#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 24
Anaendelea Mhe. Lissu
Ukiangalia maelezo ya mashahidi ambao ni raia wa kawaida yanatofautiana na maelezo ya mapolisi wenzao.
Maelezo ya AMANI MICHAEL kwenye orodha ni No. 20.
Huyu ni Detective Kopro ukisoma maelezo yake kuna askari amemuandika Kopro Robert, amemuandika maelezo Kopro Amani.
ASP Masalanga No. 21 na huyo vilevile ameandikiwa maelezo yake na another officer, nathibitisha kwa uaminifu nimemuandika na nimempa asome.
ASP. Charles Makunja kutoka kule Songea uthibitisho mimi D.cp ... nathibitisha nimemuandika maelezo na nimempa asome ameridhika yako sawa.
Sasa waheshimiwa mtapata muda kuangalia hayo niliyosema hapo juu.
Maelezo ya mashahidi yanapaswa kuandikwa kwa mujibu wa sheria kabisa na yakiandikwa yapelekwe kwa DPP na baadae yawe committed na tunafika Mahakama kuu.
Maelezo hayo yote yalisomwa Mahakama ya Kisutu kama yalivyo na yapo kinyume na sheria.
Hao waliojiandikia sio maelezo na yapo cha Sheria.
Sasa naomba nihamie kwenye maelezo ya akina P kuanzia P1 hadi P11 yalisomwa hadharani kama yalivyo na yameletwa mahakamani kama yalivyo. Yenye majina ya akina P.
Yanakiuka kifungu cha 194(4) cha CPA na rule 7 za kanuni ya ulinzi wa mashahidi.
S. 194 cha CPA inasema AMRI ya kuficha mashahidi hupaswi kuwatoa kabisa.
Sheria inasema maelezo hayo mtuhumiwa hapaswi kupewa pale ambapo mahakama imetoa amri ya maeneo fulani yasipewa kwa accused person.
Ndio sheria inasema hata kama sipendi.
Kanuni ya 7(3) ya ulinzi wa mashahidi inasema pia hivyo hivyo.
Kesi inapaswa kusikilizwa kwa amri husika.
Amri ya mahakama kuu katika kesi hii kwamba majina ya mashahidi yasiwepo na utanbulisho wao wote na mashahidi wote ambao mahakaama ilitoa amri ya kuwalinda haijawalinda.
Tunafahamu makazi yao, mitaa yao, kazi wanazofanya hadi namba zao za simu tumepewa.
Sasa kwa mazingira hayo maana yake mashahidi wameandaliwa bila kufuata utaratibu kabisa.
Ni wasilisho langu kuwa Waheshimiwa Majaji mna maelezo ya mashahidi ambayo yamekiuka sheria kwa mujibu wa Sheria zetu.
Maelezo yote hayo yanapaswa kuwa expunged from the record.
Sasa hatuhitahi kwenda huko maana tunaweza kulimaliza hapa.
Naomba sasa niwape authority waheshimiwa majaji.
Kesi ya Benga Said Kasamwa Abuu Rajabu
abou Masoud Criminal session Case.
Kwenye hiyo kesi wakati wa Commital proceedings kwa ajili ya kesi ya mauaji taarifa iliyokuwa committed high court maelezo yalikuwa na maelezo ya juu tu.
Hiyo statement ilisomwa kwenye committal na ikapelekwa Mahakama kuu na Mahakama kuu ikasema kwasababu hakujaonekana ukurasa wa pili basi taarifa yote ikawa quashed. Iliondolewa information yote.
Jaji alisema hayo masharti ni masharti ya lazima ni lazima yafuatwe.
Hizo witness statement zote na mashahidi wote waliopaswa kulindwa na hawajalindwa ukizifuta maana yake hakuna kesi ita collapse kabisa.
Out of 30 witness statement zinaondoka 23.
Nini kinabaki hapo?
Zifutiliwe mbali.
Sasa Waheshimiwa majaji naomba naomba kumalizia.
Naomba nimalize kwa swali lifuatalo.
Kifungu cha 295(1) cha CPA kinasema the information inayotakiwa kufutiliwa mbali ni ile ambayo s.294 haijazingatiwa.
Is this information capable to sustain?
Hapana haina miguu ya kusimamia hii.
Ni wasilisho langu kwamba haiwezi kurekebishika.
Nimesema tangu jana, haioneshi kosa lolote la jinai, haioneshi kosa la uhaini nililoshtakiwa nalo.
Sasa unarekebishaje kitu ambacho hata sio kosa kabisa hayo maelezo ambayo wanasema niliyasema hayajafafanuliwa.
Hawakusema walielewaje nikisema kukinukisha maana yake ni nini?
Haya mambo hayawezi kurekebishika kwa hatua ya sasa huwezi rekebisha ambacho hakipo..
Hawawezi kuleta pleading mpya ya overt act.
Part 25 itaendelea kwenye post inayofuata
Naomba repost yako kwenye tweet hii.