Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Leo Oktoba 24, 2025

Jana tuliishia part 142 so leo tunaendelea na-;

Part 143

Mhe. Lissu ameingia.

Inapigwa courtttttttttt.

Watu wote wanasimama kwa heshima na nidhamu kubwa sana.

Majaji wanaingia na kutoa heshima.

Tunakaa wote chini.

Karani anasimama anasoma jalada hapa na namba ya kesi ya Uhaini.

Upande wa Jamuhuri anasimama Renatus Mkude anatambulisha jopo na anasema wapo tayari.

Anasimama Mhe. Lissu anasema pia yupo tayari.

Renatus Mkude anaieleza Mahakama kuwa mpaka sasa wameleta mashahidi watatu na ameendelea kueleza kuwa Mashahidi wengine wanatoka mkoani hivyo siku ya leo hawatakuwa na shahidi wanaomba kuahirisha shauri na kutokana na ratiba leo ilikuwa siku ya mwisho ya usikilizwaji mpaka itakapopangwa tena.

Mhe. Lissu anasimama na kusema yafuatayo:

Nimesikiliza maombi yaliyosemwa na wakili wa Serikali na ninaomba niseme yafuatayo:

Kwa kifupi leo wameweka mpira kwapani, naona tafakari yao ya jana haijazaa matunda yoyote, kesi imewashinda hii na imedoda kweli kweli kama tulivyoambiwa na Mh. Lissu jana kwamba kesi ilishaisha labda kama anashikiliwa kwa ajili ya Uchaguzi.

Kama Mashahidi Mapolisi ushahidi wao ndio hao mabodaboda waliowakuta vijiweni na kuwatengeneza kuwa walihamasika na maneno ya Lissu watakuja kusema kipi kipya? ngoja tuwasubiri, nafikiri baada ya tarehe 29 kutakuwa na sura tofauti kabisa ya kesi hii ngoja tuone.

Mh. Lissu sasa anaanza na yeye kutoa maelezo yake kuhusu ombi la Mawakili wa Serikali la kuahirisha kesi hii.

Jambo la kwanza sababu iliyotolewa ya kuomba ahirisho sio sababu ya msingi ya kuahirisha kesi.

Kesi hii yote inategemea vielelezo vilivyokataliwa na Mahakama kuu hakuna shitaka ambalo lipo nje ya hizo flash disk na memory card na yaliyomo, Hakuna.

Mashahidi wale ambao wanadaiwa wapewe ulinzi ushahidi wao ni walichoona mtandaoni, mashahidi wa polisi waliobaki ushahidi wao unatokana na yale yaliyodaiwa kuwa mtandaoni.

Mashahidi pekee na ushahidi wao hauuhusiani na mambo ya mtandaoni ni afisa wa uhamiaji aje aseme kwamba mm ni mtanzania ili iweje?

Mwingine ni yule anaekuja kusema nilienda JKT ili iweje? Ili wathibitishe nini??

Wakati kesi ni mambo yaliyokuwa mtandaoni, Kesi hii ilishaisha Waheshimiwa Majaji, maneno haya ya Mawakili wa Serikali ni maneno ya bure kabisa na kutaka kutupotezea muda tu.

Ombi hili ni la kurefusha shauri hili ili niendelee kukaa gerezani ili Uchaguzi Mkuu upite.

Hawawezi kuthibitisha chochote kwasababu flash disk na memory card vimekataliwa, hawana kesi hapa.

Waheshimiwa Majaji kama mtaona ni sawa sawa kuahirisha shauri hili naombeni nipate dhamana ya mahakama kuu kwa mujibu wa kifungu 302(3) cha CPA.

Mahakama inaweza kumuachia mshtakiwa kwa dhamana, mm siendi popote. Nitakuwepo tu mtaani.

Kwasababu ya maamuzi ya jana na juzi hamna kesi hapa kama mtaaamua kuahirisha nipewe dhamana ili nisiendelee kuteseka kwa kitu ambacho hakiendi popote nitakuwa tayari kesi iahirishwe katika mazingira hayo.

Leo ni siku ya 202 nipo gerezani ni miezi sita na nusu nipo gerezani kwa haya ambayo tumeyaona na kuyasikia kuna kesi gani hapa kama sio umbea na uoga wa Serikali kwa watu wanaowapinga?

Kwahiyo waheshimiwa Majaji Ombi lao likataliwe mkikubali nipewe dhamana ni sawa hilo halitakuwa na shida ya kuahirisha.

Sijawahi kukimbia kesi yoyote na wamenifungulia kesi nyingi tu.

Mimi sio mtu wa kukimbia kesi tena kesi zenyewe za uongo uongo wa hawa Mapolisi, nikimbie kwenda wapi, nitamalizana nao hapa hapa Mahakamani walipoamua kunileta.

Nimeshafanya kazi hiyo vizuri na sitakuja kuacha kuifanya ilimradi watanileta tena.

Ni hayo tu waheshimiwa Majaji kwa sasa.

Waheshimiwa majaji wanaandika na kujadili kidogo kilichosemwa.

Anasimama Renatus Mkude tumesikia reply ya mshtakiwa, hapa anajibu pingamizi la Mhe. Lissu.

Msingi ni kwamba hatuna shahidi kifungu cha 302 CPA

Part 144 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
Kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Tundu Lissu imehairishwa leo, Ijumaa Oktoba 24.2025 hadi Novemba 03.2025

Kesi hiyo imehairishwa kufuatia ombi la Jamhuri lililowasilishwa Mahakamani hapo likieleza kuwa, leo ilitakiwa wamlete shahidi wa Nne (4) aanze kutoa ushahidi wake baada ya yule wa Tatu (3) kukamilisha hapo jana, lakini wameshindwa kuleta shahidi hii leo kutokana na kwamba wameshindwa kumsafirisha kwa wakati na mashahidi wao hitajika nje ya Dar es Salaam (wapo mikoani)

Lissu alionekana kupinga vikali hoja hiyo akidai kwamba hiyo ni janjajanja ya Jamhuri kutaka aendelee kukaa gerezani hadi Uchaguzi Mkuu umalizike hivyo kuiomba Mahakama kuilazimisha Jamhuri kuendelea na kesi leo au Mahakama impatie dhamana aende nyumbani

Katika uamuzi wake, Mahakama kupitia jopo la Mawakili watatu (3) wanaosikiliza kesi hiyo wamesema kesi inayomkabili haina dhamana, na kwamba suala la kuomba hairisho kutokana na changamoto la mashahidi linakubalika kisheria na ikizingatiwa kuwa tangu kesi hiyo ianze hakuna siku ambayo Jamhuri imeshindwa kumleta shahidi

Hivyo kesi hiyo imehairishwa sasa hadi Novemba 03.2025 ambapo shahidi wa Nne (4) wa Jamhuri ataanza kutoa ushahidi wake
Tupo pamoja mkuu
tupia vitu hii kesi inaisha leo hii hii!

.
 
UJUMBE WA MATESO KUTOKA KWA MH. TUNDU LISSU AKIWA GEREZANI UKONGA.

“Ndugu zangu,
Kwa wiki kadhaa sasa nimewekwa kwenye total isolation “upweke wa kulazimishwa”

Wale wafungwa wenzangu waliokuwa nami kwenye selo moja, ambao walikuwa wamehukumiwa adhabu ya kifo, wametolewa wote nimeachwa peke yangu.

Selo yangu sasa imewekwa kamera za ufuatiliaji (CCTV) zinazorekodi kila kitu ninachofanya, hadi wakati ninapokojoa au kubadilisha nguo.

Sina faragha yoyote tena. Hili si suala la usalama bali ni kudhalilishwa kwa utu wangu kama binadamu.

Naomba jambo hili lipigiwe kelele kwa nguvu zote, kwa sababu ni ukiukwaji wa wazi wa haki za binadamu na ni kosa kisheria chini ya Kanuni za Umoja wa Mataifa za Matunzo ya Wafungwa (Mandela Rules), ambazo zinasema wazi kuwa:

•Utu wa binadamu unabaki kuwa wa heshima hata akiwa gerezani (Kanuni ya 1),

•Upweke wa muda mrefu au unaomnyima mfungwa mawasiliano ni ukatili na mateso (Kanuni ya 43 na 44).

Pia ni ukiukwaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 12 na 13, zinazolinda hadhi ya mtu na kumzuia kuteswa au kudhalilishwa.

Niko tayari kuvumilia hali yoyote kwa ajili ya imani yangu na msimamo wa wananchi katika haki na uhuru wa watu wetu, lakini udhalilishaji wa utu wa binadamu hauwezi kukubalika, si kwangu tu, bali kwa yeyote anayebeba jina la mwanadamu.
 
Ndugu yangu na mzee wangu Mshana Jr nataka kujua hari yako kama u bukheri na umepona kwenye yale mauaji, na pia nataka kujua baada ya kutajwa tarehe ya kuendelea na kesi vipi mbona mpaka sasa kupo kimya?
 
Ndugu yangu na mzee wangu Mshana Jr nataka kujua hari yako kama u bukheri na umepona kwenye yale mauaji, na pia nataka kujua baada ya kutajwa tarehe ya kuendelea na kesi vipi mbona mpaka sasa kupo kimya?
Nashukuru sana ndugu yangu kwa upendo na kujali .. Kesi ilisimama hivyo leo ndio inaendelea
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Leo Novemba 10, 2025

Last time tuliishia part 144 so Leo tunaendelea na-;

Part 145

Imepigwa Courttttttttt.

Majaji wanaingia sasa.

Watu wamesimama na kuinama kutoa heshima.

Majaji wanakaaa na karani anasoma namba ya shauri.

Mheshimiwa Lissu hajaletwa leo maana kesi inasomwa bila mtuhumiwa.

Mawakili wa Serikali yupo Job Mrema, Thawabu Issa na Cathbert Mbiringe.

Naona wanateta jambo hapa kimya kimya.

Majaji nao wanateta jambo sijui wanaambiana nini? Kuna kimya kinatawala kidogo.

Hata wale maaskari magereza ambao huwa wanamleta Mh. Lissu leo hawapo kabisa. Wapo wengine. Sijui kwanini hawajamleta.

Anasimama Wakili wa Serikali sasa, anajitambulisha na kuwatambulisha wenzake.

Anasema Waheshimiwa Majaji kama mnavyoona Mshitakiwa hayupo mahakamani na sababu za kutokuwepo ni suala la usalama kuwa mdogo.

Hivyo tunaomba tupatiwe ahirisho la siku 14 ili tuweze kuja kuendelea kama usalama utakuwa umetengamaaa. Leo ameshindwa kufikishwa kutokana na sababu hiyo tuliyotoa ya hali ya usalama waheshimiwa Majaji.

Wakili Thawabu Issa ndio anayeiaddress Mahakama.

Anaendelea kusema wao hawakujua kama Mshitakiwa hataletwa walipofika Mahakamani wakashangaa hawamuoni ndio wakaamua kuwasiliana na Mkuu wa Gereza ndie amewaambia kuwa hawatamleta kwa sababu za kiusalama.

Thawabu kanyanyuka hapa na inaidress Mahakama ya kuwa Leo wameshindwa kumleta TAL kwa sababu za kiusalama hivyo wanaomba hairisho la siku 14 waweze kuendelea.

Jaji anawasha kipaza sauti na kusema;

Mahakama baada ya kusikiliza hoja za State attorney inasema kwa leo hatutaendelea kwa kuwa mshitakiwa hajaletwa.

Lakini tunaelekeza kwa State Attorney next time waseme hizo sababu za kiusalama ni zipi zinazofanya hadi shauri liahirishwe?

Na pia Mahakama haiwezi kuwapa siku 14 kama walivyoomba hivyo shauri linapangwa tena kusikilizwa tarehe 12/11/2025 (Jumatano ya wiki hii) na summons za mashahidi na Mshitakiwa zitolewa na kesho zifuatiliwe na wahusika wafikishiwe.

Kwahiyo tunaomba tukutane hapa kesho kutwa.

Inapigwa High Courttt nyingine kubwa na ya kidaku sana wanasimam Majaji wanatoka.

Leo Jamhuri wameweka mpira kwapani tena.

Kumbe Nchi yetu haiko salama kabisa.

Tulidanganywa mambo yanaendelea kama kawaida lakini Magereza na Mawakili wa Serikali leo wanatuambiana Mahakamani nchi sio salama kama watu wanavyoweza kudhani.

Ndio maana barabara na vyombo vya kumleta Lissu Mahakamani vimeshindikana.

Leo siku imekuwa fupi kihivyo.

So Tukutane Hiyo Tar. 12/11/2025 saa tatu kamili asubuhi.

Naomba unisaidie kushare ujumbe uende mbali
 
ANAANDIKA WAKILI GASTON GALUBINDI

UPDATE KUTOKA UKONGA GEREZANI DAY 252:

Leo nimemtembelea Mteja wangu Mhe Lissu, Ukonga Gerezani kujadiliana naye hatima ya kesi zinazomkabili, ashukuliwe Mungu kwa kuendelea kumjalia afya na siha njema kiongozi.

Gerezani kuna utaratibu mpya umeanzishwa ambao ni kinyume cha sheria, Nilichokutana nacho leo ni kama ifuatavyo;

Mosi, Nimeshindwa kutekeleza majukumu yangu kama wakili kutokana na Magereza kulazimisha mazungumzo yangu kama wakili na Mteja wangu Tundu Lissu yafanyike mbele ya Maafisa wa Magereza Ukonga wakisikiliza kinyume na Katiba ya nchi, Kinyume na sheria ya Magereza, Kinyume kanuni za Kimataifa, hivyo nimekataa kuzungumza na mteja zaidi ili tutafute kwanza haki ya usiri wa mazungumzo kati ya mawakili na mteja wetu.

Kwenye hili, Magereza wanafahamu misingi ya kazi, kitendo mnachofanya mnafahamu ni kinyume cha ibara ya 13 ya Katiba, Ni kinyume cha sheria za nchi kuhusu haki za wafungwa na Mahabusu, lakini mnafanya kwa makusudi. Ni lazima kuchukua hatua dhidi yenu.

Pili, Mheshimiwa Lissu aliandika barua kwa Naibu msajili wa Mahakama kuu, tarehe 5 December 2025 akitaka kufahamishwa tarehe rasmi ya session ya kesi ya uhaini inayomkabili pamoja na mwenendo wa kesi hadi ilipoishia. (Taarifa ya Mhe Lissu kuandika barua ilitolewa pia kwa umma) sasa Pamoja na kwamba aliandika barua tarehe 5, cha ajabu ni kwamba barua hizo zinaonekana zilifika Mahakamani tarehe 15 December 2025, yaani juzi Jumatatu.

Kwa mnaofahamu Jiografia ya Jiji la Dar Es Salaam kutoka ukonga hadi Mahakama kuu pale posta , imewachukua Magereza siku 10 kufikisha hiyo barua.

Itakumbukwa session ilipoahirishwa ilipaswa kuanzia November 3 na kukoma tarehe 11 November 2025, lakini hakuletwa Mahakamani hadi siku ya tarehe 11 na tangu siku hiyo hakuna tarehe rasmi iliyopangwa.

Ni muhimu pia kukumbuka kwamba, utaratibu wa session ni tofauti na utaratibu wa kawaida wa kusikiliza mashauri ya kawaida. Leo session haijulikani itaanza lini, Lissu anaendelea kushikiliwa kwa siku 252 sasa na hakuna kesi inayoendelea.

Tatu, Kuhusiana na Maombi yake ya kuomba kuunganishwa kwenye kesi ya Mali za Chama. Mhe Lissu ameandika barua rasmi kwenda Mahakama kuu, kuifahamisha Mahakama kwamba atajiwakilisha yeye mwenyewe kwenye Maombi namba 28922/2025 , Tundu Antiohas Lissu dhidi ya Said Issa Mohamed & wenzake.

Katika barua hiyo, pamoja na taarifa hiyo ya kujiwakilisha, Mhe Lissu pia ameitarifu Mahakama iwe inampatia nyaraka na taarifa zote kuhusiana na shauri hilo yeye binafsi kupitia Mkuu wa Gereza Ukonga.

#she_is_not_my_president #tanzaniamassacre
#SAMIAMUUAJI
#SAMIAMUSTGO

HUYU HAPA
1766050001452.jpg
 
ANAANDIKA WAKILI GASTON GALUBINDI

UPDATE KUTOKA UKONGA GEREZANI DAY 252:

Leo nimemtembelea Mteja wangu Mhe Lissu, Ukonga Gerezani kujadiliana naye hatima ya kesi zinazomkabili, ashukuliwe Mungu kwa kuendelea kumjalia afya na siha njema kiongozi.

Gerezani kuna utaratibu mpya umeanzishwa ambao ni kinyume cha sheria, Nilichokutana nacho leo ni kama ifuatavyo;

Mosi, Nimeshindwa kutekeleza majukumu yangu kama wakili kutokana na Magereza kulazimisha mazungumzo yangu kama wakili na Mteja wangu Tundu Lissu yafanyike mbele ya Maafisa wa Magereza Ukonga wakisikiliza kinyume na Katiba ya nchi, Kinyume na sheria ya Magereza, Kinyume kanuni za Kimataifa, hivyo nimekataa kuzungumza na mteja zaidi ili tutafute kwanza haki ya usiri wa mazungumzo kati ya mawakili na mteja wetu.

Kwenye hili, Magereza wanafahamu misingi ya kazi, kitendo mnachofanya mnafahamu ni kinyume cha ibara ya 13 ya Katiba, Ni kinyume cha sheria za nchi kuhusu haki za wafungwa na Mahabusu, lakini mnafanya kwa makusudi. Ni lazima kuchukua hatua dhidi yenu.

Pili, Mheshimiwa Lissu aliandika barua kwa Naibu msajili wa Mahakama kuu, tarehe 5 December 2025 akitaka kufahamishwa tarehe rasmi ya session ya kesi ya uhaini inayomkabili pamoja na mwenendo wa kesi hadi ilipoishia. (Taarifa ya Mhe Lissu kuandika barua ilitolewa pia kwa umma) sasa Pamoja na kwamba aliandika barua tarehe 5, cha ajabu ni kwamba barua hizo zinaonekana zilifika Mahakamani tarehe 15 December 2025, yaani juzi Jumatatu.

Kwa mnaofahamu Jiografia ya Jiji la Dar Es Salaam kutoka ukonga hadi Mahakama kuu pale posta , imewachukua Magereza siku 10 kufikisha hiyo barua.

Itakumbukwa session ilipoahirishwa ilipaswa kuanzia November 3 na kukoma tarehe 11 November 2025, lakini hakuletwa Mahakamani hadi siku ya tarehe 11 na tangu siku hiyo hakuna tarehe rasmi iliyopangwa.

Ni muhimu pia kukumbuka kwamba, utaratibu wa session ni tofauti na utaratibu wa kawaida wa kusikiliza mashauri ya kawaida. Leo session haijulikani itaanza lini, Lissu anaendelea kushikiliwa kwa siku 252 sasa na hakuna kesi inayoendelea.

Tatu, Kuhusiana na Maombi yake ya kuomba kuunganishwa kwenye kesi ya Mali za Chama. Mhe Lissu ameandika barua rasmi kwenda Mahakama kuu, kuifahamisha Mahakama kwamba atajiwakilisha yeye mwenyewe kwenye Maombi namba 28922/2025 , Tundu Antiohas Lissu dhidi ya Said Issa Mohamed & wenzake.

Katika barua hiyo, pamoja na taarifa hiyo ya kujiwakilisha, Mhe Lissu pia ameitarifu Mahakama iwe inampatia nyaraka na taarifa zote kuhusiana na shauri hilo yeye binafsi kupitia Mkuu wa Gereza Ukonga.

#she_is_not_my_president #tanzaniamassacre
#SAMIAMUUAJI
#SAMIAMUSTGO

HUYU HAPA
View attachment 3517073
Samia anaroho mbaya kama ufupi wake
 
ANAANDIKA WAKILI GASTON GALUBINDI

UPDATE KUTOKA UKONGA GEREZANI DAY 252:

Leo nimemtembelea Mteja wangu Mhe Lissu, Ukonga Gerezani kujadiliana naye hatima ya kesi zinazomkabili, ashukuliwe Mungu kwa kuendelea kumjalia afya na siha njema kiongozi.

Gerezani kuna utaratibu mpya umeanzishwa ambao ni kinyume cha sheria, Nilichokutana nacho leo ni kama ifuatavyo;

Mosi, Nimeshindwa kutekeleza majukumu yangu kama wakili kutokana na Magereza kulazimisha mazungumzo yangu kama wakili na Mteja wangu Tundu Lissu yafanyike mbele ya Maafisa wa Magereza Ukonga wakisikiliza kinyume na Katiba ya nchi, Kinyume na sheria ya Magereza, Kinyume kanuni za Kimataifa, hivyo nimekataa kuzungumza na mteja zaidi ili tutafute kwanza haki ya usiri wa mazungumzo kati ya mawakili na mteja wetu.

Kwenye hili, Magereza wanafahamu misingi ya kazi, kitendo mnachofanya mnafahamu ni kinyume cha ibara ya 13 ya Katiba, Ni kinyume cha sheria za nchi kuhusu haki za wafungwa na Mahabusu, lakini mnafanya kwa makusudi. Ni lazima kuchukua hatua dhidi yenu.

Pili, Mheshimiwa Lissu aliandika barua kwa Naibu msajili wa Mahakama kuu, tarehe 5 December 2025 akitaka kufahamishwa tarehe rasmi ya session ya kesi ya uhaini inayomkabili pamoja na mwenendo wa kesi hadi ilipoishia. (Taarifa ya Mhe Lissu kuandika barua ilitolewa pia kwa umma) sasa Pamoja na kwamba aliandika barua tarehe 5, cha ajabu ni kwamba barua hizo zinaonekana zilifika Mahakamani tarehe 15 December 2025, yaani juzi Jumatatu.

Kwa mnaofahamu Jiografia ya Jiji la Dar Es Salaam kutoka ukonga hadi Mahakama kuu pale posta , imewachukua Magereza siku 10 kufikisha hiyo barua.

Itakumbukwa session ilipoahirishwa ilipaswa kuanzia November 3 na kukoma tarehe 11 November 2025, lakini hakuletwa Mahakamani hadi siku ya tarehe 11 na tangu siku hiyo hakuna tarehe rasmi iliyopangwa.

Ni muhimu pia kukumbuka kwamba, utaratibu wa session ni tofauti na utaratibu wa kawaida wa kusikiliza mashauri ya kawaida. Leo session haijulikani itaanza lini, Lissu anaendelea kushikiliwa kwa siku 252 sasa na hakuna kesi inayoendelea.

Tatu, Kuhusiana na Maombi yake ya kuomba kuunganishwa kwenye kesi ya Mali za Chama. Mhe Lissu ameandika barua rasmi kwenda Mahakama kuu, kuifahamisha Mahakama kwamba atajiwakilisha yeye mwenyewe kwenye Maombi namba 28922/2025 , Tundu Antiohas Lissu dhidi ya Said Issa Mohamed & wenzake.

Katika barua hiyo, pamoja na taarifa hiyo ya kujiwakilisha, Mhe Lissu pia ameitarifu Mahakama iwe inampatia nyaraka na taarifa zote kuhusiana na shauri hilo yeye binafsi kupitia Mkuu wa Gereza Ukonga.

#she_is_not_my_president #tanzaniamassacre
#SAMIAMUUAJI
#SAMIAMUSTGO

HUYU HAPA
View attachment 3517073
the puppet with his mercenary,
very nice photo :KasugaYeah:
 
Andika Wakili Paul Kisabo.
Jana Disemba 24, 2025, nilimtembelea Mhe. Tundu Lissu, katika Gereza la Ukonga, Dar es Salaam, na kufanya mazungumzo naye.

Kupitia mazungumzo hayo, Mhe. Lissu amewaomba Watanzania wote wapokee salamu za heri ya Krismasi na Mwaka Mpya 2026. Amesema kuwa tangu mwaka 2017 amekuwa na utaratibu wa kuandika na kutoa salamu za Krismasi na Mwaka Mpya kwa Watanzania, lakini mwaka huu ameshindwa kufanya hivyo kutokana na kuwa gerezani.

Aidha, Mhe. Lissu ameeleza kuwa tarehe kama ya leo mwaka 2002, siku ya mkesha wa Sikukuu ya Noeli, alikuwa mahabusu katika Kituo cha Polisi Dar es Salaam, akituhumiwa kwa kosa la uchochezi. Hiyo ilikuwa kesi yake ya kwanza ya jinai tangu aanze kutetea haki za binadamu.

Kumbukumbu hiyo imejirudia tena baada ya miaka 23, ambapo mwaka huu yupo gerezani, hii ni kumbukumbu nzito katika historia yake ya maisha na mapambano ya haki.
1766651817836.jpg
 
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Pwani Boniface Jacob (Boni Yai) amesema kuwa anaamini kuwa CHADEMA chini Mwenyekiti wake wa sasa ngazi ya taifa Tundu Lissu imeimarika na kupata ufuasi mkubwa ndani na nje ya chama hicho.

Boniface ameyasema hayo akizungumza kwenye mahojiano maalum na Jambo TV, Jumanne Desemba 23, 2025 hasa alipoulizwa swali lililoonekana kulenga kupata ulinganifu wa CHADEMA chini ya uenyekiti wa Freeman Mbowe na chini ya ya Lissu.

"Mbowe amefanya kazi nzuri sana ndani ya CHADEMA, kuijenga CHADEMA, kuitengeneza CHADEMA na kuieneza CHADEMA, na huwezi kuandika historia ya CHADEMA bila kumtaja Mbowe. Lakini nataka nikuhakikishie mwaka mmoja wa Lissu chama hakijarudishwa nyuma. Yaani mwaka mmoja wa Lissu chama kimepanda. Ukiniambia mimi kukubalika kwa CHADEMA nitakuambia kumeongezeka ndani ya mwaka mmoja huu. Kwa sababu gani? Kwanza wananchi wanapenda mtu anayejua kusimamia misimamo yake, hiyo obvious Lissu amefanikiwa", ameeleza Boniface.
FB_IMG_1766656767035.jpg
 
Wakati Tundu A. M. Lissu akiendelea kuzuiliwa kwa tuhuma za uhaini, amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti Mtendaji wa Umoja wa Kimataifa wa Demokrasia (IDU) - muungano wa kimataifa wa vyama vya kidemokrasia vya mrengo wa kati-na anamaliza 2025 huku jina lake likienezwa miongoni mwa watu wanaotarajiwa kuteuliwa kuwania Tuzo ya Amani ya Nobel. Wakati huo huo, wale waliohusika na kifungo chake wanakabiliwa na uchunguzi unaoongezeka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu. Nenda kwenye takwimu. Muda utasema. Ukweli na haki hatimaye vitatawala.
1766896677650.jpg
 
Back
Top Bottom