The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Dua,
Mbona mkuu tunarudi nyuma tena.. ya Salim tulikwisha yajadili sana na namfahamu alikotoka...Salim hakupendwa na wengi tu kwa sababu moja kubwa.

Aliipenda sana nchi yake utadhani ni mali ya baba yake!..
Hiii ilikuwa ni kosa kubwa kwa kiongozi ambaye yupo radhi kufa maskini, kama tulivyomwona Abraham Babu hakuna hata siku ya kumkumbuka isipokuwa kina Karume!.

Mkuu Salim anakubalika kwa wananchi both visiwani na Bara isipokuwa tu kinachowatisha wengi ni UJAMAA wake...Akiwa PM huweizi kabisa kunipa maovu yake mkuu hata Zitto kisha wahi kuja hapa na kuweka record sawa.

As a fact hata mimi binafsi namuogopa kwa hilo hasa ktk dunia hii ya leo. Lakini kutokana na yote haya yaliyokwisha tokea nipo radhi kuanza mwanzo na najua hna muda mrefu wa kutawala - umri tena, kwa muda huu anaweza kusafisha njia kwa viongozi wengine watakao fuatia..
 
Baada ya kupitia majina na mapendekezo ya kila mtu, inaelekea wazi na ni dhahiri kuwa Tanzania hatujui ni nani wa kumuamini awe nahodha wetu kutuokoa kuzama.

Suala si kutafuta mtakatifu, bali ni mtu ambaye dhamira yake itakuwa ni kuleta suluhisho la matatizo ya Tanzania ambayo yanalea unyonge.

Binafsi sijali chama, nauliza je huyu mgombea, ana sifa gani nimuamini na kumpa kura yangu? je atanitumikia mimi Mtanzania na kunilindia maslahi yangu?

Uongozi si lelemama, unahitaji moyo, utashi na uhuru wa kufanya mambo bila woga au kusukumwa na kikundi fulani au chama.

Kwa mtaji huo, wa majibu yenu wote, inaelekea ni heri Zimwi likujualo na hilo ndilo linaloonyesha wazi ni vipi sisi kama Taifa tunaamua kumpa usukani mtu awe nahodha wetu.
 
Baadhi ya sifa za kiongozi tunayemhitaji Tanzania katika muda huu ni kama zifuatazo:

(a) Mwenye akili ya kuchambua na kuona mambo kwa mbali.
(b) Mwadilifu, na mwenye uzalendo.
(c) Mchapa kazi, na anayesimamia sheria za nchi bila upendeleo.
(d) Anayeheshimiwa, na kusikilizwa na viongozi wenzake ndani na nje ya nchi
(e) Zaidi ya kuheshimiwa, lazima pia awe anaogopwa kiutendaji na wafuasi wake.

Swala la umri linaweza kuwa zuri lakini halina nguvu sana; kuna nchi zilizofanikiwa kutokana na ungozi wa vijana na vile vile kuna zile zilizofanikuwa kwa kuwa na viongozi wazee.

Katika kuangalia hawa waliokwisha jitokeza na kiuongozi hadi wakati huu, mimi ninabaki na watu wachache sana wa kusimamisha.

(a) Namba moja mimi ninampa Dr. Slaa. Mwaka uliopita umedhihirisha kuwa bwana huyu anazo sifa zote niliozotaja hapo juu ingawa sina uhakika kama kweli yeye mwenyewe ni mwadilifu. Mabalozi wa nchi za nje wamekuwa wanachukulia kauli zake kwa uzito sana ndiyo na maana waliweka shinikizo kwa serikali kufuatilia swala la ufisadi lililotamkwa na Dr. Slaa. Watu kadhaa akiwemo mheshimiwa Mkono ambaye ni mwanasheria wa kuogopwa walitishia kumshitaki mahakamani lakini kama sote tunvyofahamu hadi leo hakuna walilofanya. Nina wasiwasi kuwa sasa hivi wanamwogopa sana mheshimiwa huyu na huwa wanapata kihoro wanapositikia kuwa anataka kuongelea jambo fulani kuhusu mafisadi.

(b) Namba mbili ninawapa watu wawili kwa mpigo: Dr Salim Ahmed Salim na Judge Joseph Waryoba. Wazee hawa wanazo sifa zote nilizotaja hapo juu, na nadhani kuwa ndiyo maana mafisadi ndani ya CCM wanawachukia jamaa hawa kwa nguvu zote.

(c) Namba tatu pia ninawapa watu wawili kwa mpigo: Dr Mwakyembe na Zitto ingawa sina uhakika sawasawa kuhusu uadilifu wao wakipata nafasi. Nadhani kuwa kiutendaji sote tunafahamu jinsi Mwakyembe na Zitto walivyoweza kuchambua na kuangalia mambo ya masalahi ya taifa kwa mbali bila kuogopa.

(d) Namba nne ninaelekea kumpa Waziri Mkuu Pinda ingawa mara kadhaa amekuwa anaonyesha uoga wa hapa na pale kuhusu kukabiliana na baadhi ya mambo hasa yahusuyo mafisadi; ninadhani kuwa yote hiyo ni kutokana na ugeni wa madaraka yake. Bwana huyu ni wa kuaminika sana kiongozi hasa ukizingatia taaluma yake kama mpelelezi. Hasiti kumtosa hata ndugu yake wa damu endapo atahusishwa na kosa lolote lile la kuvunja sheria.
 
Mchungaji,
Binafsi, naona kwa upande wa CCM, Kikwete atagombea tena, ila, mgombea mwenza wake asiwe Shein. Ingefaa awe Dk. Mwinyi. Sababu ni hii; Dk Shein si kiongozi mbaya, ila hajaonyesha kuwa ni mtu mwenye kutake charge tangu wakati wa Mkapa. Haimaanishi kuwa Dk. Mwinyi ndio ameonyesha kutake charge. Hii itampa Muungwana fursa ya kumwandaa Dk. Mwinyi kumrithi mwaka 2015 ambapo Dk. Mwinyi atakuwa ni mgombea kutoka visiwani, atakuwa na uzoefu wa kuwa wizara ya afya, ulinzi na umakamu wa rais. Dk. Mwinyi ni kiongozi kijana ambaye naamini hajawa polluted na makada wa CCM wenye mitazamo ya kizamani na ubabe kama KNM.

Kwa upande wa upinzani, nasikitika kusema bado sijaona japo kuna potentials. Unajua, watu wametajwa na wanaJF wengine kutokana na kuchangia kwao kwenye Bunge au kuchangia kuuza magazeti (news makers). Lakini, wengi tunasahau urais si lelemama. As much as I would love to see upinzani wakishinda, sijaona chama chochote chenye sera tofauti na CCM. I mean, hakuna tofauti kubwa (kiitikadi) kati ya CCM na upinzani kama ilivyo Labor Party na Torries au Republicans vs. Democrats. Tofauti iliyopo ni chama kimoja kimeshika hatamu tangu uhuru, viongozi wake (baadhi ya) ni wezi, wagumu kubadilika na wapinzani wanawakosoa. Sijui kama Freeman (au Zitto au Mrema au yeyote yule) ataleta sera mpya na hatuna ushahidi kuwa upinzani hautaibia taifa. Hata wanaCCM kama Mwakyembe, mama Killango-Malecela na wengineo, ni viongozi wazuri, lakini sidhani kuwa kazi ya urais ni yao. Mahali walipo (Bungeni) ni mahali pema kabisa ambapo wao ndio watahakikisha kuwa checks and balances zinafanyika badala ya kuwa na wabunge ambao ni yes men.

Nasikitika kusema kuwa nyakati za Warioba na Salim zimepita na hakuna wa kumlaumu bila sisi wenyewe. Nasema sisi wenyewe kwani wawakilishi wetu wangepiga kelele, hawa mabwana wangeweza kuwa katika chaguzi zilizopita. Umri umewafika wa wao kubakia kama washauri na sio viongozi.

Upinzani ambao unaweza kutokea na kufanya kuwa political process kuwa effective, bado una nafasi ya kutokea ikiwa wahusika watatokea CCM kama mwalimu alivyosema wakati wa uhai wake. Ikitokea mtu kama Mwandosya (wasifu wa uzoefu wa uongozi katika sekta muhimu kama madini, mazingira, miundombinu, sayansi na usomi) akijitenga na kutafuta viongozi wengine ambao watatoa Chama kilicho tofauti kabisa na CCM (mfano: CCM wanasema Ujamaa na kujitegemea wakati chama kipya kinasema Ujasirimali{ubepari}na maendeleo) na wazingatie mambo makuu kama elimu za aina zote, mipango, maendeleo, mazingira, nishati nk. basi hapo ndipo nitapata msisimko zaidi wa upinzani. Kwa sasa, tofauti iliyopo kati ya CCM na upinzani ni namna ya kuendesha serikali na kwa hilo CCM inawapiku wapinzani.
 
Unfortunately sijui uzuri wa Dr. Mwinyi kama anaweza kumudu kazi ya urais pamoja na kuwa baba yake alikuwa rais.

Ninajua kuwa aliwahi kufukuza madaktari pale Muhimbili halafu wananchi wetu wakapata tabu sana wakati madakitari wale waliofukuzwa walikaribishwa kwa mikono miwili huko Botswana na Namibia ingawa walikuwa hawajamaliza hata zile internships zao. Kitendo kile kilionyesha jinsi gani aanvyoweza kutumia madaraka yake.

Inawezekana kweli anamudu majukumu hayo au ana watu wa kumpigia debe ili ajaribu kuyatafuta.
 
Unfortunately sijui uzuri wa Dr. Mwinyi kama anaweza kumudu kazi ya urais pamoja na kuwa baba yake alikuwa rais. Ninajua kuwa aliwahi kufukuza madaktari pale Muhimbili halafu wananchi wetu wakapata tabu sana wakati madakitari wale waliofukuzwa walikaribishwa kwa mikono miwili huko Botswana na Namibia ingawa walikuwa hawajamaliza hata zile internships zao. Kitendo kile kilionyesha jinsi gani aanvyoweza kutumia madaraka yake.

Inawezekana kweli anamudu majukumu hayo au ana watu wa kumpigia debe ili ajaribu kuyatafuta.


Huyo mtoto wa Mwinyi anapigiwa debe awe Rais wa Zanzibar...Naona sasa nchi yetu imekuwa ya kutawaliwa na watu wa kutoka familia moja! Yaani imeshakuwa kama taaluma, vile baba akiwa daktari basi anataka na mtoto wake naye asomee udaktari na aje awe daktari. Ndivyo wanavyotaka kufanya na kwenye nafasi nyeti kama urais wa nchi!

Vizazi vijavyo vitawalilia !
 
Ndugu wana JF na hasa mliopo huko Tanzania, nimesikia majibu yanayotolewa na serikali hususani fedha za EPA. Ni muda muafaka ifikapo 2010 angalau kuongeza idadi ya wabunge wa upinzani bungeni, pia spika atoke kambi ya upinzani. Bila kufanya hivyo kila siku hatutakua na majibu ya kuridhisha hata kidogo. Bunge angalau liwe 60% kutoka kambi ya upinzani, pia spika

Naomba kutoa hoja. Bila kufanya hivi hatutasogea.
 
Nice dream!!! JF yenyewe bado ina akina Machambuzi na Mugongox2 kibao. Sasa huko mtaani sijui vipi. I hpoe it will happen in TZ but not that soon!
 
Mwaka 2010 ni mwaka wa kuongeza vijana bungeni wenye kuweza kukabiliana na mshike mshike wa siasa za kidunia za ushindani. Vijana hao wanaweza kupitia chama chochote makini Tanzania.

Katika ya changamoto inayokwamisha vijana kushinda chaguzi ni ukosefu wa rasilimali. Je, vijana wanaweza kukukabiliana vipi na changamoto zinazokabili? Je mikakati kama huu wa CHADEMA unaweza kusaidia?

Tujadili. Sasa ni Julai 2008, miaka miwili kabla ya kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2010. Kwa wale wanaowaza kugombea huu ndio wakati wa kuvaa jezi na kuanza kupiga jaramba.

Na kwa wale wanawake wenzangu, safari hii tusisubirie viti maalumu, hebu tujiandae tujitose majimboni. Kama wao wanaweza wananini hata sisi tushindwe tuna nini?

Huu ni mfano tu toka kwa CHADEMA "Nachukua fursa hii kukumbusha tena dhamira ya mfuko wetu. Mfuko wa Vijana na Ubunge ni mfuko unaounganisha wafanyakazi wote wa Tanzania, waliodhamiria kwa dhati kuunganisha uzalendo wao kwa manufaa ya taifa lao, kwa kuchangia raslimali na ustadi wao wa kitaaluma ili kufanikisha azma ya kuongeza Wabunge Vijana kuanzia mwaka 2010 kupitia chama mbadala - CHADEMA. Mfuko huu ni wa jumuia ya siri ya vijana wafanyakazi inayojulikana kama Y4C (Youth for Change) ambayo iko chini ya kurugenzi ya vijana wa CHADEMA. Dira ya mfuko huu ni kuwa na; Bunge lenye uwakilishi mzuri wa vijana, lenye ushindani, na lenye kusimamia kikamilifu utendaji na uadilifu wa serikali kwa manufaa ya umma. Mfuko utatunisha angalau Tsh. Bilioni moja ndani ya kipindi cha miaka 3, kwa kuanzia mwaka 2008 - hadi Septemba Mosi 2010. Wazalendo 4,000 kama wewe watafikiwa nchi nzima na mfuko huu ambapo kila mmoja atachangia walau laki moja kwa mwaka ama elfu kumi kwa mwezi. "


Nimeipata toka: http://www.chadema.net/mabaraza/bavicha/08/waraka1.php

http://www.chadema.net/mabaraza/bavicha/08/waraka1.php

http://www.chadema.net/mabaraza/bavicha/08/waraka1.php

http://www.chadema.net/mabaraza/bavicha/08/waraka1.php


Lakini CHONDE, vijana hao wawe makini kama wakina Zitto wasiwe kama wakina Peter Serukamba maana watatuabisha zaidi na kulitia hasara taifa.

Je, kuna upekee wa kuwa na wabunge vijana ambao unaweza kupatikana tofauti kuwa na wabunge lilijaa wazee?

Je, sasa hivi- tuna wabunge wangapi vijana kwa maana ya miaka kati ya 18 mpaka 35? Tunaweza kuwataja kwa majina?

Manake nasikia bungeni letu zaidi ya robo tatu ya wabunge ni kati ya miaka 50 na kuendelea. Yaani bunge la wastaafu!

Asha
 
Mwaka 2010 ni mwaka wa kuongeza vijana bungeni wenye kuweza kukabiliana na mshike mshike wa siasa za kidunia za ushindani. Vijana hao wanaweza kupitia chama chochote makini Tanzania.

Katika ya changamoto inayokwamisha vijana kushinda chaguzi ni ukosefu wa rasilimali. Je, vijana wanaweza kukukabiliana vipi na changamoto zinazokabili? Je mikakati kama huu wa CHADEMA unaweza kusaidia?

Tujadili. Sasa ni Julai 2008, miaka miwili kabla ya kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2010. Kwa wale wanaowaza kugombea huu ndio wakati wa kuvaa jezi na kuanza kupiga jaramba.

Na kwa wale wanawake wenzangu, safari hii tusisubirie viti maalumu, hebu tujiandae tujitose majimboni. Kama wao wanaweza wananini hata sisi tushindwe tuna nini?

Huu ni mfano tu toka kwa CHADEMA "Nachukua fursa hii kukumbusha tena dhamira ya mfuko wetu. Mfuko wa Vijana na Ubunge ni mfuko unaounganisha wafanyakazi wote wa Tanzania, waliodhamiria kwa dhati kuunganisha uzalendo wao kwa manufaa ya taifa lao, kwa kuchangia raslimali na ustadi wao wa kitaaluma ili kufanikisha azma ya kuongeza Wabunge Vijana kuanzia mwaka 2010 kupitia chama mbadala - CHADEMA. Mfuko huu ni wa jumuia ya siri ya vijana wafanyakazi inayojulikana kama Y4C (Youth for Change) ambayo iko chini ya kurugenzi ya vijana wa CHADEMA. Dira ya mfuko huu ni kuwa na; Bunge lenye uwakilishi mzuri wa vijana, lenye ushindani, na lenye kusimamia kikamilifu utendaji na uadilifu wa serikali kwa manufaa ya umma. Mfuko utatunisha angalau Tsh. Bilioni moja ndani ya kipindi cha miaka 3, kwa kuanzia mwaka 2008 - hadi Septemba Mosi 2010. Wazalendo 4,000 kama wewe watafikiwa nchi nzima na mfuko huu ambapo kila mmoja atachangia walau laki moja kwa mwaka ama elfu kumi kwa mwezi. "


Nimeipata toka: http://www.chadema.net/mabaraza/bavicha/08/waraka1.php

http://www.chadema.net/mabaraza/bavicha/08/waraka1.php

http://www.chadema.net/mabaraza/bavicha/08/waraka1.php

http://www.chadema.net/mabaraza/bavicha/08/waraka1.php


Lakini CHONDE, vijana hao wawe makini kama wakina Zitto wasiwe kama wakina Peter Serukamba maana watatuabisha zaidi na kulitia hasara taifa.

Je, kuna upekee wa kuwa na wabunge vijana ambao unaweza kupatikana tofauti kuwa na wabunge lilijaa wazee?

Je, sasa hivi- tuna wabunge wangapi vijana kwa maana ya miaka kati ya 18 mpaka 35? Tunaweza kuwataja kwa majina?

Manake nasikia bungeni letu zaidi ya robo tatu ya wabunge ni kati ya miaka 50 na kuendelea. Yaani bunge la wastaafu!

Asha

Interesting...kujua idadi ya vijana wabunge kwa sasa
 
Sasa hivi nikisikia "vijana" huwa naona kichefuchefu. No offense. Utawala ulioko madarakini sasa uliingia kwa gear ya "ujana" look at the mess and failures. It is total failure.

NI kama nchi imeuzwa kwa kundi la wachache na sisi tunaendelea kujiita nchi. So sad. Unless hiyo"vijana" iwe well defined, tusije tukapata kina RA, EL, Karamagis etc etc. Vijana wengi kwa siasa zetu za sasa do not stand a chance of making it.

Kwa sababu kwanza lazima wajifunze kuwa waongo, wahongaji, kushirikiana na wezi na kuwa hodari kwenye kupoiga blaa blaa. Sijui kama kuna kijana of Zitto type angependa kuingia kwenye mambo kama haya. Unless vijana wote wagombee kwa tickte ya opposition
 
vijana au wazee sio factor ,tunataka wachapa kazi wenye akili tuu,kuna vijana kama serukamba na nyalandu lakini level yao ni ya chini kuliko yule mbunge aliye forge vyeti(jina sikumbuki)
 
vijana au wazee sio factor ,tunataka wachapa kazi wenye akili tuu,kuna vijana kama serukamba na nyalandu lakini level yao ni ya chini kuliko yule mbunge aliye forge vyeti(jina sikumbuki)[/QUOTE]

Anaitwa Chitalilo.

Anyway nadhani ni wazo zuri kuwa na vijana wengi wenye mawazo pevu na sio kuendeleza mawazo mgando ya 'huu ni mwiba..... mguu utaota tende'(SM)
 
Inategemea kijana ameletwa na nani bungeni maana sio kila kijana atakuwa na mtizamo wa kuwakomboa wananchi, kuna kina nyarandu, nchimbi na wengine hawa hawawezi kuwa na mawazo ya kiukombozi kwani wameletwa bungeni kwa fadhila za watu furani na sio kwa nguzu zao, wakisema kitu hawa hawataonekana tena kwenye siasa kwahiyo lazima wajipendekeze hata kama ni kumaanisha kuua proffessional zao lakini watajikomba kwa kuwa ndo wanachikiona kinafaa wakati huu.

Ukiwa kijana na ukawa na mawazo ya kiukombozi wakati wamekuweka uwatete huwezi kudumu bungeni kwani utakuwa unawawekea kiwingu na watakutafutia dozi kidogo ya kuangaika nayo mfano Amina chifupa aliwakaa kooni wakaamua kumuondoa ili asiwe kikwazo kwao.
 
Asha hoja yako ni nzuri. Hata hivyo nadhani ingekuwa vema kufikiri juu ya utendaji wa mtu na uchungu wake kwa nchi na maendelea ya raia wake kuliko kuangalia umri wake tu. Hivi mtu Kama Dr. Slaa ana umri gani? Je, anaingia katika kundi la vijana? Je, mtu mwenye umri kama wake au zaidi na mwenye msimamo kama wake katika maswala ya nchi aachwe kwa sababu tu si kijana? Watu kama Kilango ana umri gani? Mwakyembe, na wengine kama hawa je?

Au kwa namna nyingine, tuwaingize watu wa aina ya kina Nchimbi, Chitatilo, Malima, Masha kwa sababu tu wana nembo ya ujana?

Mimi ninasema hapana. Tuangalie uwezo wa mtu katika kutetea maslahi ya nchi, usafi wa mtu (asiye na tabia ya ufisadi) na mwenye sifa za uongozi zinazofaa kwa taifa letu bila kujali umri wake.

Mimi ninapendekeza wana JF tujadili zaidi sifa za viongozi tunaowahitaji kuliko kujadili umri wa mtu.
 
Kujua idadi ya wabunge vijana hebu kwanza tuwekane sawa hasa unaposema kijana unaongelea atmost umri gani?, maana kuna wabunge wengi wanaojiita vijana hata kama wana miaka 50, hebu tuwekane sawa. Hapa suala si ujana suala ni wabunge wenye uwezo wa uchambuzi wa mambo kuendana na hali halisi ya dunia kwa sasa na ambao hawafungwi mdomo na chama chao.

Tukipata hawa hata 50 tu bungeni tutashuhudia mapinduzi makubwa sana ya kifikra. Na njia pekee ni kuhakikisha kuwa wabunge wengi wanatoka opposition na hiyo haitoshi wawe na uwezo hapa namaanisha shule iwe imetulia sio uzoefu wa kuchonga kama walivyokuwa wakina Tambwe wakati kichwani majivu.
 
Asha hoja yako ni nzuri. Hata hivyo nadhani ingekuwa vema kufikiri juu ya utendaji wa mtu na uchungu wake kwa nchi na maendelea ya raia wake kuliko kuangalia umri wake tu. Hivi mtu Kama Dr. Slaa ana umri gani? Je, anaingia katika kundi la vijana? Je, mtu mwenye umri kama wake au zaidi na mwenye msimamo kama wake katika maswala ya nchi aachwe kwa sababu tu si kijana? Watu kama Kilango ana umri gani? Mwakyembe, na wengine kama hawa je?

Au kwa namna nyingine, tuwaingize watu wa aina ya kina Nchimbi, Chitatilo, Malima, Masha kwa sababu tu wana nembo ya ujana?

Mimi ninasema hapana. Tuangalie uwezo wa mtu katika kutetea maslahi ya nchi, usafi wa mtu (asiye na tabia ya ufisadi) na mwenye sifa za uongozi zinazofaa kwa taifa letu bila kujali umri wake.

Mimi ninapendekeza wana JF tujadili zaidi sifa za viongozi tunaowahitaji kuliko kujadili umri wa mtu.

Mtuwamungu,

Asha hakusema tuondoe wenye uwezo kama ni wazee. Amesema Tuongeze idadi ya vijana. Kuna nafasi nyingi za wabunge ambao wanazembea tu hata huwasikii wakitoa mchango wowote huko Dodoma. Hizo nafasi ndio zinazoongelewa.
 
Wanaopanga kumpinga Kikwete 2010 wamekumbuka vya kunyonga vya Mkapa

Na Mbasha Asenga
Mwanahalisi~Maslahi ya Taifa Mbele

KUNA uvumi uliotamalaki kwamba ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), lipo kundi la watu linalojiandaa kumpinga rais wao mwaka 2010.

Kwamba sasa hawautaki ule utaratibu wa CCM ambao haujaandikwa kokote wa kumuacha rais atetee vipindi viwili vya miaka mitano kila kimoja. Sasa wanataka kumpinga katika kipindi cha pili.

Huu ni uvumi ambao umekuwako kwa muda sasa. Hakuna ushahidi wa kuthibitisha haya isipokuwa kwa kuwa ni mambo yanayosemwa si vema kuyapuuzia, yafaa tu kuupa umuhimu uvumi huu.

Katika hali ya kawaida mtu angejiuliza maswali magumu kidogo; kwamba wakati hata Rais Jakaya Kikwete hajamaliza nusu ya muda wake wa miaka mitano ya kwanza amewakosea nini wenzake hadi waanze kufikiria kumpiga?

Swali hili ni gumu kwa sababu kwa rais aliyeshinda kwa wingi wa kura kama za Kikwete, na kwa sifa alizokuwa akimwagiwa wakati wa kampeni, inakuwa ni vigumu kujua kilichotokea hadi wenzake sasa wafikiri kumpinga 2010?

Kubwa zaidi, watu wanajiuliza nini kinapeka mawazo ya watu mwaka 2010 wakati hapa katikati kuna mambo mengi tu ya kimsingi ya kujadili kuhusu maendeleo na mustakabali wa taifa hili? Sina majibu ya maswali haya yote.

Hata hivyo, tafakari ya kina inasogeza mawazo yangu kwamba uvumi huu wa watu wanaoutaka urais ndani ya CCM mwaka 2010 unachochewa na watu ambao hawafurahishwi na mwendeno wa mambo ndani ya serikali ya awamu ya nne.

Watu hawa wasiofurahishwa na mwenendo wa mambo, wanadaiwa kuwa na hasira dhidi ya Kikwete kwa sababu kuu moja.

Kwamba, amekuwa ni rais mlaini mno anayeruhusu watu kuichononoa serikali yake, kuchokonoa mawaziri wake, kuchokonoa maamuzi ya serikali kiasi cha kufanya watu waliozoea kufanya mambo watakavyo kuwa na wakati mgumu.

Watu hawa wanaompinga Kikwete wanaufananisha utawala wake na ule wa mtangulizi wake, Benjamin Mkapa. Wakati wa utawala wake, Mkapa hakuruhusu hata serikali yake kunyooshewa kidole achilia mbali kuwatikisa mawaziri wake.

Watu hawa wenye hasira na Kikwete wanasukumwa na sera mpya za uwazi za Kikwete tofauti na uwazi wa Mkapa ambao kwa hakika ulikuwa uimla na usiri usioelezeka.

Wanaotaka kumpinga Kikwete mwaka 2010 wanasumbuliwa na kitu kimoja tu, kwamba kwa nini serikali ikubali kuchukua hatua kwa kila tuhuma inayotolewa dhidi yake, wakati ingeweza tu kupuuza na kuacha mambo kama yalivyokuwa.

Ni hasira za mwizi anayehoji sababu ya mwenye mali kushtuka kwamba anaibiwa wakati mwizi anaamini ana haki ya kujichukulia tu mali ya watu atakavyo.

Kwa maana hiyo, basi kitendo cha Rais Kikwete kuruhusu Bunge kuunda tume kujadili suala la Richmond ambalo liliishia kuvunjwa kwa Baraza la Mamwaziri; kukubali ukaguzi ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kupitia Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) na hatua yake ya kuruhusu uchunguzi wa mikataba ya madini katika migodi mikubwa.

Hatua ya Kikwete kukataa kuwatetea mawaziri wake wenye kashfa na hivyo kulazimika kujiuzulu kama Edward Lowassa, Dk. Ibrahim Msabaha, Nazir Karamagi na hivi karibuni kabisa Andrew Chenge; kwa ujumla ni mambo ambayo hayawafurahishi watu waliozoea kuvuruga mambo na kutetea na Rais wao.

Ndiyo! Tunakumbuka Rais Mkapa akitetea polisi walipoua wananchi kule Pemba, 27 Januari 2001; tunakumbuka Mkapa akitetea mikataba ya ovyo kabisa ambayo viongozi wetu waliitumia kuitumbukiza nchi katika vifungo vya kiuchumi.

Kubwa zaidi, wananchi wanakumbuka jinsi Mkapa alivyokuwa na ujasiri wa kutetea maovu na maamuzi ya ovyo kabisa ya utawala wake, bali pia alithubutu kuwatukana wananchi.

Alisema kwamba ni wavivu wa kufikiri na wengine wana wivu wa kijinga pale wanapohoji ukwasi wa kupindukia na wa ghafla wa watawala wetu!

Kwa maana hiyo viongozi waliolelewa na sera na mikakati ya kibabe ya Mkapa, kauli za kuwabeza na kuwakejeli wananchi, matamshi ya kuwadhalilisha wampinzani kuwa ni wachumi na wanasiasa ucharwa; sasa wanajihisi kubanwa katika awamu hii.

Hawaoni raha tena waliyokuwa wanapata chini ya Mkapa. Viongozi hawa ndio wanaojipanga na kueneza uvumi kwamba mwaka 2010 ni lazima Kikwete apingwe.

Wanampinga Kikwete si kwa sababu wana mkakati wa ziada wa kuharakisha maendeleo ya wananchi, ila wanataka kumweka kibaraka wao ambaye atahalalisha uharamia kama ulivyowahi kuhalalishwa huko nyuma.

Hawa ni watu waliochoka, walafi na wanasukumwa na tamaa ya kurejesha Watanzania utumwani. Ingawa watu wanaokusudia kumpinga rais Kikwete mwaka 2010 wanajenga hoja kwamba serikali ya awamu ya nne imepwaya kwa sababu rais wake amekosa umakini (soften) na kwa maana hiyo kumuachia aongoze nchi mapaka 2015 ni sawa na kulitumbukiza taifa kwenye maafa, ukweli wa mambo unabakia kuwa mmoja, hawana jipya wanalokusudia kuleta isipokuwa kuendekeleza ubinafsi wao.

Ebu tufikiri kwa kina zaidi! Ni vigumu kutathmini matatizo ya Tanzania nje ya mfumo mzima wa utawala ulioasisiwa na CCM. CCM ina kila sababu ya kubebeshwa mzingo kuhusu matatizo ya nchi hii. Kama ni rushwa nchini imeletwa na CCM! Kama ni uporaji wa mali ya umma nchi hii umeletwa na CCM kama ni viongozi wazembe nchi hii CCM ni namba moja kwa viongozi wazembe, kuanzia walioko kwenye chama hadi walioko serikalini.

CCM ni muasisi wa matatizo ya taifa hili. Ndiyo maana sisi tunapowatazama watu wanaojitutumua kuutaka urais mwaka 2010 tunawaona kama watu wanaosukumwa na kitu kimoja tu, ubinafsi na tamaa ya kutaka kuendeleza ya kale. Ni watu wasiotaka mabadiliko, ni watu wasiofurahishwa na mwenendo mpya wa uwajibikaji wa kila mmoja kwa makosa yake. Ndiyo maana wanataka kumwengua Kikwete ili warejeshe zimwi likujualo halikuli likakwisha. Laiti wangelikuwa ni watu wapenda mabadiliko ya kweli, umma ungesimama nyuma yao, lakini kwa historia yao ni watu wanaolililia kurejea ukale wao.

Kwa Wakristo wanafahamu kwamba Musa alipowaongoza wana wa Israel kutoka utumwani Misri kwenda nchi ya ahadi, Kaanani, wapo waliofika njiani na kutamani kurejea utumwani kwa sababu walikumbuka nyama za bure. Wanopanga kumpinga Kikwete 2010 wamekumbuka vya kunyonga, wamekumbuka nguvu zao za kujichukulia kila walichotaka bila kuhojiwa kokote, wamekumbuka utukufu waliojitwalia miaka ya nyuma wanatamani hali hiyo.

Hakika nia yao si kuwatumikia wananchi.
 
CCM wamtimua Shibuda


*Atupiwa virago kwenye Kamati ya Siasa
*Adai ni kundi la wanaojifanya watu wa JK


Na Suleiman Abeid, Shinyanga

MBUNGE wa Maswa mkoani hapa, Bw. John Shibuda, amejikuta katika wakati mgumu baada ya kutimuliwa kwenye kikao cha Kamati ya Siasa ya CCM ya wilaya ya Maswa, akidaiwa kutokuwa mjumbe halali.

Hali hiyo ilijitokeza jana muda mfupi kabla kikao hicho hakijaanza katika ofisi za CCM wilayani hapa, ambapo Bw. Shibuda alionekana akitoka nje ya ofisi hizo, huku akihangaika kufanya mawasiliano na viongozi wa ngazi za juu wa chama hicho.

Akizungumza na Majira baada ya kutimuliwa katika kikao hicho, Bw. Shibuda alisema kitendo hicho kilichofanywa na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya hiyo, Bw. Peter Bunyongoli na Katibu Mwenezi na Itikadi, Bw. Jeremiah Makondeko, ni cha kumdhalilisha na kumvunjia heshima ndani ya Chama.

Bw. Shibuda alisema anavyofahamu yeye ni mjumbe halali wa Kamati hiyo ya Siasa kwa mujibu wa Katiba ya CCM Ibara ya 81(1)(f) ambayo inaonesha wazi kuwa wajumbe wa kamati hiyo ni pamoja na wabunge wa majimbo, wenyeviti wa halmashauri za majiji, manispaa, miji na wilaya.

Ibara hiyo inasomeka: “Mbunge, au wabunge wanaotokana na CCM wanaowakilisha wilaya hiyo au wabunge wa aina nyingine wanaoishi katika wilaya hiyo,” ni wajumbe halali wa kamati ya siasa ya CCM wilaya.

Bw. Shibuda alielezea kushangazwa kwake na hatua hiyo ndani ya kikao hicho, ambapo siku zote amekuwa akialikwa kuhudhuria vikao vya kamati hiyo akiwa mjumbe na kuonesha ushahidi wa baadhi ya barua za mialiko kwa vikao hivyo alizokuwa akipelekewa.

Baadhi ya barua hizo za mialiko zilikuwa ni zenye kumbukumbu namba CCM/KS/28/46 ikiwa ni ya mwaliko wa kikao cha dharura cha Julai 16 mwaka huu; Kumbukumbu namba
CCM/MSW/KS.15/VOL.III/47 ya Juni 28 mwaka huu na kumbukumbu namba CCM/MSW/K.50/13/3/50 ya Julai 12, mwaka huu, ikiwa ni mwaliko wa kikao ambacho alitimuliwa kwa kuelezwa kuwa si mjumbe.

Alisema pamoja na juhudi za kumweleza Mwenyekiti wake asome Katiba vizuri, alikataa kwa kueleza kuwa toleo la Katiba chapisho la hivi karibuni halioneshi kuwa wabunge ni wajumbe wa kamati za siasa za wilaya.

Bw. Shibuda alisema Mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa yeye ni Mwenyekiti wa Wilaya hiyo na kwamba uamuzi wake ni wa mwisho na kuendelea kumtaka atoke nje ya kikao mara moja ili wao waweze kuendelea na kikao.

“Kwa kweli nimesikitishwa sana na kitendo hiki cha kufukuzwa ndani ya kikao kama mbwa, tena mbele ya kadamnasi, sijui Mwenyekiti huyu anajivunia kitu gani, nahisi ni kile ambacho amekuwa akitamba nacho kila siku kuwa yeye ana uhusiano binafsi na Rais Jakaya Kikwete, wakati Rais alishasema hana makundi,” alidai Bw. Shibuda.

Hata hivyo, alisema hali hiyo imeanza kumpa wasiwasi iwapo atatendewa haki atakapoamua kugombea nafasi yoyote ya uongozi ambayo inahitaji kuthibitishwa na vikao vya chama, na kusema kuwa ni wazi hawezi kutendewa haki.

Akizungumza na Majira kwa njia ya simu, Katibu wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, Bw. Gustav Muba, alisema wabunge wote wa majimbo ya uchaguzi ni wajumbe halali wa kamati za siasa za wilaya.

Bw. Muba alisema iwapo kweli viongozi wa CCM wa wilaya ya Maswa watakuwa wamemfukuza ndani ya kikao Bw. Shibuda, watakuwa wamefanya makosa, na pia aliahidi kufuatilia hali hiyo mara baada ya kupokea taarifa rasmi.

“Wabunge wote wa majimbo kwa tiketi ya CCM ni wajumbe halali wa vikao vya kamati ya siasa ya wilaya, inawezekana viongozi wa Maswa watakuwa wameitafsiri vibaya Katiba, au kuna kosa fulani limefanyika katika uchapishaji, nitafuatilia hali hiyo, baada ya kupewa taarifa rasmi,” alieleza Bw. Muba.

Kwa kipindi kirefu sasa, uongozi wa CCM wilayani Maswa, umekuwa na mgogoro mkubwa unaotokana na kambi wakati wa uchaguzi wa kura za maoni za uteuzi wa wagombea ubunge ndani ya chama hicho, hali ambayo inaonekana kukithiri kadri siku zinavyokwenda.

Juzi Makamu wa Rais, Dkt. Ali Mohemmed Shein, aliwataka viongozi wa wilaya hiyo kuwa na mshikamamo wa pamoja, ili kutekeleza kikamilifu Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005, ili kulinda imani ya wananchi kwa chama hicho, lakini hata kabla hajamaliza ziara yake mkoani hapa, malumbano yameanza kujitokeza.
 
Back
Top Bottom