The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
kikwete anaweza kuwa forced kutumia brutality na corruption kuliko ya 2005 ili ku cling to power.

One thing is certain, kama ataondoka ni kwa kutaka yeye mwenyewe lakini hakuna kitakachomzuia kuiba kura na pesa ili kurudi Ikulu mpaka 2015.

Hatuna utamaduni wa a one term president.

Now why would he do that?

Waafrika Ndivyo Tulivyo au...?
 
Hao wagombea wa CCM sio mafisadi?
 
wapinzani watafute njia ya kuongeza wabunge,hiyo ndoto ya uraisi wajaribu kutafuta watu wengine na sio wao.yatakuwa yale yale ya mrema na lipumba.

Nilisema ktk post yangu moja kuwa kwa nini wapinzani wameshindwa kupata wabunge ktk miji mikubwa kama Dar, Mwanza, Arusha na mingine.
 
wapinzani watafute njia ya kuongeza wabunge,hiyo ndoto ya uraisi wajaribu kutafuta watu wengine na sio wao.yatakuwa yale yale ya mrema na lipumba.
Nilisema ktk post yangu moja kuwa kwa nini wapinzani wameshindwa kupata wabunge ktk miji mikubwa kama Dar,Mwanza,Arusha na mingine.

you are very right,
kinachohitajika sasa ni uwiano wa kutosha bungeni.

Vyama vilivopo haviko tayari kuongoza Taifa. Sio tu kwa kukosa sera zinazotekelezeka, pia kwa ukosefu wa network ya kuwawezesha kuendeleza ujenzi wa taifa iwapo wataingia madarakani.

Ushauri ninaoweza kuutoa kwa vyama vya upinzani ni kila kiongozi wao mwenye uwezo wa kushinda jimbo basi na akaligombee. Ndoto za urais hamko tayari kuziota sasa hivi.

Mbowe kuacha kugombea jimbo na kugombea urais anaojua wazi kuwa haupati was a mistake, in my view Lipumba pia ilibidi agombee ubunge, msirudie makosa kama hayo kwenye uchaguzi ujao. Hii ni kwa manufaa ya Taifa.
 
Nimefurahi sana na majibu yote toka Upinzani.. Dr. Slaa hongera mkuu umeiva kisiasa..
Zitto, mkuu niseme nini zaidi na heshima kubwa nakupa niliposoma habari hizi kuwa upo karibu sana na wazee viongozi wetu waliokwisha staafu.

Hakuna somo kubwa kama hilo mkuu zidi kujenga Phd ya elimu dunia...
 
Membe na Masha? Duh hapo sina cha kusema!!

Mkuu heshima mbele, hapo kuna makundi mawili ambayo ni bitter, moja la muungwana mwenyewe, na lingine la Rostam, just fasten your belt....maana kinachokuja ni an ugly ride!
 
you are very right,
kinachohitajika sasa ni uwiano wa kutosha bungeni.

Vyama vilivopo haviko tayari kuongoza Taifa. Sio tu kwa kukosa sera zinazotekelezeka, pia kwa ukosefu wa network ya kuwawezesha kuendeleza ujenzi wa taifa iwapo wataingia madarakani.

Ushauri ninaoweza kuutoa kwa vyama vya upinzani ni kila kiongozi wao mwenye uwezo wa kushinda jimbo basi na akaligombee. Ndoto za urais hamko tayari kuziota sasa hivi.

Mbowe kuacha kugombea jimbo na kugombea urais anaojua wazi kuwa haupati was a mistake, in my view Lipumba pia ilibidi agombee ubunge, msirudie makosa kama hayo kwenye uchaguzi ujao. Hii ni kwa manufaa ya Taifa.

Naona wewe unadhani kuwa tuko bado kwenye mfumo wa chama kimoja. Kuna sababu gani ya kutogombea nafasi ya uraisi. Uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na kama ikitokea kuwa wanashindwa basi hiyo ni matokeo ya uchaguzi.
 
Mkuu heshima mbele, hapo kuna makundi mawili ambayo ni bitter, moja la muungwana mwenyewe, na lingine la Rostam, just fasten your belt....maana kinachokuja ni an ugly ride!

Ndio maana nimekaa kimya mkulu, maana yule ndugu yetu naye na mihasira yake si patakuwa hapakaliki.
 
Naona wewe unadhani kuwa tuko bado kwenye mfumo wa chama kimoja. Kuna sababu gani ya kutogombea nafasi ya uraisi. Uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na kama ikitokea kuwa wanashindwa basi hiyo ni matokeo ya uchaguzi.

Unajua katika siasa kuna ushindi wa aina nyingi, hauoni itakuwa vizuri sana kama asilimia kubwa ya wabunge watakuwa wa upinzani? itakuwa ni pigo kubwa pale CCM itashindwa kuunda serikali kwa sababu ya uchache wa wabunge wao. Sioni haja ya kuwa na raisi wa upinzani ambaye hatakuwa na nguvu ya kubadilisha mwelekeo wa nchi.

kama msemaji mmoja alivyosema anayejua ana uwezo mkubwa wa kushinda ubunge akagombee na vyama vya upinzani wakiweza kukubaliana wasimamishe mbunge mmoja badala ya kila chama kuweka mgombea wake kwa kila jimbo la uchaguza. Kama CUF wanaona jimbo fulani is thier strong hold wasimamishe mtu hapo na wengine wawape support na kuwafahamisha wapiga kura what is going on. Watanzania wengi wataona nia ya wapinzani na itasaidia kuongeza imani kwao
 
Power, Nakuunga mkono 100% najua tutakumbana na upinzani mkubwa sana kwenye hili hapa JF. Kwa mtazomo wangu tunahitaji mtu mmoja tuu kwenye nafasi ya Uraisi kutoka upinzani, na awe ni mtu ambaye hajawahi kugombea nafasi hiyo. Wengine woote waliobaki waende kugombea ubunge.

Tupate wabunge wengi kutoka upinzani. Mrema nenda Vunjo kamtoe Kimaro. Mbowe nenda Hai, Lipumba nenda Tabora tena kwa ubabe kamtoe Rostam, Mvungi nenda hata Moshi vijijini, na wengine wote waliotaka uraisi waende kwenye majimbo watapata.

Naamini hata wale wapiga kura wetu wanaodanganywa na kanga na sukari kukiwa na watu wachache kwenye karatasi ya kupigia kura wanaweza kufanya uamuzi sahihi zaidi.
 
Kiti cha U rais si lelemama!
Hata JK naye alikuja kwa aina yake na hakuanza kujionyesha kuwa anahitaji hata alipoulizwa na wasomi wa Udsm alipozuru wakati akiwa na waziri wa mambo ya nje alijibu kisiasa kwamba kwa mda ule hajafikiria kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa.

Nakumbuka kama asingepitishwa wakati mchakato wa sisiem kulingana na propaganda iliyokuwepo wengi walidhani angehama chama chake aingie vyama vya upinzani kama CUF n.k.

Naamini Candidate aliye na nia ya dhati ya kugombea kuteuliwa ktk hicho hawezi kujionyesha kwa sasa maana wanasiasa wanaogopa kuchafuana kwa kuwa ndo mfumo wa siasa ulivyo kama alivyochafuliwa Dr.Salim kuwa ni Hizbu.

Hiyo mipango ya chini chini itaendelea lakini haiwezi kuwa dhahiri kwa majira haya tuliyo nayo ya ufisadi na kuumbuana.
 
Mimi ni mmoja wa walioshitushwa na habari za watu kuwania urais tena wa mwaka 2010 leo hii tukiwa 2008! Ni mapema jamani!

Ubavu wa kukabili mafisadi, kuweka mifumo mipya yenye maslahi ya taifa, kuondosha Richmond, Buzwagi, IPTL, Kiwira, Meremeta si kazi ya kujitangazia mapema namna hii.

Ila nitafurahi iwapo ndani ya CCM watatunishiana msuli wa kulazimisha JK atawale miaka 5 na awe mstaafu maana Ikulu imemshinda.
 
Mwaka 2010 siyo rahisi kutabiri nini kitatokea. Nguvu ya CCM haitakuwepo sana kutokana kutokuwepo kwa fedha za misaada (i.e EPA , Off Shore companies, NSSF etc).

CCM as a organization is huge , kuanzia tawi mpaka Taifa na kujumulisha jumuiya zake. Kutukuwepo kwa hizi fedha kutayumbisha CCM. To a certain extent watakuwa at equal/level playing ground na wapinzani.

Age ya voters nayo itachangia kuuamua nani atashindi. At least eighty percent ya wapiga kura hawatukuwa wanamfahamu Nyerere ni nani .
Mtu yeyote anaweza kuchaguliwa siyo hao wanaotajwa tu.
 
Kama Salim atakimbilia kwenye Upinzani basi naamini kabisa sio atakuja peke yake bali kundi kubwa ambalo limeng'amua njama alizofanyiwa zilikuwa za kumpaka matope ambazo wengi walioshiriki wanajuta ataondoka nalo wakiwamo wanachama wa CCM na ndio itakuwa mwisho wa CCM ,wacheni mchezo huyu jamaa anakubalika kabisa ndani ya Tanzania bado kinyota anaonekana anang'ara na ana msukumo na nguvu za kiutawala.

Kuna watu wanaweza kuwa viongozi lakini hawana nguvu za kiutawala na nguvu hizi inakuwa mtu anazaliwa nazo ,Salim amezaliwa na nguvu za kiutawala au ana uso wa kiutawala ,ila huyu jamaa anaweza akawafunga watu au mafisadi bila ya kupitia mahakamani nikimaanisha watakaotaka kujitetea watafanya hivyo wakiwa behind bars.

Maana kuwa kiongozi wa Nchi na wananchi wake inatakiwa pasiwepo uswaiba wa huyu ni mwenzetu mambo ya Raisi kuzungumza na wengine kama wapo kwenye maskani yanakuwa hayatakiwi , mambo ya huyu ni mwenzetu hayatakiwi na nina hakika Salimu anayaweza hayo bila ya kumuonea haya mtu.

kama utamchunguza Nyerere alikuwa hana mambo ya uswahiba anapokuwa katika shuguli kubwa kubwa za mikutanao na mawazri wake ,kama ukimwangalia sana utamwona uso huwaka ameukunja na ameweka ndita kali na macho yamekuwa makubwa kuliko kawaida ,huyo ndie Nyerere hana mchezo na mtu katika anga zake na ni zipi anga za Nyerere ,anga za Nyerere ni zile sehemu ambazo yeye kama raisi ana mamlaka nazo ,hivyo aliweza kumuumbua mtu mbele ya mkutano kwa maneno yenye uzito.
 
Viongozi wote wa CCM na sirikali wakiwamo mawaziri hawafai kugombea urais kutokana na kimya chao kizito kuhusiana na swala la ufisadi. Wataendeleza usanii tu hawa tuwaulize je, wakati nchi ilipogubikwa na ufisadi nyinyi kama viongozi mlitoa ushauri gani?

Je mliwaambia Watanzania kitu gani kuhusiana na ufisadi huo? Kama hamkusema chochote, kwanini mliamua kukaa kimya?
 
Viongozi wote wa CCM na sirikali wakiwamo mawaziri hawafai kugombea urais kutokana na kimya chao kizito kuhusiana na swala la ufisadi. Wataendeleza usanii tu hawa tuwaulize je, wakati nchi ilipogubikwa na ufisadi nyinyi kama viongozi mlitoa ushauri gani? Je mliwaambia Watanzania kitu gani kuhusiana na ufisadi huo? Kama hamkusema chochote, kwanini mliamua kukaa kimya?

Unajua sababu kubwa ya watu wa CCM kukaa chonjo ni kuacha waliofaidika wajipapatue si wanasema kila mtu atabeba mzigo wake.Wao wakae kimya tu inatosha.
 
Tunataka kuwa kama Wamarekani sasa ambao as soon as rais anachaguliwa watu wanaanza scheming kuhusu the next president.Hata kazi ya kuwatumikia watu inasahaulika.

Nampongeza Slaa kwa kulielewa hili na kusema kuna mengi ya kufanya sasa badala ya kutafuta urais.Ukifanya kazi watu watakuona na unapata hata issues za kucampainia.Sasa bwana HAmad ana ujiko gani wa ku campain on?
 
Naomba kutoa changamoto kwa wote wana CCM na wale ambao si Wana CCM.

Je ni nani mawazoni mwenu mnafikiri atafaa kuwa mgombea wa Urais wa Muungano kwa upande unaoutaka? Naomba ukitoa jina utoe na sababu pamoja na wasifu wa kutosha kutokana na mgombea huyu unayemdhania.

Ni nani watafaa kugombea Urais Zanzibar? same rule apply, name, reason and work history.

Natanguliza shukrani.
 
Mkuu kwa mwenendo uliopo sasa, naona JK anafaa kuendelea na kipindi kingine. Nadhani kubadilisha mwingine itakuwa kumtwisha mzigo usiostahiki. Kwanza i hope this time hakuna atakayetaka kukimbilia ikulu
 
Upande wa CCM kusema kweli sioni ndani kabisa... hakuna mwanga kwa sababu hili kundi hili kama bado lipo uraiani sidhani kama kuna mtu CCM anaweza kufaa kuwa rais.


Nani huko anaweza kulikemea kundi hili kwa kuwataja majina!... kama tunavyofanya hapa JF?. NANI kama yupo basi huyo huyo, hii ni kwa manufaa ya taifa.

Zanzibar nako sioni zaidi ya kuendeleza utawala wa hilo baraza la wadandiaji Mapinduzi! Nasema hivi, hakuna hata mmoja wao alishiriki ktk mapinduzi hayo! usiku huo wote walikuwa wamelala...Hakuna mwana mapinduzi wa Kweli isipokuwa Salim A. Salim na kundi lake ya UMMA party!
 
Back
Top Bottom