Doctor Mama Amon
Platinum Member
- Mar 30, 2018
- 2,311
- 3,490
Wadau,
Kwa mujibu wa kifungu cha 20 cha Sheria ya Tume za Uchunguzi (Commissions of Inquiry Act), Sura ya 32, Toleo la 2023, Rais anapounda Tume ya Uchunguzi husika, Tume hiyo inapaswa kuanza kazi baada ya Uamuzi wa Rais kuchapishwa kwenye Gazeti la Serikali .
Taarifa ya gazetini inapaswa kutaja mambo kadhaa yakiwemo: (1) Jina rasmi la Tume, (2) muundo na Wajumbe wa Tume, (3) majukumu ya Tume, (4) Ratiba ya kazi, (5) Hadidu za rejea za Tume husika, na (6) Maelekezo maalum kwa Tume husika.
Mwaka 2006, Rais Jakaya Kikwete alifanya hivyo alipounda Tume ya Uchunguzi wa mazingira, sababu na matokeo ya mauaji ya Ephraim Chigumbi na Wenzake (Kiambatanisho A).
Tayari Rais Samia ameunda Tume ya Kuchunguza Mazingira, Sababu na Matokeo ya Uvunjifu wa (Haki na) Amani katika wiki ya uchaguzi Mkuu wa 2025.
Lakini bado sijapata nakala ya Tangazo la Serikali lenye kutaja mambo hayo hapo juu.
Tangazo la Ikulu kwa umma kupitia vyombo vya habari (KIambatanisho B) halitoshelezi matakwa ya kisheria.
Nataka Kufuatilia kwa karibu utendaji wa Tume hii.
Hivyo, nomba mtu yeyote mwenye nakala yake aniwekee hapa kwa ajili ya kazi maalum.
Naambatanisha:
- Kiambatanisho A: Tangazo la serikali kuhusu sakata la chigumbi na wenzake mwaka 2006
- Kiambatanisho B: Taarifa ya ikulu kwa vyombo vya habari kuhusu Tume ya Uchunguzi wa matukio ya Wiki ya Uchaguzi Mkuu 2025
KIAMBATANISHO A: TANGAZO LA SERIKALI KUHUSU SAKATA LA CHIGUMBI NA WENZAKE MWAKA 2006
KIAMBATANISHO B: TAARIFA YA IKULU KWA VYOMBO VYA HABARI