Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 31

Tumerudi sasa.

Sauti ya High Court imepigwaa na askari kwa sauti fulani hivi ya kinyonge sana.

Majaji wanaingia tayari.

Mhe. Lissu ameingia pia.

Mawakili wa serikali tunawaona.

Anaandika kidogo Jaji Nduguru na anamuuliza Mhe. Lissu kama yuko tayari.

Mhe. Lissu anasema yuko tayari na anaweza kuendelea.

Katuga: Mh. Coram iko vile vile kama ya asubuhi.

Lissu anaanza sasa.

Waheshimiwa Majaji nawashukuru sana kwa nafasi na naomba nianze kusema kosa hili ni kosa kubwa kuliko yote na lipo kwenye Katiba na adhabu yake ni kifo.

Sheria zinazotumika kwenye makosa ya jinai kama uhaini? Ni sheria za jinai. Hizo ndio hutumika. Sheria za Jinai zina utaratibu wake wa namna ya kutafsiri.

Kanuni ya Msingi ni strictly interpretation hakuna utaratibu wa kutanua au kubana kwa kadri unavyotaka.

Sheria za jinai they are interrelated strictly.

Kwa msingi huo vifungu ambavyo nimevitaja katika hoja yangu ya msingi na vifungu ambavyo amevitaja wakili wa serikali Katuga vinapaswa kuwa interpreted strictly hakuna latitude ya kutafsiri hizo sheria.

Wakili wa Serikali amekubaliana na mimi kwamba masharti ya kifungu cha 135 cha CPA basi hati hiyo inafutwa.

Pia amekubaliana na mimi kuwa Mahakama yetu ya Rufaa inasema usipozingatia kifungu cha 135 cha CPA hati ya mashitaka inafutwa.

Kwanini usipozingatia hiyo section 135 inafutwa?

Sababu imesemwa hapo hapo kwenye hicho kifungu kuwa lazima itamke statement of the offence, ionyeshe maelezo muhimu ya kumuwezesha mshitakiwa kuelewa kesi inayomkabili, kwahiyo maelezo ya shitaka yasipoeleza kosa linalomkabili basi hiyo hati ni batili na inafutwa kwasababu haitamuwezesha mshitakiwa kujua kosa linalomkabili.

Sasa waheshimiwa Majaji tumeletewa kifungu cha 138 cha CPA na mkaambiwa kwa kifungu hicho hii hoja ya pingamizi haipaswi kuruhusiwa.

Waheshimiwa majaji kifungu cha 138 cha CPA hakihusu na hakina uhusiano kabisa na content za particulars of the offence.

Hii section inaeleza tu form ya Charge sheet yani muundo wa Charge sheet na haisemi Charge Sheet inatakiwa i disclose the offence hayo yamesemwa kwenye kifungu cha 135.

Ndo maana waheshimiwa Majaji hutaona mahakama ya rufani inazungimzia 138 utaona ni 135 tu kwasababu ndio inayozungumzia hati shitaka lazima ioneshe kuna kosa.

Lakini pia naomba nidraw your attention kwenye hiyo s.138 ya CPA.

Inasema hivi……… anasoma hapa.

Kifungu hicho kikasema lazima vifungu vingine vizingatiwe.

Sasa hivyo vifungu vingine ni vipi?

Cha kwanza ni s 135 ambacho kinasema lazima hati ya mashitaka iwe na maelezo ya kosa kumueleza mshitakiwa alichokosea.

Kifungu kingine ni 295 inasema pale ambapo taarifa ina makosa na haiwezi kurekebishwa under 294 itafutwa na inafutwaje kwa hoja ya pingamizi ambayo italetwa na mshitakiwa.

Sababu ya kufutwa ni kwamba inakuwa na kosa lisilorekebishika.

Kifungu kingine ni 294 inayosema kama kuna pingamizi every objection to any formal defect shall be taken immediately after the accused person charge read over.

Mapema mtuhumiwa akisomewa shitaka anapaswa kuweka hilo pingamizi na ndo nilichofanya mimi.

Hoja ya kwamba mapingamizi ya namna hii kuwa hayaruhusiwi kwa mujibu wa kifungu cha 138 ni hoja potofu kweli kweli na inatolewa na mtu asiyejua sheria pekee na si vinginevyo.

Hoja sahihi ni kwamba hati ya mashitaka au taarifa isipoonyesha kosa inafutwa. Under 295 ya CPA.

Part 32 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 32

Anaendelea Mhe. Lissu

Sasa Waheshimiwa Majaji wakili wa serikali akaenda kwenye kifungu cha 39(d) cha Penal Code yaani Kanuni ya Adhabu juu ya Uhaini na akarudi kesi za Grey Likungu Mataka.

Na akasema kwa Mujibu wa Grey Likungu Mataka kwamba mambo yanayofanya kosa la uhaini ni matatu makuu ndio alivyosema Katuga.

1. Utiifu kwa jamhuri ya muungano

2. Kutengeneza nia yaani nia ya kutenda kosa la uhaini.

3. Uthibitisho wa kutenda hiyo nia ya kosa la uhaini. Manifestation.

Wakili wa serikali amesema hayo masharti matatu sio pekeee.

Sasa mimi namuuliza so what?

Hayo masharti mengine mimi sijalalamikia.

Utiifu kwa jamhuri mimi sina shida na sharti hilo na hoja yangu haipo hapo.

Hoja yangu ni kwamba kulikuwa na nia ya kuunda kosa la uhaini.

Na pili hiyo nia ilithibitishwa kama inavyotakiwa?

Sharti la pili la hicho kifungu cha 39(2) cha Penal Code. Hati ya mashitaka inapaswa kuonyesha ulitengeneza nia ya kutenda kosa la uhaini.

Taarifa iliyoko mbele yenu waheshimiwa majaji inasema nilitengeneza nia ya kuhamasisha watu kuzuia uchaguzi mkuu.

Anaisoma hapo hiyo taarifa yaani Charge sheet ile hati ya mashitaka.

Wakili wa serikali hajagusa hilo hata kidogo kwamba nilihamasisha watu kuzuia uchaguzi sio kosa la uhaini wala kosa lolote la jinai.

Amekimbia kwenye hili
Hajagusa hata kidogo. Hakuna nia na sijatengeneza nia ya kutenda uhaini.

Ila nimetengeneza nia ya kufanya watu kuzuia uchaguzi wa Tanzania na hiyo sio kosa la uhaini.

Huwezi kuelewa mambo haya kama hujui sheria.

Nilisema mambo yako zaidi ya 10 yanayotengeneza kosa la uhaini wakili wa serikali akasema yako 13 sasa naomba kumuuliza kwenye hayo 13 je ni kitendo gani kinasema kuzuia uchaguzi ndio uhaini? Hakipo na hajasema hapa.

Wakili wa serikali Mkuu alivyokimbia kwenye hoja hiyo akasema kwamba.

Hii taarifa iko sawa sawa kwasababu imetaja jina langu, tarehe, kwamba mimi ni mtiifu wa jamhuri hayo yote wapi nilisema yana shida?

Anasema alitengeneza nia ya kuzuia uchaguzi mkuu wa 2025. Kama nilivyosema Waheshimiwa Majaji hilo sio kosa wala sio inshu kabisa.

Infact kwa kusema hayo anathibitisha niliyosema nia ni kuzuia uchaguzi. YES. That is not an offence under the laws of the National Republic of Tanzania.

Anasema kwa lengo la kuitisha serikali ya Jamhuri ya Muungano.

Watu wazuie itishike Serikali. Waheshimiwa majaji naomba angalieni hiyo information kuna mahali nimetaja serikali? Huwezi kusema ana lengo la kuitaja serikali wakati hajaitaja serikali sikutaja hata MWENYEKITI WA KIJIJI sio serikali tu.

Sasa hayo anayosema yalipaswa kuwepo kwenye taarifa yanapaswa kuwepo kwenye hati ya mashitaka.

Iseme ulitisha serikali yenyewe inasema nilikuwa na nia ya kuzuia uchaguzi, hakuna kosa la kumshitakia mtu hapa labda uwe hujitambui.

Akasema haya mambo ni ya ushahidi. Sasa watambue kuwa tukienda kwenye ushahidi hawatakuja kusema ilitishwa serikali wakati humu wamesema walikuwa na nia ya kuzuia uchaguzi.

Wasifikiri tukienda kwenye ushahidi wasifikiri wataenda kwenye UVUVI WA USHAHIDI kwamba waseme lolote.

Na facts zako kwenye Charge sheet hazioneshi chochote kuhusu kutisha serikali na kosa la uhaini. Hawatatengeneza kosa la uhaini kwenye ushahidi kosa linatengenezwa kwenye hati ya mashitaka.

Part 33 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 33

Anaendelea Mh. Lissu.

Watu wanafurahi kumsikiliza.

Mawakili wa serikali wamesema hati ya mashitaka kuhusu publication na kifungu cha 39(2) cha Penal Code.

Publication maana yake maneno yaliyochapishwa kwenye karatasi yaani writing au printing.

Nilimsikia anasema nilichapisha na nikaweka kwenye mitandao ya kijamii.

Angalieni kwenye hati ya mashitaka kuwa nilichapisha kwenye mitandao ya Kijamii.

Sasa angalieni hayo maneno kama yapo kwenye hati ya mashitaka kuwa nilichapisha hayo maneno kwenye mitandao ya kijamii.

Kama yapo niambieni ili nikae chini kama maneno hayo hayapo hawawezi kuja kusema wakati wa ushahidi.

Hivyo basi publication by writing or printing haipo kokote sasa Waheshimiwa Majaji kuna kitu nimesikia kwa mara ya kwanza katika maisha yangu.

Kwamba maneno ni matendo. The deed of uttering words. Waheshimiwa majaji maneno sio matendo ieleweke vizuri.

Huyu Katuga ni mtu mwema sana alituletea maana ya deed kutoka Black's law dictionary anaisoma hapa.

Deed sio maneno, something that is done or carried out na sio kusema, kuongea. Hiyo ndio Deed.

😂😂😂😂Katuga alisoma maana ya Deed kwenye blacks law dictionary hakuelewa.

Anaendelea Lissu.

Kwa mara ya kwanza nimesikia kwa Katuga kuwa maneno ni matendo hiyo tafsiri tumuachie Katuga akae nayo mwenyewe ni yake.

Amegundua hili yeye.

Mahakama ya rufani ya Tanzania ilisemaje juu ya maneno na uhaini, nafikiri hata hili Katuga hajalielewa na halifahamu kabisa.

Tutaelekezana pia katika hili.

Mahakama ya rufani ya Tanzania ilisema hivi ...... Kwenye uhaini maneno ni nini?

Ukurasa wa 55 mere words do not amount to overt act on a treason charge na ikasema maneno matupu haitengenezi kosa la uhaini isipokuwa hayo maneno yanaelezea kitendo cha uhaini.

Maana yake ni kwamba wanaopanga uhaini wanakaa vikao na kupeana maelekezo hapo utasema maneno hayo ni vitendo vya uhaini eti kuhamasisha wananchi kuzuia uchaguzi. Hii ni kesi ya Khatibu Gandi.

Sasa kama Mahakama ya Rufani imesema Maneno hayatengenezi matendo ya uhaini nani anayeweza kubisha?

Ni huyu Katuga?

Pia ukurasa wa 67 inasema hivi Francis Nyalali Jaji mkuu anasema kanuni kuu maneno hayatengenezi matendo ya uhaini lakini wakiwa wengi inaweza kuwa vinginevyo na isipokuwa mshitakiwa akiwa mmoja huwezi kusema maneno yake yanatengeneza uhaini.

Kwa kifupi akisema mtu mmoja kama nilivyosema mimi na nikashitakiwa mtu mmoja kama nilivyoshitakiwa mimi basi hakuwezi kuwa na uhaini ndio msimamo wa sheria ya uhaini as we speak today.

Hajalijibia hili amekimbia kimbia tu sasa kwahiyo nimesema hakuna nia ya kufanya kosa na hakuna publication na maneno matupu hayavunji mfupa kwenye uhaini.

Kuna kitu hapa amekisema sana katuga, umma, umma, umma.

Hivi UMMA ni nini? Anaongea ongea tu umma. Umma ni watanzania milioni 63+ hayo majina yanapaswa kuwepo kwenye hati yaje kuwa pleaded nimezungumza na watu fulani usipowataja ni kosa, umekosea kuandaa hati ya mashitaka.

Haya hayahitaji ushahidi, hati ikiwa mbovu inafutwa kabla mshitakiwa hajajibu shitaka, inafutwa kabla ya ushahidi ieleweke hivyo.

Anaendelea Lissu.

Waheshimiwa Majaji kabla sijaondoka kwenye habari ya publishing kwasababu sheria inasema publishing by writing or printing sasa hiyo writing or printing ni lazima iwe pleaded.

Mtakaposoma Grey Likungu mtaona hao waliopanga kupindua serikali walikuwa wanaandikiana baru na kulikuwa na chapisho linaloitwa Ukweli na hayo yote yalikuwa set out kwenye hati ya mashitaka.

Waheshimiwa majaji mkiangalia kwenye kesi hiyo hiyo kwenye ukurasa wa mwisho kabisa, ameainisha hizo overt act zaidi ya 34 because the were pleaded ziliwekwa kwenye hati ya mashitaka.

Huwezi ukasema alichapisha halafu ukaishia hapo, unapaswa kusema alichapisha nini, wapi, akapeleka wapi? Hata walete mashahidi hayapo kwenye information.

Part 34 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali
 
1758210617955.jpg
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 36

Anaendelea Mhe. Lissu

Wakili wa serikali alisema utaratibu upi unapaswa kutumika? Na Jaji Nyalali akamjibu na makubaliano yakawa utaratibu huo utumike hadi utakapokuja kubadilishwa.

Sasa hadi leo hakuna kilichobadilishwa, hizi kesi zote mbili ni za kwao hawa ma DPP sasa leo wanasema tuendeleee. HAIWEZEKANI.

Mahakama hii isiwaruhusu kuleta mambo ambayo yalishawekwa sawa na watu waliowatangulia kwenye maofisi yao.

Mwisho naomba nimalizie kwa kusema yafuatayo.

1. Je makosa haya yote yanarekebishika? Kama hujataja kosa unarekebishaje? Hiyo maana yake ni hakuna.

Mahakama ya rufani inasema hiyo ni sifuri. Unarekebishaje sifuri kwahiyo hayarekebishiki na kama hayarekebishiki the information must be quashed.

2. Maneno sio kosa ila nia ya kuitisha serikali juu ya kuzuia uchaguzi.

Hayo maneno ya kuitisha serikali yako wapi kwenye hiyo charge sheet? Wapi serikali imetajwa? Wapo viongozi wake wametajwa? Haipo kabisa.

Habari ya kuitisha serikali kwenye maneno haya haipo kabisa ni maneno matupu haya. Tufuate msimamo wa Khatibu Gandi kuwa maneno matupu hayafui dafu katika hili.

Naomba waheshimiwa majaji hati hii ya mashitaka ifutwe mara baada ya mawasilisho hayo.

Amemaliza Mhe. Lissu.

Naona Majaji wanaandika kidogo naona pia wananong'onezana wote watatu. wanaandika tena.

Ngoja tusubiri watasema uamuzi ni lini?

Naona majaji wanacheka kimya kimya. hawataki tuwaone wanacheka.

Si unajua zile style za vicheko vya majaji ni kama hawacheki hivi.

Wanacheka na kujikausha kama hawajacheka vile.😂😂😂

Jaji Nduguru amesema Mahakama itatoa uamuzi siku ya Jumatatu saa tatu asubuhi.

Naomba nisaidie kushare.
 
Back
Top Bottom