Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 103

Mahakama imetulia sana hata hakohoi mtu baada ya hiyo speech.

Watu wameingiwa ubaridi ni kama maneno yamewaingia kila aliyepo hapa.

Jaji amewasha kipaza sauti na kumwambia shahidi uko chini ya kiapo.

Endeleeni.

Mhe. Lissu: Ni kweli au sio kweli hiyo video ya Tarehe 03/04 ilichapishwa kwenye Jambo Tv na mitandao mingine na walichapisha Jambo Tv wenyewe?

Kaaya: Aliyechapisha sifahamu.

😂😂😂 kumbukeni kosa la Lisu ni kuchapisha na kusambaza.

Mhe. Lissu: Ni kweli Mkutano wangu wa tarehe 03/04 ulirushwa mubashara na Jambo Tv?

Kaaya: Ni kweli.

Mhe. Lissu: Na ni kweli au sio kweli mimi sina uhusiano wowote na Jambo TV?

Kaaya: Mimi sikufanya upelelezi wa kuhusu wahusika wa Jambo TV ni akina nani.

Mhe. Lissu: Ile Flash Disk XIOXIA yenye rangi nyeupe unaikumbuka ulisema.

Kaaya: ndio nakumbuka

Mhe. Lissu: Je uliandika aina hiyo ya Flash na rangi yake kwenye maelezo yako Polisi?

Kaaya: Sikuandika.

Mhe. Lissu: Umezungumza sana kuhusu video na kuwaonyesha wakubwa zako na kuipakua na kuweka kwenye flash disk umezungumza sana asa waeleze majaji kama umewasilisha hiyo flash disk au hiyo video mahakamani hapa.

Kaaya: Bado sijaiwasilisha.

Mhe. Lissu: Ni sahihi nikisema hakuna mtu aliyeiona isipokuwa wewe hiyo video, Majaji hawajaona, Mawakili hawajaona na mimi sijaona.

Kaaya: Ni kweli.

Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama unafahamu au hufahamu hiyo video vilevile haikuwasilishwa wala kuonyeshwa kwenye committal Kisutu?

Kaaya: Sifahamu.

Mhe. Lissu: Sasa shahidi unakumbuka kwenye ushahidi wako ulieleza jinsi ulivyoona hiyi video na kutoa taarifa kwa mkuu wa kitengo?

Kaaya: Ni kweli.

Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama kwenye maelezo yako Polisi au hapa Mahakamani ulimtaja huyo Mkuu wako wa kitengo kwa jina?

Kaaya: Sikumtaja.

Mhe. Lissu: Unakumbuka nilikuuliza maswali mengi juu ya kesi mbalimbali zilizofunguliwa na watu tofauti tofauti kuhusu masuala ya Katiba na mabadiliko yake.

Kaaya: Nakumbuka.

Mhe. Lissu: Waelelze majaji kama unafahamu au hufahamu kwamba tarehe 13/06/2023 Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Wananchi ilitoa uamuzi kwamba Serikali ya Tanzania ibadilishe sheria ya Uchaguzi ili kuhakikisha sheria za uchaguzi zinakuwa za haki kwenye kesi ya BOB CHACHA WANGWE.

Ni kesi ya Bob Chacha Wangwe akiwa na Legal and Human Right Center wakiwashitaki AG, Tume ya Uchaguzi. Alikuwa anawapa full citation hapo majaji anawatajia na namba ya kesi hiyo.

Mhe. Lissu: sasa kuzuia uchaguzi ni uhaini mnasema hivyo kwenye ushahidi wako ulieleza kuzuia uchaguzi bila kufuata utaratibu wa kisheria kama vile kupata amri ya mahakama ni kuitisha serikali.

Kaaya: Nakumbuka.

Mhe. Lissu: Utaratibu huo wa namna ya kuzuia uchaguzi upo katika sheria gani?😂

Kaaya: Sifahamu.

Ushahidi ni kazi sana jamani.

Leo kumbukeni kuna ile kesi yetu pia niliyofunguliwa na Viongozi wa Chama ndio inaanza muda huu ila Mimi siendi wataingia Mawakili wetu kwa niaba yetu.🤦🏾‍♀️

Mhe. Lissu: Katiba unaifahamu shahidi?

Kaaya: Ndio naifahamu.

Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama upo utaratibu wa kuzuia uchaguzi mkuu?

Kaaya: Haupo. Haujaanishwa kwenye Katiba.

Mhe. Lissu: kwahiyo utaratibu haupo?

Kaaya: Zipo sheria zingine lakini.

Mhe. Lissu: Hivi unaelewa swali langu au unatuchelewesha kwenda kwenye mazishi?

Kaaya: haupo

Mhe. Lissu: Je ni kweli Uchaguzi mkuu wa Tanzania unaendeshwa na inayoitwa Tume Huru ya Uchaguzi?

Kaaya: Ni kweli.

Mhe. Lissu: Je ni kweli Katiba inasema tume ni chombo huru na haitakiwi kuingiliwa na Mamlaka au mtu yeyote?

Kaaya: Sikumbuki.

Mhe. Lissu: Anasomewa Katiba hapa ibara ya 74(11) kuhusu Tume na uhuru wake na pia anasomewa sheria ya Uchaguzi kuhusu wajibu wa Tume.

Kwamba tume haitakiwi kupokea maelekezo yoyote kutoka serikali wala chombo chochote cha serikali.

Kaaya: Ni sahihi.

Part 104 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 104

Mhe. Lissu: Sasa waeleze majaji kuwa serikali haihusiki chochote na uchaguzi na uchaguzi uko chini ya Tume huru?

Kaaya: Hapo ni kweli serikali haihusiki ni tume ndio inahusika.

Mhe. Lissu: Sasa naambiwa nilitengeneza nia ya kuhamasisha wananchi wazuie uchaguzi mkuu unalifahamu hilo?

Kaaya: Inategemea.

Mhe. Lissu: Inategemea nini wewe Polisi mi nakwambia kuhusu mashitaka yangu. Hiyo hati umeisoma? Unajua nashitakiwa na nini?

Kaaya: Mimi sijaisoma hiyo Hati ya Mashitaka.

Mhe. Lissu: Kwahiyo hujui mashitaka yanasema nini? Kama hujaisoma huwezi kuijua.

Kaaya: amenyamaza anatoa macho.😂

Mhe. Lissu: Haya umegoma kujibu. Mimi nakuacha tuendelee. 😂

Mhe. Lissu: Kwenye maneno ninayotuhumiwa nayo sijaitaja kabisa serikali?

Kaaya: umeitaja kwa namna fulani hujataja kwa uwazi.

Mhe. Lissu: Hiyo namna fulani ndio wamekufundisha akina Kingai ambao nao pia sio Mawakili wamekudanganya umekalili na unakimbia na haya mambo ya uongo unaona unavoteseka hapa sasa nakusomea maneno yaliyopo kwenye hati ya mashitaka

"Walisema msimamo huu unaashiria uasi ni kweli kwasababau tunasema tutazuia uchaguzi hii ndio namna ya kupata mabadiliko. Tutaenda kukinukisha sana.

Hayo ndio maneno nashitakiwa nayo sasa katika hayo maneno kuna neno serikali?

Kaaya: Hapo neno Serikali lipo kwa maana ukitafsiri

Mhe. Lissu: Nakuuliza kuhusu maneno niliyosema mimi nimetaja serikali?

Kaaya: kwenye maneno hujataja ila lipo.

Anasimama Job Mrema anasema tuna pingamizi tunaona shahidi ameshajibu hili Swali.

Jaji: Hebu tuendelee sioni pingamizi hapo.

Mhe. Lissu: Kwenye hayo maneno ninayosadikika kuyasema kama nimetaja Tume huru ya Uchaguzi?

Kaaya: Hujataja Tume Huru ya Uchaguzi.

Mhe. Lissu: Hii habari ya kutishia serikali sasa ulisema umesoma Criminal Law? Ni kweli?

Kaaya: Ni kweli nimesoma Criminal Law.

Mhe. Lissu: Je umesoma Penal Code? Kanuni ya adhabu umeisoma. Wewe si umesoma LL.B?

Kaaya: Nimesoma.

Mhe. Lissu: Kifungu cha 39(2)(d) cha Penal Code sasa waeleze kwenye kifungu hicho neno kutishia kama limefafanuliwa?

Kaaya: Sikumbuki.

Mhe. Lissu: Neno lililotumika ni intimidation. Je waeleze kama hilo neno limefafanuliwa? Nikupe sheria usome ili unataka kuropoka.

Kaaya: Sikumbuki.

MheLissu: Nikikwambia hilo neno halijajatafsiriwa kokote kwenye Penal Code utasemaje?

Kaaya: Sikumbuki.

Mhe. Lissu: Je kwenye hati ya mashitaka hilo neno kutishia serikali limefafanuliwa?

Kaaya: Sikumbuki.

Mhe. Lissu: Hata kwenye hati ya mashitaka hicho kinachoitwa kutishia Serikali halijafafanuliwa utasemaje?

Kaaya: Sina uhakika.

Mhe. Lissu: Sasa naomba apatiwe maelezo yake exhibit D1 sasa tuyapitie shahidi na usinisumbue.

Je maneno yafuatayo ni ya kihaini yapo kwenye ukurasa wa 2 wa maelezo yako.

Umesema matamshi mengine ni-;

Umesema mambo ya majaji kuwa ma ccm na wanataka vyeo.

Umeyaona hayo maneno?

Kaaya: Ndio nayaona.

Mhe. Lissu: Sasa Je hayo maneno ni uhaini?

Kaaya: Hapana sio ya uhaini.

Mhe. Lissu: pia ulisema maneno mengine ambayo mimi nimeyasema kwamba nilisema wapinzani walienguliwa kwa amri ya Rais. Je hayo nayo ni Uhaini?

Kaaya: Inategemea. Wapelelezi wanajua.

Mhe. Lissu: Nakuuliza wewe hayo ni Uhaini? Kama kuna mtu mwingine anajua wewe umekuja kufanya nini hapa?

Kaaya: Mimi ni Mpelelezi lakini sijapeleleza hilo mimi.

Mhe. Lissu: Na mimi nataka kuchaguliwa kwenye kacheo fulani na nyie mnataka kuchaguliwa pia sasa mnafikiri tunafanyaje kwa mazingira haya. Je hayo pia ni uhaini.

Kaaya: sasa hadi nichunguze ndio nitajua.

Mhe. Lissu: Ulichunguza?

Kaaya: Mimi sio Mpelelezi. Sikuchunguza hili.

Mhe. Lissu: Unajua Uchaguzi wa Serikali za mitaa unaendeshwa na TAMISEMI?

Kaaya: Ni kweli.

Mhe. Lissu: Ni kweli kwamba uchaguzi huo unaendeshwa kwa kanuni za uchaguzi huo zinazotungwa na waziri?

Kaaya: Sifanyi kazi huko kwahiyo sifahamu.

Lissu: Huyo Waziri ni mteule wa Rais?

Kaaya: Mimi sijui.

Part 105, itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 105

Mhe. Lissu: Kwahiyo wewe hufahamu mtu anayeteua Mawaziri nchi hii wewe humfahamu?

Kaaya: Mawaziri wanateuliwa na Rais.

Mhe. Lissu: Kwahiyo Mohamed Mchengerwa ni mteule wa Rais Samia? Huyo ni waziri wa TAMISEMI.

Kaaya: Ni kweli.

Mhe. Lissu: Je ni kweli au sio kweli ni Waziri ambae anatoa tangazo la uchaguzi na ratiba yake ya huo uchaguzi wa serikali za mitaa?

Kaaya: Sina Uhakika.

Mhe. Lissu: Ni kweli au sio kweli wasimamizi wakuu wa uchaguzi huo ambao ni returning officer ni wakurugenzi wa halmashauri mbalimbali?

Kaaya: Sijui.

Mhe. Lissu: Ni kweli au sio kweli Wakurugenzi wote wa halmashauri za Wilaya ni wateule wa Rais?

Kaaya: Sifahamu.

Mhe. Lissu ; Askari Polisi mwenye cheo cha Inspector hafahamu wakurugenzi wanateuliwa na nani? Vituko na aibu. (Nimechomekea mimi hii)

Mhe.Lissu: Ni kweli kwamba watumishi wote wa serikali za mitaa wanaohusika na uchaguzi wa serikali za mitaa wanafanya kazi kwa niaba ya Rais au maelekezo ya Rais?

Kaaya: Sina Uhakika.

Mhe. Lissu: Ni kweli uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 kwa maelfu walienguliwa na kuzuiwa kugombea?

Kaaya: Sina uhakika.

Mhe. Lissu: Ni kweli au si kweli baada ya kuenguliwa kelele ikawa kubwa hadi Dr. Nchimbi katibu mkuu wa CCM alielekeza pia warudishwe?

Kaaya: Sina Uhakika.

Mhe. Lissu: Ni kweli baada ya kelele zote hizo Waziri wa Tamisemi Mchengerwa aliomba muda uongezwe na kubadili ratiba ya Uchaguzi?

Anasimama Renatus Mkude anasema Mheshimiwa Jaji imefika saa tano kamili naomba turuhusiwe kwenda msibani na tutafikisha salamu za rambirambi pia za Mshitakiwa.

Jaji Ndunguru: Shahidi tukutane kesho saa tatu asubuhi. Tunaahirisha shauri hili.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali
 
Tundu Lissu aiambia Mahakama: Tunafanya mambo ya hovyo kuliko Wazungu waliotutawala

Majaji wameingia na Shahidi naye kama kawaida ameingia yupo hapa, Inspekta wa Polisi John Kaaya.

Karani anasimama Criminal Session No. 19605 Jamhuri dhidi ya Tundu Lissu.

Iwapendeze naitwa Renatus Mkude Wakili wa Serikali niko na Job Mrema, Ignas Mwinuka, Harrison Lukosi, Winiwa Kasawa tunaiwakilisha Jamhuri. Na Mshitakiwa yupo. Lakini pia tuna jambo tunaomba kuiambia Mahakama.

Mhe. Lissu anasema na mimi niko tayari na pia nitakuwa na jambo la kuieleza Mahakama.

Renatus Mkude, tulipokea taarifa ya Msiba wa Msajili wa Mahakama Kuu kanda ya Shinyanga.

Tumekuwa na utaratibu wa kwenda kushiriki matukio kama haya na tulipanga kuhudhuria kwenye msiba huo kwa vile ni jambo la kibinadamu ilikuwa na rai yetu itakapofika saa tano twende tukamuage huyu ndugu yetu ili tuendelee kesho tena. Ni hayo tu.

Mhe. Lissu anasimama kwenye hilo mimi sina pingamizi lolote na ikiwapendeza wakienda kwenye huo msiba wanipelekee salamu zangu za rambirambi kwa wafiwa.

Lakini pia niwaeleze kuhusu watu waliokuwa wanazuiwa kuingia Mahakamani, nimesema sana jambo hili.

Kasoro juzi Jumatatu sikulizungumzia kwasababu niliambiwa wangeruhusiwa siku hiyo lakini walikuja wakazuiliwa hapo getini.

Kwa taarifa nilizonazo walichukuliwa na maafisa wa uhamiaji na baadae wakafukuzwa nchini ili wasiweze kuingia Mahakamani kushuhudia kesi hii.

Sasa waheshimiwa majaji hii ni mara ya tatu kwa watu wanaotaka kuja kuhudhuria mahakama hii kufukuzwa nchini.

Walianza na Ujumbe uliotoka Kenya ukiongozwa na Jaji Mkuu mstaafu wa Kenya, Willy Munyoki Mutunga.

Wakafuata Boniface Mwangi na Agatha Atuhire walikamatwa na kuteswa na kupelekwa mipakani na kutupwa.

Na sasa hili limetokea kwa raia wa Ujerumani na Marekani walioingia nchini kihalali kuja kutaka kuona kinaendelea nini.

Hii ni kesi kubwa kuliko zote ndivyo inasema Katiba yetu ni kesi inayo draw Regional and International attention.

Haya yaliyofanyika Kisutu tayari yapo kwenye Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa yapo katika mahakama za haki za binadamu na watu Afrika.

Kwa hiyo haya sio mambo madogo kabisa. Mahakama inapoingiliwa inasababisha sintofahamu kwenye mfumo wetu wote wa haki jinai ndani ya Taifa letu.

Mwaka 1958 kulikuwa na kesi kubwa sana katika Mahakama ya Wilaya Dar es salaam Kivukoni ambayo ni Regina Vs Julius Nyerere na wenzake wawili mmoja wapo Robert Makange na mwingine Rashid Bagdellah.

Wakoloni wa Kiingereza did not dare kuzuia watu kwenda kushuhudia kesi ya kiongozi wao na wanaofahamu historia ya nchi hii Mwalimu alitetewa na Wakili kutoka Wingereza.

Wakoloni hawakukataza pia hawakupiga watu wasiingie Mahakamani.

Kesi ya Jomo Kenyatta pia ilikuwa kubwa sana ambayo ilifanyika katikati ya Vita vya Mau Mau, Waingereza did not dare kuzuia watu kwenda kusikiliza the trial of Jomo Kenyatta ilifuatiliwa.

Mwaka 1956 mpaka 1961 tulikuwa na kesi ya Uhaini Afrika Kusini imeelezwa kwenye Long Walk to Freedom, Kesi ya Nelson Mandela hakuna mtu aliyepigwa wala kuzuiwa kwenda Mahakamani, hakuna watu walioteswa ili wasiingie Mahakamani.

Sasa nchi hii baada ya miaka 64 ya Uhuru Serikali yetu na vyombo vya Ulinzi na Usalama inazuia watu wasiingie Mahakamani kwenye nchi ambayo sheria zinasema mahakama ni ya wazi.

Tunafanya mambo ya hovyo kuliko Wazungu waliotutawala sisi hapa Tanganyika, walioitawala Kenya na wale wa Afrika Kusini, sasa mimi niko Gerezani na Mahakama imeshindwa kufanya lolote.

Sasa ili isije kuja kusemwa baada ya mimi na nyie majaji kutoweka hapa Duniani kuwa nilikuwa kwenye dhambi ya watu ambao walinyamaza kimya mambo haya kutokea. Nimesema kutimiza wajibu wangu na sitaki dhambi ya kunyamazia uovu au maovu, naomba kumalizia hapo.
1760546973915.jpg
1760546981303.jpg
 
Tundu Lissu aiambia Mahakama: Tunafanya mambo ya hovyo kuliko Wazungu waliotutawala

Majaji wameingia na Shahidi naye kama kawaida ameingia yupo hapa, Inspekta wa Polisi John Kaaya.

Karani anasimama Criminal Session No. 19605 Jamhuri dhidi ya Tundu Lissu.

Iwapendeze naitwa Renatus Mkude Wakili wa Serikali niko na Job Mrema, Ignas Mwinuka, Harrison Lukosi, Winiwa Kasawa tunaiwakilisha Jamhuri. Na Mshitakiwa yupo. Lakini pia tuna jambo tunaomba kuiambia Mahakama.

Mhe. Lissu anasema na mimi niko tayari na pia nitakuwa na jambo la kuieleza Mahakama.

Renatus Mkude, tulipokea taarifa ya Msiba wa Msajili wa Mahakama Kuu kanda ya Shinyanga.

Tumekuwa na utaratibu wa kwenda kushiriki matukio kama haya na tulipanga kuhudhuria kwenye msiba huo kwa vile ni jambo la kibinadamu ilikuwa na rai yetu itakapofika saa tano twende tukamuage huyu ndugu yetu ili tuendelee kesho tena. Ni hayo tu.

Mhe. Lissu anasimama kwenye hilo mimi sina pingamizi lolote na ikiwapendeza wakienda kwenye huo msiba wanipelekee salamu zangu za rambirambi kwa wafiwa.

Lakini pia niwaeleze kuhusu watu waliokuwa wanazuiwa kuingia Mahakamani, nimesema sana jambo hili.

Kasoro juzi Jumatatu sikulizungumzia kwasababu niliambiwa wangeruhusiwa siku hiyo lakini walikuja wakazuiliwa hapo getini.

Kwa taarifa nilizonazo walichukuliwa na maafisa wa uhamiaji na baadae wakafukuzwa nchini ili wasiweze kuingia Mahakamani kushuhudia kesi hii.

Sasa waheshimiwa majaji hii ni mara ya tatu kwa watu wanaotaka kuja kuhudhuria mahakama hii kufukuzwa nchini.

Walianza na Ujumbe uliotoka Kenya ukiongozwa na Jaji Mkuu mstaafu wa Kenya, Willy Munyoki Mutunga.

Wakafuata Boniface Mwangi na Agatha Atuhire walikamatwa na kuteswa na kupelekwa mipakani na kutupwa.

Na sasa hili limetokea kwa raia wa Ujerumani na Marekani walioingia nchini kihalali kuja kutaka kuona kinaendelea nini.

Hii ni kesi kubwa kuliko zote ndivyo inasema Katiba yetu ni kesi inayo draw Regional and International attention.

Haya yaliyofanyika Kisutu tayari yapo kwenye Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa yapo katika mahakama za haki za binadamu na watu Afrika.

Kwa hiyo haya sio mambo madogo kabisa. Mahakama inapoingiliwa inasababisha sintofahamu kwenye mfumo wetu wote wa haki jinai ndani ya Taifa letu.

Mwaka 1958 kulikuwa na kesi kubwa sana katika Mahakama ya Wilaya Dar es salaam Kivukoni ambayo ni Regina Vs Julius Nyerere na wenzake wawili mmoja wapo Robert Makange na mwingine Rashid Bagdellah.

Wakoloni wa Kiingereza did not dare kuzuia watu kwenda kushuhudia kesi ya kiongozi wao na wanaofahamu historia ya nchi hii Mwalimu alitetewa na Wakili kutoka Wingereza.

Wakoloni hawakukataza pia hawakupiga watu wasiingie Mahakamani.

Kesi ya Jomo Kenyatta pia ilikuwa kubwa sana ambayo ilifanyika katikati ya Vita vya Mau Mau, Waingereza did not dare kuzuia watu kwenda kusikiliza the trial of Jomo Kenyatta ilifuatiliwa.

Mwaka 1956 mpaka 1961 tulikuwa na kesi ya Uhaini Afrika Kusini imeelezwa kwenye Long Walk to Freedom, Kesi ya Nelson Mandela hakuna mtu aliyepigwa wala kuzuiwa kwenda Mahakamani, hakuna watu walioteswa ili wasiingie Mahakamani.

Sasa nchi hii baada ya miaka 64 ya Uhuru Serikali yetu na vyombo vya Ulinzi na Usalama inazuia watu wasiingie Mahakamani kwenye nchi ambayo sheria zinasema mahakama ni ya wazi.

Tunafanya mambo ya hovyo kuliko Wazungu waliotutawala sisi hapa Tanganyika, walioitawala Kenya na wale wa Afrika Kusini, sasa mimi niko Gerezani na Mahakama imeshindwa kufanya lolote.

Sasa ili isije kuja kusemwa baada ya mimi na nyie majaji kutoweka hapa Duniani kuwa nilikuwa kwenye dhambi ya watu ambao walinyamaza kimya mambo haya kutokea. Nimesema kutimiza wajibu wangu na sitaki dhambi ya kunyamazia uovu au maovu, naomba kumalizia hapo.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Leo Oktoba 16, 2025

Jana tuliishia part 105 so leo tunaendelea na-;

Part 106

Muda huu ni saa tatu asubuhi.

Tumefika Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es salaam.

Hali ya Mahakama ni nzuri.

Tunawashuhudia Waandishi wakichukua picha mgando na mnato kwa watu mbalimbali waliopo hapa Mahakamani.

Askari Magereza wale wa Kikosi Maalum yaani KM wako hapa ndani ya Chumba cha Mahakama wanazunguka zunguka kama wanakagua lindo vile.

Wasaidizi wawili wa Majaji tunawaona wako hapo mbele, Mwanamke mmoja na Mwanaume Mmoja kwa wasiofahamu hawa wanaoitwa Wasaidizi wa Majaji kitaaluma ni Mahakimu Wakazi.

Cheo chao ni sawa na Mahakimu waliopo Kisutu pale hawa hufanya kazi ya kuwasaidia majukumu ya kufanya research mbalimbali za masuala ya kisheria.

Wameingia hapa Majaji watatu kama kawaida ambao ni Jaji Dunstan Ndunguru, James Karayemaha na Ferdinand Kiwonde. Wakiwa kwenye magauni yao nasikia yanaitwa majoho mekundu.

Limesomwa shauri hapa na karani na amesimama Renatus Mkude Wakili Mkuu wa Serikali na ametambulisha wenzake muda huu, anasema upande wa Jamhuri wako tayari.

Mhe. Lissu ameulizwa yuko tayari na anaomba akumbushwe shahidi aliishia wapi kujibu maswali yake.

Amekumbushwa anasema anaomba aanze sasa.

Mhe. Lissu: Shahidi umeamka salama?

Kaaya: Nimeamka salama Mheshimiwa Lissu.

Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama ulieleza kwamba fomu No. 145 kwamba haikusomwa wakati wa committal Kisutu?

Kaaya: Sikuwepo Kisutu.

Mhe. Lissu: Je umeileta hapa Mahakamani?

Kaaya: Sijaileta pia.

Mhe. Lissu: Sasa turudi tulipoishia jana. Maelezo yako Polisi ulitoa maneno mengi ikiwemo "Baadhi ya maneno mengine aliyotamka Rais alitoa maelekezo kuwa hakikisheni wapinzani hawaendi kokote....."

Naomba majaji shahidi apewe Exhibit D1 ili twende pamoja.

Sasa shahidi baada ya kelele nyingi za wapinzani kuenguliwa akiwemo Nchimbi alisema mambo kuhusu uchaguzi.

Je unafahamu Mchengerwa Waziri wa Tamisemi alisema wakikata rufaa wagombea walioenguliwa watarudishwa?

Kaaya: Sikumbuki.

Mhe. Lissu: je unafahamu Mchengerwa aliongeza muda wa rufaa ili watu wakate rufaa?

Kaaya: Sikumbuki.

Mhe. Lissu: Unafahamu wagombea angalau wa Chadema kwa maelefu walikata rufaa ndani ya huo muda wa rufaa ambao uliongezwa na Mchengerwa?

Kaaya: Sikumbuki.

Mhe. Lissu: Rufaa za Uchaguzi wa serikali za mitaa zinasikilizwa na Kamati za Wilaya?

Kaaya: Sina kumbukumbu.

Mhe. Lissu: Je unafahamu wenyeviti wa kamati za rufaa za Wilaya ni Makatibu tawala wa Wilaya ambao ni wateule wa Rais?

Kaaya: Sina Uhakika.

Mhe. Lissu: wote waliokata rufaa waliorudishwa hawafiki hata 10?

Kaaya: Hilo silifahamu.

Mhe. Lissu: Ila maneno yangu unasema ya uongo kuhusu uchaguzi wakati wewe kila kitu hujui?

Kaaya: Kimya.

Mhe. Lissu: Sasa watu wanaosimamia uchaguzi wote wa serikali za mitaa ni watu wa Rais kama nilivyokuonyesha mimi nakosea wapi?

Kaaya: Rais akishachaguliwa anafanya kazi kwa niaba ya Serikali na sio Chama chake.

Mhe. Lissu: Kwahiyo akikosea na mimi nikimpinga nikisema anafanya mambo ya hovyo kuengua watu wa Chadema nakosea wapi? Hapo anakuwa ameacha kuwa mwana CCM?

Kaaya: Haachi kuwa Mwanaccm.

Mhe. Lissu: Sasa wewe fundi wa Viyoyozi hebu tuambie kazi za Mwenyekiti wa CCM anazifanya nani kipindi akiwa Rais?

Kaaya: Anaendelea kuzifanya mwenyewe.

Mhe. Lissu: unafahamu zaidi ya asilimia 98 ya wenyeviti wa mitaa waliochaguliwa ni wa CCM?

Kaaya: Sifahamu.

Mhe. Lissu: Je unafahamu kwamba mwaka 2014 kwenye Uchaguzi wa Vijiji na mitaa ambao wagombea wa upinzani hawakuenguliwa walipata asilimia 33 ya viti vyote vya serikali za mitaa?

Kaaya: Sina Takwimu hizo.

Mhe. Lissu: Je unafahamu mwaka 2014 asilimia zaidi ya 20 walienda kwa upinzani ulienda kwa upinzani?

Kaaya: Hilo nilisikia.

Mhe. Lissu: Uchaguzi wa 2019 ambao wagombea walienguliwa wa upinzani CCM ilipata wenyeviti wa mitaa 100%?

Kaaya: Sikumbuki.

Part 107 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 107

Mhe. Lissu: Uchaguzi wa 2019 Serikali za mitaa CCM ilipata asilimia 98 ya wenyeviti wa Vijiji?

Kaaya: Sina Kumbukumbu

Mhe. Lissu: Je unafahamu uchaguzi mkuu wa 2020 ndio ulikuwa na wagombea wengi wa ubunge kuenguliwa kuliko chaguzi yoyote toka uchaguzi uanze?

Kaaya: Ukikosa sifa unaenguliwa tu.

Mhe. Lissu: Wewe ni fundi viyoyozi mambo ya sifa unayajulia wapi? Haya jibu swali langu.

Kaaya: Sikuwahi kufanya huo utafiti.

Mhe.Lissu: Kwamba wagombea 63 kati ya 244 walienguliwa wa ubunge?

Kaaya: Sijawahi kuwa mwanaCHADEMA.

Mhe. Lissu : Hata magazeti husomi ndugu yangu?

Kaaya: Sifahamu mimi.

Mhe. Lissu: wagombea wa udiwani 1150 kati ya 3900 walienguliwa mwaka 2020 unafahamu?

Kaaya: Sina takwimu mimi. Sijui.

Mhe. Lissu: Wagombea wa CCM 872 wa udiwani walipita bila kupingwa kutokana na kuenguliwa kwa wapinzani kwa mujibu wa taarifa rasmi ya tume?

Kaaya: Sijawahi kuisoma hiyo taarifa.

Kaaya: Waheshimiwa Majaji mimi nilisikia wagombea walipita bila kupingwa lakini idadi ya 28 sikumbuki.

Mhe. Lissu: Mimi nasoma ndio maana najua walikuwa 28 wewe unatengeneza Viyoyozi.

Kaaya: Mimi ni askari Polisi sio fundi viyoyozi.

Mhe. Lissu: Kwahiyo hukusema hapa kuwa umesomea Air Condition? wewe ndio ulituambia haya mambo ya viyoyozi au nani alituletea?

Kaaya: Nilisema basi yaishe.

Mhe. Lissu: Kwahiyo toka 1995 hakuna mgombea hata mmoja wa CCM amewahi kuenguliwa kwa kukosa sifa?

Kaaya: Unaweza kuwa sahihi.

Mhe. Lissu: Waangalizi wa AU wa uchaguzi umewahi kuwasikia? AU election expert mission walitoa ripoti inayolalamikia kuenguliwa kwa wapinzani?

Kaaya: Nimewasikia lakini ripoti sikuisikia.

Mhe. Lissu: Je jumuiya ya Ulaya walituma EU election observation mission walituma waangalizi pia na kulalamikia kuenguliwa kwa wapinzani?

Kaaya: Silijui kiukweli.

Mhe. Lissu: Ongeza sauti basi unamnong'oneza nani?

Kaaya: Sijui

Mhe. Lissu: Je waangalizi kutoka jumuiya ya madola ambao ni Commonwealth observer group walitoa ripoti kulalamikia vitendo vya kuengua wapinzani?

Kaaya: Kweli.

Mhe. Lissu: Watizamaji wa Umoja wa Afrika walipendekeza kuwa serikali iondoe vikwazo vya kiuchaguzi kabla ya uchaguzi wa 2025?

Kaaya: Sina uhakika kabisa.

Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama unafahamu mashirika ya kiraia walituma waangalizi Tanzania?

Kaaya: Walitumwa kwenda wapi?

Mhe. Lissu: Kuja Tanzania.

Kaaya: Basi msemaji wa Serikali anazo hizo taarifa.

Mhe. Lissu: Msemaji wa Serikali ni shahidi namba ngapi?

Kaaya: Sijui

Mhe. Lissu: Shahidi hapa ni wewe jibu swali langu.

Kaaya: Sijui.

Mhe. Lissu: Sasa unajua watizamaji wa ndani pia wa Uchaguzi huu wapo nao wamekuwa wakitizama uchaguzi miaka yote wanaitwa Tanzania Election Monitoring Committee ikijumuisha viongozi wa dini na chuo kikuu cha Dar es salaam (TEMCO)?

Kaaya: Ni sahihi.

Mhe. Lissu: Je umewahi kusoma ripoti ya hao TEMCO hata moja?

Kaaya: Sijawahi kuziona hata kwa sura wala kuzisikia.

Mhe.Lissu: so huwezi kufahamu mashirika haya kuwa nayo yamelalamikiwa mfumo wa uchaguzi na kuondolewa kwa wapinzani?

Kaaya: Sifahamu na sio majukumu yangu.

Mhe. Lissu: Sasa mimi kulalamikia uchaguzi unasema nasema uongo kwanini wakati huna unalojua?

Kaaya: Kusema Rais ndio niliona kuna shida.

Mhe.Lissu: Uchaguzi wa mwaka huu mgombea Urais wa ACT Wazalendo ameenguliwa na Tume ya Uchaguzi?

Kaaya: Hajakidhi vigezo.

Mhe. Lissu: Kaenguliwa na tume au hajaenguliwa?

Kaaya: Kaenguliwa na tume kweli.

Mhe. Lissu: Je Mwenyekiti wa Tume na Majaji waliokataa kesi jana wote si wateuliwa wa Rais?

Kaaya: Ni kweli.

Mhe. Lissu: sasa ulitegemea Mpina apate haki kutoka wapi kama wote aliokuwa anategemea wampe haki ni wateule wa Rais?

Kaaya: Ingekuwa ngumu sana kiukweli.

Part 108 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 108.

Mhe. Lissu: Jana ulisema hujasoma hati ya mashitaka vipi leo umeisoma?

Kaaya: Nimeisoma.

Mhe. Lissu: anamsomea hati ya mashitaka yote.

Sasa nataka useme kuhusu tuhuma nilidhihirisha nia kwa kitendo cha kusema na kuchapisha.

Swali langu.

Hayo maneno yapo kwenye video clip?

Kaaya: Ni sahihi.

Mhe. Lissu: Tukitaka kujua maana ya Kuchapisha tuangalie Sheria ya mitandaoni yaani Cyber Crime Act?

Kaaya: Tunaweza kupata kupitia sheria ya makosa ya mtandaoni na sheria zingine.

Mhe. Lissu: Zingine ni zipi mimi najua moja.

Kaaya: kama zipo

Mhe. Lissu: mimi sizijui wewe niambie ni zipi?

Kaaya: Nikizijua nitakwambia.

Mhe. Lissu: Sasa mimi sihangaiki na huo umbea wewe soma Section 3 ya hiyo Sheria ili usitupotezee muda. Je kwenye hiyo Sect 3 kuna maana ya neno uttering yaani kusema?

Kaaya: kuna neno hapa offering in other way

Mhe. Lissu: We afande unasikia kweli? Nimesema neno uttering sio offering

Kaaya: Uttering halipo hapa.

Mhe. Lissu: Tafuta neno lingine ambalo ni publishing

Kaaya: Lipo means distributing, transmitting, disseminating, circulating, delivering, exhibiting, exchanging, barter, printing, copying, selling,…

Mhe. Lissu: Waeleze majaji sasa hiyo video iliyoko kwenye mtandao wa Jambo Tv nani ameiweka huko?

Kaaya: wewe ndio uliiweka.

Mhe. Lissu: je mimi nilikuwa na password yaani nywila.

Kaaya: Sina Uhakika.

Mhe. Lissu: Nani aliyeisambaza?

Kaaya: Wewe kupitia Jambo TV.

Mhe. Lissu: Nani aliyedisseminate?

Kaaya: Wewe.

Mhe. Lissu: Nani aliyecirculate?

Kaaya: wewe kupitia Jambo TV.

Mhe. Lissu: Nani aliyeonyesha?

Kaaya: Jambo TV ndio alionyesha.

Mhe.. Lissu: Nani aliyefanya Exchange. Kutoa Jambo kwenda Clouds kwenda The Chanzo kwenda vyombo vingine?

Kaaya: Sifahamu.

Mhe. Lissu: Nani aliyefanya printing and bartering?

Kaaya: Sifahamu.

Mhe. Lissu: Copying je?

Kaaya: sijui.

Mhe.Lissu: je kuna malipo hawa watu wa youtube huwalipa hao wanaorusha haya video?

Kaaya: Nasikia ila sijui.

Mhe. Lissu: sasa nani aliyepata pesa za viewers wa hizo videos?

Kaaya: sijui.

Mhe. Lissu: Sasa niliwezaje kuingia kwenye hizo system za Jambo Tv na kusambaza?

Kaaya: Hilo sifahamu kabisa.

Mhe.Lissu: Kama hufahamu kama nilikuwa na uwezo au sina unawezaje kusema niliingia na kufanya. Tuseme ukweli wa Mungu. Hebu tueleze.

Kaaya: Lengo lake kuita waandishi ilikuwa ni ili wasambaze.

Mhe. Lissu: Unakumbuka nilikuuliza idadi ya watu waliotazama na kusema wamecomment?

Kaaya: Nakumbuka.

Mhe. Lissu: Je umepata wasaa wa kutizama tena?

Kaaya: Sijatizama.

Mhe. Lissu: Je bado ni msimamo wako kuwa hiyo video ina comments 300 tu?

Kaaya: niko sahihi.

Mhe. Lissu: Je sasa umetoa kielelezo chochote kuthibitisha idadi hiyo ya comments 300. Sina maswali zaidi na shahidi huyu.

Kaaya: Sijatoa kabisa.

Mh. Lissu sina swali lingine.

Anasimama Katuga kwa ajili ya Re Examination kwa shahidi.

Majaji wanaandika kidogo.

Katuga: Nikupe Pole kwa maswali mengi ya siku nyingi.

Sasa relax umesharelax tayari?

Kaaya: sawa

Katuga: Uliulizwa kuhusu ajira yako na ulianza lini haswaa.

Kaaya: Ukiteuliwa kuanza mafunzo ya Polisi ndio ajira yako inakuwa imeanza hapohapo. Ukishahitimu ndio unaweza kuanza kutekeleza majukumu yako.

Katuga: Sasa ifafanuliwe Mahakama.

Kaaya: Nilipoteuliwa ndio nilianza kuwa askari na nilipotamka mwaka 2006 ndio mwaka niliohitimu mafunzo na kuanza kazi rasmi.

Katuga: Yale maelezo yako ya Polisi uliulizwa mambo mengi sana kuhusu hili limo na hili halimo.

Kaaya: Nilikuwa naelezea substance ya ushahidi wangu lakini ushahidi niliouwasilisha nilikuwa naelezea zaidi kuhusu maelezo niliyokwisha aandika.

Nilichokifanya ni kuelezea kwa upana kile nilichokuwa nimekiandika kwenye maelezo yangu.

Part 109 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 109

Katuga: Uliulizwa kuhusu suala la Notebook kama hiyo notebook umeileta. Je kwanini hujaileta.

Lissu anasimama napinga hilo swali la sikufika huko hakutoa sababu za kwanini hakuileta.

Katuga: Mhe. Jaji alimzuia shahidi asiendelee kutoa maelezo kwanini hakuleta.

Jaji: Hayo mambo ni mapya hatuwezi kukuruhusu. Uliza swali lingine.

Katuga: uliulizwa nani aliyechapisha ulisema ni wewe siku nyingine ukasema sifahamu na leo pia umesema ni yeye kupitia Jambo Tv. Sasa sisi tunataka ufafanuzi

Kaaya: Kupitia Jambo TV alichapisha maudhui yaliyopo kwenye hati ya mashitaka kitendo cha yeye kuwaalika wanahabari na kutoa maudhui yale ni tayari alikuwa ameridhia kutoa maudhui yale mtandoani.

Katuga kila baada ya swali moja anafanya vikao na mawakili wenzake sita hapa Mahakamani. Hii Re Examination yao imekuwa ngumu sana aiseee. Wanahangaika halafu ni kama shahidi anawajibu namna ambavyo walikuwa hawatarajii. Hawayafurahii majibu ya shahidi wao kabisa.

Katuga: Waheshimiwa Majaji naomba tuishie hapa kwenye maswali ya ufafanuzi kwa shahidi wetu. 😂

Hadi majaji wamecheka hapa kimya kimya. Hii re examination ilikuwa ngumu sana. Mhe. Lissu kamshona shahidi hadi upande wa Jamhuri wameshindwa kujua Shahidi atoe ufafanuzi wa jambo gani.😀

Jaji shahidi unaruhusiwa kuondoka. Tunakushukuru kwa ushahidi wako.

Insp. John Kaaya amejaribu kutoka kwa speed kidogo amejikwaa hapa kwenye kiti ametaka kumdondokea Askofu Mwamakula maana amekaa nae karibu na kizimba pale. 😂

Watu wamecheka inaonekana huyu Polisi alikuwa amechoka sana hii kazi kwakweli. ametoka kama haamini kweli amemaliza huu msala.

Amesima Renatus Mkude anasema tunae Shahidi wa tatu ambae ni SAMWEL ELIBARIKI KAAYA.

Jaji sasa huyu shahidi nae aje tuendelee.

Ananingia hapa Askari Mfupi wa kimo, ana kipara na ndevu nyinginyingi kidogo ambazo hazina afya zile ndevu kipilipili.

Jaji unaitwa nani?

Naitwa Samwel Elibariki Kaaya.

Mkaguzi wa Jeshi la Polisi.

Anaangalia kwa chini chini kwa kumuangalia tu muonekano wake inaonekana ana roho ngumu sana.

Anasema ana miaka 39.

Dini yangu ni Mkristo.

Anapelekewa Biblia aweze kuapa.

Anaishika mkono wa Kulia na amenyanyua juu.

Naapa ushahidi nitakaoutoa ni wakweli ewe Mwenyezi Mungu nisaidie.

Renatus Mkude anasimama naomba aongozwe na Thawabu Issa Wakili wa Serikali.

Huyu Thawabu Issa Wakili wa Serikali ndo yule alijifanya kurusha ngumi juzi kati anajikuta Rashid Matumla.

Amesimama ana kipara kama cha ushahidi.

Thawabu: Uongee kwa Sauti shahidi.

Jaji: Na wewe Wakili ongeza sauti sasa.

Thawabu: Kitengo gani upo?

Samwel Kaaya: Kitengo cha picha Kamisheni ya Uchunguzi sayansi jinai.

Sasa I tabidi huyu Shahidi nimuite Samweli maana na yeye ni Kaaya kama aliyetoka.😂

Thawabu: Kinajihusisha na nini kitendo hicho.

Samwel: Kitengo hicho kinajihusisha upigaji picha wa matukio mbalimbali lakini pia kurekodi matukio mbalimbali ya uhalifu. Kurekodi picha mjongeo za watuhumiwa wa uhalifu.

Thawabu: Upo kama nani kitengoni hapo?

Samwel: Niko kama mtaalamu wa picha baada ya kuteuliwa na DPP na kutangazwa na gazette la serikali GN. No. 745/2022.

Thawabu: Majukumu yako ni nini?

Samwel: Kupiga picha, kurekodi matukio ya uhalifu, kufanya uchunguzi wa picha mbalimbali kwa maana ya picha mjongeo na mnato.

Elimu yangu imegawanyika katika makundi mawili.

Elimu ya Kipolisi mwaka 2013/2014 nilihudhuria mafunzo ya awali ya Polisi. Recruit Course chuo cha Polisi Moshi CCP. Na mwaka 2014 nilimaliza na kutunukiwa Certificate of Competence.

Huko CCP Moshi nilijifunza criminal Laws, Evidence Law, Criminal Procedure, Bionnet, Parade Training, Parade la kutuliza ghasia, Self defense kwa maana ya Judo na Karate na Medani za Kivita.

Thawabu: Ulitunukiwa nini?

Samwel: Cheti cha Umahiri.

Thawabu: Kingine nini?

Samwel: Nilipata cheo cha awali cha Police Constable.

Part 110 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 110

Thawabu: Baada ya kuwa Police Constable nini kilifuata?

Samwel: Nilipangiwa kitengo cha picha yani sayansi jinai.

Mwaka 2014 nilianza mafunzo yanayohusu upigaji wa picha zote yaani video na picha mnato. Nilijifunza pia SOP for Photography laboratory.

Mafunzo hayo yalichukua miezi 6 hayo ya SOP.

Mafunzo mengine mwaka 2021 hadi 2022 nilihudhuria mafunzo ya mkaguzi msaidizi wa jeshi la polisi kwa maanaa ya ACP niliyachukulia Moshi huko.

Yalikuwa ya miezi minne nilijifunza leadership, criminal procedure na sheria ya ushahidi Evidence Law, Criminal Law na Parade, First Aid, Medani za Kivita, Arresting, Drill Parade. Nilipata cheo cha mkaguzi msaidiz wa Polisi.

Kundi la pili linahusu elimu ya ujuzi yaani professional qualification mwaka 2010 nilihudhuria mafunzo ya stashahada ya teknolojia ya habari na mawasiliano yaani diploma in Information technology.

Pia nilihudhuria Mafunzo taasisi ya Uhasibu arusha. Anajisemea hapa alijifunza multimedia, web designing, graphical designing , OOP Object oriented programing language, sema anaongea haraka kama chiriku majaji wanashindwa kumpata vizuri mda mwingine.

Anaendelea hapa alijifunza Computer mathematics, business mathematics, communication skills, database management baada ya hapo nilitunukiwa diploma in Information technology.

Anasema pia alihudhuria mafunzo 2015 ya forensic video examination and data dot technology and itching technology katika chuo cha HAMASCRA College , Gauteng Province , South Africa.

Akajifunza video analysis, email analysis, facial recognition, motor vehicle chassis number examination mafunzo yalichukua muda wa miezi 6 na akapata certificate of competence.

Anaulizwa tena kama anaujuzi mwengine?

Anasema 2016 hadi 2019 alihudhuria mafunzo ya shahada ya kwanza ya elimu ya mawasiliano alisoma IFM.

Anaanza kulist masomo alisoma data base management, computer network,object oriented programming language, supply chain management, artifical intelligence technology, development studies😂😂wanatuchosha tuu hawa.

Alipomaliza alipata Bachelor of Science in Information technology 2019.

Mwaka 2024 alihudhuria mafunzo ya CCTV Forensic Gandinaghar, gujarat state India. Sema shahid nae kutamka alikosoma hawezi anataka atuandikie hapa na hakuna ubao.

Anasema alisoma National Forensic Science University alisoma kwa miezi 3 CCTV surveillance au monitoring, NVR technology network video recorder vs digital video recorder baada ya kuhitimu alipewa certificate of attendance.

Anasema Shughuli hizi kazifanya kwa miaka 12 (utaalamu wa picha)

Anaulizwa maabara ya uchunguzi wa picha inafanyaje kazi?

Anasema wanafanya kwa kuzingatia SOP Standard Operating Procedure za maabara.

Anakuwa na mtaalam mchunguzi wa maabara anaitwa Photographic Expert majukumu ya huyu mtaalamu ni kupokea barua mbalimbal kutoka kwa requesting authorities na kuhakiki vielelezo mbalimbali vinavyotoka sehemu mbalimbal, kuhakiki kama vielelezo vimekidhi matakwa ya kiuchunguzi.

Baada ya kuridhika vile vielezo vimekidhi matakwa hayo vinasajiliwa kwenye laboratory register book yaani PF113 akimaliza kusajili anatoa namba ya usajili kwa ajili ya ufuatiliaji.

Akishatoa hio namba anafungua jalada la uchunguzi wa kimaabara kwa kurejea zile namba alizoziandika

Baada ya kusajili namba hio mchunguzi atapeleka jalada kwa mkuu wa kitengo kwa ajli ya assignment

Mkuu wa kitengo akishapelekewa ataasign mchunguzi ni kwa ajili ya kumantain chain of custody baada ya mkuu wa kitengo kumuassign mchunguzi ataondoka na jalada na vielelezo hivyo.

Mchunguzi akiondoka na vielezo hivyo vinaenda kufanyiwa kazi anasema hapa ofisi yao inafanya kazi mtindo wa FIFO First in First Out yaani kilichoanza kuja ndiko kitafanyiwa kazi.

Kanuni ya FIFO ikizingatiwa mchunguzi ataanza kuja na ataendelea na uchunguzi wake uchunguzi unafanyika katika njia kuu 3.

Wakipokea kielelezo cha picha mjongeo au video utaratibu unakuwa hivi.

Part 111 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 111

Wakipokea kielelezo cha picha mjongeo au video utaratibu unakuwa hivi-;

1. Programu endeshi "operating system"
2. Programu Chunguzi "Forensic Software"
3. Programu Linzi "Security Software"

Hizo ndio njia zinazotumika kufanya uhakiki wa video au picha wakizipokea.

Thawabu anamuuliza kinachofanyika ni nini haswaaa.

Tunachokifanya Computer ni hardware kitu kinachoshikika unakikagua. Kama inaweza kuwa inainteract yaani kuoana na programu endeshi inaweza kuanza kufanya kazi.

Jaji: Shahidi nendeni taratibu msiwe na haraka. Hatuwaelewi kabisa ni kama mnaambiana huko.

Sawa Jaji tunaanza vizuri. Anasema Thawabu Issa.

Hardware ni kitu chochote kinachoshikika. Unachokagua ni utimamu wa Computer kama unafanya kazi. Unakagua programu endeshi ambayo ipo kwenye computer.

Je mfano wa programu endeshi ni nini? Wakili anamuuliza.

Mfano ni kama Window OS ndio programu endeshi.

Thawabu: Endelea sasa

Samweli Elibariki Kaaya: Anaendelea hapa. Unaangalia program endeshi kama iko updated na unaangalia programu chunguzi kama iko poa na Forensic Investigation programu nayo unaiangalia kama iko poa.

Kwenye programu Chunguzi unachokagua ni je program iko updated na inaweza kufanya uchunguzi? Programu linzi yenyewe mfano wake ni CasperSky hizi ndio Security Software. Huko tunakagua programu hiyo ni current au ya zamani isije ikala file.

Thawabu: Tuendeleee Shahidi.

Samwel: Baada ya hapo tunaanza uchunguzi wa awali ambao ni preliminary investigation.

Uchunguzi wa awali tunatizama physical examination na kuangalia content au maudhui yaliyoko kwenye picha mjongeo hio yaliyoko labda kwenye kibebeo chochote mfano flash, solid state drive, au hard disk external hard disk.

Ukimaliza kutazama kielelezo chako utafungua kifaa kwenye komputa ulionayo hio komputa ndio zile komputa zao za kazi.

Ukishafungua utatazama maudhui na picha mjongeo hio picha mjongeo ni video Utanote kwa penseli ulichoandika kupitia police notebook.

Tunanukuu kwenye notebook ili kupata taarifa, uchunguzi na kutunza kumbukumbu.

Baada ya kutazama mchunguzi atafanya confirmatory test au uchunguzi wa kisayansi hapa hii ni stage ya pili baada ya uchunguzi wa awali.

Tunaangalia rangi ya picha na mwanga wa picha yaani RGB anasema hii ni primary colour anaangalia kama ni halisi.

Pia anaangalia movement ya lips na matamshi kama viko sambamba.

Tunaangalia pia necessary au unnecessary movement of things akimaanisha anaangalia vitu vinavyopita kwa kuongoza au vyenyewe automatically mfano kupita kwa mtu kupeleka Mike kwenye podium, kupita kwa nzi.

Anatazama pia mwendelezo wa matukio

Kama kuna kukatika kwa picha au jamshot

Anaangalia mstari mshazari au line of perspective

Hivi vitu vinasaidia kujua maudhui ni halisi au sio halisi kwenye uchunguzi wa awali.

Mstari mshazari unanisaidia kung’amua uhalisia wa picha kwa kuonyesha ukaribu ulioko baina ya object na length ya camera.

Jamshot inasaidia kungamua kujua kama video imekatwa kipande au haijakatwa...

Necessary au unnecessary movement of things inasaidia kujua vitu vinavyopita bila kutarajia.

Unapoona viumbe wanapita hata watu inakuwa sio movement ya kupanga inasaidia kuonyesha originality ya video.

Ukiangalia lips utaona zinatofautiana kama video haitakuwa rahisi.

Huo ndio Uchunguzi wa awali unavyofanyika, nimeeleza hapo awali.

Hatua inayofuata ni Uchunguzi wa Kisayansi ambao ni SCIENTIFIC EXAMINATION.

Huko kinajiri nini?

Anajibu huko tunaenda ku confirm tulivyoviona uchunguzi wa Awali kama ni sahihi ndo maana tunaita confirmatory test.

Huko tunafanya Data Analysis ambapo Meta Data Analysis tunaifanya kupitia program chunguzi ambayo ni Amped Authenticate.

Part 112 itaendelea kwenye post inayofuata,

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 112

Anaendelea Wakili wa Serikali Thawabu Issa

Hii Meta Data ni nini hasa?

Meta Data ni Data about Data. Yaani picha mjongeo ni Data ndani ya Picha mjongeo kuna Data nyingine ambazo ni taarifa. Hzio taarifa zinaweza kuwa tarehe, jina na kadhalika. Taarifa hizo mjongeo zilizopo kwenye picha mjongeo ndio tunaita Meta Data.

Anasimama Renatus Mkude Wakili Mkuu wa Serikali huyu Baba ni mstaarabu kwakweli. Yeye muonekano wake hana nouma. Anaongea kistaarabu sana. Hana arrogance yoyote. Kwa kumuona tu haoneshi kuwa kisirani kama mawakili wengine wa Serikali.

Anasema kwa sasa ni saa saba naomba tupate break watu wakapate Chakula.

Majaji wanaandika kidogo.

Wanamuuliza Mshitakiwa. Anasema sina pingamizi.

Wanaandika kidogo. Wanasema sasa twendeni break tukutane baada ya lisaa limoja kutoka sasa. Tumeishia hapo kwa sasa. Tukirudi Shahidi ataendeelea kutoa ushahidi wake kwa maana ya EXAMINATION IN CHIEF ITAENDELEA.

Kumbuka jina la Shahidi ni SAMWEL ELIBARIKI KAAYA alkiongozwa na Wakili wa Serikali Thawabu Issa.

Tukutane baadae kidogo.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 113

Thawabu Issa anasema Uliishia kwenye kutazama Meta Data.

Sasa endelea.

Samwel: Nilisema tunafanya Meta Data Analysis. Kuna kitu kinaitwa JSON tunatumia kuidentify taarifa za kidigitali. Pia inaweza ku identify taarifa mbalimbali kama vile aspect ratio kwa maana ya ukubwa wa video na picha yenyewe.

Kingine tunafanya uchunguzi wa Chron analysis. Hii maana yake ni namna ya kufanya utambuzi ili kung'amua kama kuna viashiria vya deep fake.

Hii deep fake ni uwezekano wa teknolojia ya Artificial Inteligence au teknolojia yeyote inayoweza kufanya Manipulation.

Kitu kilichofanyiwa Chron maana yake mifumo mingi inayoendeshwa kwa AI hivyo basi upo uwezekano wa kuweka sura ya mtu au sauti ya mtu kwenye mwili wa mtu mwingine.

Hii AI ni alogarithm ambayo ina learn behaviour ya kitu na kuiga kufanya kitu hicho. Hivyo ni muhimu kufanya Chron analysis ili kuthibitisha.

Yote hayo yapo kwenye programu chunguzi yaani Amped Authenticate. Unaenda kwenye button ya Chron Analysis. Hapo itakuonesha sehemu za trace. Yaani ni sehemu zilizofanyiwa Chron.

Ukishajiridhisha unaenda kwenye hatua inayofuata. Unafanya kitu kinaitwa error level data analysis. Hapo utabaini whether picha mjongeo ni compressed au decompressed. Yaani je video imefinywa au iko halisi? Hapo ndio utajua.

Tunaenda kwenye button iliyoandikwa error hapo ndio tunaangalia vitu viwili. Ambavyo ni V CODEC na A CODEC.

Unaposema VCODEC maanaa yake ni video compression and decompression.

A CODEC audio compression and decompression.

Hatua nyingine tunafanya (PRNU) Cencor patern analysis Hii ni Photo Response Non Uniformity ambayo unaitumia ku identify kwamba picha mjongeo hiyo kama ina alama ya kipekee ambayo ndio hiyo video printing.

Digital signature inaacha camera inatambulisha camera yenyewe.

Baada ya hapo naenda kwenye hatua inayofuata noise analysis ambayo natazama usafi wa picha mjongeo tutakayoichunguza yaani VIDEO CLEANLINESS.

Hapo kwenye noise ni kama chengachenga zikisambaa zinadistort au kuharibu uhalisia wa video

Maelezo yote haya anaelezea ufundi wakuangalia video

Anasema video ikirekodiwa usiku inakuwa na chenga chenga wakat mwingine kama ile rekodi haikuwa nzuri zile chengachenga zinaweza sababisha picha isionekane vizuri.

Nimepata dharura nalazimika kutoka mazingira ya hapa so sitaweza kuendelea kuwapa updates za kesi naomba radhi kwa usumbufu wote uliojitokeza.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Leo Oktoba 17, 2025

Jana tuliishia part 113 so leo tunaendelea na -;

Part 114

Imepigwa high courttttttt watu wote wamesimama.

Majaji wameingia wapo watatu kama kawaida yao.

Karani anasoma namba ya kesi.

Anasimama Wakili Mkuu wa Serikali anatambulisha jopo lake.

Renatus Mkude anamwambia Jaji anaomba Thawabu Issa aendelee alipoishia jana.

Shahidi ulisema kwamba baada ya kufanya analysis ya picha nini huwa kinafuata?

Baada ya kumaliza kufanya hio analysis kinachofanyika ni kuscreenshot ambako ni kupiga picha kutumia interface ya kioo taarifa za kidigitali kupitia metadata.

Baada ya kuscreenshot nitazichapisha kwa maana ya kuziprint kwa ajili ya kuambatanisha na taarifa ntakayoiandaa kwa ajili ya Uchunguzi.

Baada ya kufikia hio hatua naandaa tarifa ya uchunguzi kwa kurejea uchunguzi niliofanya kwa kuangalia police notebook na taarifa nilizoandika.

Taarifa hio huwa inaenda sambamba na covering letter na covering letter kwa ajili ya kuwajibu requesting authority walioomba niwajibu baada ya kufanya uchunguzi huo.

Baada ya kuandaa tarifa hiyo taarifa ya uchunguzi inakuwa na majina ya mchunguzi, logo ya jeshi la polisi, mchunguzi akishamaliza kuandaa tarifa hiyo ataisign, kugonga muhuri wa commission ya uchunguzi wa sayansi jinai (forensic).

Baada ya kugonga muhuri itasainiwa na mnadhimu wa sayansi jinai kwa niaba ya kamishna wa uchunguzi jinai.

Kama mnadhim hayuko basi afisa kwenye rank ya assistant commissioner ataisign.

Mchunguzi atapaki vielelezo kwenye bahasha, atasign bahasha iliyobeba vielelezo na kugonga muhuri.

Barua na covering letter tunaweka kwenye bahasha na kuandika maeneo zinakoenda, kusign na kuweka muhuri.

Baada ya hapo ofisi itawasilana na requesting authority kupata majibu ya kielelezo cha uchunguzi husika.

Iambie mahakama tarehe 8 Mwezi wa 04, 2025 ulikuwa wapi?

Samwel: Kama afisa mchunguzi wa zamu katika kitengo cha picha nilipokea barua mbili zenye kumbukumbu Na DA. 223/476/01DB/168 nyingine ikiwa DA.223/476/01DB/169 na ikiwa imeambatana na flash disk moja aina ya XIOXIA yenye ukubwa wa GB 8 Na flash disc ikiwa na alama ya DM na Ilikuwa iko attached Na. PF145 (exhibit label)

kielelezo kingine kilikuwa Secured Digital SD Adapter ilikuwa imepewa alama ya X Sticker na adaptor hio ilikuwa ina rangi nyeusi ndani ya SD Adaptor kulikuwa na memory card aina ya aldeepo.

Kielelezo hiko kilikuwa kwenye kibahasha kidogo kilichokuwa attached na PF-145 exhibit level

Waheshimiwa majaji barua hizo na vielelezo hivyo vililetwa na Assistant inspector Michael Gyumi.

Vikitokea ofisi ya mkuu wa upelelezi kanda maalum ya Dar es salaam.

Baada ya kupokea vielelezo hivyo na kusign dispatch book Waheshimiwa majaji nilihakiki vielelezo nilivyoletewa kama vinakidhi matakwa ya uchunguzi.

Nilihakiki vifaa vilivyoletwa kama ndivyo vilivoandikwa kwenye barua ya requesting authority.

Katika kuhakiki nilibaini vinakidhi matakwa ya uchunguzi wa kisayansi.

Katika maabara yetu tunapokea vifaa vibebeshi ni kama vile flash disk, memory card baada ya kujiridhisha na uhakiki wa vielelezo nilivyoletewa nilisajili vielelezo hivyo laboratory book register PF 113.

Nilisajili kwa barua yenye kumbukumbu namba DA. 223/476/01B/168 nilisajili kwa namba FB/PH/LAB/106/2025 na barua yenye kumbukumbu namba DA.223/476/01D/169.

Nilimuandikia hizo namba Insp. Michael Gyumi kwa ajili ya ufuatiliaji.

Zile nambari zinatokana na sequence and series jinsi tupokeavyo vielelezo.

Kikipokelewa cha kwanza January kitaandikwa namba moja.

Tunakwenda hivyo hivyo hadi mwisho.

Nilifungua majalada mawili ya uchunguzi wa kimaabara jalada hilo lilirejea namba nilizosajili kwenye PF 113.

Na baada ya usajili huo nikapeleka kwa Mkuu wa kitengo kwa ajli ya assignment kwa hayo majalada niliyoyafungua kwa ajili ya uchunguzi.

Part 115 itaendelea kwenye post inayofuata

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
Back
Top Bottom