Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 8

Tumerudi Majaji wameingia.

Kama kawaida wako watatu.

Kumbukumbu ni kwamba tuliahirisha ili Mh. Lissu akasome nyaraka za proceedings alizopewa leo mara baada ya zile za kwanza alipewa nusu ambazo zimeanzia Tar. 18/08 na sio kuanzia Tar. 10/04.

Ngoja tusubiri mrejesho.

Je tutaendelea na shauri au hatutaendelea nalo? Je Mhe Lissu amesema amekuta mambo gani huko kwenye nyaraka alizopewa leo na je zina utofauti gani na zile alizokuwa amepewa mwanzo. Tutajua muda sio mrefu.

Majaji waaandika kidogo hapa.

Jaji anasema naomba tuendeleee.

Anasimama Katuga anasema Corum iko vilevile na mshitakiwa yupo.

Jaji anasema ongeza sauti.

Katuga anarudia hapa alichokuwa anazungumza.

Mshitakiwa yupo na shauri linakuja kuendelea na kusikiliza mapingamizi au wasilisho wa mshitakiwa kwenye suala la mamlaka ya mahakama hii.

Lakini pia tulikuwa na concern kwamba wenzetu wa Magereza wanasema barabara haziko vizuri tunaomba tusifike usiku sana.

Ni hayo tu mheshimiwa Jaji.

Kwa maneno mengine KATUGA anatuambia barabara za nchi hii ni tatizo sana.

Anapewa nafasi Mh. Lissu.

Mh. Lissu anasema sitawaweka sana kwa leo asiwe na hofu.

Nimepata hii record saa 10 kasoro dakika mbili na mlisema tukutane saa 10 na dakika kumi. Kwahiyo nimepata dakika 12 pekee za kupitia hiyo nyaraka.

Sasa sijaenda mbali sana kwenye kuisoma hii record. Hivyo naomba niseme lifuatalo.

Ukizisoma hizi nyaraka mbili ambazo zote nimeletewa.

Ukisoma zote kuna jambo limefanyika nafikiri litakuwa ni kosa la jinai.

Kuna criminality involved.

Record mliyoagiza nipewe na nimepewa. Precedings za Tar. 18/08 nilizopewa mwanzo.

Kwenye hii mpya niliyopewa Proceedings za Tar. 18/08 zinaanzia ukurasa wa 80.

Kwahiyo kwa kuhesabu idadi ya kurasa hizi nyaraka nilizopewa zinatofautiana.

Jambo lingine from page 86 kwenye hii niliyopewa leo kuna kitu kimeandikwa proceeding halafu kuna COURT ORDER iko page 86 hadi 89 lakini kwenye hii niliyoletewa mwanzo. Hiyo ORDER haipo kabisa.

Niliyoletewa gerezani haina hizo page kabisa za hiyo Court ORDER.

From page 94 to 98 kwenye niliyoletewa mahakamani ziko page 6 to 14 kwenye niliyopewa mahakamani.

Sasa hizi nyaraka zote nimepewa zikionekana ni nyaraka za mahakama?

Kwanini zitofautiane? Kwanini niletewe nyaraka gerezani ambayo sio yenyewe na ambayo nilipaswa kupewa.

Wako watu wamegushi kuna doctoring hapa. Zimeghushiwa. Zimefanyiwa mchezo mchafu.

Part 9 itaendelea kwenye post inayofuata.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 9

Anaendelea Mhe. Lissu

Kwenye ukurasa wa 61 wa hii niliyopewa leo kuna taarifa kwamba kunashauri yamefunguliwa mahakama kuu kuhusu kuficha mashahidi na mkiangalia.

Pia font ya nyaraka niliyoletewa awali na font niliyoletewa leo. Ombi langu hatuwezi kuendelea leo naomba tuahirishe mnipe muda. Usiku wa leo utanitosha kesho turudi nije kuwaonyesha uchafu uliofanyika hapa.

Documents zimekuwa falsefied naomba tuahirishe turudi kesho ili nije kuendelea.

Kwa kifupi ni kwamba wahuni walitengeneza nyaraka mbili tofauti wakampelekea nyaraka tofauti.

Anasimama Katuga hapa, anaomba azungumzie hiyo criminality.

Jaji anasema ukitaka ku respond kwenye hilo utatuvuruga subiri basi akimaliza na wewe utapata muda wa kujibia huko mbele.

Lissu anasema Wakili atakuwa na hoja asitupotezee muda hapa.

Wananchi wanacheka. 😂😂😂

Majaji wanaandika hapo tusubiri maelekezo yao. Wameanza kuteta kidogo.

Jaji anasema tunaomba utunze maoni yako. Utapata muda wa kujibu maana hajamaliza na linaweza kuibuka lingine utapata muda wa kujibu uwe na utulivu tu Wakili.

Mheshimiwa Lissu amesema yeye usiku wa leo unamtosha ataenda kusoma kila kitu. Tukutane kesho asubuhi.

Tunawasubiri majaji sijui wanasema nini?

Maana ilitakiwa Mtuhumiwa apewe proceedings zote zimekamilika ametokea muhuni mmoja huko ameandika summary tena nyingine kwa mkono vi page kama 20 hivi halafu wakagonga mihuri ya mahakama.

Jaji anasema tukutane kesho saa nne asubuhi.

Mahakama imeahirishwa.

So kutane hapa kesho saa 4 asubuhi.
 
Niko tayari kukaa jela hata miaka 20 kama ni lazima. Hatuwezi kuruhusu wafanye wanavyotaka kwa sababu ya kutafuta uhuru wangu, kila tundu linalocheza na sheria lazima likabiliwe ili msingi wa kesi hii uwe msingi wa kushinda uovu na hila zake na kulinda haki na sheria.

Tundu Lissu
20250909_035722.jpg
 
Mwalimu wa sheria Tundu Lissu anaacha watu kwenye mataa,Lecture imekolea 🤣🤣🤣🤣🤣

"Mheshimiwa Jaji, Tundu Lissu tukimuacha aendelee hivi tunaweza mkamatia mbali sana,angalieni namna ya kumdhibiti Lissu, atatuacha nawaambieni waheshimiwa majaji."

- Wakili wa Jamhuri Job Mrema
1757418596786.jpg
 
NI KWA MASLAHI MAPANA YA UMMA SHAURI LA TUNDU A.M.LISSU KURUSHWA MUBASHARA.

Jopo la Majaji Watatu wa Mahakama Kuu likijumuisha Waheshimiwa Jaji Ndunguru, Kiwonde na Karayemaha wamepangwa kusikiliza na kuamua Kesi ya Uhaini baina ya Jamhuri dhidi ya Tundu Lissu, Shauri la Jinai Na. 19605 ya 2025 .

Mahakama ilianza vizuri kurusha mubashara katika hatua za awali ni rai yetu kwamba isirudi tena gizani na kuzuia kuoneshwa Mubashara kwa kesi hii muhimu.

Mahakama ijitahidi kuwa na consistency pale inapofanya mambo mazuri hasa ya kuhakikisha uwazi katika uendeshaji wa shauri labda iwe kwa matukio machache yenye uhitaji wa usiri kiusalama kwa mashahidi wale wanaozungumzianmambo ya ndani kuhusu taasisi zetu za usalama na siyo ushahidi wa kawaida.

NI VEMA KUHAKIKISHA KUWA SIYO TU HAKI ITENDEKE BALI IONEKANA BAYANA IKITENDEKA.

BAK Mwabukusi.
FB_IMG_1757467950343.jpg
 
NI KWA MASLAHI MAPANA YA UMMA SHAURI LA TUNDU A.M.LISSU KURUSHWA MUBASHARA.

Jopo la Majaji Watatu wa Mahakama Kuu likijumuisha Waheshimiwa Jaji Ndunguru, Kiwonde na Karayemaha wamepangwa kusikiliza na kuamua Kesi ya Uhaini baina ya Jamhuri dhidi ya Tundu Lissu, Shauri la Jinai Na. 19605 ya 2025 .

Mahakama ilianza vizuri kurusha mubashara katika hatua za awali ni rai yetu kwamba isirudi tena gizani na kuzuia kuoneshwa Mubashara kwa kesi hii muhimu.

Mahakama ijitahidi kuwa na consistency pale inapofanya mambo mazuri hasa ya kuhakikisha uwazi katika uendeshaji wa shauri labda iwe kwa matukio machache yenye uhitaji wa usiri kiusalama kwa mashahidi wale wanaozungumzianmambo ya ndani kuhusu taasisi zetu za usalama na siyo ushahidi wa kawaida.

NI VEMA KUHAKIKISHA KUWA SIYO TU HAKI ITENDEKE BALI IONEKANA BAYANA IKITENDEKA.

BAK Mwabukusi.View attachment 3468686
Mshana chukua like file la HILDA NEWTON la kesi ya mahakama kuu from day one liweke hapa Asante
 
Lisu anawapa changamoto kubwa sana kwenye taasisi ya mahakama.

Kizazi kitamkumbuka kwa weledi, uzoefu na elimu anayoiacha kwenye viunga vya mahakama.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 6

Anaendelea Mhe. Lissu

Katuga anasema kifungu cha sheria 266(1) cha CPA kwamba nyaraka nitapewa trial ikianza.

Hoja yangu ni kwamba what is a trial?

Sasa ngoja niwapeleke kwenye Black's Law Disctionary ni likitabu kubwa sana jekundu mtoto wa miaka mitano habebi. Analifungua kwa mizuka.

A trial does two things, examine evidence and adjudicate legal claims. Hiyo ndio trial.

Sasa hapa tuna àdjudicate legal claim. Hatujafika kwenye mashahidi lakini tayari tuko kwenye trial tunajadili masuala ya kisheria.

Sasa kama mahakama hii haiko kwenye trial ipo kwenye nini hapa?

Kwenye kesi zote ambazo mahakama kuu ina original jurisdiction.

Lazima zije hapa kupitia committal proceedings. Iwe ya Kisutu au ya Mbinga.

Sasa kama mahakama ya Kisutu haikuwa na mamlaka maana yake kazi yao ilikuwa ni SUFULI.

Hii ameitamka kama nilivyoandika. Kaitamka kinyaturu kabisa🤣🤣

Anaendelea kwahiyo kinachoendela hapa ni SUFULI pia.

Hatuwezi kuendelea na mambo ya SUFULI. yaani sifuli au zero.

Ndio anamaanisha hapo muelewe.🤣

S. 263 ya CPA aliyoisema Katuga sasa nakala niliyopewa ina kurasa 16 na nilipoanza kusema mambo yako tofauti ndio ikabidi nipewe rekodi za mahakama.

Sasa Katuga alikuwa ana justify anasema utaratibu tuliokuwa tunatumia siku zote ni huo.

Mambo ya practical experience kama ni kweli wamekuwa wanafanya hivyo. Basi naomba niseme huo ni uzoefu katika uvunjaji wa sheria.

Unajisifia uzoefu kuvunja sheria hoja hapa ni sheria inasema nini? Kama wao wamekuwa wanavunja sheria basi mahakama hii isiwakubalie kuendelea uzoefu huo.

Na kuna kifungu naona kama kinawatatiza sana na hawakielewi mawakili wa serikali sasa naomba nikisome ili wakielewe.

Anakisoma hapa. Mhe. Lissu nae anapiga Kingereza fulani ambacho sijui kama hawa Mapolisi angeamua kuwa anaongea nao kingereza huko Polisi wangeweza kumuhoji lolote.😁😁😁

Anaendelea hapa Mhe. Lissu.

S. 263(6) of CPA inasema nyaraka gani napaswa kupewa na mahakama ya ukabidhi na mimi sijapewa hizo nyaraka.

Practical experience itatupeleka kwenye shimo refu sana.

Katuga amehoji kwamba kuna criminality kuhusu nyaraka. Katuga anasema je hizi nyaraka ni za kughushi?

Waheshimiwa majaji naomba niseme Na nitafafanua.

Sio tu kuna ushahidi wa kughushi bali kuna conspiracy to defeat justice.

Anasimama Katuga anasema conspiracy haikuwepo asiende huko.

Lissu anasema siendi subiri sasa.

Waheshimiwa majaji sorry makaratasi yamekuwa mengi.

Kwanini nasema kuna forgery

1. Niliyopewa ina kurasa 16 na iliyopo mahakamani ni 101

2. Scanned berg pia nyaraka ya mahakama lakini ile ya karatasi 18 haikuwa na uthibitisho kuwa ni nyaraka ya mahakama na imeletwa na mahakama na ameitoa Kiswaga. Nikapewa

3. Inaanzia tar. 18 na inaishia siku hiyo hiyo. Document ya mahakama inaanzia tar. 10/04 hadi 18/08

4. Angalia ukurasa wa 1 wa nyaraka niliyoletewa gerezani haina submission kwenye page 1 lakini page ya 86 ya document ya mahakama inaonesha kulikuwa na submission page 86. Mahakama ilitoa uamuzi nyaraka inaonesha.

Aliyetengeneza hizi nyaraka alikuwa na nia gani kama sio kughushi ni nini?

Na Katuga alisema tuangalie kifungu cha 393 kuhusu forgery lengo ni kudanganya.

Hiyo nyaraka ilikuwa na lengo la kunideceive. Inawezekanaje kesi ya miezi mitano inaletwa rekodi ya siku what was the intent if it was not to deceive?

Part 7 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Leo September 10, 2025

Part 1

Kesi imeanza

Kasimama Wakili Nassoro Katuga anatambulisha Jopo la Mawakili wa Serikali kama kawaida yao.

Wapo mawakili sita wanaiwakilisha Jamhuri.

Katuga anasema mshitakiwa yupo.

Anaulizwa Mhe. Lissu nae anasema yupo tayari.

Majaji kama kawaida wapo wote watatu.

Katibu Mkuu wa Chama pia yupo hapa ameingia.

Kumbukeni leo tuna kesi mbili na ile ya mgawanyo wa mali za CHADEMA

Baadhi ya Mawakili wameanzia huko.

Sasa anasimama Job Mrema Wakili wa serikali.

Job Mrema: Naomba nianze kusema naunga mkono yote aliyosema Nassoro Katuga na naomba niongeze baadhi ya vitu.

Kuhusiana na Presidential Affairs Act kifungu cha 9 kinaelezea utaratibu ambao upande wowote unataka kuwaita mashahidi kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Lakini kifungu cha 9 tulichosema jana kilikuwa cha zamani lakini kwa mabadiliko ya sheria ya sasa sio kifungu cha 9 bali ni cha 10. Kwahiyo tunaomba ieleweke kuwa ni kifungu cha 10 pale kwenye tisa sio.

Kifungu cha 2 cha Sheria hii kinamtaja Rais, Makamu na Waziri Mkuu.

Hivyo kwa utaratibu ulioainishwa kwenye kifungu cha 10 unawazungumzia hawa vipngozi watatu wote.

Mashahidi hao wakihitajika utaratibu wa kufuatwa ni huo hapo.

Naomba nikisome tafadhali.

Anaanza kukisoma hicho kifungu cha 10.

Kingereza fulani cha Uyole 🤣🤣huyu sijui kama ni mchaga kweli.

Kwahiyo tumesema haya ili utaratibu ueleweke.

Compliance ya hiki kifungu haikufanyika. Na mshitakiwa alishauriwa kama anataka hao wawe mashahidi wake atakuja kuomba jambo hilo hapa mahakama kuu.

Mahakama hiyo ndio hii tuliyopo sasa anapaswa kuomba sasa kwasababu ndio inauwezo wa kusikiliza shauri.

Na kimsingi naomba kusisitiza hajaathirika na chchote kwasababu ndio kwanza mahakama inaanza.

Waheshimiwa majaji jambo kubwa tunalofahamu kwamba mahakama hii itajiuliza.

Je pingamizi lililoletwa na mtuhumiwa liko sawasawa mbele ya mahakama hii.

Lakini pia naomba kufanya marejeo ya kesi kama tatu.

1. George Aldon Kilinga and another vs Anna Joseph Riwa and another Civil appeal no. 6 2023 TZ HC 19093.

2. Joseph Mkenda vs Ladislaus PC Civil Appeal No. 132, 2023 [2024] HC 56

3. Commissioner General Tz Revenue Authority and AG vs Milambo Limited Civil appeal No. 62/2022

Anasimama Mh. Lissu anaomba wampe Nakala ya kesi wanazotaja.

Jaji anasema mpatieni sasa.

Katuga anasimama anasema jaji zipo kwenye mtandao hizi kesi.

Mh. Lissu anasema sasa niko gerezani nazipataje huko mtandaoni? Watu wanacheka🤣🤣

Jaji anasema sasa mawakili wa serikali mpo wengi sana chaguaneni mmoja akazilete hizo printed case.

Anaondoka Wakili mmoja.

Anasimama Katuga anasema naona mahakamani yupo mtoto ni kinyume na sheria kifungu cha 193 cha CPA.

Jaji anasema haya muondoeni huyo mtoto.

Ni kama watu wamesikitika fulani. 🤣 ika ndio sheria sasa.

Dogo alikuwepo ana umri kama wa miaka 13 hivi amekula suti amependeza sana na alikuwa anasikiliza kwa hisia sana.

Anaonekana ana ndoto ya kuwa Wakili pia huyu na alivyo alivyo huyu dogo ni kama anamkubali Mh. Lissu.

Ipo siku tutapata story yake bila shaka hata kama ni baada ya miaka 15. Kuna siku anaweza kuja kulielezea Taifa kuhusu kisa hiki akiwa tayari amekuwa Wakili labda enzi hizo wahenga wanasema muda ni mwalimu mzuri.

Haya anaendelea Mrema sasa.

Mleta pingamizi hakuieleza mahakama anaposema mahakama hii haina jurisdiction kwa mfano pecuniary jurisdiction au nyingine.

Alivyotaja hiyo pecuniary mawakili wamecheka.

Watakuwa wameelewa jambo ambalo sisi ma layman hatuelewi.

Mawakili wamecheka kwa dharau nahisi kutakuwa na kaujinga hapo.😂😂😂

Nitawauliza niwape mchapo baadae.

Je mahakama hii ina mamlaka au laa ndio hoja kubwa sasa mwenzetu hajasema hayo mamlaka ni yapi katika zile aina za mamlaka zinazojulikana kisheria.

Part 2 itaendelea kwenye post inayofuata.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 2

Anaendele Wakili wa Serikali Mrema

Jana kwenye mawasilisho yetu tulisema kifungu cha 184 cha CPA ndio kinaipa mahakama hii uwezo wa kuendelea na hiyo kesi.

Sasa ukisema mahakama hii haina mamlaka maana yake una question existence of power iliyopo kwenye sheria.

Kwenye kusisitiza na kupambanua. Mamlaka ambayo mahakama hii inayo sio makubaliano ya pande mbili kwamba sasa hii mahakama hii haina mamlaka.

Hatuwezi kukaa kikao na Tundu Lissu tukakubaliana kuwa mahakama haina mamlaka.

Lile shauri la George Kilinga kanuni ni kwamba jurisdiction ni jambo lililopo kisheria na shauri la Mkenda ukurasa wa 16 mashauri yote ni mahakama kuu. Lakini lile shauri la mwisho ni la mahakama ya rufaa.

Mahakama ya rufani kwenye kesi hiyo ilijiuliza swali what amount to jurisdiction.

Ukurasa wa 17 mahakama ilitoa maana ya jurisdiction.

Anasoma hapa kingereza chake akisoma ni kama mtu anaongea kilugha huwezi elewa. Bora hata Katuga hapendi mambo ya vingereza.

Amejijulilia mapema mwenzake ila huyu analazimisha uzungu sasa ZE ZE ZE ni nyingi mno.

Majaji wanauliza kila saa eti unasema??????😂

Tunaendelea kukomaaa kumsikiliza.

Anaendelea kwa kusema hizo kesi zote zinamaanisha ni lazima uwe specific unapo rise hiyo objection ya jurisdiction.

Leo pia hapa Mahakamani yupo Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, Boniface Mwabukusi yupo hapa anafuatilia kwa umakini.

Lakini pia Makamu Mwneyekiti wa Chama, John Heche yupo hapa.

Tuendelee na Mrema

Haya aliyosema mheshimiwa Lissu ni mapungufu. Sasa hayo mapungufu hayawezi kuifanya hii mahakama kuwa haina mamlaka.

Kwahiyo pingamizi hilo halina mashiko kwasababu Tundu Lissu anahoji usahihi ama kutokuwa na usahihi na proceedings ambazo zimefanyika kule chini.

Sasa niweke sawa kwenye haya niliyokuwa nasema. Pengine labda sijaeleweka.

Sasa naomba niweke sawa. Waheshimiwa majaji ili kulimaliza hili mapema naomba kurejea mahakama ya rufaa iliketi mwanza criminal appeal no. 260

Jaji anamwambia una cite vipi anza na jina kwanza.

Anasema sawa naweka sawa

Elias Daniel Doto, Musa Paulo Manyanza vs Republic.

Naomba nieleze mahakama kwamba laiti Bwana Tundu Lissu angekuwa na uamuzi huu asingeleta pingamizi lake kwenye hii mahakama.

Kwa mujibu wa hili shauri lilijitokeza mahakama kuu pale Mwanza wakati wanasikiliza shauri la mauaji lilikuwa committed kutoka mahakama ya wilaya Chato.

Iliibuka hoja kuhusu propriety ya committal proceedings iliyotoka Chato.

Mahakama iliamua kuwa hilo shauri lirudi mahakama ya Chato likaanze upya kufanyiwa committal baada ya kugundulika kuwa kulikuwa na makosa huko chini.

Nafikiri huyu Mrema hajaelewa anachokitaka Lissu hii kesi aliyoleta ni kama inambeba Mh. Lissu.

Sijui ndo yale maombi ya NOVENA yameanza kufanyakazi.

Maana Lissu yeye anasema hataki kesi yake ibariki mifumo mibovu ya kuonea watu wengine baada yake.

Nafikiri hata mahakama ikifuta mwenendo ule wa Kisutu ni ushindi kwa Lissu.

Haya ya kukaa mda mrefu gerezani Mhe. Lissu alishasema kwake sio shida yeye anachotaka Haki itendeke basi.

Part 3 itaendelea kwenye post inayofuata.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 3

Anaendelea Wakili wa Serikali Mrema

Anasema lakini shauri hili la Mahakama ya Rufaa linatofautiana na kesi hii iliyopo hapa maana lenyewe mapungufu yake ilikuwa ni kwamba hakimu hakuandika maneno kuwa namcommitt mtuhumiwa kwenda high court.

Anaikataa tena kesi yake.

Anasema zinatofautiana na kesi iliyopo hapa.

Anasoma huo uamuzi wa hiyo kesi.

Anasema nilikuwa natamani kuionesha mahakama ilivyo na uwezo na kuonesha style ambayo alitakiwa kuja nayo.

Pia kuna hoja aliomba mahakama ifute proceedings arudi nyumbani akalale.

Ni kama nilimsikia hivyo.

Mahakama hii ijue mwongozo upo kwenye hii rufaa.

Na mimi naomba kwamba kama mahakama itaona kuna shida irudishe file mahakama ya chini ili jambo hilo likafanyike vizuri.

Mheshimiwa Tundu Lissu anacheka sana wakati huyu Job Mrema anazungumza.
.

Sisi wengine hatuelewi sasa sijui anacheka nini?😀

Pengine tutajua hilo akianza kumjibu baadae ila ni kama anamuona huyu mtu mbona Kama ni mjinga mjinga.😀

Sasa anaendelea Mrema, anasema yale mambo kwamba alikamatwa Mbinga na kuletwa Dar es salaam.

Ni hoja yetu kwamba shauri lile la Kapufi aliloleta Lissu lilikuwa linahusiana na nini na lake linahusiana na nini? Ni mashauri tofauti haya.

Mhe. Jaji tunaomba kuongeza kifungu cha 187 cha CPA

Ukikisoma na kutafsiri pamoja na kesi ya Kapufi utaona kesi hiyo inaunga mkono msimamo wetu.

Wakati Lissu anasema alikuwa anaonesha kuhusu zile tarehe hiyo sip fatal ni sleep of a pen.

Haiwezi kuvitiate proceedings. Hili suala la tarehe ni dogo tu.

Jamhuri tunaomba kusema makosa ya kibinadamu yapo.

Yanatokea kwa binadamu yeyote na hicho ndio tunasema sleep of a pen.

Watu wanacheka.😂😂😂

Anasema hii sleep of a pen ina madhara gani? Imetokea Kwenye kesi nyingi sio kwenye kesi hii tu.

Shauri la Baraka Mashaka vs R CRIMINAL APPEAL No. ... ukurasa wa 5 mahakama ilipima na kuona it was mere a sleep of a pen na mahakama ilisema hicho ambacho kilitokea kwenye ukrasa wa 55 ni makosa madogo hayaathiri chochote.

Kwahiyo tunaialika mahakama hii ione. Hata kama na kama tulivyosema kwenye rekodi kuonekana makosa ya tarehe hatuoni shida.

Tundu lissu hajatuambia kama rekodi zina shida kwamba hazijaandikwa ila analalamikia tarehe.

Yeye amezungumzia tarehe na nukta.

Wakati mwingine mahakama inaweza muelewa kama ni oversight tu kwake

Lakini pia amesema kuna affidavit mbili hakuwahi kupewa ambazo ni nyaraka zinatokana na Misc. Cr application no 17059/2025.

Wapo ndege hapa wameingia mahakamani sijui wametoka wapi?

Wanatupigia kelele kidogo., wanarukaruka. Wasije kutua kwenye kipara cha Mrema bure.😀😀😀

Tuendelee na Mrema

Naomba niseme kusema kuhusu 262(4) ya CPA. Uchunguzi ukifanyika na pale inabainika ushahidi unatosha baada ya kuridhika kwa mkurugenzi wa mashtaka.

Ndipo ambapo Jamhuri inaleta taarifa mahakama kuu na taarifa hiyo kwa maana ya information ikishakuwa filed mahakamani ndio mahakama ya chini nayo inajulishwa.

Kwenye kuiweka sawa hii waheshimiwa majaji information inayofiliwa mahakama kuu inaambatanishwa na nyaraka mbalimbali kama vile maelelzo ya mashahidi.

Hoja ya msingi ni kwamba anachokiomba Bwana Lissu je hizo zilikuwa sehemu ya information iliyopandishwa?

Hizo hazikuwa nyaraka huko kwenye commital sio viambatanisho.

Part 4 itaendelea kwenye post inayofuata.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 4

Anaendelea Wakili wa Serikali Mrema

Upande wa Jamhuri tulikuwa tunajiuliza jambo moja DPP yeye ameshajiridhisha kwa mujibu wa taratibu zake kwamba nyaraka hizi zinafaa ndio kaziwasilisha.

Sasa hatuoni kama ilikuwa ni busara kama nyaraka haijawasilishwa wewe kuiomba kwa utaratibu kama huu.

Hivyo basi principle ambayo inaambatana na haya ni kwamba the burden of proof lies to the prosecution.

Sasa huwezi kumshauri mkurugenzi wa mashitaka ushahidi gani autumie dhidi yake.

Waheshimiwa Majaji mahakama hii imepiga hatua sana. Mambo ya ufundi kwamba jambo fulani limekujaje.

Tunaikaribisha mahakama hii ireje principle ya Oxygen rule ukisoma inakuonesha kwmaba hakuna shida ambayo inaenda kwenye root ya kesi ya msingi.

Mahakama hapa tunaposema oxygen rule hapa anayepewa oxygen anayepewa hiyo oxygen ni yeye.

Alishasema kuwa amechoka kukaa ndani.

Sasa kwa tunavyoendelea akifanikiwa analotaka ataenda kisutu.

Sasa yeye avute hiyo hewa kutoka mahakamani ili shauri hili lifike mwisho kwa harakal, avute hewa.

Swali ninalojiuliza hapa. Document ambayo haijakuwa imetajwa na haikusomwa pale kwenye committal Court inaweza kutumika hapa juu bila kufuata utaratibu?

Hizo affidavit hazikusomwa wala hazikutumika.

Naomba sasa tena tuirejeshe mahakama kwa kufahamu mawanda kesi ya Michael Maige vs R criminal appeal no. 222.

Ukurasa wa 11 mahakama ya rufaa iliona na kutoa mtizamo kuwa nyaraka ambayo haikutajwa kule chini haiwezi kutumika huku juu.

Sasa hata mimi sio wakili ila Job kweli haelewi anaongea vitu tofauti.

Kuitumia wataitumia wao kwahiyo hawawezi kuitumia kama haiko kwenye orodha.

Ila mtuhumiwa anachokisema yeye ni kwamba nyaraka ambazo zinamuhusu zote na zilikuwa sehemu ya kesi yake wampatie hata kama hawatazitumia yeye anaweza zitumia kujitetea, Hili nalo linahitaji uwakili wajameni?😁😁😁

Lissu anaomba nakala wanasema hawana tena.

Wanaambiwa Kimbieni mkalete, kuweni serious kidogo.

Jamaa anaondoka na joho lake hapa.😀

Mrema anasema sasa mheshimiwa jaji naomba tu kama ndio hivyo nimalizie hapa.

Katuga anasema tumemaliza sisi.

Jaji anauliza sasa Mshitakiwa unaweza kuendelea bila hizi kesi zao kukupatia. Walizoenda kutoa copy.

Mhe. Lissu anasema niko tayari kuendelea zitanikuta mbele ya safari hakuna shida. Mimi acha nianze kupiga nondo zisitucheleweshe.

Zitakapofika nitazisoma hapa hapa na kuzijibia.

Anaanza Mhe. Lissu nawashukuru Majaji kwa nafasi hii na mimi nijibu hayo majibu yao waliyotoa kwenye hoja zangu.

Nianze na huyu Katuga na nitaenda kwa mtiririko huo huo.

Suala la kwanza alisema Katuga ni suala la mamlaka ya mahakama ni suala la kisheria. Na leo kalirudia huyu mwenzake.

Jurisdiction is created by statute and it is limited by statute.

Waheshimiwa majaji hiyo principle kama nilivyosema juzi ilitokea kwenye kesi ya Farid kwamba Jurisdiction ni creature ya sheria.

S. 262 inasema apelekwe kwenye mahakama ambayo iko mahali alipokamatiwa.

Sasa kama jurisction ni suala la kisheria basi sheria yenyewe ndio hii sasa ninayoitaja kifungu cha 262 cha CPA

Sasa ukisema Kisutu ina mamlaka ya kusikiliza kesi ya mtu ambae sheria inasema kwenye mashauri ya ukabidhi mtuhumiwa anapaswa kusomewa mahali alipokamatiwa.

Na hapa wasichanganye mambo wao wanafikiri tunazunguzia kesi ya wizi wa kuku. Kwneye mashauri ya committal mambo ni tofauti kidogo. Hii ni sheria wanapaswa kuelewa na sio kukalili tu vitu.

Hoja ya msingi kwenye mahakama ya ukabidhi. Hoja sio umefanyia wapi kosa hoja ya msingi mshitakiwa amekamatiwa wapi.

Ni muhimu hawa wenzetu wakaelewa tunazungumzia jambo gani? Wasipoelewa hapo watahangaika sana.

Eti Katuga anasema Mbinga hawana tuhuma zake asingeweza somewa huko Mbinga.

Sasa na mimi namjibu kama Mbinga hawakuwa na tuhuma zangu au kesi zangu kwanini walinikamata huko Mbinga. Walimkamata mtu ambae hawajui tuhuma zake?

Part 5 itaendelea post inayofuata.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 5

Anaendela Mhe. Lissu

Kama ilivyowezekana if you choose where to arrest you should know which court you need to take the accused

Katuga anasema kwa busara tu ndio maana tuliletwa Kisutu kwasababu kosa lilifanyika huku.

Sasa mimi nasema Tafsiri ya masuala ya kisheria haipaswi kuwa tafsiri ya busara. Hii sio mahakama ya busara ni mahakama ya sheria. Ingekuwa mahakama ya busara msingekuwepo hapa mahakamani leo. Pengine huko mtaani wapo watu wengi wangekuwa majaji na nyie mngekosa kazi hii mliyonayo.

Ila sisemi kwamba hamna busara ila ninachosema ni kwamba nyie ni majaji kwasabbau ya sheria.

Ungekuwa ni mpira ukimuona Messi au Mpanzu anacheza mpira unaweza kuamka kesho asubuhi ukaenda kununua viatu na wewe uwe mcheza mpira.

Ndio hivyo kwenye sheria ukimsikiliza Lissu akionngea sheria unaweza kwenda kununua suti na mafile kesho na wewe uingie mtaani.

Tusomesheni watoto ndugu zangu.😁

Sasa sheria ya mamlaka za mahakimu amezitaja Katuga nashangaa zinahusiana nini na kesi hii.

Katuga ametaja kifungu cha 5 ambacho kiuhalisia kinanibeba mimi kwasababu hicho kifungu kinasema mamlaka ya hakimu kinatakiwa kuzingatiwa sheria zingine mahsusi zinazoelezea mamlaka ya mahakama.

Sasa je sheria gani inahusiana na mambo ya ukabidhi?

Yaani commitall ni MCA? HAPANA.

Ni sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai yaani CPA. Na ndio inasema nipelekwe Mbinga kusomewa sio kisutu ndio nilikokamatiwa.

Kwahiyo Katuga ameleta kifungu cha 5 cha sheria ya mamlaka za mahakimu kunaunga mkono hoja yangu nafikiri amesema mambo ambayo haelewi. Hii sheria imeandikwa kingereza sasa sijui tatizo ni nini?

Anasimama Katuga anasema Mh. Anaenda mbali sana. Section nyingine sikusema.

Mh. Lissu anasema alisema kama hakusema niambieni majaji?

Majaji wansema endelea Lissu.

Lissu anaendelea 😂

Hicho kifungu cha 41 cha MCA kinaleezea kule kwenye schedule yake sheria za ulevi, pombe mambo ya mitaro na maji machafu.

Sasa huyu Katuga analeta mambo haya kwenye hii kesi lakini hii sheria mwisho inasema mahakama hiyo ya wilaya itakuwa na mamlaka kusikiliza kesi zingine kwa mujibu wa sheria zingine.

Kwahiyo hata hii 41(1) ya MCA nayo inaunga mkono hoja yangu entirely kwamba turudi kwenye sheria za committal na sheria za commitall ndio ziansema msomeee shitaka mahali ulipomkamatia mtuhumiwa. Kanuni ni hiyo.

Ananendelea Mh. Lissu

Sasa mawakili wa serikali waliitaja kesi ya Farid Had Mohamed ambayo mimi niliiwasilisha hapa.

Ukurasa wa 9 wa kesi hii unasema s. 243 to 246 ya CPA na kwasasa tunasema ni s. 261 hadi 264 kwa sheria ya sasa.

Mahakama ya rufaa inasema hizo ndio crucial section za committal proceedings.

Sasa tuanzie 264 ambayo inatoa limitations and exceptions. Inayoweka nipaka na utaratibu wa Committal. Tumetumia miezi mitano Kisutu bila mamlaka.

Nimekalishwa gerezani miezi mitano na mahakama ambayo haina mamlaka. Ukweli ndio huo.

Sasa Waheshimiwa Majaji mahakama ya rufaa kwenye Dodoli Kapufi ilisemaje? Na pia hiyo kesi ya Hadi.

Ili mahakama kuu ipokee shauri for trial lilitokea mahakama ya ukabidhi.

Mahakama ya rufaa inasema it should be properly investigated and properly committed. It said duly committed.

Duly committed maana yake it has been committed in accordance of the legal requirement. Then, can any one serious should say kuna kesi imeletwa mahakama kuu? Hayupo.

Katuga alisema sielewi hoja ya mahakama ya kisutu imetokea wapi?

Jibu langu kwake ni Kwamba Someni sheria mtajua hoja hiyo imetokea wapi?

Usiposoma sheria utajuaje mamlaka hewa ya mahakama ya kisutu.?

Wasome sheria wasipofanya hivyo hawataelewa hoja zinatokea wapi.

Hilo naishia hapo naenda kwenye hoja nyingine

Part 6 itaendelea kwenye post inayofuata.

Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 6

Anaendelea Mhe. Lissu

Katuga anasema kifungu cha sheria 266(1) cha CPA kwamba nyaraka nitapewa trial ikianza.

Hoja yangu ni kwamba what is a trial?

Sasa ngoja niwapeleke kwenye Black's Law Disctionary ni likitabu kubwa sana jekundu mtoto wa miaka mitano habebi. Analifungua kwa mizuka.

A trial does two things, examine evidence and adjudicate legal claims. Hiyo ndio trial.

Sasa hapa tuna àdjudicate legal claim. Hatujafika kwenye mashahidi lakini tayari tuko kwenye trial tunajadili masuala ya kisheria.

Sasa kama mahakama hii haiko kwenye trial ipo kwenye nini hapa?

Kwenye kesi zote ambazo mahakama kuu ina original jurisdiction.

Lazima zije hapa kupitia committal proceedings. Iwe ya Kisutu au ya Mbinga.

Sasa kama mahakama ya Kisutu haikuwa na mamlaka maana yake kazi yao ilikuwa ni SUFULI.

Hii ameitamka kama nilivyoandika. Kaitamka kinyaturu kabisa🤣🤣

Anaendelea kwahiyo kinachoendela hapa ni SUFULI pia.

Hatuwezi kuendelea na mambo ya SUFULI. yaani sifuli au zero.

Ndio anamaanisha hapo muelewe.🤣

S. 263 ya CPA aliyoisema Katuga sasa nakala niliyopewa ina kurasa 16 na nilipoanza kusema mambo yako tofauti ndio ikabidi nipewe rekodi za mahakama.

Sasa Katuga alikuwa ana justify anasema utaratibu tuliokuwa tunatumia siku zote ni huo.

Mambo ya practical experience kama ni kweli wamekuwa wanafanya hivyo. Basi naomba niseme huo ni uzoefu katika uvunjaji wa sheria.

Unajisifia uzoefu kuvunja sheria hoja hapa ni sheria inasema nini? Kama wao wamekuwa wanavunja sheria basi mahakama hii isiwakubalie kuendelea uzoefu huo.

Na kuna kifungu naona kama kinawatatiza sana na hawakielewi mawakili wa serikali sasa naomba nikisome ili wakielewe.

Anakisoma hapa. Mhe. Lissu nae anapiga Kingereza fulani ambacho sijui kama hawa Mapolisi angeamua kuwa anaongea nao kingereza huko Polisi wangeweza kumuhoji lolote.😁😁😁

Anaendelea hapa Mhe. Lissu.

S. 263(6) of CPA inasema nyaraka gani napaswa kupewa na mahakama ya ukabidhi na mimi sijapewa hizo nyaraka.

Practical experience itatupeleka kwenye shimo refu sana.

Katuga amehoji kwamba kuna criminality kuhusu nyaraka. Katuga anasema je hizi nyaraka ni za kughushi?

Waheshimiwa majaji naomba niseme Na nitafafanua.

Sio tu kuna ushahidi wa kughushi bali kuna conspiracy to defeat justice.

Anasimama Katuga anasema conspiracy haikuwepo asiende huko.

Lissu anasema siendi subiri sasa.

Waheshimiwa majaji sorry makaratasi yamekuwa mengi.

Kwanini nasema kuna forgery

1. Niliyopewa ina kurasa 16 na iliyopo mahakamani ni 101

2. Scanned berg pia nyaraka ya mahakama lakini ile ya karatasi 18 haikuwa na uthibitisho kuwa ni nyaraka ya mahakama na imeletwa na mahakama na ameitoa Kiswaga. Nikapewa

3. Inaanzia tar. 18 na inaishia siku hiyo hiyo. Document ya mahakama inaanzia tar. 10/04 hadi 18/08

4. Angalia ukurasa wa 1 wa nyaraka niliyoletewa gerezani haina submission kwenye page 1 lakini page ya 86 ya document ya mahakama inaonesha kulikuwa na submission page 86. Mahakama ilitoa uamuzi nyaraka inaonesha.

Aliyetengeneza hizi nyaraka alikuwa na nia gani kama sio kughushi ni nini?

Na Katuga alisema tuangalie kifungu cha 393 kuhusu forgery lengo ni kudanganya.

Hiyo nyaraka ilikuwa na lengo la kunideceive. Inawezekanaje kesi ya miezi mitano inaletwa rekodi ya siku what was the intent if it was not to deceive?

Part 7 itaendelea kwenye post inayofuata.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 7

Anaendelea Mhe. Lissu

Hichi kinachoonekana intended to deceive me.

Sasa niendelee nafikiri hiyo hoja tumeiweka vizuri.

Wakili Kiswaga samahani Wakili Katuga.

Watu wanacheka. 😂

Nimelelewa na one among the best state attorney naomba nisamehewe.

Sio Wakili Kiswaga ni Wakili Katuga. Naomba niendelee ni rafiki zangu hawa.

Ni kama Katuga alisema unalalamika nini wakati sisi ndio tulikuombea.

Kwahiyo huna ulichonisaidia.

It was My own expozeeee🤣 nililiibua mimi sio Katuga. Asijipe umuhimu kwenye hili.

Hoja ya tatu ya Katuga juu ya maahirisho.

Naomba kuna kitu niseme kidogo kwenye forgery zipo proceedings za Tar. 13 hazijawahi kuonekana. Hazipo.

Anasimama Katuga anasema hayo ya Tar 13 hakusema.

Lissu anasema nilisema hayo na mahakama iangalie kama sikusema basi naomba niendelee na nyie angalieni huko.

Sasa nirudi kwenye maaahirisho.

Sasa kwamba sheria kuhusu adjournment haikufuatwa basi ni grievances yaani malalamiko tu na hapa sio mahala pake.

Sasa namjibu kwamba kweli I was aggrieved by the adjournment. Sikufurahishwa nayo kabisa. Hilo la kwanza.

Na my grievances zipo kufungu cha 265(1) cha CPA kinaleeza utaratibu wa kuahirisha kesi wakati wa committal.

So of course I'm aggrieved kwasababu sheria imekiukwa at my expense.

S. 265 ya CPA inasema anaisoma.

Tafsiri yake ni kwamba kila kesi inapoahirishwa wakati wa committal lazima sababu zitolewe.

Na zile kesi za akina Kapufi zilisema mahakama ya ukabidhi lazima ifuate sheria za ukabidhi.

Kwanini sheria inataka sababu za msingi ziwepo na sababu hizo ziandikwe?

Mimi naishi gerezani kwenye maximum security prison. Najua nini maana ya kuishi kule.

Nafikiri Katuga hajui labda amwambie haya maneno naona hayasemi hapa.🤣

Sasa sheria inasema labda sababu za msingi ziwepo pale unapoamua kumpeleka gerezani uwe na sababu za msingi. Na hizo sababu ziandikwe. Hiyo ni sheria inasema sio Katuga.

Katuga anakuna kinywa Kama mtu mwenye mba ule unaochoma choma hasa ukisuka nadhani hapa wadada wenzangu mnanielewa vema, nyie kaka zangu hamuwezi kuelewa hii.😂

Haya tuendelee na Mhe. Lissu

Katika mara 13 ambazo kesi iliahirishwa ni mara tatu tu ndio ilitoa sababu mara 10 walikaa kimya.

Kama nilivyoonesha kwenye rekodi ilipigiwa kelele na mawakili wangu na baadae nilipoamua kujitetea mwenyewe. Hatukuacha kupiga kelele.

Na Hakimu Kiswaga ali ignore concern zetu na hata hakuandika sababu za kuahirisha.

So I paid for those adjournments sasa anaposema sijaonesha namna gani nimeathiriwa na maahirisho hayo.

Sasa unahitaji kuwa katili kiasi gani? An innocent man as per Constitution living with condemned prisoners

Halafu anatokea mtu anasema eti ameumiaje?

Amesimama Katuga anasema hakusema kama aliathirikaje kwahiyo asiende huko.

Lissu anasema nilisema Mhe jaji siku kadhaa. Anarudia maneno aliyosema.

Jaji Ndunguru anasema hayo ni kweli ulisema.

Katuga anasema sasa jaji hakusema aliathirika vipi?

Watu wanazomea.😁😁😁😁

Jaji anasema nafikiri alisema Tundu Lissu hebu endelea.

Waheshimiwa majaji wanaoahirisha kesi na wanaotakiwa kutoa sababu ni mahakama ya kisutu na Wakili wa serikali Katuga akiwa hapa Mahakama kuu.

Haya aliyosema wakili wa serikali Katuga yalipaswa yaonekane kwneye rekodi za mahakama. Iseme mahakama yenyewe.

Hakuna mahali kwenye rekodi zinasema tunaahirisha kwasababu mtuhumiwa hayupo. Haipo.

Sasa yeye aliyokuwa anasema kuwa eti kuna siku mtuhumiwa hakuwepo. Hayo tunayapata wapi? Ukurasa wa ngapi? Hajaonesha na haipo.

Nimesema ni mara tatu tu mahakama imewahi kuahirisha kw kutoa sababu na hizo sababu haijawahi kutolewa kuwa ni mtuhumiwa hayupo kwenye hizo mara tatu.

Hili jaribio la to shift the burden with the committal Court wanataka tushare dhambi. Mimi siko tayari. Labda Katuga na Kiswaga ila mimi hapana siko tayari kushare hiyo dhambi.

Part 8 itaendelea kwenye post inayofuata.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 8

Anaendelea Mhe. Lissu

Katuga jana anasema mahakama ilikuwa inapewa sababu na mahakama inaamua.

Sasa nimwambie Katuga S. 265 inasema sababu zinazohitajika ni za mahakama na sio za wakili wa serikali.

Alipaswa kutuambia mahakama ilisema nini wakati inaahirisha na sio Katuga aliiomba nini ili mahakama iahirishe.

Ni anakili kuwa mahakama haikuwa inatoa sababu ila sababu zilikuwa ni zake.

Hakuna mahakama imezifanya hizo sababu kuwa zake na kuzitoa yenyewe.

Wakili wa Serikali Mkuu, Katuga anasema utaratibu uliofanywa na Hakimu Kiswaga na yeye kuandika amri zake nje ya amri zilizotolewa na Jaji Mtembwa.

Sasa naomba niseme kwamba kuna ukiukwaji wa sheria hasa kwenye committal proceedings zinajumuisha proceedings za sect. 194 za witness protection measures.

Nilisema mtakumbuka effect ya mahakama kutoa amri ya kuficha mashahidi.

Amri ya Jaji Mtembwa hakikisheni mnaficha utambulisho wa hao mashahidi. Sasa clearly S. 194(2) cha CPA hakikuzingatiwa.

Sasa wao wamenipa nyaraka ambazo zina ninafanya niwafahamu hao mashahidi.

Kanuni ya 8 inasema endapo amri ya ulinzi imetolewa nyaraka zote zinazohusiana na amri ya ulinzi vitaambatanishwa na kupewa mtuhumiwa.

Sasa committal proceedings zilitakiwa kuendeshwa kwa mujibu wa amri ya Jaji Mtembwa na sio amri ya Franco Kiswaga PRM.

Amri ya ulinzi ya Jaji sio ya Franco Kiswaga. Ieleweke hivyo.

Waheshimiwa majaji wakili wa serikali sikuonesha sheria iliyovunjwa?

Sasa nilipaswa kuonyesha nini zaidi ya haya?

Kwa kumalizia hiyo hoja, Mahakama ya Hakimu mkazi kisutu haikuwa na mamlaka yoyote once the high Court made six orders the commitall Court was duty bound to respect and act in accordance with the High Court directives.

Sasa mahakama kuu itaendeleaje kwa kutumia committal order ambayo haikuzingatia amri ya mahakama kuu.

Magistrate should not in this country have power to vary orders of superior courts.

Wakili Kiswaga sorry Wakili Katuga.

Alisema kwani kulikuwa na shida gani kwa mahakama kufunga live streaming wakati yenyewe ndio iliyotuhusu hiyo live streaming.

Kwahiyo tulipata kwa ufadhili wa mahakama na na imeondoa kwa ufadhili huo.

Rekodi ya tarehe 13 au 18 nilisema pale Kisutu kuwa wayu wa nchi hii wana haki ya kikatiba kuona kinachowahusu. Kesi ya uhaini niliwaambia juzi kuwa they come once every two generation.

Nilisema juzi kuwa kwenye katiba yetu inasema kwamba kosa kubwa kuliko yote ni kosa la uhaini.

Mahakama ya hakimu kisutu iliombwa ikakubali na yakatangazwa karibu miezi miwili.

Anaendelea Mh. Lissu Mahakama kuu haikukataza live streaming, haikukataza publication of the proceedings. Hayo hayakukatazwa.

Yaliyokatazwa nilishasema na anayataja hapa kutoka kichwani amezikalili zozote.

Sasa haya ya kisutu yalitokea wapi? Kiswaga alisema ukisema hata kwenye social media utaenda jela. Sasa wapi Mtembwa alizungumzia watu kupost kwenye mitandao.

Amri ya Kiswaga ilikuwa kinyume na sheria na kinyume na amri ya Mtembwa.

Sasa kila saaa tunasikia hilo tu, hiyo tu. Ndio tufute proceedings yote? Wanasema hivyo.

Sasa naomba tuelewane kuwa tunapaswa kuziangalia hizi irregularities that was very systematic.

If that was the case mahakama kuu haiwezi kuassume hizi records za namna hii.

Waheshimiwa Majaji naomba sasa nizungumzie yale maelelzo ya mtuhumiwa.

Wakili Kiswaga ala samahani sana. Alisema huo utaratibu wa s. 263(4)(5) ya CPA unahusika pale mtuhumiwa anapokiri kosa tu yaani admission au confession.

Kwamba baada ya kukiri asomewe hayo maneno yake ili aongeze hayo maneno ndio anasema hivyo.

Kwa vile mimi sikukiri kosa kwahiyo hakukuwa na sababu ya mimi kupewa nafasi.

Kwa maneno hayo nashukuru upande qa jamhuri wanakubali kuwa hayo masharti hayakufuatwa.

Na hayakufuatwa kwasababu sikukiri kosa.

Part 9 itaendelea kwenye post inayofuata.
 
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI

Part 9

Anaendelea Mhe. Lissu

Sasa hoja ni je yanayozungumzwa kwenye hivyo vifungu yanazungumzia confession peke yake?

S. 263(3) of CPA inasema you may say anything that relevant to charge against you and will be written and may be used in evidence at your trial.

Sasa kwenye kifungu hiki kuna admission yoyote?

Kesi ya Dodoli Kapufi mahakama ya kabidhi hairuhusiwi kufanya maamuzi ya maswala ya kisheria 266(6)

Anasoma hapa hiki kifungu....

Anaanza kuelezea hapa kwamba Hakimu alipaswa kuandika maelezo ya Lissu kama yalivyo na sheria imeandika kabisa kuwa inampasa na kumlazimu kuandika maelezo hayo ila mahakama ya kabidhi ilizuia maelezo hayo kuandikwa.

Kwahiyo Waheshimiwa Majaji haya maneno niliotakiwa kusema yalikuwa ushahidi wangu unaopaswa kutumika kwenye mahakama hii.

Wakili Katuga anasema bila kusomewa hayo maelezo Lissu kaathirika vip?Lissu anajibu kuwa maelezo yangu ambayo ni ushahidi hayakuchukuliwa hio ilikuwa kinyume na sheria na kinyume na haki.

Anaendelea hapa anasema twende kwenye mashahidi wangu mtakumbuka mashahidi aliowataja walikuwa Rais, Waziri Mkuu, Makamu Rais.

Ukisema Shahidi yangu Yesu basi atakuuliza nipe anuani yake hiyo ndio gist ya 264 ya CPA.😂

Sio kusema sitaki kuandika.

Presidential affairs Act imesemwa jana na imerudiwa leo hii mahakama hii imeambiwa kuwa hawa wana kinga za kupewa summons za mahakama kuja kitoa ushahidi mahakamani.

Mmesomewa kifungu cha 10 jana kilitajwa cha 9 leo wamerekebisha.

Anasoma kifungu cha 10 cha Presidential Affairs Act. .....

Kwahiyo Rais hawezi pelekewa Summons ya Mahakama kwa maneno hayo niliyosema.

Sheria inasema unatakiwa umuone Katibu Mkuu Kiongozi au Katibu wa Rais au Katibu Mkuu baada ya kuombwa na mahakama wa kuomba msaada wa kumserve Rais huyo Katibu wa Rais au Katibu Mkuu kiongozi watatoa utaratibu.

Sasa haya ndio yanayotoa zuio? Au wanasoma sheria kwa namna gani?

Walisema kifungu hiki kinawahusu Waziri Mkuu na Makamu wa Rais sasa katika kifungu hiki wapi wamesemwa hawa aliowataja Mrema leo?

Sasa Mheshimiwa Jaji kuna kitu hakisemwi naomba nikiseme mimi.

Sect. 9 ya sheria hiyo ya Sasa. Presidential Affairs Act.

Kinasema immunity of Arrest au kumlazimisha aje mahakamani.

Sasa mimi nimeomba Rais akamatwe? Hakuna nilipoomba.

Kifungu cha 9 kinasema kama yupo mtu atahitaji Rais awe shahidi Mahakama itamnotify Rais kuhusu nia ya mtu huyo.

The court is required to notified the President. Ana kinga ya kutokushitakiwa tu na sio kinga ya kuja kutoa ushahidi.

Mahakama inapaswa kumpelekea Katibu Mkuu kiongozi au katibu wa Rais na hao wanapaswa kuisaidia mahakama kumfikishia Rais sio kwa mujibu wa sheria kuwa jambo hilo limekatazwa. Sio kweli.

Hiyo hoja ni ya bure. 😁😁😁

Naomba sasa nijielekeze kwenda kusoma haya maamuzi waliyonipa ili tuweze kurudi kesho nije kujibu kuhusu hayo.

Jaji anasema Katuga unasemaje.

Katuga anajibu kuwa mimi sina shida. Akasomeee tukutane kesho.

Majaji wanateta hapa kidogo.

Wanaandika wakiwa wameinama chini. Tusubiri maelekezo. Kuna dalili tutakutana kesho hapa.

Jaji anasema kutokana hakuna pingamizi lolote tunaahirisha shauri hili saa tatu asubuhi kesho tutakuja kukusikiliza umalizie

Shauri limeahirishwa hadi kesho asubuhi saa tatu.
 
Tundu Antipas Mugway Lissu siyo wakili tuu anayejua kuongea na kupanga hoja.

Kwasanaa ya sheria watu wa namna hii huwa tunawaita "Legal Maneac" ni watu wenye ueledi wa kina na ubobevu ambao huwezi kuupata Darasani... NI CHUO KIKUU CHA HIYARI CHA TAFAKURI ZA KISHERIA.

BAK Mwabukusi.
1757522357627.jpg
 
Back
Top Bottom