John Mnyika
JF-Expert Member
- Jun 16, 2006
- 713
- 1,249
Mnyika nimekupata, inatia moyo kwamba angalau mmeongea and I was wrong in my earlier analysis.I understand you may not want to go into bunge's technicalities for tactical reasons, but without even knowing the details I can tell the technicalities are unhealthy if they can be abused to silence genuine opposition.The question is, what is the opposition doing to adress this?
Bab kubwa, kuwa balozi wa mabadiliko vijijini huko na tupe ripoti ya maendeleo ya mwamko katika ngazi ya vijijini.
Pundit
Upinzani unamwaga yote kwa umma, kama wabunge wameshindwa kuwawakilisha wananchi basi tunayapeleka kwa wananchi wenyewe. Na wananchi wanaamua hatua gani za kuchukua.
Naona wameanza kwa kuwazomea na hakupunguza imani nao(mintaarafu ripoti ya REDET). Na naona bunge limeshtuka kwamba wanazidi kudharaulika, naamini kuundwa kwa haraka haraka kwa kamati teule ya Richmond katika suala ambalo Lowassa alikuwa akilizimia kwenye kamati ya Wabunge wa CCM kunaonyesha pengine wanajaribu kurejesha imani.
Pia wanajaribu kupiga baragumu kuwa kanuni za bunge zimebadilishwa, kwamba sasa wabunge watakuwa na uhuru zaidi wa kuikosoa serikali! Sisi tunaendelea kufuatilia tu; kadiri bunge linavyoshindwa kuiwajibisha serikali kwa sababu ya hodhi ya chama kimoja bungeni ndio kadiri wabunge wa CCM wanavyojichimbia kaburi la kisiasa. Sasa ikifika 2010 unatajua upinzani utafanya nini.
JJ