atakapomtembelea maafisa wanaweza kumuona ila sio kumsikiliza. Anaisoma hiyo kanuni kwa kingereza hapa.

Sasa Waheshimiwa majaji kumekuwa na tatizo kubwa kuhusiana na haki yangu ya kuzungumza na mawakili wangu bila kusikilizwa na maafisa wa magereza.

Muda wote wako pembeni yangu hadi ninapozungumza na mawakili.

Tatizo hili sio jipya lilianza toka niko Kisutu.

Anasimama Nasoro Katuga anasema tulikuwa na concern aliweka pingamizi halijaamuliwa anaanza kusema mengine. Naomba mwongozo katika hili.

Jaji anaandika kidogo.

Anamuuliza Lissu unasemaje?

Lissu anasema kifungu cha 48 nilichosema kinasema ni draw attention yenu sio kuomba chochote. So i'm drawing the attention to you. Mkiona mnachakufanya fanyeni mkiona hamna msifanye. Wajibu wangu ni kuwaeleza kinachoendelea.

Jaji anasema nafikiri uendelee haya madai ya Katuga ameeelewa baada ya jibu lako.

Tarehe 12/11/2025 tulivyoahirisha kesi mambo yakabadilika tena wakili akifika anapelekwa ofisi ya Mkuu wa Usalama wa Gereza na mimi na Wakili wangu tunapelekwa huko huku wakitusikiliza nikiwa nazungumza na kikundi, kuanzia Mkuu wa Gereza, maafisa wengine zaidi ya watano wanatusikiliza wakati sheria haitaki hivyo.

Siku 88 toka kesi imeahirishwa mwaka jana wananisikiliza kila Mawakili wangu wanaponitembelea.

Mimi na Mawakili wangu tukiuliza, tunaambiwa ni Maagizo kutoka juu, Huko juu ni wapi juu mbinguni au wapi? Mungu anajua.

Hilo ni jambo langu la kwanza.

Nimewapa taarifa kwa mujibu wa kifungu cha 48 mtajua chakufanya ili kuhakikisha sheria inalindwa.

Jambo la Pili, linahusu kutembelewa na watu wengine wasiokuwa wanasheria. Kanuni zinasema unaruhusiwa kutembelewa na watu sio ndugu pekee.

Part 152 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ili ujumbe uwafikie wengi.
 
Selemani Saidi Ally Bungara (BWEGE) aliyekuwa Mbunge wa Kilwa Kusini mapema leo akiwasili Mahakama Kuu Kanda ya Dar es salaam kufuatilia mwenendo wa kesi ya Uhaini inayomkabili Mhe. Tundu A. M. Lissu
1770657568513.jpg
 
Wawakilishi wa Balozi mbalimbali wakiwa katika ukumbi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es salaam kufuatilia mwenendo wa kesi ya uhaini inayomkabili Mhe. Tundu A. M. Lissu
1770658025098.jpg
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 157

Anamalizia Mhe. Lissu

Vinginevyo haitakuwa Mahakama ya Haki na kanuni zinataka usikilizwaji wa mashauri haya uwe wa haki kwa pande zote.

Ni hayo tu waheshimiwa majaji.

Anamaliza Mheshimiwa Lissu hapa.

Majaji wanateta huku wakiandika kidogo.

Mheshimiwa Lissu anakusanya makabrasha yake taratibu hapa. Bila shaka kesi itaahirishwa leo. Watahitaji kuandika uamuzi wa hoja zilizowasilishwa.

Anawasha kipaza sauti Jaji Ndunguru hapa akiwa serious sana na kama amechoka. Anaonesha hana nuru kabisa. 😂

Naomba niseme yafuatayo kabla sijaahirisha shauri.

Mtakumbuka leo tumevumiliana sana kuhusu simu zinazopiga kelele kama tunashindwa kukaa na simu basi kwenye ukaguzi tutaomba mziache.

Naomba mtambue uvumilivu wa leo hautaendelea kuwepo kuhusu masuala ya simu.

Shauri linaahirishwa hadi Tarehe 11/02/2026 saa tatu asubuhi.

Naomba nisaidie kushare
 
Back
Top Bottom