Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Mhe. Lissu: Mimi nashitakiwa kwa kuweka hiyo video huko Jambo Tv basi na mimi nitumie fursa kusema Mwenyezi MUNGU akurehemu na kukubariki sana maana kama mtaalamu umesema mimi sijaweka huko hiyo video nani mwingine atakuja kusema mimi niliweka hiyo video. Ahsante sana.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 141

Mhe. Lissu: Ulisema maneno ya kuwa msimamo wetu unaashiria uasi yaanzia dakika 8 kwenye video. Je hayo nayo yapo kwenye maelezo yako Polisi?

Samuel Kaaya : Hayapo.

Mhe. Lissu: Ulisema ukitumia Amped Authenticate inaweza kukusaidia ukajua camera iliyotumika kupiga hizo video?

Samuel Kaaya : Sahihi nilisema.

Mhe. Lissu: Je ulieleza hiyo camera uliyoitaja ilikuwa ni mali ya nani?

Samuel Kaaya : Sijaeleza ilikuwa ni mali ya nani?

Mhe. Lissu: Je umeeleza nani alikuwa anaitumia siku hiyo pale Mikocheni Makao makuu ya Chadema?

Samuel Kaaya : Sijui pia.

Mhe. Lissu: kwahiyo hujui aliyekuwa anapiga picha na aliyekuwa anaimiliki hiyo camera.

Samuel Kaaya : Sijui kiukweli.

Renatus Mkude: Anasimama Mh. Imefika saa saba na dakika tunaomba mapumnziko ya lisaa limoja.

Mhe. Lissu: Naomba niulize la mwisho tu halafu tukapumnzike.

Sasa shahidi swali la mwisho mtu ambae hana password wala username anaweza ku upload video kwenye ukurasa wa Jambo TV?

Samuel Kaaya : Akihuck anaweza kuingia.

Mhe. Lissu: Sasa kwenye mazingira ambayo hakuna Hacking tuhuma zinasema mimi ndio nimeupload hizo video kwenye mtandao wa Jambo TV. Tusaidie kwa ufahamu wako unaelewaje?

Samuel Kaaya : Hakuwa mtu anaweza kuingia kwenye mtandao wa mtu kama hana hizo credentials za kuingilia au ku hack ndio unaweza kuingia.

Mhe. Lissu: kwahiyo ni either una password, password creaker au unafanya Hacking?

Samuel Kaaya : Ni sahihi kabisa.

Mhe. Lissu ; Je mimi nina password?

Samuel Kaaya : Sijasema unazo na sijui pia.

Mhe. Lissu: Password creaker je?

Samuel Kaaya : Sijui na sijasema unayo..

Mhe. Lissu: Je nilifanya Hacking?

Samuel Kaaya : Hukufanya.

Mhe. Lissu: Waheshimiwa Majaji Tukale sasa.

Jaji anasema tutakutana baada ya lisaa limoja na nusu.

Turudi hapa saa nane na nusu.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali
 
Mhe. Lissu: Mimi nashitakiwa kwa kuweka hiyo video huko Jambo Tv basi na mimi nitumie fursa kusema Mwenyezi MUNGU akurehemu na kukubariki sana maana kama mtaalamu umesema mimi sijaweka huko hiyo video nani mwingine atakuja kusema mimi niliweka hiyo video. Ahsante sana.😂😂😂😂😂
Aisee huyu jamaa sheria anaijua! Sasa hao mashahidi waliobaki watakuja kusema nini, kama siyo kupoteza tu muda!

Vielelezo muhimu vimeondolewa! Mtaalam anasema hajui aliyeweka hiyo video youtube! Shahidi anaulizwa mambo ya kawaida kabisa, anajifanya hajui! Ni kama amelazimishwa tu kuja kutoa ushahidi!

Katika hili tukibali tu serikali inajidhalilisha sana.
 
Tukale kwanza mkuu!
Seafood ndio yenyewe
1761208569000.jpg
 
Aisee huyu jamaa sheria anaijua! Sasa hao mashahidi waliobaki watakuja kusema nini, kama siyo kupoteza tu muda!

Vielelezo muhimu vimeondolewa! Mtaalam anasema hajui aliyeweka hiyo video youtube! Shahidi anaulizwa mambo ya kawaida kabisa, anajifanya hajui! Ni kama amelazimishwa tu kuja kutoa ushahidi!

Katika hili tukibali tu serikali inajidhalilisha sana.
Waache wazidi kuumbuka
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 142

TumerudI Mahakamani.

Mawakili wa Serikali wanasema uwakailishi wao ni kama asubuhi.

Mhe. Lissu yuko tayari pia.

Anaendelea kumfanyia Cross-examination Samuel Elibariki Kaaya

Mhe. Lissu: Je umehesabu maswali uliyoulizwa na Wakili wa Serikali.

Samuel Kaaya : Sijui.

Mhe. Lissu: Maswali 165 umeulizwa unasemaje?

Samuel Kaaya : Sijui.

Mhe. Lissu: Majibu uliyotoa 112 HAYAPO kwenye maelezo yako ya Polisi unasemaje?

Samuel Kaaya : Sina uhakika.

Mhe. Lissu: Mambo ambayo hayapo kwenye maelezo yako polisi ni mengi sana unasemaje?

Samuel Kaaya : Sina la kusema.

Mhe. Lissu: Je ulitoa sababu kwanini hukuandika mambo hayo mengi kule Polisi?

Samuel Kaaya: Maelezo ni summary tu.

Mhe.Lissu: Umeelewa swali ? Nimekuuliza ulitoa sababu kwanini hukuandika mambo hayo Polisi?

Samuel Kaaya : Sikueleza.

Mhe. Lissu: Waeleze Majaji nani aliyeandika haya maelezo yako?

Samuel Kaaya : Nimeandika mimi.

Mhe. Lissu: Nani aliyekukanya kwamba ukisema uongo utashitakiwa?

Samuel Kaaya : Maeelezo ya shahidi hayana onyo.

Mhe. Lissu: Nani aliyekwambia maneno ya kwamba unapaswa kusema ukweli?

Samuel Kaaya : Niliandika Mwenyewe.

Mhe. Lissu: kuna mtu huwa anathibitisha maelezo yakiandikwa?

Samuel Kaaya : ndio.

Mhe.Lissu: Yako nani aliyathibitisha?

Samuel Kaaya : Mimi Mwenyewe.

Mhe. Lissu: Nani ananyewafundisheni Mapolisi namna ya kuandika haya maelezo?

Samuel Kaaya : Polisi wenzetu.

Mhe. Lissu: Unafahamu PGO?

Samuel Kaaya : Ndio nafahamu.

Mhe. Lissu: Mara ya mwisho ulisoma lini PGO?

Samuel Kaaya : Leo asubuhi.

Mhe. Lissu: Je hizi PGO zinakuruhusu wewe kujiandikia maelezo yako ya ushahidi?

Samuel Kaaya : Sijui.

Watu wanacheka.😀😀😀😀

Mhe. Lissu: Umeandika katika maelezo chini ya kifungu cha 10 cha CPA kwamba ndio uliandika hayo maelezo.

Samuel Kaaya : Ndio.

Mhe. Lissu: Hicho kifungu unajua kinasemaje? Je kinakuruhusu kujiandikia?

Samuel Kaaya : Mimi Sijui Sheria.

Mhe. Lissu: Wanasema mimi nilirusha live, nilikuwa mzungumzaji pia siku hiyo na pengine nilishika na camera kujichukua hizo video. Hivi hayo mambo yanawezekana kweli?

Samuel Kaaya : Hayawezekani.

Mhe. Lissu: Naishia hapo Jaji.

Wanaitwa Mawakili wa Serikali kwa ajili ya Rejoinder.

Anasimama Thawabu Issa na kumuuliza shahidi kuwa nina swali moja tu la ufafanuzi.

Kwanini maelezo yako ya Polisi yanatofautiana na ulichosema hapa Mahakamani?

Samuel Kaaya : Mimi sikuandika yote kwenye maelezo yangu kwasababu maelezo ni summary tu.

Mhe. Lissu : anasimama anasema hayo majibu ni mapya na sikusema aseme sababu kwahiyo majibu yake yasiingie.

Jaji anasema basi shahidi tunakuruhusu.

Anasimama Renatus Mkude na kusema tunaomba ahirisho hadi kesho saa tatu asubuhi lakini bado tunatafakari pia ruling za Mahakama.

Mhe. Lissu: Waheshimiwa Majaji naomba wakati wanaendelea na hizo tafakari zao pia wasiache kutafakari kama kweli bado kuna UMUHIMU WA KUENDELEA NA KESI HII baada ya Mahakama kutoa hizo ruling.

Jaji Ndunguru : Tunaahirisha shauri hadi kesho saa 3 asubuhi tukutane kesho basi naomba muwe watulivu wakati mnatoka Mahakamani.

Kwa leo tunaishia hapa so tukutane tena kesho saa tatu asubuhi kama kawaida.

Mungu awabariki sana.🙏🏻

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali
 
Aisee huyu jamaa sheria anaijua! Sasa hao mashahidi waliobaki watakuja kusema nini, kama siyo kupoteza tu muda!

Vielelezo muhimu vimeondolewa! Mtaalam anasema hajui aliyeweka hiyo video youtube! Shahidi anaulizwa mambo ya kawaida kabisa, anajifanya hajui! Ni kama amelazimishwa tu kuja kutoa ushahidi!

Katika hili tukibali tu serikali inajidhalilisha sana.
Hatari sana sheria imelala hapo, hate him or love him he is good
 
Hatari sana sheria imelala hapo, hate him or love him he is good
Tundu Lissu ni moto wa kuotea mbali!
Sasa mlinganishe na mtu kama Samia Suluhu Hassan!

Aaaah! hiyo ni kumwonea Samia.
Mimi naomba umlinganishe na mtu Kama Kabuti Kalamaganda, mtu mwenye mimacho kama chura!
 
Back
Top Bottom