CCM ninayoifahamu kidogo haina "mpango" wa KUMWONDOA Kikwete hiyo 2010 labda kwa mapenzi ya Mungu. Na ninavyowafahamu WaTz na CCM yao mmh!
Kimsingi wewe ndio umedhihirisha kwamba umekomaa kisiasa.Maana mtu aliyekomaa kisiasa anatakuja na maoni yenye kuelezea ukweli wa mambo kama ulivosema wewe.Itakuwa ni kupoteza muda hapa kuanza kufikiria suala la mgombea wa CCM mwaka 2010. Ni wazi kwamba mgombea wa CCM mwaka 2010 nafasi ya urais wa muungano ni Mh.
Rais Jakaya Kikwete. Hilo wala halina ubishi. Labda kwa wale wenye hulka ya kuweka ligi isiyokuwa na maana ndio wanaweza kupingana na ukweli huo. Hata wanaCCM makini wanaoota ndoto za urais hawaoti ndoto za urais kwa 2010, bali wamejielekeza mwaka 2015 pindi kipindi chake kitakapokuwa kimeisha.
Sababu kubwa ni kwamba huo ndio utamaduni wa chama.Sasa kama kuna mtu anamkataa JK na CCM kwa ujumla kwa sababu zozote zile, basi hilo ni suala lake binafsi na ni haki yake kufanya hivyo.
Sasa kwa mtu yeyote asiyeridhika na uongozi wa JK/CCM njia pekee na inayoweza kutekelezeka ni kumkataa kwenye kura tu,sio hapa JF wala kwingineko.itakuwa ni kusumbua vichwa vya watu hapa kuanzisha mjadala ambao hauna tija na ni dhahiri kwamba uko kinyume na hali halisi ya mambo.
Kama tunazungumzia urais wa Tanzania visiwani,hilo sawa. Linajadilika kwa sababu Rais wa sasa Mh.Aman Karume, anazuiwa na katiba ya Zanzibar kuendelea na kipindi cha tatu cha utawala. Hivyo ni lazima CCM impitishe mwanachama mwingine kuwania nafasi hiyo.
Sasa, kwa upande wa Zanzibar mimi binafsi, kwa mtizamo wangu na kwa vigezo vyangu,namauona Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mh.Dr.Mohamed Shein kama anafaa.Sababu ziko nyingi,lakini kwa kutaja baadhi tu:
1.Ni mzanzibar
2.Ana akili timamu
3.Ni msomi mzuri
4.Ni mtulivu
5.Ana uzoefu wa uongozi.Nina amini kwa kufikia ngazi ya umakamu wa Rais wa jamhuri ya muungano kumempa nafasi ya kupata uzoefu wa uongozi.
Lakini zaidi ni kwamba ofisi yake ya makamu wa rais wa muungano ndio kiungo cha Muungano wa bara na visiwani.
Kwa hiyo, kwa kuwepo kwake katika ofisi hiyo kumempa nafasi ya kuijua vema Tanzania bara na hivyo kuwa katika nafasi nzuri ya kuyashughulikia masuala ya muungano kwa umakini na ufanisi wa hali ya juu.