The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Upande wa CCM kusema kweli sioni ndani kabisa... hakuna mwanga kwa sababu hili kundi hili kama bado lipo uraiani sidhani kama kuna mtu CCM anaweza kufaa kuwa rais..
Nani huko anaweza kulikemea kundi hili kwa kuwataja majina!... kama tunavyofanya hapa JF?... NANI kama yupo basi huyo huyo, hii ni kwa manufaa ya taifa.
Zanzibar nako sioni zaidi ya kuendeleza utawala wa hilo baraza la wadandiaji Mapinduzi!
Nasema hivi, hakuna hata mmoja wao alishiriki ktk mapinduzi hayo! usiku huo wote walikuwa wamelala...Hakuna mwana mapinduzi wa Kweli isipokuwa Salim A. Salim na kundi lake ya UMMA party!
Heshima mbele!
Sasa kama CCM hakuna mtu, tutakuwa hatuna raisi? Nadhani kama unaona CCM hakuna mtu tutajie wa upinzani basi.
 
Dk Slaa,Mengi,Salim,Mbatia,Mrema, na muhimu sana ni yule atakayetuwakilisha wananchi vizuri huko bungeni wakati huu..ule atakayepigania haki yetu sisi..Yule atakayesema SASA KAMATA FISADI.

Atakayesema sasa Tuwaite watuhumiwa wote wa RICHMOND, EPA NK kwenye mahojiano na wananchi kwa kupitia wawakilishi wao huko Bungeni. Huyo ndiye atakayekuwa shujaa wetu.

Adawais still ni Alfa Lela ulela.
 
Sam,
Sikusema CCM hakuna mtu isipokuwa hakuna mwenye ubavu wa kusimama dhidi ya kundi hilo la mafisadi. Kifupi wameshinda kila kona hivyo hakuna deal hapa.

Laukama tukiondoa hii UHUJUMU UCHUMI wapo wengi sana wanaweza kuongoza nchi as a fact hata Kikwete mwenyewe anaweza kuwa kiongozi mzuri sana lakini kazidiwa nguvu.

Now, mimi natzama nje ya uwezo binafsi wa mtu kwa sababu anachoongoza ni system iliyokwisha jengwa.

Ndio maana hata Obama anatazamwa kwa kutazama uwezo wake kulingana na mazingira ya Marekani, hiyo system iliyokwisha jengwa.

Labda niwakilishe hivi.. rais anayefaa tanzania ni yule atakayeweza kuwahukumu hawa jamaa!.. iwe chama CCM, CUF, Chadema, TLP au NSSR maadam hawa watu wanakula meza koja sioni mtu mmoja kuongoza nchi bali nguvu ya umoja wa wananchi..wananchi wakishinda vita hii basi ni rahisi sana kumwona nani kiongozi bora kwa sababu mimi nazungumzia mtu wa KUTUKOMBOA!... hapa nachoona mimi tunapigania UHURU wa kweli na kiongozi unayejaribu kumsema wewe ni yule wa kutuletea maendeleo ambao wapo wengi sana ikiwa tu nchi ni shwari isokuwa na uhujumu uchumi.

Niliyasema haya toka zamani na JK failed me! Maendeleo hayawezi kuja ikiwa bado hatujajikomboa! - Maneno ya mwalimu alipokuwa akizungumzia kuhusu ARDHI...
 
2. JOSEPH SINDE ..... ameweza mara kadhaa (japo si mara zote ) kukemea na kuichukia rushwa. Miongoni mwa waadilifu mbele ya macho ya KCC, hutoa nafasi na wengine (wachache) nao wasikilizwe. yupo tayari kupokea mawazo/michango mizuri hata kwa wale ambao si wa itikadi moja naye!

3. JOSEPH BUTIKU miongoni mwa watu wanaochukia maovu (ufisadi), yupo tayari kukemea uovu/uozo kati ya watu wenye itikadi moja naye. Huyu naye hujali wengine kuliko yeye, close follower of JKN
 
Mkuu kwa mwenendo uliopo sasa, naona JK anafaa kuendelea na kipindi kingine. Nadhani kubadilisha mwingine itakuwa kumtwisha mzigo usiostahiki. Kwanza i hope this time hakuna atakayetaka kukimbilia ikulu

Hapo pana tabu...Muda nao unaweza kutumika kuendelea kuficha madhambi na maybe kuuana ama kupotezana ili kuendelea kuuficha ushahidi hence unjust decision TO THE PEOPLE, na by the time Salim anaingia ndani naye keshategwa kama Kikwete kwenye EPA VS CCM, ama kurogwa.
WAKATI WA UKOMBOZI NI SASA!
 
Sam,
Sikusema CCM hakuna mtu isipokuwa hakuna mwenye ubavu wa kusimama dhidi ya kundi hilo la mafisadi. Kifupi wameshinda kila kona hivyo hakuna deal hapa.

Laukama tukiondoa hii UHUJUMU UCHUMI wapo wengi sana wanaweza kuongoza nchi as a fact hata Kikwete mwenyewe anaweza kuwa kiongozi mzuri sana lakini kazidiwa nguvu.

Now, mimi natzama nje ya uwezo binafsi wa mtu kwa sababu anachoongoza ni system iliyokwisha jengwa.

Ndio maana hata Obama anatazamwa kwa kutazama uwezo wake kulingana na mazingira ya Marekani, hiyo system iliyokwisha jengwa.

Labda niwakilishe hivi.. rais anayefaa tanzania ni yule atakayeweza kuwahukumu hawa jamaa!.. iwe chama CCM, CUF, Chadema, TLP au NSSR maadam hawa watu wanakula meza koja sioni mtu mmoja kuongoza nchi bali nguvu ya umoja wa wananchi..wananchi wakishinda vita hii basi ni rahisi sana kumwona nani kiongozi bora kwa sababu mimi nazungumzia mtu wa KUTUKOMBOA!... hapa nachoona mimi tunapigania UHURU wa kweli na kiongozi unayejaribu kumsema wewe ni yule wa kutuletea maendeleo ambao wapo wengi sana ikiwa tu nchi ni shwari isokuwa na uhujumu uchumi...

Niliyasema haya toka zamani na JK failed me!
Maendeleo hayawezi kuja ikiwa bado hatujajikomboa! - Maneno ya mwalimu alipokuwa akizungumzia kuhusu ARDHI...
Mkandara,
Hapo ndipo huwa napingana na watu, matatizo ya ncho yetu ni ya kiuchumi siyo kisiasa. Tunahitaji mtu ambaye anaweza kutatua matatizo hayo. Kuwahukumu watu siyo solution ya matatizo unakuwa kama unaondoa unaondoa watu unaleta wengine wale.

Kwa mfano ukachukua mafisadi wote ukwaua kwa mabomu mbele za TV unataka kusema huo ndio utakuwa mwisho wa ufisadi? Lazima tuzuie kwanza. Katika CHADEMA ninaweza kukuambia ni Zitto pekee ambaye anaongea ufumbuzi wa matatizo, siku aliposimama bungeni na kutoa sababu kwa nini tunahitaji umoja wa EA nikaona tunahitaji mtu kama huyu tatizo lake akitoa comments kwenye mambo ya administration ananiacha hoi naamini akifika umri wa kugombea atakuwa amejifunza mengi.

Nakubaliana na wewe kuhusu SAS lakini hana nafasi kwenye siasa za sasa, unatakiwa uwe na mdomo mkubwa kama Obama.

Rev. hii topic inabidi usilale watu wakiamka itachafuka.
 
Mkandara,
Hapo ndipo huwa napingana na watu, matatizo ya ncho yetu ni ya kiuchumi siyo kisiasa. Tunahitaji mtu ambaye anaweza kutatua matatizo hayo. Kuwahukumu watu siyo solution ya matatizo unakuwa kama unaondoa unaondoa watu unaleta wengine wale. Kwa mfano ukachukua mafisadi wote ukwaua kwa mabomu mbele za TV unataka kusema huo ndio utakuwa mwisho wa ufisadi? Lazima tuzuie kwanza. Katika CHADEMA ninaweza kukuambia ni Zitto pekee ambaye anaongea ufumbuzi wa matatizo, siku aliposimama bungeni na kutoa sababu kwa nini tunahitaji umoja wa EA nikaona tunahitaji mtu kama huyu tatizo lake akitoa comments kwenye mambo ya administration ananiacha hoi naamini akifika umri wa kugombea atakuwa amejifunza mengi. Nakubaliana na wewe kuhusu SAS lakini hana nafasi kwenye siasa za sasa, unatakiwa uwe na mdomo mkubwa kama Obama.
Rev. hii topic inabidi usilale watu wakiamka itachafuka.

Nothing is worse than doing nothing...It is therefore true that something is better than nothing at all...However...This time around we want everything!
As in a whole package for justice.
 
List starts,

1. Salim Ahmed Salim,

next...

Huyo hata mimi namuafiki, lakini ameshakula chumvi nyingi. Ndiye aliyestahili kuchukua nchi 2005 lakini wa visiwani wenziye wakamharibia. Pia inasemekana Fisadi Mkapa alikuwa hataki kabisa kumuona SAS anakuwa Rais wa Tanzania, nadhani alikuwa anajua madudu yake kama tunavyoyafahamu sasa, SAS asingemuonea aibu.

Sasa hivi ndani ya CCM sioni mtu waliopo wote hawafai kabisa kupewa nchi. Upinzani Slaa anastahili kabisa kuwa Rais ila sijui kama hajala chumvi nyingi.
 
Mkuu kwa mwenendo uliopo sasa, naona JK anafaa kuendelea na kipindi kingine. Nadhani kubadilisha mwingine itakuwa kumtwisha mzigo usiostahiki. Kwanza i hope this time hakuna atakayetaka kukimbilia ikulu

BL, kwa maoni yangu itakuwa ni makosa makubwa sana kumrudisha huyu jamaa madarakani maana mpaka sasa kazi aliyoitaka imemshinda vibaya sana.

Kama kutakuwa na mabadiliko makubwa ya utendaji wake kati ya sasa na 2010 basi anaweza akastahili kurudi, lakini sioni uwezekano wa hilo hivyo inabidi astaafu ili akamsaidie rafiki yake Sinclair kuchukua rasilimali zetu.
 
Anne kilango!anafaa sana kuwa raisi wa nchi yetu,anaifahamu nchi kwa maana ya ya wananchi,yupo kwa ajili ya wananchi na si kwa ubinafsi.
 
Naomba kurudia ombi langu tena ili nieleweke.

Naomba majina, wasifu na historia ya kazi na milestone muhimu.

Mambo ya Ufisadi, EPA, Richmond na mengine sikuwa nimedhamiria kuyafanya kuwa sehemu ya thread hii, otherwise ningeanzisha thread mahsusi bila kutoa vigezo nilivyoomba.

Tusianze kuteka thread na kuleta U-Ballali na uchawi!
 
List goes

1. Salim
2. Warioba
3. Butiku
4. Slaa
5. Mengi
6. Kilango-Malecela

next please...

Give name, reason and short CV listing achievements and accomplishment.

It does not matter where the person comes from. Ndio maana nimeomba kutoka CCM na wale ambao si wa CCM!
 
JINA: Rostam Aziz
SABABU: Kama alivyoweza kutajirika kwa haraka, atawezesha Tanzania kupata maendeleo ya haraka. 🙂
 
Mkuu kwa mwenendo uliopo sasa, naona JK anafaa kuendelea na kipindi kingine. Nadhani kubadilisha mwingine itakuwa kumtwisha mzigo usiostahiki. Kwanza i hope this time hakuna atakayetaka kukimbilia ikulu

Lo, yaani tupoteze miaka 10 badala ya kupoteza miaka 5? Sioni sababu hapo! The soon he can be replaced the better! Life is too short! and Time is Precious!
 
Mkuu Rev. Kishoka,swali lako ni gumu lakini ni muhimu mno.Kwa Mtazamo wangu katika Orodha ya wana-ccm bado Salim Ahmed Salim ndiye mtu pekee anayefaa kuwa Kiongozi wa Nchi kwa sasa.Tatizo kubwa ninaloliona kwa Ndugu huyu ni Umri,kwani sasa hivi amekwishakuwa mtu mzima mid 60's.

Salim ni Muadilifu hana Makuu na si Fisadi.Kiongozi huyu ni mzoefu karibu kwenye nyadhifa zote za juu serikalini,kwenye kumbukumbu inaonyesha kuwa ameanza kuitumikia serikali toka akiwa mdogo wa umri wa miaka ya 20.Salim ni Miongoni mwa viongozi waanzilishi kwenye Chama cha Mapinduzi,kwa maana hiyo anajua vyema Muundo na madhumuni ya Chama cha Mapinduzi ambayo nia yake ya dhati ilikuwa ni kumkomboa Mkulima na Mfanyakazi,na sio kujali Wafanyabiashara na Wajasirimali kama ilivyo sasa.

Ndugu Rev Kishoka,Ni imani yangu kuwa kuna Viongozi wazuri katika Kambi ya Upinzani,Lakini bado Upinzani haujajiimarisha vyema vijijini ambako ndio kuna Wapiga kura wengi.Vyama vingi vya Upinzani vina nguvu kubwa Mijini ambako ndio kuna wasomi,wanaoangalia mambo kwa kina,lakini nguvu ya vyama hivi bado sio kubwa Vijijini.Inabidi vyama hivyo vitafute mbinu ya kujitawanya Vijijini,labda kwa kuanzisha Matangazo ya Redio ambayo yataeleza mipango yake ya maendeleo na kueleza Ufisadi na Ahadi za uongo za CCM.Kutawanya vipeperushi vinavyoonyesha mabaya ya CCM na kutoa njia mbadala, na mambo haya yafanywe labda kila baada ya miezi miwili/mitatu na sio kungoja wakati wa Uchaguzi.Suala hili linataka funds,na vyama vingi vya upinzania havina miradi mikubwa,vinaendeshwa kwa pesa ndogo ya Ruzuku.

Haitokuwa Rahisi kwa kiongozi yeyote Tanzania kuonekana Mzuri ikiwa tu atatoka CCM,kwani system nzima imeharibika...Ili kiongozi aonekane mzuri inabidi system yote ipanguliwe.Kwa mtazamo wa mtu mmoja mmoja Salim ndio pekee katika CCM anayeweza ku-deliver.Kuna Viongozi wengi Vijana ndani ya CCM ambao watakuja kuwa wazuri,ikiwa tu watazingatia miiko ya kazi zao,na kuwa hapo kwa lengo la kuwatumikia watanzania na sio kujilimbikizia mali.

Rais wetu wa sasa, Mh Mrisho Jakaya Kikwete,ameshindwa kabisa kazi!,Toka aingie madarakani amekuwa mtu wa kutoa ahadi zisizotekelezeka,na sasa serikali yake imeandamwa na kashfa ambazo hatujapata kuziona toka tupate Uhuru (1961).Muungwana huyu ataomba mwenyewe kutoendelea na Term yake ya pili,kwani humo ndani ya CCM kuna upinzani mkubwa dhidi yake,baada ya kugeukana na waliomuweka yeye kwenye Madaraka..
 
Njellu kasaka,sina wasifu wake zaidi ya kumsikia zamani akiitetea Tanganyika
 
Butiku is a looser..hiyo MNF ..anautafuna, salim is always good but umri umeenda...as well as warioba.....

tunaingia kwenye kizazi kipya cha siasa....wanasiasa vijana kama kina lau masha et al wanasubiri 2015...

mwaka 2010 tunawaachia size ya jk kama kina mwandosya na sumaye....hawa wangeweza kuwa bora kuliko jk
 
Dr. Slaa,
sihitaji kusema mengi lakini mtu aliye weza kuthubutu kuwataja hadharani kwa majina watekaji nyara wa nchi yetu.

Mtu makini anaye chukua muda wake kusoma na kutafuta kweli juu ya kiini cha tatizo letu watz.

Angalia alivo leta maendeleo jimboni kwake.

Kikubwa zaidi, kwa Tanzania tuliyo nayo tunahitaji mtu ambaye anaweza kurejesha nchi yetu toka mikononi mwa kikundi cha watu wachache (aka fisadi), Anaye weza kusema NO palipo na NO. Na si mwingine huyo bali ni a man of God Dr Slaa.
 
Back
Top Bottom