Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Alert🚨🚨
Ukurasa rasmi wa Mahakama ya Tanzania kwenye YouTube, unaojulikana kama "Mahakama ya Tanzania", umeondoa video zote za matangazo ya moja kwa moja (live streaming) zinazohusu kesi ya uhaini na uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Antipas Lissu.

Video hizo zilikuwa zikirushwa wakati wa hatua za awali za kesi (committal proceedings) katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, kabla ya kesi kuhamishiwa Mahakama Kuu ya masijala ndogo Dar

Hii ni hatua moja wapo ya kufuta ushahidi wa utetezi uliofanyika mahakamani kwa baadhi ya mashahidi wa upande wa serikali walioshindwa kuthibitisha makosa ya Lissu
1766983567688.jpg
 
 
TUJADILI KWA PAMOJA

Je imefika wakati kujiuliza Gen Z Tanzania ni akina nani ?

Baadhi yetu tukitambua kuwa GenZ ni vijana waliozaliwa kati ya kipindi cha miaka ya 1997 hadi 2012 na wengi wao ni Wanafunzi au bado hawana ajira rasmi

Lakini kitendo cha kupigiwa mfano cha kumchangia Mheshimiwa Tundu Lissu zaidi ya shilingi milioni ishirini (20,000,000) ndani ya masaa 24 kinachoelezewa kufanywa na Gen Z Tanzania kina tutaka tutafakari na kujiuliza maswali kadhaa ikiwa ni PAMOJA na Je :
1. Gen Z Tanzania ni aina ileile tulio ifikiria au ni aina nyengine ?
2. Ni wepi viongozi wakuu wa Gen Z Tanzania?
3. GenZ Tanzania wanaweza wakawa wana mlengo mmoja kisiasa, kijamii au kidini ?
4. Utaratibu huu uliotumiwa na Genz unaweza kutumika kusapoti utatuzi wa changamoto nyengine zinazowakabili GenZ
5. Kutoka kwako mchangiaji ......

*Angalizo:
Tafadhali tutumie lugha mzuri katika kuwasilisha mawazo yetu
1767337346521.jpg
 
TAARIFA KWA UMMA.

KESI YA UHAINI DHIDI YA Mhe LISSU KUENDELEA.

Nawafahamisha kwamba kesi ya uhaini dhidi ya Mhe Lissu, Criminal session case No. 19605/2025 imepangwa kuendelea Mahakama kuu, Kanda ya Dar Es Salaam kuanzia tarehe 09 February 2026 hadi tarehe 06 March 2026.

Ikumbukwe kwamba kesi hiyo inasikilizwa na Majaji watatu, Mhe Jaji D. Ndunguru, Mhe Jaji J. Karayemaha na Mhe Jaji Kiwonde.

Tayari Mhe Lissu jana alipokea taarifa rasmi kutoka kwa Naibu Msajili wa Mahakama kuu.

Tukutane Mahakamani.

Gaston Galubindi
Mkurungenzi wa Sheria CHADEMA Taifa,
IMG-20260115-WA0045.jpg
 
Akiwa anatimiza Siku 283 gerezani, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu amevunja rekodi ya kuwa kiongozi wa kwanza wa juu kabisa wa chama cha upinzani nchini kuwekwa kizuizini kwa muda mrefu zaidi tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa mwaka 1992.

Lissu ambaye alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho Januari 22 mwaka jana, alikamatwa wilayani Mbinga mkoani Ruvuma Aprili 9 mwaka jana na kisha kusafirishwa hadi Dar es Salaam alikofunguliwa shtaka la uhaini ambalo hali dhamana kwa mujibu wa sheria.

Lissu alikamatwa alipokuwa akiendelea na mkutano wa hadhara wa chama chake katika operesheni yao iliyojulikana kama 'No reforms no election' ambayo ilikuwa ikiendelea katika kanda ya kusini baada ya kumalizika katika kanda zingine ikiwamo kanda ya ziwa.

Licha ya kwamba wapo baadhi ya viongozi wakuu wa vyama vya upinzani waliowahi kuwekwa kizuizini kwa muda mrefu ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, Freeman Mbowe aliyekaa gererezani kwa zaidi ya siku 220 lakini hakuna aliyefikia rekodi ya Tundu Lissu aliyefikisha siku 283.

Kama ilivyokuwa kwa Lissu ,Mbowe alikamatwa mkoani Mwanza usiku wa kuamkia Julai 21, 2021 na kisha kusafirishwa hadi Jijini Dar es Salaam alikounganishwa na wenzake katika kesi ya Ugaidi kesi iliyoendelea hadi Machi 4,2022 baada ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa serikali kusema hana nia ya kuendelea na kesi hiyo hivyo kuachiwa huru.

Makosa ya Ugaidi na Uhaini yote hayana dhamana kwa mujibu wa sheria jambo lililofanya viongozi hao wawili kusota gerezani kwa muda mrefu. CHADEMA ipo katika kumbukumbu ya miaka 33 tangu kuanzishwa kwake wakati huu ambapo kiongozi wao mkuu bado yupo gerezani.

Imeandikwa na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

HUYU HAPA
1768668212017.jpg
 
Happy birthday shujaa wetu, Mhe. Lissu Mwenyezi Mungu akujalie maisha marefu yenye baraka na amani tele.

Tunathamini sana mchango wako maana umelipa na unaendelea kulipa gharama kubwa sana katika mapambano haya ya kupigania Haki na Demokrasia ya kweli katika Taifa letu

Siku ya leo nakuombea Mwenyezi Mungu akupe ulinzi wa KIUNGU mtu/watu yeyote ambae anania ovu na Uhai wako, Mungu wetu akashughulike nao.
1768912545280.jpg
 
Nilitakiwa nitoke jela kwanzia Mwaka mpya , ila haitowezekana kwa sababu wamenikamata kienyeji na niko jela kwa kosa la kubambikiziwa , sasa hapo kinachotakiwa ni mahakama ndio iniachie na nilipwe fidia ya kupotezewa mda pamoja na matibabu ya mwili wangu, ili nikae kwa amani kwenye nchi yangu lasivyo nitabaki jela mpaka wao watakapo ona inatosha.

Tundu Lissu
1769351839651.jpg
 
 
Kesi ya Uhaini namba 19605/2025 inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Taifa Mhe. @TunduALissu imepangwa kuendelea katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam tarehe 09 Februari 2026.

Zimebaki siku saba tu — tujitokeze kwa wingi kupata darasa la sheria kutoka kwa Mhe. Lissu.

#FreeLissu
1770019796496.jpg
 
God bless this guy .

though we will never be the same

but i believe the God I'm serving is the GOD of fresh bread 🍞.
 
Kesi ya Uhaini namba 19605/2025 inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Taifa Mhe. @TunduALissu imepangwa kuendelea katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam tarehe 09 Februari 2026.

Zimebaki siku tatu tu— tujitokeze kwa wingi kupata darasa la sheria kutoka kwa Mhe. Lissu.

#FreeLissu
1770369490657.jpg
 
Back
Top Bottom