Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

Tundu Antipas Lissu special thread (CHADEMA CHAIRMAN)

1755509511124.jpg
 
MH. HAKIMU: Mshitakiwa Mashahidi wako ni kina Nani?

MH. LISSU: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Makamu wake na waziri mkuu Majaliwa (List ikaendelea). na ameiomba mahakama iwaandikie barua ya wito chap😅🙌🏼

Na hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 39 cha Kanuni ya Adhabu sura na. 16.

Nyie huyu mzee, atawatoa watu Bandama😅🙌🏼
1755563300996.jpg
 
Labda kama kuna kitu umeshtukia tizama nchi ilivyo na utulivu
Ni jambo la kushukuru kwamba maandalizi ya uchaguzi mkuu yanekwenda vizuri sana kwa amani, na August 28 kampeni zinaanza kuelekea uchaguzi mkuu wenyewe Oct 29,2025🐒
 
JE, LISSU ANAPASUA JIPU WAKATI WA KULA?

Tundu Lissu anaambiwa na Hakimu awataje mashahidi wake. Lissu anawataja Rais Samia Suluhu Makamu wa Rais Philipo Mpango na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa! Lakini baada ya kusikia majina Hakimu anakataa kuyaandika na pia hatoi sababu ya kukataa kuyaandika majina na hatoi kifungu cha sheria kinachomuongoza asiandike majina ya mashahidi wa mtuhumiwa.

Hapa kuna maswali ya kujiuliza! Kama Hakimu alijua kuwa hataandika majina ya mashahidi, ni kwa nini alimtaka mtuhumiwa ataje majina ya mashahidi wake? Ni kwa nini Hakimu alikataa kuandika majina ya mashahidi hao? Je, katika kesi ya uhaini kuna watu hawana sifa ya kuwa mashahidi? Je, ni watu gani hao na ni kifungu gani cha sheria au cha katiba ya nchi ambacho kinawazuia baadhi ya watu kutoa ushahidi wa kesi inayowahusu na kuwa na madhara kwao?

Kama Rais, Makamu wa Rais au Waziri Mkuu atavamiwa na kuumizwa na ikatakiwa afike au awepo mahakamani kuthibitisha juu ya kuumia kwake hatakwenda? Na kama wakati tukio hilo linatendeka alikuwepo yeye na waliomuumiza na ikatakiwa awatambue mahakamani, hatafika kwenda kuwatambua? Je ni kwa nini sasa watu hao wasiandikwe kama mashahidi katika kesi hii ambayo kimsingi mmoja wao alilengwa kwa 'uhaini wa Tundu Lissu'?

Je, Tundu Lissu anataka kupasua jipu lililooza wakati ameketi mezani na wenzie kula chakula na je, watakubali kuona usaha wenye harufu?
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Itunge, Dar es Salaam; 19 Agosti 2025; saa 5:33 asubuhi
FB_IMG_1755681627115.jpg
 
Saa chache baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kupiga marufuku urushaji wa moja kwa moja wa kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Tundu Lissu, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Karagwe Dkt. Benson Bagonza ameeleza kuwa hatua hiyo ni sawa na “kuwapindua wananchi.”

Katika andiko lake alilolitoa Agosti 18, 2025, Bagonza amesema kesi hiyo inamhusu siyo tu Lissu, bali wananchi wa Tanzania kwa ujumla kwa kuwa inalenga usalama wa taifa na mamlaka ya wananchi.

“Mahakama ya Hakimu Mkazi ‘imetupindua’ katika kesi inayomkabili huyo ‘mpenda madaraka’ Tundu Lissu…Sisi wananchi wa Tanzania (Jamhuri) tumeandaa mashahidi wetu ili kuhakikisha tunamtia hatiani na kumnyonga. Tuna uhakika tutamtia hatiani kwa ushahidi tulio nao,” ameandika.

Askofu Bagonza amesisitiza kuwa Lissu hashtakiwi na Rais wala Jeshi la Polisi, bali na wananchi wenyewe. Aidha, ameonya kuwa kutolewa ushahidi kwa siri na kuendesha kesi kwa siri kunaweza kuchukuliwa kama njama za kumtorosha mtuhumiwa.

“Sisi wananchi wa Tanzania (Jamhuri), kwa uzalendo tulio nao, tuko tayari kutoa ushahidi hadharani ili kila mtu ajue na hao wanaomtuma Tundu Lissu wajue kuwa tuko imara. Tundu Lissu hashtakiwi na Rais wala na Jeshi la Polisi. Anashtakiwa na sisi wananchi wa Tanzania (Jamhuri). Tunataka watu wote hasa chama cha Tundu Lissu, wajue kuwa Jamhuri yetu (wananchi) hatuna mchezo. Tutailinda nchi yetu kwa wivu mkubwa. Kesi hii iwe fundisho kwa wote wanaodiriki kuchezea mamlaka ya wananchi. Ili hili fundisho liwe kamili, kesi hii tungetamani ifanyike uwanja wa taifa. Watu waone na kusikia, na akipatikana na hatia anyongwe hadharani, siyo gerezani”.

“Kwa kuwa hata uhai wa jambazi ni muhimu utolewe kwa utaratibu, tunataka uhai wa wahaini wote utolewe kwa utaratibu na kwa uwazi. Sisi wananchi (Jamhuri) hatujamtuma yeyote kuficha chochote. Sisi ndio walalamikaji. Wananchi (Jamhuri), wana haki ya kuhisi kuwa kuna njama za kutaka kumwachia Tundu Lissu pale wanapotaka kesi iendeshwe kwa kifichoficho na ushahidi utolewe kwa siri, ipo hatari ya kuja kutuambia alitoroka!”.
 
Back
Top Bottom