Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 371,881
- 861,451
- Thread starter
- #541
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo Oktoba 24, 2025
Jana tuliishia part 142 so leo tunaendelea na-;
Part 143
Mhe. Lissu ameingia.
Inapigwa courtttttttttt.
Watu wote wanasimama kwa heshima na nidhamu kubwa sana.
Majaji wanaingia na kutoa heshima.
Tunakaa wote chini.
Karani anasimama anasoma jalada hapa na namba ya kesi ya Uhaini.
Upande wa Jamuhuri anasimama Renatus Mkude anatambulisha jopo na anasema wapo tayari.
Anasimama Mhe. Lissu anasema pia yupo tayari.
Renatus Mkude anaieleza Mahakama kuwa mpaka sasa wameleta mashahidi watatu na ameendelea kueleza kuwa Mashahidi wengine wanatoka mkoani hivyo siku ya leo hawatakuwa na shahidi wanaomba kuahirisha shauri na kutokana na ratiba leo ilikuwa siku ya mwisho ya usikilizwaji mpaka itakapopangwa tena.
Mhe. Lissu anasimama na kusema yafuatayo:
Nimesikiliza maombi yaliyosemwa na wakili wa Serikali na ninaomba niseme yafuatayo:
Kwa kifupi leo wameweka mpira kwapani, naona tafakari yao ya jana haijazaa matunda yoyote, kesi imewashinda hii na imedoda kweli kweli kama tulivyoambiwa na Mh. Lissu jana kwamba kesi ilishaisha labda kama anashikiliwa kwa ajili ya Uchaguzi.
Kama Mashahidi Mapolisi ushahidi wao ndio hao mabodaboda waliowakuta vijiweni na kuwatengeneza kuwa walihamasika na maneno ya Lissu watakuja kusema kipi kipya? ngoja tuwasubiri, nafikiri baada ya tarehe 29 kutakuwa na sura tofauti kabisa ya kesi hii ngoja tuone.
Mh. Lissu sasa anaanza na yeye kutoa maelezo yake kuhusu ombi la Mawakili wa Serikali la kuahirisha kesi hii.
Jambo la kwanza sababu iliyotolewa ya kuomba ahirisho sio sababu ya msingi ya kuahirisha kesi.
Kesi hii yote inategemea vielelezo vilivyokataliwa na Mahakama kuu hakuna shitaka ambalo lipo nje ya hizo flash disk na memory card na yaliyomo, Hakuna.
Mashahidi wale ambao wanadaiwa wapewe ulinzi ushahidi wao ni walichoona mtandaoni, mashahidi wa polisi waliobaki ushahidi wao unatokana na yale yaliyodaiwa kuwa mtandaoni.
Mashahidi pekee na ushahidi wao hauuhusiani na mambo ya mtandaoni ni afisa wa uhamiaji aje aseme kwamba mm ni mtanzania ili iweje?
Mwingine ni yule anaekuja kusema nilienda JKT ili iweje? Ili wathibitishe nini??
Wakati kesi ni mambo yaliyokuwa mtandaoni, Kesi hii ilishaisha Waheshimiwa Majaji, maneno haya ya Mawakili wa Serikali ni maneno ya bure kabisa na kutaka kutupotezea muda tu.
Ombi hili ni la kurefusha shauri hili ili niendelee kukaa gerezani ili Uchaguzi Mkuu upite.
Hawawezi kuthibitisha chochote kwasababu flash disk na memory card vimekataliwa, hawana kesi hapa.
Waheshimiwa Majaji kama mtaona ni sawa sawa kuahirisha shauri hili naombeni nipate dhamana ya mahakama kuu kwa mujibu wa kifungu 302(3) cha CPA.
Mahakama inaweza kumuachia mshtakiwa kwa dhamana, mm siendi popote. Nitakuwepo tu mtaani.
Kwasababu ya maamuzi ya jana na juzi hamna kesi hapa kama mtaaamua kuahirisha nipewe dhamana ili nisiendelee kuteseka kwa kitu ambacho hakiendi popote nitakuwa tayari kesi iahirishwe katika mazingira hayo.
Leo ni siku ya 202 nipo gerezani ni miezi sita na nusu nipo gerezani kwa haya ambayo tumeyaona na kuyasikia kuna kesi gani hapa kama sio umbea na uoga wa Serikali kwa watu wanaowapinga?
Kwahiyo waheshimiwa Majaji Ombi lao likataliwe mkikubali nipewe dhamana ni sawa hilo halitakuwa na shida ya kuahirisha.
Sijawahi kukimbia kesi yoyote na wamenifungulia kesi nyingi tu.
Mimi sio mtu wa kukimbia kesi tena kesi zenyewe za uongo uongo wa hawa Mapolisi, nikimbie kwenda wapi, nitamalizana nao hapa hapa Mahakamani walipoamua kunileta.
Nimeshafanya kazi hiyo vizuri na sitakuja kuacha kuifanya ilimradi watanileta tena.
Ni hayo tu waheshimiwa Majaji kwa sasa.
Waheshimiwa majaji wanaandika na kujadili kidogo kilichosemwa.
Anasimama Renatus Mkude tumesikia reply ya mshtakiwa, hapa anajibu pingamizi la Mhe. Lissu.
Msingi ni kwamba hatuna shahidi kifungu cha 302 CPA
Part 144 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
Leo Oktoba 24, 2025
Jana tuliishia part 142 so leo tunaendelea na-;
Part 143
Mhe. Lissu ameingia.
Inapigwa courtttttttttt.
Watu wote wanasimama kwa heshima na nidhamu kubwa sana.
Majaji wanaingia na kutoa heshima.
Tunakaa wote chini.
Karani anasimama anasoma jalada hapa na namba ya kesi ya Uhaini.
Upande wa Jamuhuri anasimama Renatus Mkude anatambulisha jopo na anasema wapo tayari.
Anasimama Mhe. Lissu anasema pia yupo tayari.
Renatus Mkude anaieleza Mahakama kuwa mpaka sasa wameleta mashahidi watatu na ameendelea kueleza kuwa Mashahidi wengine wanatoka mkoani hivyo siku ya leo hawatakuwa na shahidi wanaomba kuahirisha shauri na kutokana na ratiba leo ilikuwa siku ya mwisho ya usikilizwaji mpaka itakapopangwa tena.
Mhe. Lissu anasimama na kusema yafuatayo:
Nimesikiliza maombi yaliyosemwa na wakili wa Serikali na ninaomba niseme yafuatayo:
Kwa kifupi leo wameweka mpira kwapani, naona tafakari yao ya jana haijazaa matunda yoyote, kesi imewashinda hii na imedoda kweli kweli kama tulivyoambiwa na Mh. Lissu jana kwamba kesi ilishaisha labda kama anashikiliwa kwa ajili ya Uchaguzi.
Kama Mashahidi Mapolisi ushahidi wao ndio hao mabodaboda waliowakuta vijiweni na kuwatengeneza kuwa walihamasika na maneno ya Lissu watakuja kusema kipi kipya? ngoja tuwasubiri, nafikiri baada ya tarehe 29 kutakuwa na sura tofauti kabisa ya kesi hii ngoja tuone.
Mh. Lissu sasa anaanza na yeye kutoa maelezo yake kuhusu ombi la Mawakili wa Serikali la kuahirisha kesi hii.
Jambo la kwanza sababu iliyotolewa ya kuomba ahirisho sio sababu ya msingi ya kuahirisha kesi.
Kesi hii yote inategemea vielelezo vilivyokataliwa na Mahakama kuu hakuna shitaka ambalo lipo nje ya hizo flash disk na memory card na yaliyomo, Hakuna.
Mashahidi wale ambao wanadaiwa wapewe ulinzi ushahidi wao ni walichoona mtandaoni, mashahidi wa polisi waliobaki ushahidi wao unatokana na yale yaliyodaiwa kuwa mtandaoni.
Mashahidi pekee na ushahidi wao hauuhusiani na mambo ya mtandaoni ni afisa wa uhamiaji aje aseme kwamba mm ni mtanzania ili iweje?
Mwingine ni yule anaekuja kusema nilienda JKT ili iweje? Ili wathibitishe nini??
Wakati kesi ni mambo yaliyokuwa mtandaoni, Kesi hii ilishaisha Waheshimiwa Majaji, maneno haya ya Mawakili wa Serikali ni maneno ya bure kabisa na kutaka kutupotezea muda tu.
Ombi hili ni la kurefusha shauri hili ili niendelee kukaa gerezani ili Uchaguzi Mkuu upite.
Hawawezi kuthibitisha chochote kwasababu flash disk na memory card vimekataliwa, hawana kesi hapa.
Waheshimiwa Majaji kama mtaona ni sawa sawa kuahirisha shauri hili naombeni nipate dhamana ya mahakama kuu kwa mujibu wa kifungu 302(3) cha CPA.
Mahakama inaweza kumuachia mshtakiwa kwa dhamana, mm siendi popote. Nitakuwepo tu mtaani.
Kwasababu ya maamuzi ya jana na juzi hamna kesi hapa kama mtaaamua kuahirisha nipewe dhamana ili nisiendelee kuteseka kwa kitu ambacho hakiendi popote nitakuwa tayari kesi iahirishwe katika mazingira hayo.
Leo ni siku ya 202 nipo gerezani ni miezi sita na nusu nipo gerezani kwa haya ambayo tumeyaona na kuyasikia kuna kesi gani hapa kama sio umbea na uoga wa Serikali kwa watu wanaowapinga?
Kwahiyo waheshimiwa Majaji Ombi lao likataliwe mkikubali nipewe dhamana ni sawa hilo halitakuwa na shida ya kuahirisha.
Sijawahi kukimbia kesi yoyote na wamenifungulia kesi nyingi tu.
Mimi sio mtu wa kukimbia kesi tena kesi zenyewe za uongo uongo wa hawa Mapolisi, nikimbie kwenda wapi, nitamalizana nao hapa hapa Mahakamani walipoamua kunileta.
Nimeshafanya kazi hiyo vizuri na sitakuja kuacha kuifanya ilimradi watanileta tena.
Ni hayo tu waheshimiwa Majaji kwa sasa.
Waheshimiwa majaji wanaandika na kujadili kidogo kilichosemwa.
Anasimama Renatus Mkude tumesikia reply ya mshtakiwa, hapa anajibu pingamizi la Mhe. Lissu.
Msingi ni kwamba hatuna shahidi kifungu cha 302 CPA
Part 144 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
