Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 17,822
- 24,481
POLENI WANA JF na smahani kama nitawakwaza wengine.
Nimekuwa nasoma post mbalimbali humu hasa zile za siasa hususani kuanzia mchakato,uchaguzi hadi matokoe yake.
Kifupi nimegundua member wengi wanaishabikia CHADEMA kama ambayo hata mimi naishabikia,naipenda na kuiamini.
Kutokana na kufuatilia post baadhi nikagundua wengi wanaochangia wana ukabila kwa kigezo kimoja. Kwamba baada ya mchakato mbovu uliomwingiza Kikwete madarakani na kwakua Kikwete alikuwepo madarakani na alikuwa kwenye nafasi ya kuweza kufanya mabadiliko lakini hakufanya kwa manufaa yake na chama chake,WATU wanamshambulia kama MKWERE*kabila* badala ya kama Kikwete au Rais aliyeshindwa kuleta matumaini aliyo ahidi 2005.
Wakati mimi naamini Kikwete ndiye anaeneza hofu ya UDINI,members wengi hapa wanaeneza UKABILA kwa hilo nililotaja hapo juu.
Members tujenge hoja za kutomtambua Kikwete kama rais bila kuhusisha kabila lake wala dini yake.
Hivi siku Wakwere wakisema mnalisema vibaya kabila lao kwa sababu ya Kikwete nao wakaanza Kulisema vibaya kabila la DR: SLAA au LIPUMBA,tutaweza kuvumilia na je ustawi wa nchi utakuwa wapi??
Sidhani kuwa kumtaja mtu kwa kabila lake ni kosa. Katika jamii zetu makabila mbalimbali yana tamaduni aa kutaniana na makabila mengine kiasi kuwa tamaduni hizo zimepanda hadi kufikia kiwango cha kuhusisha taifa zima. Utasikia mtu anajulikana kwa majina kama NSHOMILE, MNYALU, au watembeza biadhaa mitaani wote wamepachikwa jina la MACHINGA ambalo ni jina la utani la kabila fulani huko kusini.
Matumizi ya majina ya utani kwa viongozi wetu ama kutokana na haiba zao au makabila yao ni mambo ya siku nyingi sana nchini kwetu. Nyerere alijulikana kama Mchonga (kutokana na meno yake kuwa yamechongeka kwa tamaduni za wazanaki) na Sokoine alijulikana moja kwa moja kama MMASAI kutokana na kabila lake. Miaka ya karibuni tumesikia Mkapa akiitwa MACHINGA kutokana na kabila lake. Sioni ajabu kabisa kwa Kikwete kuitwa mkwere labda kama hataki kabila lake lijulikane, au mwenendo wake haukubaliwi na kabila zima la wakwere kiasi kuwa hawataki kuhusishwa naye tena.