LISSU ANAJIBU HOJA MAHAKAMA KUU: I
11 Septemba 2025, Mh Lissu anamalizia kujibu hoja za mawakili wa serikali. Tumefanya uhariri kidogo maelezo yale yaliyoandaliwa na timu maalum iliyojitolea kufanya haya mtandaoni.
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Mzizima, 11 Septemba 2015; saa 4:40 asubuhi
Majaji wanaingia na watu wote wamesimama.
Karani anaita kesi Criminal Case No. 19605/2025.
Jaji: Jamhuri karibuni.
Katuga: Nipo na Misieh Kahima, Thawabu Issa, Harrison Lukosi, Cathbert Mbiringe wote ni mawakili wa Serikali ambao ni 6 tunaiwakilisha Jamhuri katika shauri hili na mshitakiwa yupo Mheshimiwa Jaji. Tunaendeela na usikilizaji wa mapingamizi na mwenzetu mshitakiwa kama yupo tayari aendeleee. Sisi hatuna shida.
Jaji: anaandika. Anamuuliza Mh. Lissu vipi uko tayari.
Mhe. Lissu: Niko tayari na imara kabisa. Jaji: anaandika na kuteta kidogo na wenzake. Sasa unaweza kuendelea ndugu Lissu.
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji nimefurahi, kuwaona na niwapongeze kwa kazi kubwa mliyofanya toka Jumatatu. Jana niliomba ahirisho ili nikasome kesi walizonipa mawakili wa Jamhuri naomba niseme hiyo kazi nimeifanya vizuri sana. Niwashukuru mawakili wa serikali kuleta hizo kesi kwa sababu zitanisaidia sana kuja kusema nitakachosema siku ya leo. Ni kesi wamezileta wenyewe sio mimi.
Wakili wa serikali Katuga na Mrema walitoa hizo kesi wenyewe kwa hiyo nitaonesha namna hizo kesi kama ni relevant au sio relevant kwa kesi tuliyonayo. Kwa kuanzia naomba nizungumzie kauli ambayo ilitolewa juzi na Wakili wa Serikali Mkuu, Katuga kwamba committal proceedings lengo lake ni kuhakikisha fair trial.
Hiyo position ipo kwenye maamuzi mengi ambayo yametajwa toka Jumatatu mimi nakubaliana na msimamo huo ni kuhakikisha kuna fair trial katika kesi zinazosikilizwa mahakama kuu. Na kesi hizo ni kesi kubwa.
Kama lengo ni kuhakikisha fair trial/hearing hivyo basi committal Court is responsible to make sure the accused person is given full opportunity Huwezi kumpa nyaraka nusunusu mtuhumiwa kwenye kesi yake, huwezi kuacha makosa mengi yote kama yaliyopo. Ni lazima mshitakiwa apewe nafasi ya kusema maelezo yake yote. Apewe hiyo fursa na ipo hoja ya whether nilipewa fursa ya kutoa maelezo yangu kwenye committal Court (Mahakama ya Ukabidhi)
Mahakama ya Ukabidhi ilipaswa pia kunipa nyaraka zote zilizopatikana kwenye committal processes. Hayo yote yakitimizwa kutakuwa na fair trial na yasipotimizwa hayo hakutakuwa na fair trial kabisa. Waheshimiwa Majaji Wakili wa Serikali Kiswaga (watu kicheko). Anasema waheshimiwa huyu Kiswaga amenikaa sana kichwani. Samahani ni Katuga. Sasa anasema lengo la niliyosema ni kuupotosha umma na nyie majaji kwa hayo ambayo nimeyasema tangu jumatatu mimi binafsi siamini kama kuna chochote nimesema cha kuipotosha mahakama. Nafikiri nimewezesha mahakama hii na umma kuwaleeza mambo mengi ambayo yalikuwa yamefichwa.
Katuga anasema kuhusu S. 265(1) of CPA anasema hayo mamlaka ya kuahirisha kesi na kutoa sababu za msingi za kuahirisha na kuandika sababu hizo alisema all that is descretion. A superior court like this should not interfere that power.
Nikapewa kesi ya Mbogo and another 1993 kwamba inaunga mkono msimamo wao huo.
Waheshimiwa majaji hiyo kesi ya Mbogo vs Shah sina library yangu ningeipata hiyo kesi yote.
Walinipa uamuzi wa kesi ya Ishengoma na wenzake sita. Kesi ya Mahakama ya Rufani hiyo Kesi ya Donatus Ishengoma ukurasa wa 15 umecite kesi ya Mbogo niliyoitaja hapo awali. Anasoma hiyo kesi hapa ilichosema. Maelezo marefu hapa.....
Waheshimiwa majaji nani ana uwezo kuwa na ubishi na hili, mimi sina. Sina ubishi na superior Court can do on interference to surbodinate court. Kifungu cha 265 hakina descretion kihivyo wanavyodhani. Its only partially decretion. Naomba nikisome hicho kifungu. Anakisoma sasa hicho kifungu hapa.
Descretion nimeambiwa hapa kwamba ni kumpeleka mtuhumiwa gerezani. Hiyo ni 265(1). Ukianza kusoma vifungu vingine ikitaka kuahirisha iandike sababu za hayo maahirisho.
Mamlaka haina option ya kutokuandika sababu na haina option ya kutokutoa reason hizo.
Naomba niendelee hiyo kesi ya ishengoma imeenda kwa kiwango hicho. Naendelea na kesi zao zingine. Waheshimiwa majaji wakili Kasuga, aahhh samahani Katuga aliuliza a very rhetorical question kwamba sasa turudi kisutu?
Hili nitalijibia la mwisho. Twende kwenye improper dating kubadilisha proceedings na kubadilisha tarehe za matukio mahakamani.
Tuliambia hiyo ni a mere slip of the pen na tukapewa Kesi ya Baraka Mashaka Kesi ya Mahakama kuu PC Civil Appeal/2023. Hoja yangu ni kwamba kukiwa na kosa moja au mawili kwenye kurasa 101 unaweza kusema ni sleep of a pen.
Sasa ukiwa na makosa mia kwenye nyaraka hiyo hilo la kukosea tarehe haliwi kosa dogo kabisa lazima yaangaliwe kwa uzito. They are part of the designing kwangu mimi na naomba hayo makosa ya kuteleza kwa mkono naomba yachukuliwe kuwa sio kuteleza kwa mkono yachukuliwe kama sehemu ya uchafu mwingi uliopo humu na niliousema toka siku ya kwanza.
Kwenye hiyo kesi hiyo mshitakiwa alihukumiwa maisha kwa kumfanya kinyume na maumbile mtoto lakini mahakama ikamfunga kwa kosa la armed robbery. Mahakama ya rufaa ilisema kwa vile adhabu ni ileile kwa makosa hayo basi ni slip if a pen. Sasa huwezi kuleta kesi ya namna hii itumike kwenye hoja za kesi tuliyonayo leo hapa. Kuna kitu amekisema sana Katuga kwamba malalamiko yangu ni kutaka huruma amekisema toka Kisutu.
Sympathy! Ilianzia Kisutu imekuja hadi mahakama hii. Pamoja na kwamba sidhani kama itaamua one way to other naomba niweke for the record kupata huruma unapoonewa sio jambo baya. Kuomba huruma unapokuwa kwenye matatizo sio jambo baya.
Kama anadhani ukipata matatizo unahitaji huruma. Sasa la msingi ni nini? Siwaombi Majaji chochote mtakachoamua msiamue kwa huruma. Muamue yote kwa haki na kwa mujibu wa viapo vyenu. Msinihurumie na sihitaji huruma yenu nahitaji muamue kwa haki.
Nayasema haya for the record nimeona Katuga anayarudia rudia sana. Kuna hoja ilitolewa na Katuga na imerudiwa na Mrema kuhusu kifungu cha 183 cha CPA. Job Mrema anasema inapaswa kusomwa na 187 pia za CPA izo zote zinazungumzia mamlaka ya mahakama. Mahakama ya Kisutu. CPA ni sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai.
S. 183 inazungumzia general authority of Court in Tanzania. Kwamba mahakama yoyote ina mamlaka ya kuamrisha mtu kwenda mahakamani ndani eneo la mahakama hiyo kama mtu huyo amefanya kosa ndani ya eneo la utawala wa mahakama hiyo. Sasa wameleta hii ili waseme kwamba uliletwa Kisutu kwasababu ulifanyia kosa Dar es salaam hicho kifungu walichotaja cha 183 kinazungumzia tayari ameshashtakiwa kinaipa mamlaka amri aletwe kwenye mahakama husika. Mimi nilikamatwa Mbinga na wakati nakamatwa sikuwa mshitakiwa. Mimi nimekuwa mshitakiwa baada ya kupelekwa Kisutu na kusomewa mashtaka.
Sababu ya pili ni kwamba kwani nilipelekwa Kisutu kwasababu mahakama iliamua nipelekwe Kisutu? Hakukuwa na order hiyo.
Kwa hiyo S. 183 haiwezi ku apply kabisa.
Tatu. Mahakama ya Rufaa kwenye kesi ya Dodoli Kapufi ilisema nini kuhusu kifungu cha 183?
Jaji Chande alisema in essence that section is deal with trial not deal with Committal. Section inayodeal na committal ni S. 261.
Nimemaliza na hiyo niendeleee na kesi yao nyingine.
Hii nayo imeletwa bure kabisa.
Sasa Waheshimiwa Majaji naomba nishughulike na JOB MREMA.
Huyu Katuga nimemaliza naye.
Anasimama Katuga anasema kifungu cha 187 hajakisemea. Mhe. Lissu anasema nawashukuru sana Katuga. Ngoja nije hapo. Hicho cha 187 trial at a place where act done.
Hii section is about trial na section about committal is 262, 263 hadi 265. Hivyo basi kama ambavyo sect. 183 ilivyo irrelevant basi hata section 187 nayo ni hivyo hivyo haihusiki hapa tunazungumzia committal. Tofautisha Committal na trial.
Sasa nirejee kwenye suala la Mashahidi. Nalo lilizunguzwa na Mrema na nimesema naanza kushughulika naye.Suala la Mashahidi wangu kutokuandikwa. Walilizungumza.
Katuga anasema hawakuitwa na kuandikwa wanaweza kuandikwa baadae hakuna tatizo. There is no prejudice.
Wakili Mrema pia alisema Mshitakiwa alishauriwa kuwa majina ya mashahidi atakuja kuwasema mahakama kuu. That one was premature kwahiyo hamna shida.
Waheshimiwa majaji naomba niwaonyeshe jinsi ambayo hii nayo ni shida kubwa.
Mashahidi kutokuandikwa kwenye commitall proceedings.
Ipo hivi Waheshimiwa majaji, Mshitakiwa ana haki ya kutamka majina na anuani ya mashahidi wake wakati wa committal maana asipoitumia inabaki fadhila ya mahakama.
Kwenye committal nilikuwa na haki ya kusema mashahidi wangu na anuani zao. Kwenye mahakama hii ni descretion yenu sio haki yangu tena. Mnaweza kuamua au msiamue sasa niwapeleke kwenye sheria. Kifungu cha 264 cha CPA ndo kinatoa haki kwa mshitakiwa kutaja majina ya mashahidi wake wote.
Nikisema nina mashahidi wewe Hakimu KISWAGA huwezi sema nitawasemea mahakama kuu, unapaswa kuandika.
Hilo halikufanyika.
Mawakili wa serikali wanasema ni premature, unaweza kuita baadae, sasa hiyo baadae iko kifungu cha 281 na 314 ya CPA. (Kumbukeni CPA ni Criminal Procedure Act - Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai)
S. 281 inasema hivi msajili wa mahakama kuu ataandaa wito kwa mashahidi wote ambao orodha yao ipo. Registrar/ msajili anatoa summons/wito kwa hao uliowataja. Kinasema hivyo.
Sasa kama hujataja nini kinapaswa kufanyika ndio S. 314 inaingia hapo. Kinasema hivyo mtuhumiwa hawezi kuwa na haki ya kuita mashahidi wake ambao hawakuwa kwenye orodha yake labda mahakama ijiridhishe kuwa kuna umuhimu wa mashahidi hao kuitwa. Sasa hii ni fadhira ya majaji haki yangu nimesema ilikuwa Kisutu. The accused person shall not be entitled to call witness without approval au consent ya majaji sasa kuna prejudice kubwa kuliko hiyo kunyang'anywa mashahidi wangu.
Haya maneno ya kwamba naweza kuwaita baadae ni maneno ya watu wenye nia mbaya sana na mimi.
Wanasema mambo ambayo sheria haiyatambui na kuyakubali, naomba waheshimiwa majaji msikubali jambo hili.
Sasa Job Mrema alisema majaji mnapaswa mjiulize hili pingamizi kama liko sawasawa mbele ya mahakama hii. Na alilisema jambo hili kwa mbewembwe kabisa. George Abdon Kilinga na wenzake vs Anna na wenzake ni mashauri ambayo aliyaleta hapa.
Kwanza hii ni kesi ya mirathi ilianzia mahakama ya mwanzo, ikaenda mahakama ya wilaya ya Babati ambayo iliamua kwamba wadaaawa wataamua watumie sheria gani? Mahakama kuu rufaa ya pili sasa Madam Justice alisema parties can not by agreement confer jurisdiction to a Court.
Wadaawa hawawezi jiamulia kuipa mamlaka mahakama hii kwasababu suala la jurisdiction (mamlaka) ni suala la
Jaji.
Kwenye kesi yangu sasa Mshitakiwa anasema alikuwa committed na mahakama ambayo haikuwa na mamlaka.