Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 115

Anaendelea Shahidi namba 3 wa Jamhuri Samuel Elibariki Kaaya

Baada ya hilo kutokea nilienda maabara kwa ajili ya kuandaa vifaa vya uchunguzi.

Barua zote mbili tukianza na ile ya FB/PH/LAB/106/2025 Ilikuwa inahusu jalada la kuchunguza uchapishaji wa taarifa za uongo na lile lenye namba /PH/LAB/107/2025 ikiwa na kosa la uhaini.

Thawabu ; umesema baada ya kuwa assigned ulienda maabara, ieleze mahakama nini ulifanya nini?

Nilifika maabara na kufanya maandalizi ya vifaa vyangu vya uchunguzi.

Maandalizi niliyoyafanya ni kuandaa vifaa chunguzi kwa maana ya computer maalumu kwaajili ya uchunguzi.

Baada ya kumaliza kuandaa computer, printer kwaajili ya uchunguzi.

Tukumbuke kwamba nilikuwa na barua mbili ambazo nilikuwa assigned kuzifanyia kazi hivyo niliamua kusoma barua hizo ili kufaham matakwa ya requesting authority wanataka nini.

Mhe Jaji Barua moja ilikuwa inahusu kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni na nyingine ilikuwa inahusu uhaini.

Barua ya uhaini ilikuwa na kumbukumbu namba DA.223/476/01B/169.

Barua hiyo pamoja na muhtasari ilinihitaji kufanya mambo yafuatayo; ilihitaji chanzo cha picha mjongeo inayopatikana kwenye flash disk aina ya XIOXIA, kuchunguza uthibitisho wa uhalisia wa maudhui ya picha mjongeo iliyopo kwenye flash disk, nichunguze chanzo cha picha mjongeo iliyopo kwenye memory card.

Pia nichunguze uhalisia wa maudhui ya picha mjongeo iliyopo kwenye memory card aina ya Aldeepo, kufanya ulinganisho wa maudhui ya picha mjongeo iliyoko kwenye flash disk aina ya XIOXIA kama yanafanana na maudhui ya picha mjongeo iliyokuwepo kwenye memory card aina ya Aldeepo.

Kiuhalisia huyu shahidi anazungumza jambo hilo hilo moja na Wakili wa Serikali anarudia kuuliza swali hilo hilo mara tatu tatu mpaka mtu unaona uvivu kuandika.

Mfano hiyo habari ya video ilisema nini au Mh. Lissu alisema nini kwenye mazungumzo yake na watia nia kwa namna kesi inavyoenda hata sio tatizo na amekuwa hapingi kuwa maneno yale sio yakwake. Swali lake na hoja yake ni kwamba je hayo aliyosema ni kosa kisheria? Ni Uhaini?

Sasa hawa mashahidi watupotezea muda wa siku kadhaa kutuambia namna walivyochunguza video wakati hiyo video mtuhumiwa hana pingamizi nayo. Nafahamu zipo hatua za kisheria zinapaswa kufuatwa ili exhibits zipokelewe Mahakamani lakini kwa shahidi huyu nimewauliza hata Mawakili wanasema kwa kiasi kikubwa wanapoteza tu muda. Mengine hata sio matakwa ya kisheria.

Acha tuendelee nae na tunasubiri muda wa yeye kuanza kuulizwa maswali ya Dodoso na Mshitakiwa ndio tutaelewana zaidi.

Samuel Kaaya: Pia niliambiwa nichunguze maudhui yafuatayo kama yanapatikana kwenye flash disk hiyo, maudhui hayo ni haya;

"wanasema hivi msimamo huu unaashiria uasi, ni kweli kabisa maana tutazuia uchaguzi, hivyo tutahamasisha uasi, hiyo ndio namna ya kupata mabadiliko, tunaenda kukinukisha sana sana, uchaguzi huu tutauvuruga maana tunaenda kukinukisha vibaya sana."

Nilifanya uhakiki wa vifaa vya uchunguzi kwa maana ya computer maalumu kwaajili ya kufanyia uchunguzi huo, printer maalum aina ya Epson, nilikagua program endeshi kwa maana ya operating system window eleven, programu chunguzi kwa maana ya forensic software and security software amped five na ampend authenticate.

Waheshimiwa majaji naomba nieleze maana ya amped five na amped authenticate.

Ampend authenticate inafanya basic and advance image analysis, pia inafanya basic and advance video analysis pia inafanya utambuzi wa sura kwa maana ya facial recognition Waheshimiwa majaji nilitazama pia programu linzi kwa maana ya security software.

Hii programu linzi ni Kaspersky antivirus ambayo kazi yake ni kulinda programu endeshi pamoja na programu zote zilizopo kwenye computer hiyo na pia inalinda vielelezo unavyovipokea visiliwe na virus au malware.

Part 116 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 116

Anaendele Shahidi Samuel Elibariki Kaaya

Tunafanya huu uhakiki kwasababu programu endeshi ndiyo inayoendesha hardware computer, kwa maana nyingine kama programu linzi isipokuwa compatible / isipoendana na hardware kwa maana ya compute hiyo, it cannot execute any task.

Sambamba na hilo programu chunguzi lazima iwe compatible na programu endeshi ili iweze kufanya majukum yake mahususi.

Waheshimiwa majaji hali ya programu kwa siku hiyo ya tarehe 08/04 ilikuwa timilifu kwa maana programu zilikuwa updated/zilikuwa salama kwaajili ya kufanya majukumu yake mahususi.

Waheshimiwa majaji baada ya kufanya uhakiki wa vifaa nilifanya uchunguzi wangu wa awali kwa maana ya preliminary examination.

Nilifungua computer yangu maalum kwa maana ya kuiwasha, nilichukua flash disk aina ya XIOXIA kwaajili ya kuifanyia uchunguzi.

Baada ya kufungua computer yangu niliiweka kwenye universal serial bus (USB).

Baada ya kuiweka kwenye USB niliifungua ili kutazama kilichopo ndani ya flash.

Baada ya kuifungua nilikuta ina nywila yaani passwords hivyo niliwasiliana na mamlaka iliyoleta vielelezo kwa ajili ya kupata nywila.

Baada ya kupata nywila niliendelea na uchunguzi wangu wa awali na nilikutana na video mjongeo moja ilikuwa na heading Tundu Lissu uso kwa uso na watia nia majimboni, no reforms no election njia panda.

Na hiyo Video ilikuwa na urefu wa masaa matatu na dakika 38 na ilikuwa katika mfumo wa MP4 file format.

MP4 inatokana na neno MPEG part 14 (kirefu cha MPEG ni Movable Picture Expert Group).

Huyu Bwana Samweli Elibariki Kaaya nae miongoni mwa kitu anatufurahisha hapa Mahakamani ni kujifanya anapenda vingereza fulani kutaja misamiati yake ya kitaalamu.

Sasa anakosea sana kutamka hayo maneno Mh. Lissu kuna muda anauliza mara mbili mbili kuwa umetamka nini?

Akirudia anawaambia tamkeni vizuri jamani kingereza cha wapi hicho, Nafikiri kama Taifa hili swala la kizungu ni ugonjwa mkubwa, inafaa utafutiwe dawa halafu huu ugonjwa kwa mapolisi unaweza kuwa ni mkubwa sana kuliko makundi mengine yote. 😂😂😂

Thawabu Issa: Kingine nini uliona:

Shahidi: Waheshimiwa majaji pia niliona maudhui yafuatayo:

Wanasema hivi msimamo huu unaashiria uasi ni kweli maana tutazuia uchaguzi hivyo tutahamasisha uasi na hiyo ndio namna pekee ya kuapata mabadiliko, tunakwenda kukinukisha sana sana tunaenda kuuvuruga uchaguzi huu, tunaenda kukinukisha vibaya sana.

Waheshimiwa majaji maudhui haya yanapatikana kwenye lisaa la pili na dakika 58.

Pia nilibaini mwendelezo wa matukio kwa maana ya continuity, pia nilibaini jup shoot kwa maana ya kuwa hakukuwa na kukatika kwa picha.

Nilibaini pia necessary or unnecessary movements, kulikuwa na movement za watu mbalimbali au mtu mmoja mmoja kutoka sehemu moja Kwenda sehemu nyingine.

Nilibaini pia uwepo wa rangi halisi na mwanga halisi wa picha mjongeo.

Naomba nifafanue kuhusu rangi na mwanga halisi.

Waheshimiwa majaji unaporekodi picha au picha mjongeo kuna kitu kinaitwa white balance.

White balance kazi yake ni kuseti mwanga na rangi asili ya vitu vinavyorekodiwa.

Hii white balance ina component chache kwa ajili ya kufanya hayo.

Mfano kama unarekodi wakati wa mvua utaiseti camera yako kwenye cloud setting, kama ni kwenye kivuli utaseti camera yako kwenye shadow, kama ni majira ya kawaida ya jua utaseti kamera yako kwenye day.

White balance ilituonyesha kwamba video hii ina mwanga halisi.

Waheshimiwa majaji pia nilitazama mstari mshazari na ninaomba nizungumzie hapa ili pakae sawa.

Katika mizania ya informatics object near the length of the camera is much greator than the object far from the length of the camera.

Mfano mzuri ni mtu anapojipiga selfie, sehemu ya Kichwa itakuwa ni kubwa kuliko sehemu ya miguu ambayo iko mbali na camera.

Kwa maana hiyo waheshimiwa majaji focal length is the basic attribute in this fact.

Part 117 itaendelea kwenye post inayofuata

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 117

Thawabu: Shahidi uliona nini ulipotazama video uliyokuwa unachunguza kuhusiana na mstari mshazari?

Waheshimiwa majaji nilibaini uwepo wa mstari mshazari kwa maana kuwa picha mjongeo ile ilikuwa ni halisi.

Mwisho wa Ushahidi wa shahidi kuhusu uchunguzi wa awali, sasa anaingia uchunguzi wa kisayansi kuhusu picha mjongeo.

Shahidi anaulizwa baada ya kumaliza uchunguzi wa awali kumalizika ulifanya nini? Waheshimiwa majaji nilifanya uchunguzi wa kisayansi maana uchunguzi wa awali hauwezi kuthibitisha kila kitu.

Hii ni kwasababu huwezi kuthibitsha uchunguzi wa kisayansi kwa kutazama tu lazima uingie kwa ndani.

Katika kufanya uchunguzi wa kisayansi nilifungu application yangu ya amped authenticate nilienda sehemu imeandikwa file na kuna menu ndani inaitwa open, niliielekeza sehemu inayosomeka flash disk XIOXIA.

Niliifungua na baada ya kuiona niliihakiki then baada ya kufungua flash hiyo nili double click picha mjongeo hiyo iliyopo kwenye flash kwaajili ya kuivuta (to export) kwenye amped authenticate interface.

Amped authenticate interface ni pale ambapo the examiner anaweza kuiona video na kuifanyia uchunguzi.

Thawabu : ulifungua nini tuendelee.

Samweli: baada ya kufungua nili click baada ya kufungua nili double click picha mjongeo iliyopo kwenye flash kwa ajili ya kuivuta kwenye Amted Authenticate interface (kuivuta ni export)

Thawabu : Tuendelee

Samweli: Amted authenticate interface ni sehemu ambayo examiner anaweza kuiona video yake na kuifanyia uchunguzi.

Samweli: baada ya kufungua export video yangu nilianza uchunguzi wa kisayansi.

Thawabu: ambapo ulifanya nini?

Samweli: Nilienda moja kwa moja kwenye media info ambayo nini JSOM.

Lengo la kwenda hapo ni kutafuta info za picha mjongeo kwa maana ya meta data.

Baada ha kwenda kwenye JSOM Kutafuta data za kidigitali za picha mjongeo nili screenshot pia nilikuwa na police notebook kwa ajili ya kurekodi kila hatua ninayofanya

Thawabu: Ulichobaini hapo ni nini?

Baada ya kupata taarifa za kidigitali nilibaini picha mjongeo ninayochunguza ni picha iliyopakuliwa kwa maana ya downloaded

Picha iliyopakuliwa kwenye mtandao wa kijamii unaotokana na website au web inayotambulika kwa URL

Thawabu : URL ni ya mtandao gani?

Samweli: youtube

Thawabu: kitu gani kingine uliona?

Samweli: Niliona URL upload ilikuwa ni at jambo Tv.

Pia nilibaini viewers walioona walikuwa takribani 52,406 lakini pia niliona wafuasi kwa maana ya subscribers ambao ilikuwa jumla ya watu 1,010,000.

Pia niliona walio-like kwa maana ya kupenda hayo maudhui walikuwa 578, vingine nitavionyesha nitakapokuwa nawasilisha taarifa yangu ya uchunguzi.

Shahidi anamaliza kueleza kuhusu uchunguzi wa kisayansi sasa anaeleza hatua inayofuata ya clone analysis.

Shahidi anaulizwa baada ya kumaliza uchunguzi wa kisayansi alifanya nini?

Baada ya kumaliza uchunguzi wa kisayansi nilifanya clone analysis.

Waheshimiwa majaji hapa tunaangalia kama kuna pandikizi labda la sura ama sauti. Clone analysis may determine if there is a deep fake.

Waheshimiwa majaji kupitia hiyo menu ya clone analysis inayopatikana kwenye amped authenticate, hii inasaidia to identify sehemu ambazo zimepandikizwa na mtu akiwa anongea itakuwa inaonyesha mark mtu akiwa anaongea ila kwenye video itakuonyesha trace ya maungio kama mtu amevalishwa sura ya mtu mwingine. Mimi nilibaini kuwa picha mjongeo niliyoletewa haikuwa na pandikizi lolote.

Shahidi anamaliza kueleza kuhusu uchunguzi wa clone analysis sasa anaeleza hatua inayofuata ya noise analysis.

Thawabu: tupo kwenye hatua ya noise analysis hebu tuendelee.

Samweli: Kwa mantiki hiyo tunapofanya mambo ya noice analysis ni namna gani kinaweza ku affect hichi kitu kinaitwa pixel

Thawabu Issa: ulibaini kitu gani kwenye noise analysis na pixel?

Samweli: Picha hiyo mjongeo ilirekodiwa day time.

Part 118 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 118

Thawabu baada ya kubani picha ilirekodiwa mchana ni nini kingine ulibaini?

Samweli: Nilikuwa na note kwenye note book yangu nikaenda hatua inayofata.

Thawabu: Hatua gani hiyo ndugu shahidi?

Samweli: Baada ya hapo nilitoa flash yangu.

Thawabu: umeitoa wapi

Kuna muda wanaulizana vitu hadi mtu unasema hivi wana akili hawa.🤦🏾‍♀️

Samweli: Nilitoa kwenye USB port kwenye kompyuta yangu ya uchunguzi.

Samweli: Nilitoa memory card inayotakiwa kufanyiwa uchunguzi pia.

Waheshimiwa Majaji nilifungua software na kompyuta ilikuwa on nika export kama nilivyosema mwanzo.

Waheshimiwa naomba niwarudishe nyuma kidogo nisije nikawa naruka nilifanya uchunguzi wa Awali wa Memory card pia.

Thawabu: Ulifanya nini kwenye uchunguzi huo wa awali?

Samweli: Nilifungua memory card ili kujua kilichopo ndani baada ya kufungua nilibaini mambo yafuatayo:

Kuwepo kwa vipande 25 vya picha mjongeo.

Thawabu: Kingine ulichobaini ni nini?

Samweli: Vipande hivyo vilikuwa kwenye folder lililoandikwa stream.

Na pia Vipande hivyo vilikuwa named kuanzia namba 6 hadi 30.

Kipande namba 28 kilikuwa na maneno yafuatayo, wanasema hivi msimamo huu unaashiria uasi, kweli maana tutazuia uchaguzi tutahamasisha uasi hiyo ndio njia pekee ya kupata mabadiliko tunaenda kukinukisha sana sana uchaguzi huu tutauvuruga tunaenda kukinukisha vibaya sana.

Maudhui hayo yalipatikana dakika ya 8 na sekunde 27.

Waheshimiwa majaji pia niliona mwendelezo wa matukio kwa maana ya continuity, niliona necessary and unnecessary movement of the things, niliona mstari mshazari, pia niliona uwepo wa rangi halisi na mwanga halisi due to the presence of white balance.

Ni hayo tu waheshimiwa majaji nilibaini na niliandika kwenye notebook yangu.

Mwisho wa ushahidi wa shahidi kuhusu uchunguzi wa awali kuhusu picha mjongeo zilizo kwenye memory card.

Thawabu Issa: Shahidi anaulizwa baada ya kumaliza uchunguzi wa awali ulifanya nini?

Waheshimiwa majaji nilipita njia zilezile nilizosema awali nilifungua ampend authenticate nilifungua menu ya file na niliclick palipoandikwa open nak u export video moja baada ya nyingine.

Waheshimiwa majaji hapa nilikuwa na video clip 25 hivyo nilichukua video moja baada ya nyingine mpaka nilipomaliza uchunguzi wangu.

Nilianza na uchunguzi unaoitwa error level analysis na hapa tunaangalia compression or decompression ya video unayoifanyia analysis.

Hapa nilitazama v codec na a codec ili kutazama kama video iliongezwa sauti au video yenyewe. Nilibaini katika uchunguzi wangu kuwa video ilikuwa ni halisi.

Waheshimiwa majaji baada ya hapo nilifanya sensory pattern analysis kwa maana ya PRNU (kirefu chake ni Photo Response Non-Uniformity).

Katika uchunguzi wangu nilibaini kamera iliyotumika ni sony hxr-nx100 kupata picha mjongeo hizo.

Baada ya kubaini hivyo niliendelea na hatua inayofuata lakini naomba kueleza mheshimiwa jaji kwamba meta data inaweza kubainisha kifaa ulichotumia.

Waheshimiwa majaji pia nilifanya clone analysis na nilibaini kuwa hapakuwa na pandikizi lolote la picha mjongeo hiyo wala sauti.

Baada hapo nilifanya noise analysis na nilibaini picha mjongeo niliyokuwa naichunguza haikuwa na noise zilizosambaa.

Uchunguzi mwingine niliofanya ni illumination analysis hapa tunaangalia kiasi cha mwanga uliotumika wakati picha inarekodiwa kwa maana ya light balance, iso, iris or aperture na mwisho ni shut up speed.

Hii ilinisaidia kutambua kuwa pich hiyo ilirekodiwa na camera hivyo ni halisi.

Shahidi anamaliza maelezo kuhusu uchunguzi alioufanya na sasa anaeleza nini alifanya baada ya kumaliza uchunguzi.

Part 119 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba Repost yako.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 119

Shahidi sasa anaulizwa baada ya kuchunguza vielelezo hivyo viwili kwa maana ya flash disk na memory card alifanya nini? Anayemuuliza ni Wakili wa Serikali Thawabu Issa.

Shahidi anajibu kuwa waheshimiwa majaji nilianza kuandaa taarifa ya uchunguzi huo.

Taarifa ambayo ilijibu kile ambacho matakwa ya requesting authority ilitaka kufanyiwa.

Requesting authory walitaka kujua chanzo cha picha mjongeo iliyopo kwenye flash disk, lakini pia chanzo cha picha mjongeo iliyopo kwenye memory card, kingine kupata uthibitisho wa uhalisia wa maudhui yaliyokuwepo kwenye picha mjongeo iliyopo kwenye flash disk na uthibitisho wa uhalisia wa maudhui yaliyokuwepo kwenye picha mjongeo iliyopo kwenye memory card, ulinganisho wa uhalisia wa picha mjongeo iliyopo kwenye flash disk na iliyopo kwenye memory card, pia kutambua kama kuna uwepo wa maudhui yafuatayo;

Wanasema msimamo huu unaashiria uasi ni kweli kwasabbau tunakwenda kuzuia uchaguzi hivo tutahamasisha uasi hiyo ndio njia pekee ya kupata mabadiliko tutakinukisha sana sana uchaguzi huu tutauvuruga tutakinukisha vibaya sana.

Kulingana na maombi kutoka kwa requesting authority niliandaa ripoti nikijibu hayo niliyoombwa kuyachunguza majibu niliyoandaa ni kama yafuatayo.

Mh. Lissu anasimama na kupinga shahidi kuanza kuzungumzia ripoti kabla ya ripoti kuwa tendered mahakamani ikiwa hivyo ni sawa na kuingiza Ushahidi kwa mlango wa nyuma.

Wakili wa Serikali Thawabu Issa ameomba kuondoa hilo swali.

Baada ya kukamilisha kuandaa report uliandaa nini? Waheshimiwa majaji niliandaa covering letter kwaajili ya kuwajulisha requesting authority kuhusu majibu ya uchunguzi huo.

Baada ya kuandaa barua hiyo ilisainiwa na mnadhimu wa maabara ya uchunguzi kwaniaba ya kamishna wa uchunguzi wa sayansi ya jinai.

Barua pamoja na ripoti ya uchunguzi ziligongwa muhuri wa kamisheni.

Baada ya hapo nilisaini taarifa yangu ya uchunguzi na tulipaki vielelezo na taarifa ya uchunguzi.

Vielelezo niliweka katika bahasha na taarifa niliweka katika bahasha. Baada ya hapo nilisaini bahasha zile na kuandika majina yangu katika bahasha sambamba na hilo niliandika maelezo ya uchunguzi nilioufanya.

Bahasha niliiwekea lakiri / reference nyekundu.

Kwenye bahasha ya taarifa niliweka covering letter, ripoti na taarifa ya uchunguzi.

Baada ya kukamilisha hayo niliwasiliana na requesting authority hapa namaanisha ofisi ya Mkuu wa upelelezi kanda maalum ya Dar es Salaam.

Thawabu Issa: Sasa nini tena kiliendelea?

Shahidi anajibu hapa.

Siku hiyo ya tarehe 08/04/2025 Assistant Inspector Michael Gyumi alivifuata vielelezo hivyo;

Nilimkabidhi vielelezo akasaini kwenye dispatch book akasaini na akaondoka na vielelezo.

Nilimkabidhi taarifa ya uchunguzi ikiwa sambamba na meta data, vielelezo pamoja na maelezo yangu.

Ieleze Mahakama unawezaje kuitambua flash disk? Ilikuwa ni aina ya XIOXIA, ukubwa wa GB 8, alama ya stika ya kijani imeandikwa DM, ilikuwa attached na exhibit label PF 145.

Ndani yake kulikuwa na video yenye title Tundu Lissu uso kwa uso na watia nia, no reforms, no election njia panda.

Waheshimiwa majaji kuhusu memory card naweza kuitambua ilikuwa kwenye sd adaptor iliyopewa alama x, ilikuwa aina ya aldeepo na ilikuwa na ukubwa wa GB 32, ilikuwa na rangi nyekundu na nyeusi, ilikuwa na jumla ya vipande vya video 25

Wakili mkuu wa serikali Renatus Mkude amesimama kuomba health break.

Wakili mkuu wa serikali Renatus Mkude amesimama kuomba health break.

Mhe. Lissu anasimama na kusema waheshimiwa majaji sitaki kuwafundisha mawakili kumi na Jamhuri namna ya kuendesha kesi yao.

Lakini kwa hapa walipofikia wanaweza ku tender vielelezo vyao ili tukienda break wawe wameshamaliza zoezi la Kutenda vielelezo labda kama wana maelezo mengine lakini kwa hapa tulipofikia nafikiri wange tender vielelezo, hapa watu wanaongea kwa hisia naona Mawakili wa Serikali wanakubaliana na hoja ya Lissu.

Part 120 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 120

Wakili Mkude anajibu kuwa waheshimiwa majaji sisi tuko tayari kuendelea.

Jaji Ndunguru anasema anaomba tuendelee.

Wakili wa serikali Thawabu Issa anaendelea na ameomba kumuonyesha shahidi bahasha na kumuuliza bahasha hii unaifaham?

Samwel ; naifaham kwasababu ina alama ya lakiri ya evidence, kuna logo au nembo ya jeshi la polisi, kuna majina na saini yangu ndio vitu vinavyoweza kusaidia kuvitambua.

Kwenye bahasha niliweka flash disk ya KIOKSIA na memory card.

Thawabu : umeweza sasa kutazama hivyo vilivyokuwepo hapo waonyeshe majaji.

Shahidi anaanza kutambua vielelezo na amesema waheshimiwa majaji hii ni flashy aina ya KIOKSIA na SD adaptor ikiwa na memory card ndani yake na stika yenye alama ya X

Anamuonyesha Mhe. Lissu na hapa Lissu anasema hawezi kuona mbali kaletewa hiko kiflash chenye label ya kijani, kasogezewa karibu karibu kabisa anakitazama ili akihakiki.

Wameambatanisha na PF 145 shahidi anaendelea na anasema pia ilikuwa attached na exhibit label.

Thawabu: Shahidi ulisema kwamba kwenye flash disk kuna kitu kinachoweza kufanya uitambue zaidi maudhui yaliyokuweko kwenye picha mjongeo ya Tundu lissu uso kwa uso na watia nia majimboni ili uweze kuona hiko inabidi iweje?

Samuel: Nikipata laptop naweza tambua kwa kuangalia

Thawabu: kwenye memory kuna nini?

Samuel; Kuna vipande vya picha mjongeo viko 25 zimekuwa named namba 6 hadi 30.

Thawabu : Hivyo vitu ulivyovianisha viko ndani ya memory na flash disk sasa unaiomba nini mahakama ili uweze kuvitambua?

Samweli ; Waheshimiwa majaji naomba chombo niweze kuweka ili niweze kuvitambua.

Shahidi anasema anahitaji chombo (computer) aweze kungamua kilichopo ndani ya vile vyombo. 😀😀😀

Wakili wa Serikali Thawabu Issa anasema waheshimiwa majaji shahidi anaomba kifaa kama laptop ili aweze kuangalia na kutambua vielelezo hivyo.

Mhe. Lissu anasimama na kusema mawakili wa serikali wana laptop 6 apewe shahidi moja aangalie kielelezo chake na aseme kama amevitambua.

Laptop ya mahakama haiwezi kutumika kwasababu ili laptop ya mahakama itumike lazima kielelezo hicho kiwe tendered mahakamani.

Mahakama imekaa kimya kwa takribani kama dakika 10 hivi.

Naona majaji wanajadiliana hapa,

Jaji Ndunguru anasema kuwa kesi inaahirishwa hadi saa tisa kamili ili shahidi akalete laptop au kifaa cha kuweza kutumia kuitambua hichio kielelezo.

Tutarejea hapa saa tisa mchana

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 122

Anaendelea Mhe. Tundu Lissu ambae ni Lecturer wa Sheria kwa umma wa Watanzania.

Hakuna Chuo kitampa Darasa lakini watanzania tumeamua kumsikiliza kupitia kesi hii.

Lakini pia wanafunzi wa vyuo nao pia wameamua kumfuatilia kwa darasa lake hata kama hajaenda huko vyuoni kwao.😂

Anaendelea kusema:

Waheshimiwa Majaji Case ya pili ni Remina omary Vs R Criminal Appeal No. 189 of 2020.

Uamuzi huu waheshimiwa majaji was delivered on march 2022 (anasoma uamuzi huo.)

Waheshimiwa majaji kesi ya tatu DPP VS Sharif s/o Mohamed elias Athuman and 6 others criminal appeal no 74 of 2016.

Waheshimiwa majaji mtaona hiyo discussion inaanzina 4-8

Mahakama ya rufani imezungumza (When the Rome speaks, It is the end of discussion) mahakama ya rufani ikizungumza that is the end of discussion huo ndio unakuwa msimamo wa kisheria.

Nyaraka zote zinazotazamiwa kutumika wakati wa usikilizwaji zinatakiwa zisomwe au zionyeshwe kwenye mahakama ya ukabidhi.

Huo ndio msimamo wa kisheria hakuna wenge lingine linahitajika.

Waheshimiwa Majaji hiki hakikufanyika kwenye kesi hii ikiwa commital, it is too late hawawezi wakakiingiza sasa hivi.

Huko ni kutanguliza mkokoteni mbele halafu farasi yuko nyuma ukitegemea huyo farasi auvute mkokoteni kuelekea mbele, haiwezekani.

Hiyo ni sababu ya kwanza na yenyewe peke yake inatosha kujibu swali la vitu hivi viingie au visiingie lakini sio sababu pekee Waheshimiwa Majaji.

Sababu ya pili ni kwamba:

Hivi vinavyotakiwa viingizwe kama vielelezo vimeletwa pre mature:

Huyu shahidi anaeleta vielelezo hivi sio shahidi wa kawaida yeye ni mtaalamu ambae ameiambia Mahakama kwamba alifanya uchunguzi wa kisayansi
Juu ya authenticity ya vielelezo na ameeleza tangu jana na ameandika ripoti ya uchunguzi wake wa kitaalamu. Hatujasema sisi hayo amesema mwenyewe.

Sasa waheshimiwa Majaji kati ya ripoti ya kitaalamu juu ya jambo lenyewe na jambo lenyewe (which comes first) taarifa yake ya kitaalamu na hizi video lipi lianze?

Unaanza kuoga ndio upake mafuta au unapaka mafuta ndio uoge? Ripoti ya kitaalamu ilitakiwa kusafisha njia ili baadae haya mengine kufanyika.

Na labda nielezee kidogo ufafanuzi wa Kesi ya pili ni ya Remina Omary Abdul versus Republic Criminal Appeal No 189 of 2020 CAT Dar es Salaam delivered 11th February and 15th March 2022.

Waheshimiwa majaji mtakaposoma mtaona imekazia kuwa documents ambazo hazikuonyeshwa wakati wa committal cannot be admitted in a trial.

Kesi ya tatu pia niliyoieleza ya CAT, DPP versus Sharif S/O Mohamed Athuman na wenzake 6, Criminal No 74 of 2016 Arusha delivered on 3rd and 5th August 2016.

The Court of Appeal has spoken kama nilivyotoa mfano wa wakatoliki hapo awali kuwa when rome speaks that’s the end of the discussion, when the Court of appeal speaks that’s the end of the discussion as per that point of the law.

Mahakama ya rufani ikisema huu ndio msimamo ndio unakuwa msimamo wa kisheria. Nyaraka zote zinazotumika kwenye kesi mahakama kuu inatakiwa zionyeshwe kwenye Mahakama ya ukabidhi

Sasa waheshimiwa Majaji hili halikufanyika kwenye kesi hii kinachotakiwa kitolewe Ushahidi kwenye kesi hii leo hakikutolewa kwenye mahakama ya ukabidhi na hawawezi kukiingiza sasahivi.

Mambo haya lazima tuyaeleze kwa uzuri na kwa msisitizo wenzetu wayaelewe. Muda mwingine huwa ni mambo magumu sana kwao kuyaelewa lakini ni vitu ambavyo kama kweli umefika shule na kuhudhuria madarasa vizuri ya sheria unapaswa kuwa unavifahamu kwa uwazi kabisa.

Na naomba pia nikazie hapo kwenye utaalamu wa shahidi:

Ameiambia Mahakama kwamba alifanya uchunguzi wa kitaalamu wa kisayansi juu ya aunthenticity ya hizi videos na ameonyesha extensively tangu jana na ameandika report juu ya utalamu wake.

Part 123 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 123

Sasa waheshimiwa Majaji kati ya report ya kitaalamu na jambo lenyewe what comes first kati ya object itself na taarifa ya kitaalamu?

Nimeeleza kinagaubaga sitaki kurudia sana ila msisitizo wangu ni kwamba kipi kinacho tangulia kati ya taarifa yake ya kitaalamu na hizi videos.

Inabidi mfikirie waheshimiwa kama report yake ikija baadae isikubaliwe halafu tuwe tumekubali hivi vifaa.

Sasa waheshimiwa majaji kwa maoni yangu kilichotakiwa kitangulie ni taarifa ya uchunguzi wa kitaalamu kama report ya kitaalamu ikikubaliwa then its almost automatic kuwa vitu vilivyochunguzwa vitakubaliwa.

Kinachofungua mlango wa kuingiza vielelezo ni ripoti ambayo shahidi aliandika, na kama sikosei shahidi amesema anayo.

Kama report ikiwa admitted videos nazo zitakuwa admitted sababu zitakuwa zimefanyiwa uchunguzi wa kitaalamu na zimepass hio test.

Waheshimiwa Majaji nawaalikeni na kusisitiza muangalie vifungu vya sheria ya Mwenendo wa Jinai kama hii kwa ajili ya ushahidi wa wataalamu nilivyosema;

Kifungu 216 cha CPA kinahusu Ushahidi wa kitalamu wa picha.
217, Government analyst, 218 Ushahidi wa Fingerprint expert, 219 Uchunguzi wa handwriting expert na 220 Ushahidi wa shahidi wa cyber forensic science kama huyu.

Waheshimiwa Majaji hivyo vifungu vinne vinavyofuatana vinashare kitu kimoja ambacho ni kama report ya huyo mtaalam ikikubaliwa mahakamani huo ndio Ushahidi na vingine vyote vinavyokuja vitakubaliwa.

Vifungu vya 216(1), 217(1), 218(1) all provide for the same thing
Kuwa report hio ikipokelewa mahakamani na vitu hivyo vitapokelewa pia.

Waheshimiwa majaji kilichotakiwa kitangulie ni taarifa aliyoiandika ili tujue kweli hizo video zimefanyiwa uchunguzi wa kitaalamu na ripoti yenyewe ndio Ushahidi, kwasabu hawajafanya hivyo, hichi kielelezo kisipokelewe.

Nimeeleza kwa kirefu na kusisitiza nafikiri yameeleweka vizuri sana.

Anaendelea Mh. Tundu Lissu na sababu ya tatu:

Hii inamuhusu shahidi mwenyewe.

Je huyu shahidi ana uwezo kisheria wa kuleta taarifa au vielelezo hivi? Ana huo uwezo kisheria?

Nilisema mwanzoni huyu sio shahidi wa kawaida yeye ni mtaalamu yeye ndio amefanya uchunguzi wa kitaalamu.

Sasa waheshimiwa Majaji vifungu husika ni vile vile nilivyotaja mwanzoni na nitaongeza kifungu na 221 cha CPA.

Hivyo vifungu vimeweka masharti kwamba watu wanaoweza kuleta ushahidi wa kitaalamu ni ushahidi wa picha kifungu cha 216 CPA ( picha za mnato)

Anaeweza kuleta ushahidi wa kitaalamu ni government chemist Sect. 217 CPA

Wataalamu wa finger print under 218 CPA

Handwriting experts under 219.

Wa mwisho ni cyber expert anaweza kuleta ushahidi under 220 CPA

Sasa waheshimiwa wataalamu wote niliowataja wanatakiwa wateuliwe na Mkurugenzi wa mashitaka under 221 na watangazwe kwenye Gazeti la Serikali.

Lazima wateuliwe na DPP na uteuzi wao uwe gazetted huo ndio utaratibu wa kisheria.

Sasa waheshimiwa Majaji kuna kitu shahidi huyu hakukisema na hicho ambacho hakukisema waheshimiwa Majaji mtakiona katika maelezo yake shahidi ambayo anasema aliyaandika na katika maelezo yake ya kitaalamu ambayo anasema aliyaandika.

Ambacho hajakisema ni kuwa yeye ni kuwa aliteuliwa na kuthibitishwa kwenye gazeti la serikali 799 of 2020.

Sasa naomba nianze na GN 799 of 15th September 2020, wahe Majaji hilo gazeti la serikali linaitwa The Criminal Procedure (appointment) for officers for processing photographic print and enlargement Order hii ndo GN iliompa shahidi mamlaka ya kufanya kazi alioifanya kama shahidi.

Waheshimiwa Majaji Paragraph 2 inasema the persons whose names appear in the schedule says:

Maafisa waliotajwa kwenye nyongeza wameteuliwa kufanya hizo shughuli na kuna watu 7 walioteuliwa na namba 5 kwenye hio list ya maafisa tajwa ni H 6108 D/C Samwel Elibariki Kaaya (PW3).

Part 124 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 124

Hio GN ndo iliyomthibitisha kama mtaalamu wa picha na anaetakiwa kuandaa ripoti ya uchunguzi kisheria.

Huyu ni mtaalamu wa picha za mnato au karatasi kisemo cha Mhe. Lissu pia proof ni kifungu cha sheria kilichotumika kumteua, ambacho amekitaja mwenyewe ambacho ni kifungu cha 216(1) cha Sheria Ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (2023) utaiona kwenye maelezo yake na pia kwenye Order ya Uteuzi wake.

Kwahiyo ni fundi wa picha za kawaida
kwenye sheria pia wanasema ateuliwe na DPP na ukisoma order hii aliofanya uteuzi ni AG badala ya DPP.

Kasheshe tayari hapa ni kama maji yamelowana na moto umeungua tena.😂

Uteuzi huu umefanywa na Adelardus Kilangi inatosha kabisa kubatilisha kila kitu alichofanya.

Anachosema hapa huyu sio mtaalamu wa chochote kwa mujibu wa hii order ambayo anasema yeye mwenyewe ameteuliwa, ni sababu mamlaka ya uteuzi sio mamlaka halali.

Katuga anashusha kamiwani hapa akitafakari utadhani amebanwa na mlango, mawakili wa Serikali kazini kwao kuna kazi sana aiseee.

Waheshimiwa Majaji, sihitaji kupoteza muda mrefu wakusema kwamba DPP na AG ni ofisi mbili tofauti zenye mamlaka mbili tofauti na sheria zinazogovern exercise zao of power ni mbili tofauti.

AG ana sheria yake inaitwa Office of AG dischare of duties act sura ya 278 na DPP sheria yake ni NPS ACT SURA YA 430.

Ofisi mbili za Kikatiba tofauti, mamlaka tofauti na sheria tofauti, AG hana mamlaka yoyote kwenye mashauri ya Jinai. Kiherehere hiki kimetokea wapi?

Sasa waheshimiwa Majaji what about ile GN alioitaja jana maana nimeisema ambayo hakuitaja, alietaja jana ilikuwa iko kwenye nyaraka zake akastuka akasema eeh huyu mtuhumiwa anaesoma kila kitu huyu…eeh.. ataniletea shida huko mbele nikienda kuchwakichwa.

What about GN NO 745 16TH December 2022?

Hii nayo imetungwa kwa Kifungu kilekile cha sheria ya CPA.

Mhe. Lissu anakisoma hapa ili aendelee kushusha nondo.

Mahakama imetulia sana watu wako kama wanasubiri kuchomwa na Sindano kuna kautulivu kakubwa sana ka kusikiliza hizi nondo.😂

Waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu.

Amri hii imesainiwa Dodoma Tar. 28/10/2022 na Sylivester Anthony Mwakitalu, Mkurugenzi wa Mashtaka.

Na waheshimiwa Majaji katika jedwali lililoambatanishwa lina majina ya maafisa 184 na mtu wa 182 ni H6108 D/C Samweli Eliariki Kaaya, imeandikwa Eliarikis sio Elibariki lakini waheshimiwa majaji niko tayari kusema labda walimaanisha ni huyu shahidi Samweli Elibariki Kaaya.

Hata hivyo waheshimiwa majaji kwa mujibu wa Tangazo hilo la Serikali huyu ni mtaalam wa picha (still pictures) sio forensic expert. Hayo mamlaka hana.

Waheshimiwa majaji, mtu asiyekuwa na utaalamu wa mambo ya videos na ameandaa ripoti ya kitaalamu na anataka kuiwasilisha mahakamani, anawezaje kuruhusiwa kuwasilisha chochote cha kitaalamu?

Sio mtaalamu wa cyber, sio mtaalamu wa videos, hajateuliwa kwenye kazi hiyo. Tukisema amekuja kufanya umbea tutakuwa tunakosea? 😂😂

Waheshimiwa Majaji nawaalikeni mkaangalia ripoti ya Tume ya Kuangalia Jinsi ya Kubooresha Taasisi za Haki Jinai Nchini ya Julai 2023 maarufu kama Tume ya Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman.

Waheshimiwa Majaji pengine sitakosea nikisema kuwa wakili wa serikali Mkuu Ignas Mwinuka alikuwa mjumbe kwenye hii tume, ameandikwaa huyu hapa (Mahakama kichekoo 😂 Mhe. Lissu anasema ni sifa maana wangapi wanateuliwa katika Tume kama hizi).

Waheshimiwa majaji nawaalika ukurasa wa 58 ambapo inasema hivi Tume imebaini kuwa weledi umepungua kwasababu askari wanapangiwa mambo wasiokuwa na taaluma nayo kama hili.

Mahakama kicheko.😂😂

Kinachoendelea hapa Mahakamani ni zile story za unasikia utamu hapohapo unasikia uchungu. 😂

Kuna Muda unapata hasira ukisikia haya mambo halafu ukimaliza unaanza kucheka tena hapo hapo.

Kwamba Mapolisi wanapangiwa majukumu ambayo hawana sifa nayo kuna muda wanalaumiwa kwenye mambo ambayo hawakutakiwa kupangiwa.

Part 125 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 125

Kwahiyo kwa kumalizia hoja hiyo ni kwamba shahidi huyu hana Competence ya kutoa hii nyaraka hapa Mahakamani.

Sababu ya nne ni Chain of custody.

Msingi wa hoja hii ni kesi maarufu ya Paulo Maduka na Wenzake 4 vs R Criminal Appeal No. 110 of 2007.

Ushahidi wa aina hii unahitaji uoneshwe kwamba kutoka mahali ulikoanzia mpaka unaletwa Mahakamani.

Kukiwa na break of chain of custody ushahidi haupokelewi.

Shahidi anasema kwenye ushahidi wake aliletewa hizo video na Michael gyumi.

Michael Gyumi alizitoa wapi??

Nakumbuka shahidi wa kwanza alisema ile memory card ilitokea Dodoma kwa mtu anaitwa P akaletewa Andrew churu na alisema kulikuwa na hati ya makabidhiano.

Hiyo hati ya makabidhiano mlileta mahakamani?

Andrew churu alimkabidhi peter Malugala

PW2 John kaaya akasema alimkabidhi Peter Malugala na alijaza PF 45 there is no documentation maana mashahidi hawajaleta hata moja.

Sasa Waheshimiwa kutokana na kesi tajwa hapo juu.

Chain of custody must always be maintained hawa Mapolisi wamemaintain kitu gani? Hakuna lolote.

Hiyo kesi niliyosema ya Paul Maduka

Maana yake ni kwamba Ushahidi wa aina hii unahitaji uonyeshwe kutoka mahali ulipoanzia paka kuletwa mahakamani unahitaji uthibitisho wa kinyaraka umepitia kwenye mikono gani.

Kesi hiyo ya Paul Maduka page 18 to 19 Mr Justice Edwin Rutakangwa anasema kapiga kiingereza hapa kuwa huo mlolongo inabidi usivunjike.

Kwahiyo Waheshimiwa Mahakama ya rufani baada ya Paul Maduka chain of custody should always be maintained it should not be broken.

Waheshimiwa Majaji hata PGO zimesisitiza hilo, Waheshimiwa majaji PGO 229 paragraph 8 inazungumzia Chain of Custody.

Na waheshimiwa Majaji nitawasomea inasema anaanza kusoma hapa anajaribu kuelezea umuhimu wa chain of custody hapa kwamba lazima ionyeshwe kuwa mlolongo wa kupokea kielelzo haujavunjwa au kielelezo kubadilishwa hapa.

Mhe. Lissu anasema kama hakuna chain of custody hakuna Ushahidi wa kuingizwa mahakamani kama hawajaestablish chain of custody hivyo ni rai yangu kuwa msikubali hizi video ziingie kama vielelezo katika mahakama yenu.

Mhe. Lissu amemaliza hivyo ni zamu ya Jamhuri kujibu sasa.

Ni kama wamechanganyikiwa hawaeleweki nani ajibu au wanataka kufanya nini? 😂

Wakili wa Serikali Mkuu Renatus Mkude anasimama na kujibu kuwa wako tayari kujibu hoja za Mh. Lissu lakini watatumia two hours. Majaji wanauliza hiyo two hours unamaanisha nini? 😂😂

Anajibu Wakili Mkude kuwa ni kutokana na hoja za Mshtakiwa alizosema lakini pia shahidi huyo ndo wa muhimu katika mzizi wa kesi hii.

Hivyo tunaomba two hours ili tusilipue katika kuisaidia Mahakama.

Kama itawapendeza tukaahirisha mpaka Jumatatu ni sawa pia Waheshimiwa Majaji.

Mhe. Jaji Ndunguru anasema,

Sasa sikiliza Wakili wa Serikali kimsingi tumeelewa uliposema tu habari ya masaa mawili ulimaanisha unaomba ahirisho hadi Jumatatu.

Mahakama kichekooo 😂😂😂😂

Kumbe hata Majaji wanajua janja janja za Mawakili wa Serikali.

Shauri linaahirishwa hadi Jumatatu saa tatu kamili asubuhi ambayo itakuwa ni Tarehe 20/10/2025.

Tukutane Jumatatu wapendwa,

Sasa ngoja nikanywe wine kidogo nikiwa nakusanya hizo nguvu za Jumatatu.

Mungu awabariki sana.
 
Dan😪😪😪🤔😭
1760718053706.jpg
 
Ilisahaulika kwenye list

#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 121

Tunaendelea na kutolewa kwa ushahidi.

Muda huu saa tisa mchana

Mhe. Lissu tayari ameingia

Inapigwa high Court waheshimiwa majaji wanaingia watu wote wanasimama.

Ukimya umetawala hata nzi akipita unasikia sauti yake.😂

Anasimama wakili wa Serikali Mkude Simba anasema coram ni ile ile na wapo tayari kuendelea. Huyo Wakili wa Serikali anaitwa Renatus Mkude.

Mhe. Lissu anasimama anasema yupo tayari kuendelea pia na yeye.

Shahidi anakumbushwa yupo kwenye kiapo.

Thawabu Issa: Kabla ya ahirisho uliomba muda wa kufata kifaa kinachoweza kukusaidia kuchezesha video hizo tuendelee hapo sasa.

Samweli: Waheshimiwa naomba nianze na flash disk ili kutambua content zilizopo waheshimiwa majaji nimeitambua video mjongeo.

Anawaonyesha majaji kupitia kompyuta yake sijui katoa wapi ka computer kenyewe kadogo hivi.😂

Mhe. Lissu na yeye anapelekewa ili aweze kuona ameshindwa kuona maana kompyuta nayo inacheza, cheza

Thawabu: Wakili wa serikali anaomba shahidi abebe kompyuta yake ili aweze kumuonyesha Mhe. Lissu maana watu wengine wakishika inahama.

Computer za Polisi utafikiri ni mali ya mganga wa kienyeji. Akishika mtu mwingine inazima akishika yeye haizimi.😂

Video clip zilikuwa 25 hapa anaongelea memory card anawaonyesha majaji.

Anatoka kwenda kumuonyesha Mhe. Lissu

Waheshimiwa majaji wanaandika kidogo hapa.

Thawabu Issa: Kuhusu vielelezo umetuonyesha flash disk, memory card na umetambua video iliyopo kwenye flash na video 25 unataka mahakama ifanye nini?

Samweli Elibariki Kaaya anajibu: Naomba mahakama ipokee vielelezo hivi kama sehemu ya ushahidi.

Thawabu Issa: Anamuuliza vielelezo kama nini?

Shahidi anajibu: Ni flash disk XIOXIA na memory card yenye alama x

Vikiwa na nini kwahiyo shahidi?

Shahidi anajibu vikiwa na PF 145 na flash disk yenye picha mjongeo na memory card.

Mhe lissu. Anasimama anasema anapinga kupokelewa kwa vielelezo hivyo nina sababu nne.

Sababu ya kwanza ni kwamba hivyo sijui niviite nini havijawa vielelezo kwa sasa...😂

Hivyo vitu havikuonyeshwa wakati wa commital proceedings.

Kifungu husika cha sheria 263 cha CPA marejeo ya 2023

Anasoma kifungu hapa kwa kingereza kilichonyooka.

Mhe. Lissu akiongea kingereza unaweza fikiri kazaliwa wapi sijui kumbe ni Kijiji cha Mahambe Ikungi huko, Singida 😂

Anaendelea mshtakiwa akiwa anapelekwa commital anasomewa ushahidi na vielelezo vingine ambavyo vinatarajiwa kutolewa wakati wa usikilizaji wa kesi.

Waheshimiwa majaji taarifa kutoka kwa mahakama kabidhi kwenye ukurasa wa kwanza kabisa inasomeka statement of witnesses 1-30.

Na maelezo hayo waheshimiwa majaji yameambatanishwa na yamesomwa yote kisutu

Baada ya hiyo orodha ya maelezo ya mashahidi kuna maelezo ya documentary exhibit zimeorodheshwa pale zipo tisa ( anazisoma) na document zote hizo pamoja zipo listed hazikusowa.

Sasa waheshimiwa majaji kinachozungumziwa hapa ni video namba 8 na 9 (anasoma kwenye orodha)

Zimezungumzwa sana hizi video zote mbili hazikuonyeshwa kisutu.

Waheshimiwa majaji baada ya orodha ya documentary exhibit kuna orodha ya physical exhibit ambazo ni flash disk na memory card hazikuonyeshwa kisutu.

Sasa waheshimiwa Majaji kile ambacho kilitakiwa kisomwe au kuonyeshwa kwenye commital court hakiwezi kuonyeshwa wala kuingia kwenye trial court.

Waheshimiwa majaji msimamo huo umewekwa katika case Musa ramadhani magae Vs Republic Criminal Appeal 545 Of 2021 judgement was delivered on April 2023.

Waheshimiwa majaji hiyo hukumu ya mahakama ya rufani sehemu kubwa inajadili swala hili effects ya kutokusoma maelezo hayo kwenye commital court

Katika kurasa 20 za hukumu kurasa 14 zinaelezea effects yake ni nini

Mahakama imesema ushahidi huo hauwezi ukakubaliwa kabisa.

Part 122 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Leo Oktoba 20, 2025

Last time tuliishia part 125, leo tunaendelea na -:

Part 126

Imepigwa high court,

Majaji wameingia, wapo watatu kama kawaida yao.

Mhe. Lissu nae ameingia,

Jaji anamwambia Karani tuendelee.

Karani anasoma namba ya kesi na anasimama Renatus Mkude kutambulisha jopo la Mawakili wa Serikali na kusema wako tayari kufanya Reply Submission kwenye lile pingamizi la Mshitakiwa.

Ataanza Nasoro Katuga Kujibu.

Nasoro Katuga Mshitakiwa katika hoja yake ya kwanza anasema visipokelewe kwasababu vina contravene kifungu cha 263(2) cha CPA.

Maelezo ya mashahidi na hati ya mashitaka na vielelezo vyote vilivyowasilishwa na DPP visomwe na kutafsiriwa ndo sheria inasema hivyo na vielelezo vinavyotaka kutolewa na flash yenye video ambayo iko katika mfumo wa kielektroniki.

Kifungu cha 3 cha Evidenece Act Cap. 6 kinatafsiri nyaraka ikiwemeo huu uliopo kwenye flash disk kwahiyo video anazotaka kutoa shahidi ni document pia.

Kwahiyo kile kifungu cha 263 nikichosema cha CPA nyaraka hizi zilipaswa zionyeshwe kule kwenye committal Court since they are documents as per the law.

Kama nyaraka hizi zilisomwa au hazikusomwa nyaraka hizi: Mahakama itajiridhisha kupitia proceedings zilizopo mahakamani na sio maelezo ambayo hayako chini ya kiapo.

Vielelezo hivyo havikusomwa mshitakiwa alisema hivy sisi tulishitushwa kwasababu tulikuwepo, mtu anayejitetea anaweza kutumia hata uongo.

Naomba niwaalike kwenye ukurasa wa 92 na 93 wa committal proceedings ambao unasema nini kilitokea.

Kurasa hizo zinasema, mahakama ilimnukuu wakili wa serikali akivitaja vielelezo.

Vilisomwa na kuchezwa vielelezo hivyo, vimeandikwa pia kwenye proceedings za Mahakama.

Baada ya kuchezeshwa na kusomewa vielelezo, ukurasa wa 97 mshitakiwa anasema hayo maneno kwenye vielelezo nimeyasema kwenye mikutano ya hadhara na ni maneno yangu.

Mahakama ni binadamu inasikia, alisema hana shida navyo lakini anasema havijasomwa.

Naialika mahakama iziamini records.

Naomba nichomekee. Kwa mara ya kwanza nimeshuhudia mtu akiongea uongo Mahakamani akizungumzia tukio ambalo mimi mwenyewe nilikuwepo na kushuhudia. Ukweli wa Mungu zile video hazikuchezwa pale Mahakamani ndo maana hata Mh. Lissu anatikisa kichwa kumsikitia. Huyu Katuga laana anayoitafuta itamtafuna yeye na vizazi vyake kwakweli, anadanganya macho yakiwa makavu kabisa.

Acha tuendeleee!

Kwa hoja ilivyo inaonesha kwamba mshitakiwa anataka ku impeach Proceedings za Committal Court na haziwezi kuwa impeached kirahisi hivyo.

Mahakama ya Rufani katika kesi ya Frank Jeremiah Maliano vs Republic CA 147 2022, Ukurasa wa 14 unasema court document is a serious document, haiwezi kuwa impeached kirahisi.

Hii hoja ni baseless na tunaona Mahakama isiizingatie kabisa na itupiliwe mbali mara baada ya Mahakama kujiridhisha na records za Committal zinavyosema. Naomba kwa hoja namba moja niishie hapo.

Hoja nyingine anasema ilipaswa kuletwa ripoti kwanza kabla ya hizi video kwasababu huyu shahidi ni mtaalamu. Hajasema point gani ya sheria mtu aliyefanyia kazi kielelezo lazima aanze na taarifa baadae ndio kielelezo, ameleta maoni na sio sheria.

Hakuna sheria mahususi inayoonesha mtaalamu aliyekuja hawezi kuwa shahidi wa kutoa na kuwasilisha vielelezo hivi mbele ya Mahakama.

Vifungu vyote alivyosema Mshitakiwa havijasema ianze kutolewa ripoti kabla ya vielelezo kuanzia kifungu cha 216 cha CPA.

Anaendelea Katuga hapa, Kesi ya Milzai ukurasa wa 6 na 7 naialika Mahakama ichukulie mfano Mkemia alianza kutoa madawa kabla ya Chemistry Report ilipokelewa na kukubaliwa.

Part 127 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba Repost yako.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 127

Anaendelea Katuga

Shahidi alitambua vielelezo pale kizimbani na ndio maana tunasema vipokelewe, alisema hawezi kutufundisha na sisi tunataka akitufundisha atufundishe kutoka kwenye Sheria.

Naomba niende kwenye hoja ya tatu ambayo inasema shahidi sio competent kutender hii exhibit na kwenye hoja hii aliialika Mahakama kwenye vile vifungu vingi kuanzia 216 hadi 221 vya CPA.

WAKATI KATUGA ANAENDELEA NI KAMA NIMEWAONA HAWA ASKARI MAGEREZA WANAOMLINDA MH. LISSU WAPO WAGENI NA SURA ZAO ZIMEKAA KAMA WALE WENZETU KWELI. WAPO WAGENI NDIO WAMELETWA HAPA. SIJUI WANA MPANGO GANI NA HAWA WALINZI WAO.

Acha tuendelee na Katuga sasa

Anataja vifungu vyote alivyovitaja Mh. Lissu na vinazungumzia nini? Kingereza chake ni kibovu sana. Akisoma mahali ZE ZE ZE ZE ZE ni nyingi sana.

PW 3 amejieleza kama yeye ni mtaalamu na alialikwa kufanyia kazi vielelezo na amejipambanua kuhusiana na umri wake na utaalamu wake. Na alifanyia kazi vielelezo hivi hivyo basi kifungu cha 52 cha Evidence Act Cap. 6 kinasema mtu mwenye uelewa na fingerprints, na ujuzi mwingine basi yanapokelewa.

Kila shahidi yuko entitled kuaminiwa unless Mahakama ije na sababu za kutomuamini.

Kesi ya Goodluck Kyando Vs Jamhuri TLR 2006 Every witness is entitled to credence.

Shahidi wetu anaomba kutoa memory card yenye video, flash yenye video.

Kifungu cha 70 cha Evidence Act Cap. 6 kinasema in any proceedings electronic evidence shall be admissible.

Mahakama ya rufaa imetoa visifa vya vitu inavyotakiwa kuzingatia kabla ya kupokea vielelezo.

Kesi maarufu ya DPP VS Sharif Mohamed, Athumani and 6 others CA 74 2016.

Kesi inasema mtu aliyefanyia kazi kielelezo ni competent ku tender pia kesi ya DPP vs Mirzai inatoa utaratibu huo wa kisheria.

Naomba kesi hizi zote nizitoe kwa Mahakama na mshitakiwa pia.

Amekuwa appointed na gazetted kwa kufanya uchunguzi na kutoa taarifa ndio kazi ya shahidi huyu.

Yeye ni shahidi wa picha mnato na mjongeo Gazeti la serikali no. 745/2022 ndio lilimtangaza kwa ajili ya kufanya uchunguzi na kutoa taarifa.

Tangazo hilo limesainiwa na DPP na kwamba title ya tangazo lile ni amri ya uteuzi wa wataalamu wa picha na mambo mengine.

Mtaalamu wetu anasema yeye ni mtaalamu wa picha mnato na picha mjongeo na mimi naialika mahakama itafute meaning ya picha, is video a picture? Vifungu vya 216 na kuendelea havioneshi mtaalamu wa video, hayupo.

Kifungu cha 220 cha CPA kwamba video ni cyber forensic expert, tafsiri ya CYBER ziko nyingi sana ikiwa ni pamoja na ushahidi wa Computer ndo maana yake.

Anachunguza devices utambuzi wa uhalisia wa picha utabaki kwa mtambuzi wa picha. Is a video a picture? Video ni picha za muendelezo.

Hapa cyber experts na photographic expert wasichanganywe ni watu wawili tofauti.

Kuna definition mbalimbali lakini kuna dictionary ya computer and internet terms ukurasa wa 363 alitafsiri photograph is a picture created by a camera whether digital or video. Ukurasa wa 513

Anasema Jaji unaenda kwa kasi sana hatukuelewi kwakweli hata unakimbilia wapi.

Au Mshitakiwa unasemaje Jaji anamuuliza. Lissu anajibu Mimi namuangalia tu naona anaongea ongea, nimemuacha.

Jaji sasa sisi tunaona ujielekeze vizuri ukiendeleea kujiongelea wewe sisi hatutaandika.

Haya rudia hapo sasa kwenye Dictionary taratibu.

Part 128 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 128

Anaendelea Katuga naomba sasa nihamie kwenye hoja ya nne.

Mshitakiwa anasema vielelezo visipokelewe eti akiwamaambia kwamba vielelezo hivi vimevunja mnyonyoro wa utunzaji.

Watu wanacheka. 😂😂😂

Ni mnyororo kumbe.

Amesema Chain of custody inathibitishwa na paper trail. The gist of chain of custody ni kuifanya mahakama ione kielelezo ni chenyewe au au vipi?

Mshitakiwa anasema kilipita kwa Michael Gyumi, sijui kikaenda kwa nani? Hicho kilichosemwa hakijajionyesha kwenye ushahidi wa shahidi wetu.

Ametajwa Churu, baadae Malugala na kujazwa ile PF No. 145.

The issue of chain of custody can no be established by a single witness. Utunzaji wa kielelezo hauwezi kuthibitishwa na shahidi mmoja.

Kuleta pingamizi la kwamba Chain of custody imevunjwa na kisipokelewe huku ni ku misplace mapingamizi.

Haya ni maneno ya Mahakama ya rufani R vs Charles Abel Gazilabo na wenzake 3 Rufaa ya jinai No. 358/2019.

Ukurasa wa 17 imejitokeza inshu ya chain of custody na kusema itatumika na kuangaliwa baada ya ushahudi wa upande wa Jamhuri ukifungwa. Prosecution case ikiwa closed sio muda huu.

Kwa maamuzi hayo Mahakama itaona hii hoja haijakuwa established kabla ya kupokelewa kwa kielelezo ila imeletwa kwa kubahatisha na kupoteza muda wa Mahakama ni ombi letu muitupilie mbali.

Kwa mapingamizi hayo yote tunaona hayana msingi kabisa na naomba niwarejeshe kwenye maamuzi aliyowaletea kesi ya Musa, Lemina Omary Abdul na Kesi ya DPP VS Sharif Mohamed.

Mashauri hayo yote yalikuwa yanahusu vielelezo ambavyo havikuwa vimesomwa au listed kwenye records.

Hayakuwa mashauri ambayo yanaonesha vielelezo kutosomwa, sisi kwetu hapa kwenye kesi hii vilisomwa na kuonyeshwa pale Kisutu.

Kwa kumalizia wakati wa hoja ya Competence pia Mahakama ilialikwa ikasome taarifa ya PW3 tulishangazwa sema tukakumbuka Mshitakiwa ni mtaalaamu wa kesi za Madai na sio jinai.

Tunaomba submission zetu ziwe considered na naomba kuishia hapo.

Renatus Mkude anamualika Ignas Mwinuka na anaomba aongeze kidogo.

Nitasema kwenye ile ground ya committal. Nitaomba mrejee ukurasa wa 93 wa Mwenendo kabidhi Mahakama imeandika, S. 263 of CPA has been complied with. Hii ni kuonesha kuwa taratibu zote ambazo zipo zilizingatiwa kwa mujibu wa Sheria.

Naomba niwarejeshe kwenye shauri la Mahakama ya rufani Jamhuri Vs Christian Muhaka Criminal Revision no. 7/2017.

Naomba Waheshimiwa Majaji kwenye shauri hilo Mahakama wa rufani wakiquote mwenendo kabidhi na kusema hawakuona mapungufu kwasababu vifungu vikiandikwa na vikishaandikwa maana yake utaratibu ulifuatwa.

Kwahiyo naomba kusisitiza kuwa hoja hiyo isikubaliwe na kuzingatiwa na mapingamizi yake yasizingatiwe na yatupiliwe mbali. Naomba kuishia hapo.

Anasimama Renatus Mkude anasema ni mwisho wa hoja zao na tunaomba kusisitiza kuwa mapingamizi yatupiliwe mbali, wanakaaa.

Tusubiri Rejoinder kutoka kwa Mhe. Lissu sasa.

Atajibu vimbwanga vyao hapa.

Part 129 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba Repost yako.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 129

Anaitwa Mh. Lissu.

Anasimama na kusema naomba na mimi nitoe Rejoinder yangu baada ya kuwasikiliza Mawakili wa Serikali.

Nitafuata utaratibu huo huo ambao wao wameufuata walipokuwa wanajibu mapingamizi yangu.

Kuhusiana na hoja ya kwanza.

Je hizo video zilichezwa Kisutu?

Je nyaraka zingine zote zilisomwa ukiaichia witness statement. Je video zilionyeshwa?

Waheshimiwa majaji mashauri ya Kisutu yalikuwa ni hadhara yalifanyika hadharani members of the public pia walikuwepo.

Amesimama Katuga anasema huko kwingine hatukwenda, tuliishia kwenye Court Records pekeee. Tusimuache aende mbali zaidi.

Lissu Mh. Jaji video hazikuchezwa na kama Wakili wa Serikali anasema hadharani kuwa video zilichezwa maana yake tuna shida kubwa sana.

Waheshimiwa Majaji, je ni kweli kwamba hii rekodi ya Kisutu haikuwa impeached? Wakili anasema kwamba record ya Mahakama haiwezi kuwa impeached?

On the question of record: kuna ruling mbili za Mahakama hii juu ya integrity ya hiyo record mtakumbuka kwamba record hii haikusema chochote juu ya majina ya mashahidi niliowataja.

Anasimama tena Katuga anasema hii ni Rejoinder tunaona anaanza kuingiza vitu vipya tena.

Katuga anaogopa kuna mambo kusemwa. 😂 anasema vitu vipya.

Mhe. Lissu anasema hii rekodi nimeichallenge mara kadhaa.

Hiyo page 92 exhibit zimekuwa listed na page 93 inasema the records has been read out.

Hiyo kuandika hivyo haina maana ukweli wangu unabadilika. It doesn't change my position.

Sitaki kukubali jambo ambalo ni uongo.

Mimi sipendi uongo na ukweli wa kwamba video haikuchezwa kisutu utabaki kuwa hivyo hapa Duniani na hata Mbinguni.

Siwezi jidanganya au kutenda dhambi ya namna hiyo namuachia Katuga pengine yeye amezoea dhambi na kudanganya mambo ambayo sio ya kweli.

Video hazikuonyeshwa anasema zimeonyeshwa tena kwa ujasiri wa kusema hadharani na hapa mahakamani.

Niendelee sasa.

Katuga anasema pia kuwa mimi nilisema kuwa sikatai maneno yangu ya tar. 03/04 pale Makao Makuu ya Chama.

Nilichosema mimi ni kuwa hizi video haziko sahihi kupokelewa kwasababu hazikuonyeshwa Kisutu.

Kwa vile hazikuonyeshwa Kisutu haziwezi kuonyeshwa hapa, zilikuwa listed YES. Hazikuonyeshwa na haziwezi kutolewa hapa Mahakama.

Kuhusu mimi kusema sina shida navyo swali linabaki kuwa haviwezi kupokelewa kama havimeet masharti ya kisheria.

Amerejea mashauri ya Mahakama ya rufani wakati natoa hoja yangu. Shauri la Sharif Mohamed athuman, Lemina Omary Abdul na Musa Ramadhani Magai.

Hakuna kesi mbili zinazofanana kwa kila jambo. Kitu muhimu what is the principle ambayo inatokana na mashauri hayo yote matatu.

Principle ni kwamba nyaraka na vitu vyote vinavyotajwa katika mashauri kabidhi kama ni vya kusomwa visomwe na kama ni vya kuonyeshwa lazima vionyeshwe kwahiyo ulitakiwa kuonyeshwa huu ushahidi kule Kisutu.

Mahakama ya rufani ilisema the issue is not authenticity basi issue ni compliance of the law.

Kwenye hoja hii ya kwanza videos ambazo hazikuonyeshwa Kisutu haziwezi kuonyeshwa hapa.

Naomba sasa niende kwenye hoja ya pili.

Kwenye ushahidi wa shahidi ambae anadai yeye ni mtaalamu.

Kitu cha kwanza ni taarifa yake ya kitaalamu na sio alichokifanyia kazi.

Katuga amesema kwamba hakuna sheria mahususi inayolazimisha tuanze na Report badala ya kuanza na video iliyochunguzwa na alisema inantegemea na mazingira ya kesi.

Hajasema mazingira gani ya kesi hii ambayo yanataka ianze report na baadae video.

Sasa katika kesi hii tunayo report ya uchunguzi asa ripoti ndio inayo estabalish genuinely ya hicho kilichofanyiwa uchunguzi.

What is the legal logic ya kutanguliza video na kuacha report ya mtaalamu.

Ukisoma vifungu 216 hadi 223 vya CPA vinasema kuhusu ripoti na sio video na ndio maana ya mfano wangu wa mkokoteni na punda.

Ushahidi wa kitaalamu unahitaji kuletwa na mtaalamu na baada ya ushahidi kuo kuletwa ndio utazingatiwa.

Part 130 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 130.

Mhe. Lissu anaendelea kufanya Rejoinder

Anasema Kwenye hoja ya pili bado nasimamia hoja ya pili kwamba video zilipaswa zitamabuliwe na taarifa ya mtaalaamu ambae ni shahidi.

Kesi ya Mirza Katuga anasema ni prosecution plan kuwa prosecution wanapanga nani wakuleta kielelezo.

Hoja nimesema kielelezo kinahusika na utaalamu basi kifuate taratibu za utaalamu.

Hoja ya tatu kuhusu competence ya shahidi vifungu kuanzia vya 216 na kuendelea, kusingekuwa na umuhimu wa sheria kusema wateuliwe.

Kinachofanya wawe wataalaamu sio maneno yao bali ni uteuzi wao.

Katuga anasema shahidi ameonysha utaalamu wake.

Je huyu ni mtaalamu? Ameteuliwa? Kama hajaonesha kuwa ni mtaalamu maneno yake ni kazi bure.

Shahidi huyu amesema kwamba ameteuliwa kwa mujibu kwa gazeti la serikali No. 799/2020 na vilevile amesema ameteuliwa kwa mujibu wa gazeti la serikali no. 745/2020

Hayo magazeti ni Sheria na ni nyaraka za kisheria. Wakili wa Serikali hakusema lolote kuhusu GN. No. 799/2020. Na anasema tusiende huko.

Na mimi nasema lazima twende huko kwasababu ni mtaalamu wa picha na sio mtaalamu wa video.

Wapo wataalamu walioteuliwa na DPP kwa ajili ya video huyu hayupo. The are withholding important information, wanaficha nyaraka muhimu na wakitaka walijibie.

Hii ni sheria ambayo walipaswa kuileta kwenu lakini walikaa kimya ni sheria inayohusiana na ni akina nani ambao ni wataalamu wa kisayansi wa mitandao ambapo wapo kwenye GN. No. 823/2024.

Ukiisoma hii GN wapo 27 hao wataalamu hayupo Samweli Elibariki Kaaya kwenye hiyo orodha.

Majaji wanateta sana hapo kama dakika 10 nadhan wanafikiria Mhe. Lissu aruhusiwe kuitoa hiyo Sheria au haruhusiwi.

Jaji ilikuwa ni haki kwa mshitakiwa kuijibia hoja hiyo maana hata Jamhuri mlituletea maana ya picha mkatuambia kuhusu dictionary.

Kwahiyo mshitakiwa endelelea.

Mhe. Lissu anawasomea hiyo GN hapo juu iliyowataja hao ma experts na anasema kwa kiswahili inaitwa AMRI YA UTEUZI WA WATAALAMU WA KISAYANSI WA MTANDAO aya ya pili ya Tangazo hilo inasema mtu ambae jina lake limetajwa katika jedwali anateuliwa kuwa mtaalamu wa kisayansi wa mtandao katika mashauri yoyote ya jinai na masuala yoyote kama hayo kwa mudhumuni hayo.

Jedwali hilo limeorodhesha watu 27 na huyu shahidi hayumo.

Amesimama Katuga anasema anaanza kutaja majina asifike huko.😂

Katuga hajui kama majina yametajwa kwenye hiyo GN yenyewe.

Huyu mtaalamu wao wamekuja nae mfukoni hayupo kisheria, hajatajwa kwenye tangazo la serikali na hajawahi kuteuliwa.

Jaji anasema hiyo ni sheria sasa kama watu wameandikwa tutaona na tutaona nani yupo na nani hayupo kwahiyo muiachie Mahakama tu.

Waheshimiwa Majaji Sharif Athuman Ukurasa wa 8 Jaji Masatti amesema:

But admissibility of evidence, it is also about the competence of the witness. It is not only about relevance, materiality and...

Jaji amesema competence ya shahidi inaweza kuwa general au specific.

Kwa huyu shahidi ni suala specific kwasababu tunazungumzia mambo ya mitandaoni na shahidi ambae anapaswa kutoa huo ushahidi ni ambae katangazwa kwa kazi hiyo.

Hivyo admissibility ya ushahidi huu inahitaji mtaalamu wa cyber forensic na sio mwingine na nimewapa hapo GN ambayo DPP ameteua watu wake.

Wakili wa Serikali anasema shahidi amesema mengi kuwa yeye ni mtaalamu.

Ni wasilisho langu kuwa kwa vile hayupo kwenye gazeti la Serikali na sio mtaalamu wa chochote huyu shahidi ni wajibu wa Mahakama kujiuliza kwa mujibu wa sheria je huyu ni mtaalamu na ameteuliwa kama nani?

Sayansi ya mtandaoni wameteuliwa yumo?

Kwenye picha za kawaida za makaratasi hilo halibishaniwi hapa, asubiri siku tukiwa na kesi ya makaratasi atakuja.

Haya ya leo ni masuala ya kimtandao.

Kifungu cha 70(1) cha Evidence Act kwamba ushahidi wa kielektroniki unakubalika hata mimi najua hilo ila hoja ni kwamba je anayeleta ushahidi kateuliwa?

Hii ndo hoja ya msingi.

Part 131 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
Part 131

Anaendelea Mhe. Lissu kufanya Rejoinder

Anasema kwahiyo Katuga ameleta hicho kifungu cha 70 kwa kutoelewa anazungumza na kuipotezea muda Mahakama akiwa anazungumza jambo gani?

Twende kwenye hoja ya nne.

Hoja ya Chain of Custody ambayo ni hoja ya nne.

Maamuzi yote niliyowasilisha mimi na waliyowasilisha wao Mawakili wa Serikali linalosema shahidi anaweza kuleta ushahidi kutoka mfukoni mwake.

Chain of custody is about paper trail na kesi inayosema hivyo ni Paul Maduka hajaigusia kabisa ukurasa wa 18 na 19 kesi imesema chronological documentation and all paper trail shows the seizure, transfer and disposition must be documented.

Waheshimiwa Majaji ushahidi unaoombwa upokelewe una hiyo chronological documentation uliyosemwa na Mahakama ya Rufani kwenye Paul Maduka?

Je una hiyo paper trail?

Naomba ikumbukwe huyu ni shahidi mtaalaamu na kwenye ushahidi wake aliandikiwa barua na vielelezo vililetwa kwa maandishi afanye uchunguzi wa hivyo vielelezo.

Hizo barua hazijawasilishwa, anasema nikisign dispatch haijaletwa mahakamani.

Anasema alivituma kwa requesting authority na kwamba vimerudije kwake tena hajasema lolote.

Leo ametuletea hivi vielelezo sisi hatujui vimefikaje kwake tena.

Wamefanya mambo kienyeji sana na mambo ya kienyeji hayakubaliwi Mahakamani.

Sasa ushahidi wa namna hii unakubaliwaje Mahakamani?

Nitamkumbusha maneno yake Wakili wa Serikali kuwa alisema Mahakama hii sio ya MAMA YANGU na Mimi namwambia leo kuwa MAHAKAMA HII SIO YA MAMA YAKE KATUGA WALA MAMA YAKE NA HUYU SHAHIDI.

Anasimama Katuga anasema Waheshimiwa Majaji Mahakama hii sio ya Mama yetu wote.

Mhe. Lissu anasema ni sawa KAMA MAHAKAMA SIO YA MAMA YETU WOTE basi na WEWE USIFANYE MAMBO KAMA UNAENDA KWA MAMA YAKO.

Tufuate tu utaratibu hicho ndio ninachokisema na ndo maana naomba vielelezo hivi visipokelewe na Mahakama hii kwa hizo hoja nne nilizosema toka awali na kusisitiza kwa sasa.

Anawaachia Majaji sasa wanaandika.

Kwa kifupi Mh. Lissu amemaliza na gia kubwa sana.

Watoto wa Mjini wanasema amepiga sana kwenye MSHONO kwa hizi nondo majaji sijui watasema tunarudi lini kwa ajili ya uamuzi mdogo wa mapingamizi haya.

Wanaandika pale mbele na kuteta kidogo.

Jaji Ndunguru anasema baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili uamuzi utatolewa siku ya Jumatano tarehe 22/10/2025 saa tatu asubuhi.

Like, share, comment na follow my page Shija Samwel
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Leo Oktoba 22, 2025

Last time tuliishia part 131 so leo tunaendelea na-;

Part 132

Ameingia Mhe. Lissu akiwa amepiga Tshirt yake Nyeusi ya Chama.

Yuko na vibe kama ilivyo siku zote.

Dakika Chache kabla Mahakama haijaanza Makamu Mwenyekiti John Heche amechukuliwa na Mapolisi na kuondoka nae.

Majaji wameingia hapa Mahakamani.

Watu wote wamesimama.

Kabla Mahakama haijaanza upande wa juu wa Mahakama ameingia mtu amesimama amesema yeye ni Nabii ametumwa na Mungu.

Anasema anaomba Majaji wamsikilize, jana alikuja hapa Mahakamani akaishia hapo Maaskari wamemdaka na kuondoka nae.

Kabla ya kuondoka nae amepiga kelele nyingi akisema YESU YESU YESU, anasema yeye ni Nabii yuko toka jana ametumwa na MUNGU kuwa Tundu Lissu aachiwe.

Leo siku imeanza kwa mambo mengi yakushangaza kama hivyo.

Jaji anaanza kusoma sasa uamuzi mdogo wa yale Mapingamizi ya Mhe. Tundu Lissu.

Wakati shahidi akitaka kutoa vielelezo mshitakiwa aliweka hoja nne kupinga. Ambazo ni;

1. Video haikuchezwa Mahakama ya Kisutu

2. Vielelezo hivyo vinatolewa kabla ya wakati.

3. Shahidi namba 3 hana uwezo wa kutoa vielelezo hivyo.

4. Upande wa mashitaka haujaonyesha mnyororo wa vielelezo katika utunzaji wake.

Upande wa Mashitaka walipinga mapingamizi hayo na Mahakama imejiuliza swali moja je mapingamizi hayo yana mashiko?

Jaji Ndunguru anaendelea kusoma.

Mahakama imeona ianze na pingamizi la tatu. Je Shahidi huyo ni competent au laa?

Mshitakiwa alisema shahidi huyu hana nguvu ya kisheria na hayupo kwenye orodha kwa mujibu wa GN. No. ... kwahiyo huyu sio mtaalamu anayepaswa kuja kutoa ushahidi.

Shahidi huyo hakuteuliwa na DPP kwa ajili ya kushughulikia hizi video na kutoa ushahidi wa namna hii.

Nao upande wa Mashitaka walijibu hoja hiyo ya Mshitakiwa na kuipinga. Wakairejea shauri la Mirzai na kusema shahidi ni mtu ambae alichunguza na kuandaa ripoti. Kwahiyo anaweza kutoa vielelezo hivyo hapa Mahakamani.

Pia Wakili wa Serikali alisema hizo video ni ushahidi wa kielektroniki hivyo unapaswa kupokelewa Mahakamani kwani sheria inaruhusu na kutoa vigezo vitatu ambao ni relevant, material na competent.

Vigezo vyote vimekidhi katika kuhakikisha ushahidi huo unapokelewa.

Pia Wakili wa Serikali alirejea Dictionary kueleza maana ya mtaalamu wa video na picha.

Mshitakiwa katika kujibu hoja za Serikali alisisitiza kuwa shahidi mtaalamu ni lazima awe ameteuliwa na kutangazwa kwenye gazeti la Serikali kama ambavyo GN. inasema.

Sasa Mahakama imefuatilia na kuchunguza kwa makini na kuamua Shahidi namba 3 ni competent na ananuwezo wa kutoa hiyo flash kwa maana ya video.

Mshitakiwa anasema shahidi hana uwezo wa kisheria kutoa hiyo flash.

Kama tulivyokubaliana vigezo ni vitatu ambavyo ni relevant, material na competent na pia shahidi anapaswa kuwa competent.

Shahidi namba 3 ni shahidi mtaalamu na sheria inasema huyo sio shahidi facts ni shahidi wa utaalamu.

Experts witnesses ni lazima wawe wameteuliwa na DPP na wametangazwa kwenye gazeti la Serikali.

Shahidi namba 3 alitangazwa kwenye gazeti la Serikali wa kuchunguza picha mwaka 2022.

GN hiyo ilitengenezwa kwa mujibu wa kifungu cha 216 cha sasa katika aya ya pili ya gazeti hilo inasema Watu ambao majina yao yameorodheshwa ni wataalamu wa picha.

GN. hiyo iliyotengenezwa kwa mujibu wa kifungu cha 216 ambacho kinampa mamlaka DPP kuteua wataalamu. Kinasema nanukuu, anakisoma hapa.

Ukisoma kifungu hicho kinazungumzia shahidi kuandaa photographic print au photographic enlargement.

GN. no. 745 imetengenezwa kwa mujibu wa kifungu cha 216 pamoja na mambo mengine inahitajika awe na Certificate ambayo itataja majina yake na kuelezea namna alivyopokea kazi ya kuchunguza na alivyofanya.

Hapa tunamaanisha ni report ya mtaalamu.

Hivyo basi kama kifungu ndio kinasema hivyo lazima tafsiri ya kila kitu kiwe kwenye njia hiyo.

Part 133 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 133

Anaendelea kusoma uamuzi Jaji Nduguru

Kilichotokea hapa Mahakamani shahidi ametender flash disk yenye hizo video na memory card.

Ingawa upande wa Mashitaka uliishawishi Mahakama kuwa hizo flash disk zimebeba picha na video na wakatumia shauri la India.

Mahakama imepitia upande wa Mashitaka na hoja zao walizoleta.

Mahakama imerejea kwenye kifungu cha 216 cha CPA kikirifaa mambo ya picha na hakisemi kuhusu video.

Hivyo vitu viwili vina maana tofauti kuhusu photograph na video na Jamhuri wameshindwa kutofautisha.

Shahidi Na. 3 alichokuwa anataka kukitoa hivyo vitu sio photographic prints wala enlargement.

Kwahiyo huyu shahidi hana uwezo wa kutoa hiyo video na Mahakama imekataa kupokea hizo video.

Wataalamu wa electronic ndio walipaswa kuja kutoa hizo video na tumeona ipo GN inayohusiana na video na mambo ya kielektroniki kwa ujumla.

Baada ya kusema hayo Mahakama inakubaliana na pingamizi la mshitakiwa.

Jaji anasema tuendelee sasa.

Kabla hatujaendelea kwa kifupi ni kwamba VIDEO AMBAYO SASA NDIO USHAHIDI WENYEWE WA KESI IMEKATALIWA. KWAHIYO HAYO WANAYOSEMA YALISEMWA NA LISSU AMBAYO NDIO UHAINI WENYEWE. MAHAKAMA IMEUKATAA. KWA KIFUPI KESI IMEISHIA LEO. HAPA TUNAPOTEZA MUDA KUSUBIRI HUKUMU.

Anasimama Thawabu Issa kuanza kumuongoza Shahidi.

Sasa shahidi ulizungumzia kuhusu taarifa ya uchunguzi.

Ukiiona utaijuaje.

Samwel Elibariki Kaaya: Nitaitambua kwa majina yangu, logo ya Polisi, signature, Muhuri na tarehe.

Thawabu Issa: Naomba Waheshimiwa Majaji naomba nimuonyeshe Nyaraka shahidi.

Jaji: Muonyeshe.

Anapewa shahidi nyaraka kadhaa.

Shahidi anasema hii ndio ripoti ya kitaalamu niliyoiandaa ina majina yangu na vyote nilivyosema awali na niliandaa mwenyewe.

Wakili wa Serikali: Unaiomba nini Mahakama?

Shahidi: Ipokee kama sehemu ya kielelezo.

Jaji: Mpatieni Mshitakiwa.

Mhe. Lissu anaiangalia anasema napinga hiyo taarifa kupokelewa kwa hoja zifuatazo.

Hii inaitwa Mbwa kala Mbwa.😀

Mhe. Lissu anaanza tena.

Waheshimiwa Majaji kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Jinai shahidi anayetakiwa kuwasilisha taarifa za uchunguzi wa kitaalamu, anapaswa kuwa ni shahidi aliyetamkwa kwenye kifungu cha 216, 217, 218 na 220 vya Sheria ya Mwenendo wa Jinai.

Sasa Waheshimiwa Majaji shahidi huyu ni shahidi wa picha za mnato kwa maelezo yake yeye mwenyewe mtayaona kwenye kielelezo anachotaka kukiwasilisha.

Mimi Samweli Kaaya Mkaguzi msaidizi wa Jeshi la Polisi ambae ni mtaalamu wa picha chini ya kifungu cha 202(1) cha CPA.

Sasa anaendelea Mh. Lissu.

Sasa Waheshimiwa Majaji hicho kifungu cha 202(1) cha CPA ndio kifungu cha 216 cha sheria ya sasa kinazungumzia hati za wataalamu wa picha mnato.

Wao wanakitumia kuleta kielelezo ambacho ni video.

Waheshimiwa Majaji WINO HAUJAKAUKA. toka muamue kuwa huyu shahidi hapaswi kuleta ushahidi wa video hapa Mahakamani maana yeye sio mtaalamu wa video.

Shahidi yeye mwenyewe amejisema kuwa yeye sio shahidi competent, amejisema Mwenyewe.

Tunaanzaje kumkubalia?

Na hawa Mawakili wa Serikali sijui wana akili au wamerogwa maana muda mfupi uliopita Mahakama imewaambia kuwa huyu mtu sio mtaalamu wa video ni mtaalamu wa picha, wao wanataka kutuletea hapa mtaalamu wa picha aliyechunguza video ni kituko.

Kwenye kielelezo chake mwenyewe shahidi anasema pia ameteuliwa na tangazo la serikali 799 lilitolewa na AG Adeladus Kilangi halikutolewa na DPP.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali hakuwa na Mamlaka na hana mamlaka ya kuteua mtaalamu yeyote aliyesemwa kifungu cha 216 hadi 220 cha CPA.

Mawakili wa Serikali wapo na ubaridi mkubwa wamekuwa wadogo sana kama Pilton.

Sect. 216 ya CPA inazungumzia Certificate ambayo ndo ripoti yenyewe ya mtaalamu na kinasema pia uteuzi wa huyo mtaalamu anapaswa kuteuliwa na DPP na sio AG.

Part 134 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba Repost yako.
 
Back
Top Bottom