Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 371,651
- 860,930
- Thread starter
- #361
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 31
Tumerudi sasa.
Sauti ya High Court imepigwaa na askari kwa sauti fulani hivi ya kinyonge sana.
Majaji wanaingia tayari.
Mhe. Lissu ameingia pia.
Mawakili wa serikali tunawaona.
Anaandika kidogo Jaji Nduguru na anamuuliza Mhe. Lissu kama yuko tayari.
Mhe. Lissu anasema yuko tayari na anaweza kuendelea.
Katuga: Mh. Coram iko vile vile kama ya asubuhi.
Lissu anaanza sasa.
Waheshimiwa Majaji nawashukuru sana kwa nafasi na naomba nianze kusema kosa hili ni kosa kubwa kuliko yote na lipo kwenye Katiba na adhabu yake ni kifo.
Sheria zinazotumika kwenye makosa ya jinai kama uhaini? Ni sheria za jinai. Hizo ndio hutumika. Sheria za Jinai zina utaratibu wake wa namna ya kutafsiri.
Kanuni ya Msingi ni strictly interpretation hakuna utaratibu wa kutanua au kubana kwa kadri unavyotaka.
Sheria za jinai they are interrelated strictly.
Kwa msingi huo vifungu ambavyo nimevitaja katika hoja yangu ya msingi na vifungu ambavyo amevitaja wakili wa serikali Katuga vinapaswa kuwa interpreted strictly hakuna latitude ya kutafsiri hizo sheria.
Wakili wa Serikali amekubaliana na mimi kwamba masharti ya kifungu cha 135 cha CPA basi hati hiyo inafutwa.
Pia amekubaliana na mimi kuwa Mahakama yetu ya Rufaa inasema usipozingatia kifungu cha 135 cha CPA hati ya mashitaka inafutwa.
Kwanini usipozingatia hiyo section 135 inafutwa?
Sababu imesemwa hapo hapo kwenye hicho kifungu kuwa lazima itamke statement of the offence, ionyeshe maelezo muhimu ya kumuwezesha mshitakiwa kuelewa kesi inayomkabili, kwahiyo maelezo ya shitaka yasipoeleza kosa linalomkabili basi hiyo hati ni batili na inafutwa kwasababu haitamuwezesha mshitakiwa kujua kosa linalomkabili.
Sasa waheshimiwa Majaji tumeletewa kifungu cha 138 cha CPA na mkaambiwa kwa kifungu hicho hii hoja ya pingamizi haipaswi kuruhusiwa.
Waheshimiwa majaji kifungu cha 138 cha CPA hakihusu na hakina uhusiano kabisa na content za particulars of the offence.
Hii section inaeleza tu form ya Charge sheet yani muundo wa Charge sheet na haisemi Charge Sheet inatakiwa i disclose the offence hayo yamesemwa kwenye kifungu cha 135.
Ndo maana waheshimiwa Majaji hutaona mahakama ya rufani inazungimzia 138 utaona ni 135 tu kwasababu ndio inayozungumzia hati shitaka lazima ioneshe kuna kosa.
Lakini pia naomba nidraw your attention kwenye hiyo s.138 ya CPA.
Inasema hivi……… anasoma hapa.
Kifungu hicho kikasema lazima vifungu vingine vizingatiwe.
Sasa hivyo vifungu vingine ni vipi?
Cha kwanza ni s 135 ambacho kinasema lazima hati ya mashitaka iwe na maelezo ya kosa kumueleza mshitakiwa alichokosea.
Kifungu kingine ni 295 inasema pale ambapo taarifa ina makosa na haiwezi kurekebishwa under 294 itafutwa na inafutwaje kwa hoja ya pingamizi ambayo italetwa na mshitakiwa.
Sababu ya kufutwa ni kwamba inakuwa na kosa lisilorekebishika.
Kifungu kingine ni 294 inayosema kama kuna pingamizi every objection to any formal defect shall be taken immediately after the accused person charge read over.
Mapema mtuhumiwa akisomewa shitaka anapaswa kuweka hilo pingamizi na ndo nilichofanya mimi.
Hoja ya kwamba mapingamizi ya namna hii kuwa hayaruhusiwi kwa mujibu wa kifungu cha 138 ni hoja potofu kweli kweli na inatolewa na mtu asiyejua sheria pekee na si vinginevyo.
Hoja sahihi ni kwamba hati ya mashitaka au taarifa isipoonyesha kosa inafutwa. Under 295 ya CPA.
Part 32 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali
Part 31
Tumerudi sasa.
Sauti ya High Court imepigwaa na askari kwa sauti fulani hivi ya kinyonge sana.
Majaji wanaingia tayari.
Mhe. Lissu ameingia pia.
Mawakili wa serikali tunawaona.
Anaandika kidogo Jaji Nduguru na anamuuliza Mhe. Lissu kama yuko tayari.
Mhe. Lissu anasema yuko tayari na anaweza kuendelea.
Katuga: Mh. Coram iko vile vile kama ya asubuhi.
Lissu anaanza sasa.
Waheshimiwa Majaji nawashukuru sana kwa nafasi na naomba nianze kusema kosa hili ni kosa kubwa kuliko yote na lipo kwenye Katiba na adhabu yake ni kifo.
Sheria zinazotumika kwenye makosa ya jinai kama uhaini? Ni sheria za jinai. Hizo ndio hutumika. Sheria za Jinai zina utaratibu wake wa namna ya kutafsiri.
Kanuni ya Msingi ni strictly interpretation hakuna utaratibu wa kutanua au kubana kwa kadri unavyotaka.
Sheria za jinai they are interrelated strictly.
Kwa msingi huo vifungu ambavyo nimevitaja katika hoja yangu ya msingi na vifungu ambavyo amevitaja wakili wa serikali Katuga vinapaswa kuwa interpreted strictly hakuna latitude ya kutafsiri hizo sheria.
Wakili wa Serikali amekubaliana na mimi kwamba masharti ya kifungu cha 135 cha CPA basi hati hiyo inafutwa.
Pia amekubaliana na mimi kuwa Mahakama yetu ya Rufaa inasema usipozingatia kifungu cha 135 cha CPA hati ya mashitaka inafutwa.
Kwanini usipozingatia hiyo section 135 inafutwa?
Sababu imesemwa hapo hapo kwenye hicho kifungu kuwa lazima itamke statement of the offence, ionyeshe maelezo muhimu ya kumuwezesha mshitakiwa kuelewa kesi inayomkabili, kwahiyo maelezo ya shitaka yasipoeleza kosa linalomkabili basi hiyo hati ni batili na inafutwa kwasababu haitamuwezesha mshitakiwa kujua kosa linalomkabili.
Sasa waheshimiwa Majaji tumeletewa kifungu cha 138 cha CPA na mkaambiwa kwa kifungu hicho hii hoja ya pingamizi haipaswi kuruhusiwa.
Waheshimiwa majaji kifungu cha 138 cha CPA hakihusu na hakina uhusiano kabisa na content za particulars of the offence.
Hii section inaeleza tu form ya Charge sheet yani muundo wa Charge sheet na haisemi Charge Sheet inatakiwa i disclose the offence hayo yamesemwa kwenye kifungu cha 135.
Ndo maana waheshimiwa Majaji hutaona mahakama ya rufani inazungimzia 138 utaona ni 135 tu kwasababu ndio inayozungumzia hati shitaka lazima ioneshe kuna kosa.
Lakini pia naomba nidraw your attention kwenye hiyo s.138 ya CPA.
Inasema hivi……… anasoma hapa.
Kifungu hicho kikasema lazima vifungu vingine vizingatiwe.
Sasa hivyo vifungu vingine ni vipi?
Cha kwanza ni s 135 ambacho kinasema lazima hati ya mashitaka iwe na maelezo ya kosa kumueleza mshitakiwa alichokosea.
Kifungu kingine ni 295 inasema pale ambapo taarifa ina makosa na haiwezi kurekebishwa under 294 itafutwa na inafutwaje kwa hoja ya pingamizi ambayo italetwa na mshitakiwa.
Sababu ya kufutwa ni kwamba inakuwa na kosa lisilorekebishika.
Kifungu kingine ni 294 inayosema kama kuna pingamizi every objection to any formal defect shall be taken immediately after the accused person charge read over.
Mapema mtuhumiwa akisomewa shitaka anapaswa kuweka hilo pingamizi na ndo nilichofanya mimi.
Hoja ya kwamba mapingamizi ya namna hii kuwa hayaruhusiwi kwa mujibu wa kifungu cha 138 ni hoja potofu kweli kweli na inatolewa na mtu asiyejua sheria pekee na si vinginevyo.
Hoja sahihi ni kwamba hati ya mashitaka au taarifa isipoonyesha kosa inafutwa. Under 295 ya CPA.
Part 32 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali