Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Lissu Mahakamani: 'Tutakinukisha kweli kweli' ni uasi? shahidi wa mshitakiwa aulizwa na wakili wa serikali
1788882973391.jpg
 
MARIDHIANO HAYAJI KWA NJIA ZA UTAPELI!

Mtu aliyetambulishwa kama Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa CHADEMA (BAZECHA) Kanda ya Kati (Morogoro, Singida na Dodoma, Acquilin Magalambula amenukuliwa akisema CHADEMA waingie maridhiano na serikali hata kama Lissu hajatoka gerezani.

Mtu ambaye aliyetambulishwa kama Katibu wa CHADEMA wa Mkoa wa Morogoro, Barnabas Okola amenukuliwa akiwashambulia Mhe. Jaji Joseph Warioba na Mhe. Anna Tibaijuka.

Lakini uchambuzi wa picha mjongeo (video) na mazingira ya mikutano yote miwili insonyesha kuwa ni mkutano mmoja kwa sababu mavazi ya wahudhuriaji yanafanana na watu wengine nyuso zao ni zile zile na kipaza sauti ni kile kile na hata wasambazaji wa video hizo ni watu au media zenye mrengo wa CCM.

Lakini waandaji wa mkutano huo ni watu wa ajabu sana. Wanasukuma maridhiano lakini hawataki Lissu atoke gerezani. Wanasukuma maridhiano lakini wanawashambulia Mhe. Jaji Joseph Warioba na Prof. Tibaijuka.

Lakini jambo lingine ni kuwa mikutano yote ya CHADEMA ina muktadha unaojulikana na hata hupambwa na bendera za chama chao na hukuwa wanachama wao wakivalia mavazi ya chama chao.

Pia, hata viongozi wa CHADEMA wakiwa katika mikutano yao lazima waseme kauli mbiu zao kama 'People's Power', nk. Lakini muktadha na mazingira ya mkutano huo au mikutano hiyo ni kinyume kabisa.

Sisi askofu tunataka kuwaeleza watu ambao wako nyuma ya mkakati huo wa kurubuni watu kwa kuwatumia watu ambao hujinasibu kama viongozi wa CHADEMA. Ujumbe wetu ni kuwa maridhiano ya kweli hayajengwi kwa kutumia njia za ulaghai, utapeli au udanganyifu. Kama CCM na serikali yake wanataka kweli kufanya maridhiano ya kweli waache kulaghai watu au kudanganya watu kwa njia hizo.

Kwa nini kauli za watu wanaohujumu ukweli na kukihujumu CHADEMA na viongozi wake pia zipate nafasi katika media za watu ambao ni wale walio karibu na CCM na serikali yake?
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Itunge, Dar es Salaam; 9 Septemba 2026; Saa 5:55 usiku.
1789002560477.jpg
 
Wakili Paul Kisabo, mmoja wa mawakili wanaounda jopo la utetezi la Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, akiwa katika picha ya pamoja na Brenda Jonas Rupia, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA na shahidi wa upande wa utetezi katika shauri la uhaini namba 19605/2025 linalomkabili Lissu.

Rupia anaendelea kutoa ushahidi mbele ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, ambapo kwa sasa anakabiliwa na maswali ya dodoso (cross-examination) kutoka kwa mawakili wa Serikali katika hatua ya ushahidi wa utetezi.

Katika ushahidi wake, Rupia amezungumzia majukumu yake ndani ya CHADEMA, akieleza namna shughuli za mawasiliano na uenezi zinavyotekelezwa na timu ya chama, pamoja na kujibu maswali mbalimbali yanayohusiana na kauli na shughuli za chama katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
1789003053192.jpg
1789003048933.jpg
 
#bahariaNEWS Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam huenda leo, Alhamisi Septemba 10.2026, ikatoa uamuzi wa pingamiz ililokuwa limewekwa na serikali katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu, inayosikilizwa mfululizo mbele ya jopo la Majaji watatu (3) wakiongozwa na Jaji Dastan Ndunguru.

Pingamizi linalosubiriwa kutolewa uamuzi ni lile inalohusu baadhi va viongozi waandamizi wa serikali walioko madarakani na wastaafu, na baadhi ya maafisa wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama wakiwemo Wakuu wa vyombo hivyo, wote hao wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kama Mahakama inakubali au inakataa kuwa sehemu ya mashahidi wa utetezi kama ilivyoombwa na mshtakiwa Tundu Lissu ambaye anajitetetea mwenyewe kwenye kesi hiyo.

Jana mchana Mahakama iliwaeleza wahusika wa pande zote mbili (2) kuwa uamuzi huo uko tayari na kwamba kama wangekuwa tayari usomwe kabla ya shahidi wa TANO wa utetezi Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tanzania Bara John Heche hajaanza kutoa ushahidi wake, lakini pande zote zilikubaliana kwamba uamuzi huo usubir kwanza kwa wakati huo, kando ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassar mashahidi' wengine wanaosubiri uamuzi huo ni pamoja na Makamu wa Rais Mstaafu Dkt. Philipo, Waziri Mkuu Mstaafu Kassim Majaliwa, na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Nchini CDF) Jenerali Jacob John Nkunda
Wengine ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Camilius Wambura, Mkurugenzi Mkuu wa ldara ya Usalama wa Taifa (DG TISS), Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Nchini (DCI Kamishna wa Polisi (CP) Ramadhan Kingai, na Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ramadhan.
1789026382278.jpg
 
Kesho inaendelea, tunaita mashahidi watatu, DCI - Kingai, IGP - Wambura na CDF - Mkunda watahojiwa na Lissu jinsi walivyo tishwa na uasi alio utangaza Lissu. Ila hawakutishika na gaidi Mbowe kwenda Ikulu akitokea Ukonga, tumefika patamu!
 
#bahariaNEWS Wakili Maduhu William Amechambua kuhusu kuitwa kwa CDF JACOB MKUNDA,,IGF CAMILLIUS WAMBURA NA DCI RAMADHAN KINGAI NA UTETEZI DHIDI YA KESI YA UHAIN NAYOMKABILI MHE LISSU

Na haya ndio maswali matatu mazito

Kwanza Je Jamhuri wanayo nafasi ya kukata rufaa juu ya haya Maamuz ya Mahakama? Na je iwapo kweli wataenda kutoa ushahidi kisha wakamgeuka Lisu nini kitatokea:

Nikamuuliza tena wakili wanaweza kuwakilishwa au ni lazima wafike Mahakamani wao wenyewe

Mwisho iwapo hawataenda Wanaweza kutolewa amri na Mahakama va kukamatwa? Yaani Mkuu wa Majeshi,DCI na IGP:

Haya hapa majibu ya wakili
kwanza ujue Mlango pekee walio nao upande wa Jamhuri ili kuwanasua mashahidi hawa ili wasije Mahakamani ni kukimbilia Mahakama ya Rufani kwa njia ya mapitio( Revision) kama nawajaridhika na uamuzi huo,, nje ya hapo hawana namna.

Ila ikitokea IGP Wambura, CDF Mkunda na DC Ramadhan Kingai wakakaidi wito wa Mahakama nini kitatokea??
Kwa sababu IGP, CDF na DCI hawana kinga ama dhidi ya kushitakiwa au kutoa ushahidi Mahakamani( yaani hawa ni both compentent and Compellable witnesses). Kwahiyo hawana namna ni lazima waje Mahakamani na kama watakaidi Mahakama inaweza kutoa wito wa kukamatwa( arrest warrant) au wanaweza kukumbana na mtego wa kosa la kuidharau Mahakama( contemp of Court)

Tatu: Nini kitatokea kama watatii wito wa Mahakama na wakaamua kumgeuka mshitakiwa na kuwa upande wa Jamhuri??

Tukumbuke hawa ni mashahidi wanakuja kwa ajil ya utetezi, hivyo watalazimika kuwa katika mlengo wa kuijenga kesi dhidi ya mshitakiwa na ikitokea wakaamua kumgeuka mshitakiwa( yaani turning into hostile witness) Mhe Lissu atalazimika kuiomba Mahakama awaulize Maswali va Dododo( cross examination) suala ambalo itawafanya wapite kwenye tanulu la moto.

Nne: Je Wanaweza kuja mashahidi kutoa kwa niaba ya CDF, IGP na DCI??

Kwa mujibu wa Sheria za Tanzania hakuna ushahidi unatolewa kwa niaba. Kwa lugha nyingine wito( summons) zitatumwa kwa majina vao binafsi( on their personal capacity) na sio kwa mwamvuli wa taasisi wanazoziongoza.
1789077033894.jpg
 
Back
Top Bottom