Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 373,352
- 865,010
- Thread starter
- #461
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 103
Mahakama imetulia sana hata hakohoi mtu baada ya hiyo speech.
Watu wameingiwa ubaridi ni kama maneno yamewaingia kila aliyepo hapa.
Jaji amewasha kipaza sauti na kumwambia shahidi uko chini ya kiapo.
Endeleeni.
Mhe. Lissu: Ni kweli au sio kweli hiyo video ya Tarehe 03/04 ilichapishwa kwenye Jambo Tv na mitandao mingine na walichapisha Jambo Tv wenyewe?
Kaaya: Aliyechapisha sifahamu.
😂😂😂 kumbukeni kosa la Lisu ni kuchapisha na kusambaza.
Mhe. Lissu: Ni kweli Mkutano wangu wa tarehe 03/04 ulirushwa mubashara na Jambo Tv?
Kaaya: Ni kweli.
Mhe. Lissu: Na ni kweli au sio kweli mimi sina uhusiano wowote na Jambo TV?
Kaaya: Mimi sikufanya upelelezi wa kuhusu wahusika wa Jambo TV ni akina nani.
Mhe. Lissu: Ile Flash Disk XIOXIA yenye rangi nyeupe unaikumbuka ulisema.
Kaaya: ndio nakumbuka
Mhe. Lissu: Je uliandika aina hiyo ya Flash na rangi yake kwenye maelezo yako Polisi?
Kaaya: Sikuandika.
Mhe. Lissu: Umezungumza sana kuhusu video na kuwaonyesha wakubwa zako na kuipakua na kuweka kwenye flash disk umezungumza sana asa waeleze majaji kama umewasilisha hiyo flash disk au hiyo video mahakamani hapa.
Kaaya: Bado sijaiwasilisha.
Mhe. Lissu: Ni sahihi nikisema hakuna mtu aliyeiona isipokuwa wewe hiyo video, Majaji hawajaona, Mawakili hawajaona na mimi sijaona.
Kaaya: Ni kweli.
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama unafahamu au hufahamu hiyo video vilevile haikuwasilishwa wala kuonyeshwa kwenye committal Kisutu?
Kaaya: Sifahamu.
Mhe. Lissu: Sasa shahidi unakumbuka kwenye ushahidi wako ulieleza jinsi ulivyoona hiyi video na kutoa taarifa kwa mkuu wa kitengo?
Kaaya: Ni kweli.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama kwenye maelezo yako Polisi au hapa Mahakamani ulimtaja huyo Mkuu wako wa kitengo kwa jina?
Kaaya: Sikumtaja.
Mhe. Lissu: Unakumbuka nilikuuliza maswali mengi juu ya kesi mbalimbali zilizofunguliwa na watu tofauti tofauti kuhusu masuala ya Katiba na mabadiliko yake.
Kaaya: Nakumbuka.
Mhe. Lissu: Waelelze majaji kama unafahamu au hufahamu kwamba tarehe 13/06/2023 Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Wananchi ilitoa uamuzi kwamba Serikali ya Tanzania ibadilishe sheria ya Uchaguzi ili kuhakikisha sheria za uchaguzi zinakuwa za haki kwenye kesi ya BOB CHACHA WANGWE.
Ni kesi ya Bob Chacha Wangwe akiwa na Legal and Human Right Center wakiwashitaki AG, Tume ya Uchaguzi. Alikuwa anawapa full citation hapo majaji anawatajia na namba ya kesi hiyo.
Mhe. Lissu: sasa kuzuia uchaguzi ni uhaini mnasema hivyo kwenye ushahidi wako ulieleza kuzuia uchaguzi bila kufuata utaratibu wa kisheria kama vile kupata amri ya mahakama ni kuitisha serikali.
Kaaya: Nakumbuka.
Mhe. Lissu: Utaratibu huo wa namna ya kuzuia uchaguzi upo katika sheria gani?😂
Kaaya: Sifahamu.
Ushahidi ni kazi sana jamani.
Leo kumbukeni kuna ile kesi yetu pia niliyofunguliwa na Viongozi wa Chama ndio inaanza muda huu ila Mimi siendi wataingia Mawakili wetu kwa niaba yetu.🤦🏾♀️
Mhe. Lissu: Katiba unaifahamu shahidi?
Kaaya: Ndio naifahamu.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama upo utaratibu wa kuzuia uchaguzi mkuu?
Kaaya: Haupo. Haujaanishwa kwenye Katiba.
Mhe. Lissu: kwahiyo utaratibu haupo?
Kaaya: Zipo sheria zingine lakini.
Mhe. Lissu: Hivi unaelewa swali langu au unatuchelewesha kwenda kwenye mazishi?
Kaaya: haupo
Mhe. Lissu: Je ni kweli Uchaguzi mkuu wa Tanzania unaendeshwa na inayoitwa Tume Huru ya Uchaguzi?
Kaaya: Ni kweli.
Mhe. Lissu: Je ni kweli Katiba inasema tume ni chombo huru na haitakiwi kuingiliwa na Mamlaka au mtu yeyote?
Kaaya: Sikumbuki.
Mhe. Lissu: Anasomewa Katiba hapa ibara ya 74(11) kuhusu Tume na uhuru wake na pia anasomewa sheria ya Uchaguzi kuhusu wajibu wa Tume.
Kwamba tume haitakiwi kupokea maelekezo yoyote kutoka serikali wala chombo chochote cha serikali.
Kaaya: Ni sahihi.
Part 104 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
Part 103
Mahakama imetulia sana hata hakohoi mtu baada ya hiyo speech.
Watu wameingiwa ubaridi ni kama maneno yamewaingia kila aliyepo hapa.
Jaji amewasha kipaza sauti na kumwambia shahidi uko chini ya kiapo.
Endeleeni.
Mhe. Lissu: Ni kweli au sio kweli hiyo video ya Tarehe 03/04 ilichapishwa kwenye Jambo Tv na mitandao mingine na walichapisha Jambo Tv wenyewe?
Kaaya: Aliyechapisha sifahamu.
😂😂😂 kumbukeni kosa la Lisu ni kuchapisha na kusambaza.
Mhe. Lissu: Ni kweli Mkutano wangu wa tarehe 03/04 ulirushwa mubashara na Jambo Tv?
Kaaya: Ni kweli.
Mhe. Lissu: Na ni kweli au sio kweli mimi sina uhusiano wowote na Jambo TV?
Kaaya: Mimi sikufanya upelelezi wa kuhusu wahusika wa Jambo TV ni akina nani.
Mhe. Lissu: Ile Flash Disk XIOXIA yenye rangi nyeupe unaikumbuka ulisema.
Kaaya: ndio nakumbuka
Mhe. Lissu: Je uliandika aina hiyo ya Flash na rangi yake kwenye maelezo yako Polisi?
Kaaya: Sikuandika.
Mhe. Lissu: Umezungumza sana kuhusu video na kuwaonyesha wakubwa zako na kuipakua na kuweka kwenye flash disk umezungumza sana asa waeleze majaji kama umewasilisha hiyo flash disk au hiyo video mahakamani hapa.
Kaaya: Bado sijaiwasilisha.
Mhe. Lissu: Ni sahihi nikisema hakuna mtu aliyeiona isipokuwa wewe hiyo video, Majaji hawajaona, Mawakili hawajaona na mimi sijaona.
Kaaya: Ni kweli.
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama unafahamu au hufahamu hiyo video vilevile haikuwasilishwa wala kuonyeshwa kwenye committal Kisutu?
Kaaya: Sifahamu.
Mhe. Lissu: Sasa shahidi unakumbuka kwenye ushahidi wako ulieleza jinsi ulivyoona hiyi video na kutoa taarifa kwa mkuu wa kitengo?
Kaaya: Ni kweli.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama kwenye maelezo yako Polisi au hapa Mahakamani ulimtaja huyo Mkuu wako wa kitengo kwa jina?
Kaaya: Sikumtaja.
Mhe. Lissu: Unakumbuka nilikuuliza maswali mengi juu ya kesi mbalimbali zilizofunguliwa na watu tofauti tofauti kuhusu masuala ya Katiba na mabadiliko yake.
Kaaya: Nakumbuka.
Mhe. Lissu: Waelelze majaji kama unafahamu au hufahamu kwamba tarehe 13/06/2023 Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Wananchi ilitoa uamuzi kwamba Serikali ya Tanzania ibadilishe sheria ya Uchaguzi ili kuhakikisha sheria za uchaguzi zinakuwa za haki kwenye kesi ya BOB CHACHA WANGWE.
Ni kesi ya Bob Chacha Wangwe akiwa na Legal and Human Right Center wakiwashitaki AG, Tume ya Uchaguzi. Alikuwa anawapa full citation hapo majaji anawatajia na namba ya kesi hiyo.
Mhe. Lissu: sasa kuzuia uchaguzi ni uhaini mnasema hivyo kwenye ushahidi wako ulieleza kuzuia uchaguzi bila kufuata utaratibu wa kisheria kama vile kupata amri ya mahakama ni kuitisha serikali.
Kaaya: Nakumbuka.
Mhe. Lissu: Utaratibu huo wa namna ya kuzuia uchaguzi upo katika sheria gani?😂
Kaaya: Sifahamu.
Ushahidi ni kazi sana jamani.
Leo kumbukeni kuna ile kesi yetu pia niliyofunguliwa na Viongozi wa Chama ndio inaanza muda huu ila Mimi siendi wataingia Mawakili wetu kwa niaba yetu.🤦🏾♀️
Mhe. Lissu: Katiba unaifahamu shahidi?
Kaaya: Ndio naifahamu.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama upo utaratibu wa kuzuia uchaguzi mkuu?
Kaaya: Haupo. Haujaanishwa kwenye Katiba.
Mhe. Lissu: kwahiyo utaratibu haupo?
Kaaya: Zipo sheria zingine lakini.
Mhe. Lissu: Hivi unaelewa swali langu au unatuchelewesha kwenda kwenye mazishi?
Kaaya: haupo
Mhe. Lissu: Je ni kweli Uchaguzi mkuu wa Tanzania unaendeshwa na inayoitwa Tume Huru ya Uchaguzi?
Kaaya: Ni kweli.
Mhe. Lissu: Je ni kweli Katiba inasema tume ni chombo huru na haitakiwi kuingiliwa na Mamlaka au mtu yeyote?
Kaaya: Sikumbuki.
Mhe. Lissu: Anasomewa Katiba hapa ibara ya 74(11) kuhusu Tume na uhuru wake na pia anasomewa sheria ya Uchaguzi kuhusu wajibu wa Tume.
Kwamba tume haitakiwi kupokea maelekezo yoyote kutoka serikali wala chombo chochote cha serikali.
Kaaya: Ni sahihi.
Part 104 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.