The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Jamani tunazungumzia muda wa miaka miwili kufikia 2010.Kwa mtazamo wangu wa chapchap ni kwamba bila ya kujipanga vizuri tutawaachia tena mafisadi warudi tena madarakani.

Sasa kabla ya kuanza kuwalaumu wananchi kwa kuipenda mno CCM huku wao wakifa masikini hebu tuangalie tu kwanza mfumo mzima wa uchaguzi nchini kwetu kama unaweza kutangaza ushindi kwa chama cha upinzani kama kikishinda.

Maana katiba bado ni ileile, mwenyekiti wa tume ya uchaguzi huteuliwa na rais, na ippmedia ya mengi nayo huipigia debe CCM.
Sasa wenzangu mnalionaje hili?

-Wembe.
 
Jamani tunazungumzia muda wa miaka miwili kufikia 2010.Kwa mtazamo wangu wa chapchap ni kwamba bila ya kujipanga vizuri tutawaachia tena mafisadi warudi tena madarakani.
Sasa kabla ya kuanza kuwalaumu wananchi kwa kuipenda mno CCM huku wao wakifa masikini hebu tuangalie tu kwanza mfumo mzima wa uchaguzi nchini kwetu kama unaweza kutangaza ushindi kwa chama cha upinzani kama kikishinda.Maana katiba bado ni ileile,mwenyekiti wa tume ya uchaguzi huteuliwa na rais,na ippmedia ya mengi nayo huipigia debe CCM.
Sasa wenzangu mnalionaje hili?

-Wembe.

Respect mkuu wangu,

Kwa kweli tunahitaji tume huru ya uchaguzi,kunhitajik mrekebisho kadhaa kwenye katiba yetu.Pia ni muda ambao kama resources zinaruhusu hata wananchi wanatakiwa wapewe elimu ya uraia yenye uamsho mpya wa kisiasa



Sasa Upinzani inabidi wajipange haraka kwani muda unaisha.Waanze kujenga mitandao ya ushindi kuanzia chini.

Hilo suala la katiba.tume na Elimu ya Uraia + kuchelewa kwa opposition kuchelewa kujipanga upya+ wananchi kukubali vitisho kutokana na kutokua na elimu ya kutosha ya uraia+Matumizi mabaya ya Dola ndiyo silaha kuu zinazowarudisha CCM na baadhi ya mafisadi kwenye madaraka.


Kwenye nchi za kidemokrasia kwa mfano hapa India hali ni tofauti sana kisiasa hasa inapofika muda wa Uchaguzi.India ina Demokrasia ambayo ni interesting sana
 
Jamani wenzangu. Watanzania wenye uchungu na nchi hii. Wajasiriamali. Masikini. Wazalendo na watoto wa Tanzania.

Kwenye jambo la kweli na lenye maslahi ya Tanzania na watu wake, lazima lisimamiwe na litetewe kwa kila tone la damu la maji ili watoto wetu, hata kama siye hatutakuwepo li kunusuru ustawi wa nchi.

Nimekutana na watu kibao, wakizungumzia kuhusu uchaguzi ujao, 2010. Yawezekana kuwa mbali, lakini lazima tukubaliane kuwa tunahitaji mtu wmenye uchungu, anayesema No na ikawa hivyo, akaisimamia na kueleza sababu za kusema hivyo. Mtu ambaye hayumbishwi na marafiki mafisadi. Mtu ambaye anaamini katika misingi ya haki kuongoza Tanzania.

Katika vikao ambavyo sivyo rasmi; katika harusi, vijiwe, ofisini, kwenye baa na vituo vya mabasi yetu ya jumla, mazungumzo sasa ni kumpata Mtanzania ambaye ana uchungu na nchi. Huyu wanamtaka awe Rais wa Tanzania 2010.

Wanamtaka warioba, Joseph Sinde achukue fomu mwaka huo utakapofika ili aokoe jahazi, kwani wanasema kuwa nchi imevurugika, haina misingi, haina visheni kwa sasa, licha ya kusifiwa na Bush na wasanii wengine wa ndani na nje.

Hebu changieni hapa wana-JF ili tupate muafaka na tukiweza tuweke msimamo wetu mapema kuwa tunampendekeza nani kwa mwaka huo, utaratibu wa kwamba rais lazima amalize miaka 10 haufai kwa sasa katika Tanzania iliyochanika kiasi hiki.

Nakulilia mama Tanzania kwa machozi ya damu kwa jinsi baadhi ya viongozi wetu wanavyokutafuna wakijitahidi kugawana fito za nyumba yako. Ee Tanzania... Ewe Tanzania.
 
Jamani wenzangu. Watanzania wenye uchungu na nchi hii. Wajasiriamali. Masikini. Wazalendo na watoto wa Tanzania.

Kwenye jambo la kweli na lenye maslahi ya Tanzania na watu wake, lazima lisimamiwe na litetewe kwa kila tone la damu la maji ili watoto wetu, hata kama siye hatutakuwepo li kunusuru ustawi wa nchi.

Nimekutana na watu kibao, wakizungumzia kuhusu uchaguzi ujao, 2010. Yawezekana kuwa mbali, lakini lazima tukubaliane kuwa tunahitaji mtu wmenye uchungu, anayesema No na ikawa hivyo, akaisimamia na kueleza sababu za kusema hivyo. Mtu ambaye hayumbishwi na marafiki mafisadi. Mtu ambaye anaamini katika misingi ya haki kuongoza Tanzania.

Katika vikao ambavyo sivyo rasmi; katika harusi, vijiwe, ofisini, kwenye baa na vituo vya mabasi yetu ya jumla, mazungumzo sasa ni kumpata Mtanzania ambaye ana uchungu na nchi. Huyu wanamtaka awe Rais wa Tanzania 2010.

Wanamtaka warioba, Joseph Sinde achukue fomu mwaka huo utakapofika ili aokoe jahazi, kwani wanasema kuwa nchi imevurugika, haina misingi, haina visheni kwa sasa, licha ya kusifiwa na Bush na wasanii wengine wa ndani na nje.

Hebu changieni hapa wana-JF ili tupate muafaka na tukiweza tuweke msimamo wetu mapema kuwa tunampendekeza nani kwa mwaka huo, utaratibu wa kwamba rais lazima amalize miaka 10 haufai kwa sasa katika Tanzania iliyochanika kiasi hiki.

Nakulilia mama Tanzania kwa machozi ya damu kwa jinsi baadhi ya viongozi wetu wanavyokutafuna wakijitahidi kugawana fito za nyumba yako. Ee Tanzania... Ewe Tanzania.

Labda kwanza atueleze vizuri na kujiosha na Meremeta; this guy has a hand in the BOT! Let him come out clean on this first!
 
Jamani wenzangu. Watanzania wenye uchungu na nchi hii. Wajasiriamali. Masikini. Wazalendo na watoto wa Tanzania.

Kwenye jambo la kweli na lenye maslahi ya Tanzania na watu wake, lazima lisimamiwe na litetewe kwa kila tone la damu la maji ili watoto wetu, hata kama siye hatutakuwepo li kunusuru ustawi wa nchi.

Nimekutana na watu kibao, wakizungumzia kuhusu uchaguzi ujao, 2010. Yawezekana kuwa mbali, lakini lazima tukubaliane kuwa tunahitaji mtu wmenye uchungu, anayesema No na ikawa hivyo, akaisimamia na kueleza sababu za kusema hivyo. Mtu ambaye hayumbishwi na marafiki mafisadi. Mtu ambaye anaamini katika misingi ya haki kuongoza Tanzania.

Katika vikao ambavyo sivyo rasmi; katika harusi, vijiwe, ofisini, kwenye baa na vituo vya mabasi yetu ya jumla, mazungumzo sasa ni kumpata Mtanzania ambaye ana uchungu na nchi. Huyu wanamtaka awe Rais wa Tanzania 2010.

Wanamtaka warioba, Joseph Sinde achukue fomu mwaka huo utakapofika ili aokoe jahazi, kwani wanasema kuwa nchi imevurugika, haina misingi, haina visheni kwa sasa, licha ya kusifiwa na Bush na wasanii wengine wa ndani na nje.

Hebu changieni hapa wana-JF ili tupate muafaka na tukiweza tuweke msimamo wetu mapema kuwa tunampendekeza nani kwa mwaka huo, utaratibu wa kwamba rais lazima amalize miaka 10 haufai kwa sasa katika Tanzania iliyochanika kiasi hiki.

Nakulilia mama Tanzania kwa machozi ya damu kwa jinsi baadhi ya viongozi wetu wanavyokutafuna wakijitahidi kugawana fito za nyumba yako. Ee Tanzania... Ewe Tanzania.

Kumbuka baada ya list of shame kutolewa na Dr. Slaa huyu warioba alionekana kuwatetea. Isitoshe siku hizi credibility yake kwenye jamii imeshuka sababu ya kuwa kinyonga
 
Warioba Nitamuunga Mkono....mnajua Kuwa Kikwete Ni One Term President?

Ambao Hawaamini Wasubiri..mwaka 2011..inshaalah Tutakumbushana Hapa, lakini Ndo Hivyo, hana Akili Wala Uwezo Wa Kutawala Miaka 10, hili Hata Yeye Analijua.
 
Mimi nadhani sii muda muafaka wa kujadiri tumuweke nani 2010 kwenye kuiongoza nchi. Cha msingi kwa sasa, ni kujadili ni kwa nini Tanzania ni Masikini na wananchi walio wengi ni walala hoi.

Pia mfumuko wa bei uko juu sana, vyakula vinapanda bei kila kukicha kwa mfano Kure Dar es Salaam, lita moja ya mafuta ya kupikia ni TShs 3,000/=, Maharage Kg ni TShs 1,400, Unga sembe ni Kg ni TShs 7,000, Petrol inapanda kilwa Kukicha lita moja ni zaidi ya TShs 1,530 bila VAT, DAWASCO wanapandisha garama za maji, umeme hali kadhalika, vifaa vya ugenzi ni juu sana, kodi za pango. Mambo haya yote yanazidi kuwa mzigo kwa mwananchi wa chini ambaye hata wezo wa kupata dola moja kwa siku hana.

Hali inavyokua mbaya mijini inaambukiza pia vijijini. Miji hutoa support kubwa sana wanaoishi vijijini.

Kuendana na Kitengo cha Takwimu, mwezi uliopita Mfumuko wa bei ulifikia 8.6% hii inatisha sana.

Nini Kifanyike

Wana JF, mimi nadhani ni muda muafaka kuwa na sera ya taifa, ya muda mfupi na mrefu kuhusu uzalishaji kwa sector zote. Tuondoe ule ukiritiba wa vyama vya kisiasa kuwa na sera. Tuwe na sera za kitaifa, vyama na wagombea wao waelezee jinsi gain watakavyotekeleza sera za kitaifa. Mojawapo ya sera za kitaifa napendekeza kama ifuatavyo

Tuwe na mapinduzi ya kilimo. Farming Revolution,
Mapinduzia ya viwanda-Industrial Revolution
Mapinduzi ya miundombinu- Infrastructure Revolution
Mapinduzi ya madini- Mineral Revolution
Investment Policy, 30% of profit should be re-invested in TZ

Mapinduzi haya nadhani yawe sera za kitaifa na sio vyama ili kuliwezesha taifa letu kuwa na mikakati ya kudumu. Sio kila chama na sera yake
 
Jamani,mie ntapinga saana,huyu bwana mkubwa kuwa president,sio kwamba namchukia,ama nina chuku binafsi dhidi yake,hapana,huyu mtu katupiga changa la macho wabongo, yaani hata hatuamini kama ndo yeye,ana mkono meremeta, lakini kubwa yumo kwa soo la BOT, kupitia ile kampuni yake pale vingunguti inaitwa Mwananchi gold, ambayo kwakiasi kikubwa imetuumiza sana wabongo na mahela yetu pale BOT.

Hafai, ameonyesha kua anatamaa,na mwenye tamaa, pale kwenye lilejumba jeupe, hafai, naomba tumpinge, anaelement za ufuisadi, ukimpa chance atakua fisadi mkubwa, mnakumbuka soo la mwanae pale manispaa ya kinondoni?alilimalizaje?
 
Kwa jibu fupi na safi nasema WARIOBA hafai kabisa .nashauri turudi kujadili hoja za Mkombozi wakati tuna waza nani anaweza Rais mwaka 2010 kama JK atakuwa kesha choka .

Labda Prof Baregu sasa asimame .Mbowe ataendelea kuwa mwenyekiti Chama kama ambavyo tunataka sasa kutofautisha uongozi wa Chama na Serikali .
 
Awali alionekana kama msafi, lakini aliamua kujichafua hadharani alipoanza kuwaponda wapinzani walipokuwa wanatetea taifa letu dhidi ya ufisadi.

Kwa vile tayari baadhi ya madai ya wapinzani yamedhihirika kuwa yalikuwa na ukweli, yeye hatufai! Ebu atuambie alikuwa na maana gani kusema watu wasimkejeri rais!! wakati walikuwa wanatetea masilahi ya taifa, alikuwa naficha nini? Binafsi naamini wapinzaniwalikuwa na nia ya kumsaidia JK kujua kero za wananchi, ilikuwa ni sauti ya wengi.

Warioba hawezi kusema hakujua huu uozo unaofunuliwa sasa hivi, yeye aliamua kuchunga kitumbua chake kwa kauli tata hiyo. Ukisha kuwa kiongozi wa ngazi yoyote ile ni wajibu kuendelea mchango wako kwa viongozi siyo kukaa pembeni ukasema acha yaendelee kama yalivyo.

JKN licha ya kuwa kasoro zake kama baadhi wanavyoziona, hakunyamaza kusema aliloona kuwa si sahihi. Aliongelea Azimio la Zanzibar wazi na leo waandishi wanaqoute. Kwa nini huyu mheshimiwa asipigie kelele ripoti yake iliyotumia pesa zetu ipatikane wazi wazi nasi tujue yaliyomo?

Warioba hatufai maana hafai hata kuwa mbunge jimboni kwake! Taifa hataliweza!JK akimaliza ngwe yake atue kwa mtu mwenye uchungu halisi na nchi yetu, awe anatoka CCM sawa, Upinzani sawa.

Muhimu asiwe mwanamtandao fisadi. labda atakuwa PINDA!! maana watawala wote huweka na Bwana!
 
Lione, mwanae gani? Soo gani Manispaa yaKinondoni? Data pleeease.
 
Warioba Nitamuunga Mkono....mnajua Kuwa Kikwete Ni One Term President??? Ambao Hawaamini Wasubiri..mwaka 2011..inshaalah Tutakumbushana Hapa...lakini Ndo Hivyo...hana Akili Wala Uwezo Wa Kutawala Miaka 10..hili Hata Yeye Analijua ....
Warioba aendelee kula pensheni yake ya WM... Inatosha!
JK is the right man at the right time in the right place... wenye chuki mjinyonge... Chini ya JK GDP imepanda na kufikia 6.2% katika 2007 na this year itafika 7.3%. Mwendo mdundo hadi 2015
 
Warioba Nitamuunga Mkono....mnajua Kuwa Kikwete Ni One Term President??? Ambao Hawaamini Wasubiri..mwaka 2011..inshaalah Tutakumbushana Hapa...lakini Ndo Hivyo...hana Akili Wala Uwezo Wa Kutawala Miaka 10..hili Hata Yeye Analijua ....

Hahahahahhhaaaha, hii inanikumbusha hata kwa George Kichaka walisema hivyo hivyo, kumbuka "usemae ndie kumbe sie na usemae sie kumbe ndie."
 
Hivi Mwungwana aliutaka urais ili afanye nini? Ametumia kipindi cha miaka kumi kuwania.
Lakini mbona visheni imempiga chenga? Mimi nadhani hapa swala si personality kwamba nani anaweza kusaidia kuwakomboa Watanzania. Suala linapaswa kuwa nini tunachopaswa kukifanya kuwakomboa Watanzania kutoka hili wimbi la mafisadi? Ni kweli Mwungwana ni mwenzao na si mwenzetu. Tuorodheshe kwanza yale yanayotakiwa kufanyika halafu ndiyo tuanze kutafuta ni nani kati yetu aliye na uchungu wa kutosha kuyafanyia kazi yale tuliyoyaorodhesha. Nakumbuka mwaka 1995 kilio kilikuwa rushwa. Mwalimu alifikiri Mkapa angetusaidia. Alipoingia Ikulu akasema hatafanya "witchhunting." Badala yake akaungana nao mafisadi. Tujifunze kutoka makosa kama haya.
 
Binafsi nina hakika CCM Asilia mwaka huo 2010, ni mwaka wao kama watajipanga vizuri laa sivyo kundi la Agenda 21 watarudi na kama kawaida yetu sisi Wadanganyika - Utulivu na Amani utakuwa ngao yao. Mtandao unakufa kifo cha nyani sasa hivi wanajinyonga wenyewe...

Kwa mtaji huu tuliokuwa nao nasema Mrema would be the best Presidaa kwa Tanzania hii ya Mafisadi.
 
Hivi Mwungwana aliutaka urais ili afanye nini? Ametumia kipindi cha miaka kumi kuwania.
Lakini mbona visheni imempiga chenga? Mimi nadhani hapa swala si personality kwamba nani anaweza kusaidia kuwakomboa Watanzania. Suala linapaswa kuwa nini tunachopaswa kukifanya kuwakomboa Watanzania kutoka hili wimbi la mafisadi? Ni kweli Mwungwana ni mwenzao na si mwenzetu. Tuorodheshe kwanza yale yanayotakiwa kufanyika halafu ndiyo tuanze kutafuta ni nani kati yetu aliye na uchungu wa kutosha kuyafanyia kazi yale tuliyoyaorodhesha. Nakumbuka mwaka 1995 kilio kilikuwa rushwa. Mwalimu alifikiri Mkapa angetusaidia. Alipoingia Ikulu akasema hatafanya "witchhunting." Badala yake akaungana nao mafisadi. Tujifunze kutoka makosa kama haya.

Yaani tunashindwa kuona ukweli? kwamba hakuna awamu iliyofichua mafisadi na kuonyesha nia ya kuwashughulikia kama hii ya nne.
 
dar es salaam,
hili ni ombi tu na sio lazima,lakini kama kweli wewe ni mzalendo halisi na kiongozi au unatoka kati ya kambi mojawapo ya asili au mtandao basi badilisha jina lako hapa ukumbini.
Kwani unatudhalilisha sisi watandanganyika kwa kubeba dhiki zako kwenye mfuko wa plstiki,maana kila unapopita kila mtu anashuhudia matatizo yako hivyo unatufanya sisi ndugu zako kudhalilika kwa kuwa tunatumia jina moja la ukoo.

JK bahati nzuri au mbaya ni mtu ambaye ameshiriki kikamilifu kutuza watanzania toka awamu ya mwinyi na mkapa na sasa yeye ameamua kufunga mahesabu kabisa kabla hajakaa pembeni 2010.kwa jinsi anavyokwenda sitegemei kupata hata chenji baada ya kumaliza uwongozi wake.

Ndio sababu ktk awamu hii umeona jinsi mafisadi wanavyogombania kile kidogo kilicho baki bila aibu.unaposema eti jk napambana na ufisadi sio kweli bali ni dangavya toto wao wanatumia ule msemo usemao panya sikuzote anauma na kupuliza.
 
..Raisi anayekuja atatoka ktk rika la kina Dr.Shukuru Kawambwa, Dr.Lawrence Masha, Dr.William Ngeleja, Dr.Deusdedit Kamala, Dr.Adam Malima,na Dr.Mathayo David.
 
Warioba aendelee kula pensheni yake ya WM... Inatosha!
JK is the right man at the right time in the right place... wenye chuki mjinyonge... Chini ya JK GDP imepanda na kufikia 6.2% katika 2007 na this year itafika 7.3%. Mwendo mdundo hadi 2015


huo uchumi wa kikwete unaopaa..na gdp...kufika 7.2% labda ...gavana awe wewe kibunango...tupe source basi..ya hiyo economic findings yako....
 
Kwa mtaji huu tuliokuwa nao nasema Mrema would be the best Presidaa kwa Tanzania hii ya Mafisadi.

I agree. Yeyote yule, au the likeness ya Mrema inafaa, lazima mtu aje na ukichaa(sina maana ya ugonjwa). Tanzania hii haiendi popote mpaka aje mtu atayekuja (to say the least) kutandika viboko wabadhirifu makazini na kuuwa wahujumu uchumi! I am for a person with Machiavelli style! Other than that...ni maikidamakida tu!
 
Back
Top Bottom