Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

FB_IMG_1755792943870.jpg
 
Saa chache baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kupiga marufuku urushaji wa moja kwa moja wa kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Tundu Lissu, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Karagwe Dkt. Benson Bagonza ameeleza kuwa hatua hiyo ni sawa na "kuwapindua wananchi."

Katika andiko lake alilolitoa Agosti 18, 2025, Bagonza amesema kesi hiyo inamhusu siyo tu Lissu, bali wananchi wa Tanzania kwa ujumla kwa kuwa inalenga usalama wa taifa na mamlaka ya wananchi.

"Mahakama ya Hakimu Mkazi 'imetupindua' katika kesi inayomkabili huyo 'mpenda madaraka' Tundu Lissu...Sisi wananchi wa Tanzania (Jamhuri) tumeandaa mashahidi wetu ili kuhakikisha tunamtia hatiani na kumnyonga. Tuna uhakika tutamtia hatiani kwa ushahidi tulio nao," ameandika.

Askofu Bagonza amesisitiza kuwa Lissu hashtakiwi na Rais wala Jeshi la Polisi, bali na wananchi wenyewe. Aidha, ameonya kuwa kutolewa ushahidi kwa siri na kuendesha kesi kwa siri kunaweza kuchukuliwa kama njama za kumtorosha mtuhumiwa.

"Sisi wananchi wa Tanzania (Jamhuri), kwa uzalendo tulio nao, tuko tayari kutoa ushahidi hadharani ili kila mtu ajue na hao wanaomtuma Tundu Lissu wajue kuwa tuko imara. Tundu Lissu hashtakiwi na Rais wala na Jeshi la Polisi. Anashtakiwa na sisi wananchi wa Tanzania (Jamhuri). Tunataka watu wote hasa chama cha Tundu Lissu, wajue kuwa Jamhuri yetu (wananchi) hatuna mchezo. Tutailinda nchi yetu kwa wivu mkubwa. Kesi hii iwe fundisho kwa vwote wanaodiriki kuchezea mamlaka ya wananchi. hili fundisho liwe kamili, kesi hii tungetamani ifanyike uwanja wa taifa. Watu waone na kusikia, na akipatikana na hatia anyongwe hadhararni, siyo gerezani".

"Kwa kuwa hata uhai wa jambazi ni muhimu utolewe kwa utaratibu, tunataka uhai wa wahaini wote utolewe kwa utaratibu na kwa uwazi. Sisi wananchi (Jamhuri) hatujamtuma yeyote kuficha chochote. Sisi ndio walalamikaji. Wananchi (Jamhuri), wana haki ya kuhisi kuwa kuna njama za kutaka kumwachia Tundu Lissu pale wanapotaka kesi iendeshwe kwa kifichoficho na ushahidi utolewe kwa siri, ipo hatari ya kuja kutuambia alitoroka!".
 

 
Wana JF kuna mahali tulipitiwa na kujisahau.. Tulipaswa kuwa na mada maalum ya Tundu Antipas Lissu.

Mwanasheria nguli, mwanaharakati wa haki za binadamu na sasa mfungwa wa kisiasa wa kesi ya uhaini na mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani Tanganyika

Ana historia yake maalum .. Ana mengi mazuri ya kiwango kaifanyia Tanganyika.. TUMUENZI SASA. NI WAKATI WAKEView attachment 3381742
(7,029) Historia fupi ya maisha ya shule ya Tundu Lissu | JamiiForums Historia fupi ya maisha ya shule ya Tundu Lissu
Respect Nyingi sana kwa huyu Mwamba
 
 
Anaanza Mh. Lissu kusema anasema nawashukuru Majaji kwa kunipatia Mawakili.

Pamoja na kwamba mimi sikumuomba na simfahamu wakili Neema Saruni alikuja mwenyewe kuniona kwenye gereza la Ukonga alijitambulisha na kuniambia yeye ndio amepewa hilo jukumu.

Nilifurahi kwa yeye kufanya hivyo. Walifanya vizuri sana.

Sasa Mh. Jaji alivyokuja na kunieleza nilimjulisha kuwa kwenye kesi kubwa kama hii ambayo ni kosa kubwa kuliko yote kwa mujibu wa ibara ya 28.

Kwenye kosa linaloshitakiwa kwa kusema maneno.

Kosa la aina hii nitajitetea Mwenyewe.

Kwasababu inabidi tuambiwe na nchi hii ukisema maneno yasiyowapendeza watu fulani fulani unaweza kuhukumiwa kifo.

Mimi niliyesema hayo maneno nitajitetea na niwasikilize hao wanaosema nimefanya uhaini kuwa nimetenda makosa hayo.

Naomba pia mfahamu kabla mahakama hii haijaniteulia mawakili toka tukiwa kisutu sijawahi kuwa na upungufu wa mawakili zaidi ya 50 na baadhi yao wapo hapa leo.

Niliwaambia ambayo nimesema haya kwenye kesi kama hii sitataka mtu anizungumzie nilisema hivyo toka Kisutu na tulielewana.

Nafahamu uzito wa kesi kama hii Waheshimiwa Majaji, anayeshtakiwa ana haki ya kuwakilishwa na mawakili hata kama hana uwezo mahakama itamtafutia Wakili wa kumsaidia.

Mimi uwezo ninao na suala la kwamba sina uwezo hilo halipo. Mimi uwezo ninao.

Pili watu wanaostahili kuwekewa mawakili ni wale ambao wanakabiliwa na makosa makubwa na hawawezi kujitetea wenyewe.

Mimi nina uwezo wa kujitetea mwenyewe. Mimi ni Wakili wa Mahakama hii kwa miaka 23 hadi leo kama Wakili.

Nimefanya kazi ya uanasheria huu ni mwaka wangu wa 31, There is no question whatsoever to defend my self.

Najitetea mwenyewe kwasababu this is ultimate test, huu ndio mtihani mkubwa kwa mfumo wetu wa kisheria.

On this one, kwa heshima zote I will take full responsibility for myself.

Nitaweza to the best of my ability.

This is about my life. I will defend myself to the fullest.

Naomba niseme jambo kuhusu hili jopo la Mawakili toka Kisutu naomba katika kesi hii waendelee kuwepo wanisaidie kwenye research maana gerezani hakuna mtandao hakuna library kule.

Waendelee kuwepo ili wanisaidie nijiteteee kwa ukamilifu.

Na kama hilo litawapendeza nitafurahi kama watatambulishwa na pia hata huyu Wakili Neema Saruni atakubali na yeye awe sehemu ya jopo hilo la Mawakili wataonisaidia kufanya research.

Thanks Thanks Quote Reply
Report
  • Thanks
  • Nzuri
Reactions:You, Atropine, LiFe 2-point-0 and 11 others
[IMG alt="ndammu"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/429/429694.jpg?1684050384[/IMG]

ndammu

JF-Expert Member​

In shaa Allah kwa uwezo wake Muumba utashinda na kila anaekunyanyasa kisa utofauti wa kisiasa Mungu ampige laana kuanzia Kiongozi wa nchi,policcm,mawakili wa serikali na majaji na wananchi wote wa ccm wanaokusingia kisa utofauti wa mawazo.

Thanks Quote Reply
Report
  • Thanks
Reactions:Atropine, Evelyn Salt, Gurugurumee and 3 others
[IMG alt="Msingida"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/32/32765.jpg?1655734611[/IMG]

Msingida

JF-Expert Member​

Dadeki!

Thanks Quote Reply
Report
  • Thanks
Reactions:Kipunguny and min -me
[IMG alt="To yeye"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/367/367662.jpg?1756888683[/IMG]

To yeye

JF-Expert Member​

Mwenyezi Mungu akusaidie Baba 🙏

Thanks Quote Reply
Report
  • Thanks
Reactions:Smart911, Evelyn Salt, Gurugurumee and 2 others
[IMG alt="naa"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/140/140810.jpg?1752591247[/IMG]

naa

JF-Expert Member​

Nilidhani leo wanaweza kumuachia lakini leo nimeona wameamua haswaaa kumnyonga 😭

Thanks Quote Reply
Report
  • Thanks
Reactions:zitto junior
[IMG alt="Izy_Name"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/590/590419.jpg?1731567572[/IMG]

Izy_Name

JF-Expert Member​

Ni noma

Thanks Quote Reply
Report
[IMG alt="Madingi ya Mbinguni"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/474/474726.jpg?1672443067[/IMG]

Madingi ya Mbinguni

JF-Expert Member​

Lisu mwamba sana mwamba kweli kweli mwamba pekee.

Thanks Quote Reply
Report
  • Thanks
Reactions:zitto junior and Kipunguny
[IMG alt="Madingi ya Mbinguni"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/474/474726.jpg?1672443067[/IMG]

Madingi ya Mbinguni

JF-Expert Member​

Wanalijaribu taifa waone watanzania watafanya nini?

Thanks Quote Reply
Report
  • Thanks
Reactions:Kipunguny
[IMG alt="zitto junior"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/176/176149.jpg?1734056858[/IMG]

zitto junior

JF-Expert Member​

View attachment 3467888

On this one, kwa heshima zote I will take full responsibility for myself.

Nitaweza to the best of my ability.

This is about my life. I will defend myself to the fullest.
Click to expand...
 

Attachments

  • 1757332455347.gif
    1757332455347.gif
    42 bytes · Views: 12
  • 1757332455324.gif
    1757332455324.gif
    42 bytes · Views: 13
  • 1757332455368.gif
    1757332455368.gif
    42 bytes · Views: 14
KESI YA UHAINI DHIDI YA TUNDU LISSU KATIKA MAHAKAMA KUU, 8 SEPTEMBA 2025

Majaji pia wameingia Mahakamani. Kesi hii itasikilizwa na majaji watatu wa Mahakama.

Anasimama kalani anasoma: Criminal case No. 19605/2025 Jamhuri dhidi ya Tundu Lissu.

Anasimama Nassoro Katuga wakili wa serikali, anajitwmbulisha na kusema: tupo pamoja na
Job Mrema, Thawabu Issa, Mossie Kahima, Harrison Lukosi, Cathbert Mbiringi na Winiwa Kasala. Mshitakiwa yupo naomba upande wa utetezi waweze kujitambulisha.

Anasimama wakili wa kike (watu wanashangaa kwani hawamjui)! Anajitambulisha na kusema: naitwa Neema Saruni ni Wakili. Namuwakilisha mtuhumiwa aliyepo mbele ya mahakama hii tukufu. Na kwa uwakilishi huo kwa mujibu wa PROBONO na nilipata wasaaa wa kuonana na mteja wangu nikakutana naye. Ninaiomba mahakama impatie nafasi aweze kuelezea.

Jaji anaandika kidogo na kisha anasema, ngoja kwanza upande wa mashitaka waseme kesi hii imekuja kwa hatua gani.

Wakili wa Serekali, Katuga anasema kesi ilikuja kwa ajili ya Preliminary hearing na ya kuwa wao wako wako tayari.

Kabla ya kuendelea na shauri Katuga anasema upande wa Jamhuri wana na concern kadhaa kama watapewa nafasi kuelezea. Anasema kuwa wako tayari na plea taking na preliminary hearing.

Jaji anamwambia subiri kwanza. Anaandika kidogo.

Anasimama wakili Neema Saruni na anasema: Tumemsikia wakili wa serikali, Katuga; lakini lipo suala la uwakilishi wangu ikipendeza mteja apewe nafasi.

Jaji amesema; sema wewe kwanza. Neema anasema: niliwasiliana na mteja wangu, yeye akasema atajiwakilisha mwenyewe, hayuko tayari nimuwakilishe.

Mh. Lissu anasimama anasema: nawashukuru majaji kwa kunipatia mawakili. Pamoja na kwamba mimi sikumuomba na simfahamu wakili Neema Saruni, alikuja mwenyewe kuniona kwenye gereza la Ukonga. Alijitambulisha na kuniambia kuwa yeye ndio amepewa hilo jukumu. Nilifurahi kwa yeye kufanya hivyo. Walifanya vizuri sana.

Sasa Mheshimiwa Jaji, alivyokuja na kunieleza nilimjulisha kuwa kwenye kesi kubwa kama hii ambayo ni kosa kubwa kuliko yote kwa mujibu wa ibara ya 28; kwenye kosa ninaloshitakiwa kwa kusema maneno kosa la aina hii nitajitetea Mwenyewe. Kwa sababu inabidi tuambiwe na nchi hii ukisema maneno yasiyowapendeza watu fulani fulani unaweza kuhukumiwa kifo.
Kwa sababu hiyo nikasema kuwa nitajitetea mwenyewe.

Mimi niliyesema hayo maneno nitajitetea na niwasikilize hao wanaosema nimefanya uhaini kuwa nimetenda makosa hayo. Naomba pia mfahamu kabla mahakama hii haijaniteulia mawakili toka tukiwa Kisutu sijawahi kuwa na upungufu wa mawakili zaidi ya 50 na baadhi yao wapo hapa leo.

Niliwaambia ambayo nimesema haya kwenye kesi kama hii sitataka mtu anizungumzie nilisema hivyo toka Kisutu na tulielewana.
Nafahamu uzito wa kesi kama hii waheshimiwa majaji. Anayeshtakiwa ana haki ya kuwakilishwa na mawakili, hata kama hana uwezo mahakama itamtafutia wakili wa kumsaidia.

Mimi uwezo ninao na suala la kwamba sina uwezo hilo halipo. Mimi uwezo ninao. Pili watu wanaostahili kuwekewa mawakili ni wale ambao wanakabiliwa na makosa makubwa na hawawezi kujitetea wenyewe. Mimi nina uwezo wa kujitetea mwenyewe. Mimi ni wakili wa Mahakama hii kwa miaka 23 hadi leo kama wakili. Nimefanya kazi ya uanasheria, huu ni mwaka wangu wa 31, 'There is no question whatsoever to defend my self'!

Najitetea mwenyewe kwa sababu 'this is ultimate test', huu ndio mtihani mkubwa kwa mfumo wetu wa kisheria. On this one, kwa heshima zote I will take full responsibility for myself. Nitaweza to the best of my ability.. This is about my life. I will defend myself to the fullest.

Naomba niseme jambo kuhusu hili jopo la mawakili toka Kisutu. Naomba katika kesi hii waendelee kuwepo wanisaidie kwenye research maana gerezani hakuna mtandao, hakuna library kule. Waendelee kuwepo ili wanisaidie nijiteteee kwa ukamilifu.

Na kama hilo litawapendeza nitafurahi kama watatambulishwa na pia hata huyu wakili Neema Saruni atakubali na yeye awe sehemu ya jopo hilo la mawakili watakaonisaidia kufanya research.

Majaji wanaandika kidogo hapa.

Wakili wa serekali, Katuga anasimama na kusema: Tumefuatilia wenzetu, mshitakiwa pamoja na wakili wake. Kwa mujibu wa kifungu cha 329 cha sheria ya mwenendo wa jinai kinatoa haki kwa mshitakiwa kuwa na uwakilishi kwenye kesi inayomkabili. Ingawa haki hii sio ya lazima, busara ya mahakama ilimpa wakili kwa ridhaa yake anaiambia mahakama hii kujitetea mwenyewe. Kwenye hiyo hoja ya kujitetea mwenyewe kwa kuwa amesema ni mbobezi wa sheria hatuna pingamizi kwenye hilo.

Lakini upande wa jamhuri unasita kukubaliana kwenye hoja ya kuwa ana mawakili ambao watamsaidia kufanya research na watambulishwe. Hatupingi wao kumfanyia research lakini tunapinga wao kuingia kwenye rekodi.Anaendelea; pale kunapokuwa na kesi ya pande mbili. Lazima wakili apate nafasi ya kuwa na mtu anayemuwakilisha, hawa wasitambulishwe kabisa.

Mh. Lissu ameulizwa unasemaje; anasema mimi sina shida hata tusipowatambulisha. Tuendelee kwenye mambo ya msingi. Nilidhani ni jambo dogo lisingekuwa na nongwa kama wenzetu wameona ni nongwa basi tuendelee na kazi ya leo, mimi sina shida.

Jaji anasema: Wakili Neema anakuwa discharged na mahakama ila kama ataendelea au kubaki na hiyo timu sisi hatuna shida mtamalizana naye. Pia kuhusu hiyo timu tunakuachia uendelee nayo kama ulivyoomba wakusaidie research.

Anasimama wakili wa serekali Katuga na kusema: Tulikuwa tumejiandaa na jukumu la leo. Lakini asubuhi ya leo tumepokea Notice of Motion kwa mujibu wa kifungu cha 294(1) na 295 cha CPA ikionekana imesajiliwa na Mshitakiwa mwenyewe na imepitishwa na Mkuu wa Gereza la Ukonga. Kama imeshafika hapa mahakamani tulikuwa na concern hiyo na ipo kwenye mfumo.

Kwenye hii Notice, waheshimiwa majaji lipo ombi la pili kuwa ambalo ameleta maombi mawili ameweka nia ya kuleta pingamizi kwenye hati ya mashitaka lakini pia ana question mamlaka ya mahakama hii kwa maana ya jurisdiction ambayo yeye anaona lipo hapa kinyume cha Sheria.

Ameeleza mengi, concern yetu sisi ni kwamba linapotokea suala la mamlaka ya mahakama (jurisduction) maamuzi mbalimbali yanasema tutaanza kwanza kutatua tatizo hilo kabla yakuendelea na jambo lingine lolote. Hii ni kwa sababu huwezi kuendelea na jambo lolote ambalo huna mamlaka nayo.

Hivyo mshitakiwa anasema lazima tujiridhishe kwa jambo hilo na yamesemwa pia kwenye kesi ya mahakama ya rufaa Thabiti Ramadhani Maziku, Kisuku Salumu Kaptura dhidi ya Amina Hamisi Tyeira and another. Rufaa Madai No. 98/2011 ukurasa wa 4 wa rufaa hiyo majaji wa rufani walisema suala la jurisdiction likiibuliwa lazima liamuliwe kwanza kabla ya kuendelea na mambo mengine. Katika mazingira haya hatuwezi kuendelea. Tuliamue jambo hili lililoletwa na mtuhumiwa. Amemaliza kusema Katuga.

Anakaribishwa Mhe. Tundu Lissu, anasema kwamba sina pingamizi na mapendekezo ya wakili wa serikali Mkuu. Kwa nini nimeleta hizo hoja mbili

1. 4/09/2025 nililetewa summons kuwa nitasomewa mashtaka leo na kuyajibu. Sasa kwenye shauri kama hili kifungu Cha 295(1) cha CPA kinasema pale ambapo taarifa information yaani charge sheet haionyeshi kosa na haiwezi kurekebishika kwa mujibu wa kifungu cha 294 basi mahakama ina mamlaka ya kufutiliwa mbali na hiyo ni immediately kabla ya mshitakiwa kujibu mara tu baada ya kusomewa hilo Shitaka.

2. Naelewa concern kwamba kuna suala la mamlaka ya mahakama hii kusikiliza. Suala la jurisdiction linapaswa kuamuliwa mapema. Ninachoweza kusema mimi nilikuwa nimejiandaa kwa hoja zote mbili. Kwamba kuna kesi hapa? Au mahakama hii ina mamlaka? Mimi niko tayari kwa lolote kati ya hayo. Mahakama iamue tuanze na lipi kati ya hayo mawili.

Mtanielekeza. Haya makosa ya uhaini yanakuja mara moja moja katika maisha ya binadamu.

Kwa mara ya kwanza 1983 ndio kesi ya kwanza ya uhani. Kesi ya R vs Khatibu Gandi na kabla ya hapo ilikuwepo 1970 kesi ya kwanza ya uhaini. Hii yangu ni kesi ya tatu ya Uhaini ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kesi kama hizi zinaweka misingi ya Kisheria katika sheria. Kwa sababu hiyo Mahakama hii kama itaridhia kujibu swali la hivi HATI YA MASHITAKA ya makosa ya uhaini inatakiwa kuwaje? Itakuwa ni Precedent nzuri na kubwa sana.

It will be unfortunately kama mahakama haitajipa fursa ya kuangalia jambo hili kuhusu makosa ya uhaini na ombi langu ni hilo. Ishu ya Jurisdiction na inshu ya hati ya mashitaka kama iko kihalali.

Tufanye hiyo kazi ili tuweke kumbukumbu sawa na rekodi hiyo itakumbukwa na dunia nzima kwamba mahakama kuu iliamua nini kuhusu mambo haya makubwa mawili hata siku ambapo mimi na nyinyi hatutakuwepo mambo haya yatakumbukwa na vizazi vyote. Ahsanteni.

Majaji wanaandika na kuteta kwa pamoja.

Anainuka wakili wa serekali Katuga, anasema anaomba rejoinder, amepewa nafasi anasema alichomuelewa mshitakiwa ni kuwa anakubaliana na maelezo yetu. Wanachoamini mashitaka yanapingwa kwenye mahakama yenye mamlaka. Kwa hiyo anasisitiza liamuliwe suala la jurisdiction halafu ndio tuanze kujadili suala la uhalali wa mashitaka. Amemaliza Katuga.

Jaji Dunstan Ndunguru anasema suala la jurisdiction ni suala la kisheria. Kwa hiyo tuanze na suala la jurisdiction halafu baadaye ndio tuendelee na suala la uhalali wa hati ya mashitaka.

NB: Taarifa hii kwa hisani ya 'mtandao'!
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Mzizima, 8 Septemba 2025; Saa 7:20 adhuhuri
 
Back
Top Bottom