The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Madela,

Yeye alidhani kuwa akitisha kushitaki magazeti ya bongo basi ndiyo itatoka hivyo. Unakumbuka hata magazeti yalikuwa yakiandika habari zake na kusema jina liko kapuni ili kusubiria ushahidi wote ukamilike.

Chenge mwenyewe alichanganyikiwa hiyo cordination ya JF na vyombo vya nje na ile story ya The Guardian imemchanganya sana mzee wetu.

Hata hivyo inabidi bado niwape pongezi Thisday kwa kuendeleza story ya Chenge kwa namna ya pekee kabisa!


Maneno yake ya kushitaki vyombo vya habari hayana tofauti na yale ya Boss wake kudai atashitaki kisa wamesema kachukua pesa Iran za Uchaguzi .Hivi ile nayo imeishia wapi vile ? Je huyu Masha na matisho yake ya hivi majuzi kesi kesha fungua ?
 
Ndugu yangu TUAMNDAMANE pole sana kwa uchungu ulionao. Naona mheshimiwa sana INVISIBLE tayari ameweka maoni yako kapuni. Ila naungana nawe kwa hasira na uchungu kwa nchi yetu inavyovurugwa na hawa "WAJANJA" wachache wanaojiita VIONGOZI. Na kwa mtaji huu nadhani hasira za wengi zitafikia kufikiria kufanya yale yaliyo sawa na wanayofanya raia wenye hasira kwenye mitaa ya DAR wanapomkamata kibaka - kumfunga tairi na kumpiga moto. Naombea tusifike hapo, lakini i'm sorry to say that we are heading for that sad but swift street justice.
 
Mkuu Halisi,

Huyu Chenge Mwizi, karudi mwenyewe au karudishwa? Nilitegemea angeelekea USA na muungwana.

Kweli sasa tumemfunga paka kengere, hivi alikuwa na nguvu hata ya kuwaangalia Watanzania usoni?


Lunyungu yuko US na msafara wa Rais kanitonya kwamba the guy has been sent back baada ya kuona mambo yamewaka .JK kasema kawajibu nikija kuwe kumetulia na si zaidi ya hapo .
 
Ndugu yangu TUAMNDAMANE pole sana kwa uchungu ulionao. Naona mheshimiwa sana INVISIBLE tayari ameweka maoni yako kapuni. Ila naungana nawe kwa hasira na uchungu kwa nchi yetu inavyovurugwa na hawa "WAJANJA" wachache wanaojiita VIONGOZI. Na kwa mtaji huu nadhani hasira za wengi zitafikia kufikiria kufanya yale yaliyo sawa na wanayofanya raia wenye hasira kwenye mitaa ya DAR wanapomkamata kibaka - kumfunga tairi na kumpiga moto. Naombea tusifike hapo, lakini i'm sorry to say that we are heading for that sad but swift street justice.
Binafsi naelewa sana kuwa mambo haya yanaudhi mno! Inafikia hatua mtu unatamani kutukana lakini lazima tutambue kuwa maandishi hufunga... Think of it buddy. Pandisha munkari na bamiza keyboard kwa nguvu zote lakini jaribu kukumbuka kuwa maandishi hayo yataendelea kuwepo hata baada ya hasira yako kupoa. Ni suala la muda... Inakera, inaudhi, inatia uchungu, inasababisha hasira sana...
 
Bilioni moja zinaitwa vijisenti....
Nina wasiwasi na akili na huyu AC...is he mentally ok? I am in a big doubt.
USIWE NA WASIWASI NA AKILI YA JAMAA IS CLEARY IN SHOCK, HE WAS NOT EXPECTING THIS HIYO QUOTE BELOW INATOKA GAZETI LA MWANANCHI
Hata hivyo, Chenge ambaye alizungumza mbele ya jopo la waandishi kutoka vyombo mbali mbali vya habari vya ndani na nje ya nchi, huku akitetemeka na kujikanganya katika kauli, alisema tuhuma zilizotolewa dhidi yake, ni nzito kupita kiasi, hivyo, hawezi kuzijibu kwa kukurupuka, badala yake anaviachia vyombo vya uchunguzi vifanye kazi yake.
 
CHENGE CHENGE NGE EEH! Tunakulilia wenye nchi! rejesha HAZINA zetu na uwape taarifa wenzako kuwa tuko nao! "List of shame" na orodha nyingine zitaibuka na kuleta mabadiliko ambayo yalikuwa hayafikiriki siku za nyuma!

JF Oyee eh!
 
Binafsi naelewa sana kuwa mambo haya yanaudhi mno! Inafikia hatua mtu unatamani kutukana lakini lazima tutambue kuwa maandishi hufunga... Think of it buddy. Pandisha munkari na bamiza keyboard kwa nguvu zote lakini jaribu kukumbuka kuwa maandishi hayo yataendelea kuwepo hata baada ya hasira yako kupoa. Ni suala la muda... Inakera, inaudhi, inatia uchungu, inasababisha hasira sana...

Kwanza asnte sana mkuu hawa jamaa wanatupeleka huko street justice kama hakuna aneongea, kilakitu wanabisha kuwa hawajafanya, mkapa kanyamaza tuu watu hawakamatwi wakajibu mashtaka etini bora warudishe hela, watu watakapo chukua sheria mkononi watawashangaa kweli??? najua maandishi hufunga lkn ukweli unabaki palepale kwa mwendo ni wao wenyewe wanatulazimisha tuongee kwa vitendo
 
Maneno yake ya kushitaki vyombo vya habari hayana tofauti na yale ya Boss wake kudai atashitaki kisa wamesema kachukua pesa Iran za Uchaguzi .Hivi ile nayo imeishia wapi vile ? Je huyu Masha na matisho yake ya hivi majuzi kesi kesha fungua ?

Na Nchimbi nae kasha shitaki tanzania daima?
 
attachment.php
 
Jamni hapa sidhani kama Chenge atakuwa na kesi wala nini

(source ThisDay April 17 08)

It has been reported that Chenge’s local legal representative in the matter is Dar es Salaam lawyer Joseph Mbuna, who incidentally is also the father-in-law of Nicholas Mkapa (the son of ex-president Mkapa) and chairman of the board of directors of Kiwira Coal and Power Company Limited.

The formerly state-owned coal mine was sold in 2005 under dubious circumstances to Tanpower Resources Limited, a private company jointly owned by the Mkapa family, former energy and minerals minister Daniel Yona, Mbuna himself, and other closely-connected shareholders.

At the same time, there are reports that Nicholas Mkapa is currently in the employ of the Director of Public Prosecutions (DPP) office - a fact that again raises fears that he may interfere in a potentially-pending prosecution of high-profile individuals linked to the dubious privatization of the lucrative Kiwira mine.

Investigations by THISDAY have established that although Chenge may have not been directly involved in the negotiations with Britain’s arms manufacturer BAE Systems for purchase of the radar, he did give crucial legal advice to the Tanzanian government in favour of the deal.
 
ok, kuna chenge, then who next?
Tunataka sasa mwingine mpyaaaaa!! hebu pekueni huko kwenye kumbukumbu zenu najua mafisadi wako wengi, tuwafichue wote halafu tuanze upya na mafisadi wachanga. (samahani just joking)

NOT FUNNY,ESPECIALLY ON AN EMPTY STOMACH,EVEN IF YOUR POCKETS ARE FULL LIKE THOSE OF THE MAFISADI.
 
Kumbukeni kuwa huyu Chenge ndio mwenyekiti wa kamati ya maadili ya CCM.

Kama mwizi huyu anaweza kupewa nafasi ya kwenda kuangalia maadili ya wenzake ndani ya chama na kuyakemea hivi hapo kuna chama kweli?

Kwa moyo wa dhati kabisa nawaomba wana CCM waliopo hapa wawe wa kwanza kuhoji na hata kumtaka walau aondoke kwenye kamati ya maadili kama mwenyekiti na hata mjumbe kwa masilahi ya taifa.

Nchi hii kuna siku inaweza kulipuka kwenye list yetu ya mafisdadi tunaona timu inapungua kila siu hivyo huienda tukaweka wachezaji wa ziada kama 7 hivi karibuni stay tuned.

Pia tumeweza kumpata kocha msaidizi wa first 11 yetu hivyo huenda tukawa tunashinda kila wakati na kila mechi.
 
tanzania ufisadi hauwezi kwisha yalianza zamani sana lakini hii ya AC inatia aibu kwani inaonyesha ni namna gani watanzania wakikabidhiwa madaraka wanavyotumia vibaya, AC inatakikana kama kweli huu ufisadi kaufanya na afilisiwe

Zungu, tunachokiona hapa ni tip of an iceberg, tumejua ya chenge sbb imetoka UK laiti kama wote wangechunguzwa na kujulikana (which ndocho kifuatacho) kwa mtindo huu hii nchi hapata kalika, I just give u a year hatutakuwepo hapa tulipo maana mengi tutakuwa tumeshayaju
 
Kumbukeni kuwa huyu Chenge ndio mwenyekiti wa kamati ya maadili ya CCM.

Kama mwizi huyu anaweza kupewa nafasi ya kwenda kuangalia maadili ya wenzake ndani ya chama na kuyakemea hivi hapo kuna chama kweli?

Kwa moyo wa dhati kabisa nawaomba wana CCM waliopo hapa wawe wa kwanza kuhoji na hata kumtaka walau aondoke kwenye kamati ya maadili kama mwenyekiti na hata mjumbe kwa masilahi ya taifa.

Nchi hii kuna siku inaweza kulipuka kwenye list yetu ya mafisdadi tunaona timu inapungua kila siu hivyo huienda tukaweka wachezaji wa ziada kama 7 hivi karibuni stay tuned.

Pia tumeweza kumpata kocha msaidizi wa first 11 yetu hivyo huenda tukawa tunashinda kila wakati na kila mechi.
 
Jamani, mimi hizi tuhuma za ufisadi wa watu zimeshanichosha! Hivi ni wapi duniani zaidi ya Afrika ambapo serikali inakuwa na mafisadi na maskendo kibao halafu hakuna hatua zozote za maana zinazochukuliwa dhidi ya watuhumiwa? Hii haingii akilini kabisa hata kwa mimi mwenye akili ya wastani.

Hivi ni wapi duniani penye demokrasia ya kweli ambapo watu watakichagua chama kilichopo madarakani kuendelea kutawala huku viongozi wa serikali yake wakiendelea kuiba (allegedly) na kuitafuna nchi huku wananchi wake wengi wakiishi maisha ya kifukara? Hivi ni watu gani duniani wanaoweza kuwachagua viongozi ambao ni mafisadi na wasiotetea maslahi yao?

Nina mengi ya kusema na nimechoka kusikia watu wakituhumiwa kwa ufisadi na nimechoka kuona watu wakiendelea kuwapigia makofi na vigelegele mafisadi ambao hata hawawajali.

Aaaagh...nimechoka hata kuandika...

NN
Hivi hujui kwa sasa tuko DUNIA YA NNE?!. Maana hataile third world tumeachwa.
 
Haya Bwana...."Andrew John Chenge is Tanzanian politician and a Member of Parliament in the National Assembly of Tanzania. After serving as Attorney-General, he was appointed as Minister of East African Affairs in the Cabinet named on January 4, 2006. He was then appointed as Minister of Infrastructure on October 15, 2006,retaining that post in the Cabinet named on February 12, 2008"

...Kwamba alikuwa mtumishi wa Serikali tangu wakati wa Azimio la Arusha...kwa hiyo vijisent alivyonavyo..kama anavyoviita" ameanza kuvikusanya wakati gani?..wakati wa Ruksa ama wakati wa Uwazi na Ukweli? ...muda wa kufanya biashara ulikuwa saa ngapi na wakuitumikia Serikali ni Saa ngapi..labda ni traveling allowances...kwenu wafuatiliaji wa Account!
 
Kwa kusema hizo hela ni vijisent inaonyesha ni kiasi gani kazoea kuiba na hiasi hicho cha pesa ni sehemu ndogo sana yamapesa aliyonayo. kama kweli hizo hela si za maajabu hebu we chenge niambie kwann uzipeleke kuzihifadhi mbali huko badala ya hapa home zizunguke kujenga nchi kuna mkuna mabenk mengi tuu hapa?
 
Huyu jamaa ana dharau sana yaani nimesoma mahojiano yake na waandishi, billioni moja anaziita "visent"? yaani mi simpatii picha,
 
Chenge kufuru tupu, amiliki bilioni 25

*Amchotea kigogo bilioni moja
*Amwashia indiketa Ben Mkapa


Na Saed Kubenea

WAZIRI wa Miundombinu, Andrew Chenge anaogelea katika utajiri wa zaidi ya Sh. 25 bilioni zenye utata huku Rais Jakaya Kikwete akiendelea kumkumbatia, MwanaHALISI limegundua.

Chenge amekuwa mfanyakazi serikalini kwa karibu miaka 30 na hafahamiki kuwa mfanyabiashara.

Kiwango kinachotajwa ni pamoja na fedha zilizogunduliwa na makachero wa Uingereza katika akaunti zake za nchi za nje.

Fedha zilizoko kwenye akaunti yake ya nchini, Na. 011101006950 katika benki ya NBC Limited, ni Sh. 25,794,805.89 za Tanzania hadi Ijumaa iliyopita, tarehe 11 Aprili 2008.

Katika akaunti yake ya Uswisi, ambako ana akaunti ya fedha za kigeni, Chenge amehamishia dola za Marekani 467,000, sawa na zaidi ya nusu bilioni kwa fedha za Tanzania.

Fedha za Uswisi zimelimbikizwa katika akaunti Na. 030105000364. Zilihamishwa kutoka akaunti Na. 011105011782 ya kampuni ya TANGOLD Limited, tangu 22 Februari 2006 kupitia NBC Limited.

Taarifa za kuaminika ambazo MwanaHALISI imezipata zinasema Chenge ni Mkurugenzi wa kampuni ya TANGOLD Limited ambayo ina dola 12,997,950.84 sawa na Sh. 15 bilioni za Tanzania katika NBC Limited tawi la Makao Makuu.

Aidha, kampuni hiyo inahifadhi Sh. 1,379, 359,367.39 katika akaunti Na. 011103024852 tawi hilohilo la NBC Limited.

Habari tulizopata wakati tukienda mitamboni, zinasema kwamba makachero wa Uingereza wanafuatilia uhalali wa Euro 3 milioni (sawa na zaidi ya Sh. 8 bilioni za Tanzania) zinazodaiwa kuwa Chenge alizipeleka kwenye akaunti zake nje ya nchi.

Taarifa nyingine ambazo hatukuweza kuzithibitisha haraka, zinasema Chenge alihamisha kwa mkupuo dola 600,000 za Marekani kwenda kwenye akaunti ya ofisa mwandamizi mmoja aliyekuwa Benki Kuu miaka kadhaa iliyopita, na ambaye kwa sasa anaongoza shirika la umma nchini.

TANGOLD ni kampuni ambayo inadaiwa kumilikiwa na serikali kwa asilimia 100 na ambayo inadaiwa pia kuwa ndiyo imerithi mali na madeni ya kampuni ya Meremeta Limited iliyokuwa ikijihusisha na uchimbaji madini, Buhemba, mkoani Mara.

Hata hivyo, kuna utata juu ya lini kampuni hiyo ilianzishwa nchini. Wakati aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Nazir Karamagi aliuambia Mkutano wa Tisa wa Bunge kuwa TANGOLD iliundwa mwaka 2006 kupitia Task Force maalum ya serikali, kumbukumbu zinaonyesha kuwa kampuni ilianzishwa mapema 2000 au kabla.


Hiyo inathibitishwa na ukweli kwamba tarehe 1 Januari 2000 walikuwa na akaunti ambayo haikuwa hata na senti moja katika akaunti zake mbili hadi 29 Desemba 2005 zilipoingizwa dola 13,340,168.37.

Fedha hizo zilikuwa zinatoka Hazina kupitia Benki Kuu (BoT).

Kwa akaunti ya fedha za Tanzania, tarehe 1 Agosti 2005, TANGOLD Limited ilichota kutoka Hazina kupitia BoT, Sh. 4,703,221,229.08 kwa hundi Na. 241741 na kufanyiwa uhamisho wa haraka (special clearance).

Chenge, akiwa mkurugenzi, anahusika na uhamishaji, ulimbikizaji na ulipaji wa fedha kutoka akaunti za TANGOLD.

Wakurugenzi na waidhinishaji malipo wengine wa kampuni hiyo ni, Daudi Ballali, Gray Mgonja, Vincent Mrisho na Patrick Rutabanzibwa.

Ballali alikuwa gavana wa BoT, Mgonja akiwa Katibu Mkuu Hazina, Mrisho akiwa Ofisi ya Waziri Mkuu na Rutabanzibwa akiwa Katibu Mkuu Maji na Umwagiliaji.

Matumizi ya fedha kutoka akaunti hizi ambako kuna mkono wa Chenge ndiyo yanaongeza utata.

Kutoka kwenye akaunti ya binafsi ya Chenge, mamilioni ya shilingi yamelipwa kwa watu mbalimbali wakiwa ni pamoja na Janet Mashale, Mary Nchimbi, Mary Chitanda na Livingstone Ruhere.

Wengine ni Getrude Mtiga, Hawa Kiama, Leocardia Kalumuna, Athumani Sheha na David Sanga.

Miongoni mwa waliolipwa ni viongozi wa CCM, waandishi wa habari na wengine ambao hawakuweza kutambulika. Muhimu ni kwamba karibu fedha hizo zote zililipwa wakati uchaguzi wa CCM mwaka jana ambapo Chenge aliwania ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC). Alishinda kwa kura nyingi.

Akaunti ya TANGOLD inaonyesha kutoingiza kiasi chochote cha fedha kwa miaka mitano, kati ya Januari 2000 na Desemba 2005.

Kampuni hiyo, ilichota kutoka Hazina kupitia BoT, tarehe 29 Desemba 2005 dola 13,340,168.37 na 30 Desemba 2005 ilichota kiasi kama hicho.

Siku hiyohiyo, 30 Desemba, kampuni ilihamisha dola 13,340,168.37 na kuzipeleka mahali ambapo hapajafahamika.

Hii ni siku ambayo Rais Kikwete alizindua Bunge jipya mjini Dodoma baada ya kumalizika uchaguzi mkuu na kabla ya kuunda baraza lake la kwanza la mawaziri.

Katika uteuzi wake wa mawaziri, Chenge alipewa uwaziri wa Afrika Mashariki kabla ya mabadiliko yaliyompeleka kuwa Waziri wa Miundombinu na kurejea kwenye nafasi hiyo rais alipounda baraza jipya baada ya kulivunja kufuatia kashfa ya Richmond.

Kwa mujibu wa taarifa ilizonazo MwanaHALISI, TANGOLD ilipokea kutoka kampuni tata ya Deep Green Finance Limited Sh. 39,761,397.98 hapo 8 Oktoba 2005 wakati tarehe 10 Desemba 2005 TANGOLD ililipa Deep Green Sh. 100,940,489.71.

Wakati wa kuchezesha malipo hayo, kulikuwa na uchaguzi mkuu ambapo inadaiwa kuwa fedha hizo huenda ziliingizwa kwenye uchaguzi huo.

Kampuni ya Deep Green ndiyo ilisajiliwa na kampuni ya uwakili ya IMMA ya Dar es Salaam, ambako mtoto wa rais, Ridhiwani Kikwete na mtoto wa Rais Amani Karume, Fatma wanafanya kazi.

Ni kampuni hii mashuhuri ambayo mmoja wa waanzilishi wake ni Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha na mmoja wa mawakili waanzilishi, Protas Mujulizi aliteuliwa kuwa jaji wa mahakama kuu.

Kampuni ya Deep Green ndiyo imetia fora kwa viroja kwa kuonyesha kuwa ilifungua akaunti yake benki siku ya Mei Mosi wakati siyo siku ya kazi.

Tarehe 23 Novemba 2005 TANGOLD iliichotea Meremeta Sh. 555,300,040 ambazo haijulikani ni kwa kazi ipi.

Siku mbili kabla ya uchaguzi mkuu wa 2005, hapo 12 Desemba, TANGOLD iliichotea tena Meremeta Sh. 551,060,000 ambazo haijafahamika zilikuwa kwa shughuli ipi.

Kinachozidisha utata ni kwamba tangu Februari 2006 baada ya kuundwa baraza la mawaziri, akaunti ya TANGOLD ya fedha za kigeni haijalipa wala kupokea fedha yoyote hadi tarehe 31 Machi 2008 huku ikiwa na akiba ya dola 12,997,950.84 (sawa na zaidi ya bilioni 15 za Tanzania).

Wakati hali ikiwa hivyo kwenye akaunti ya nje, akaunti ya ndani ya TANGOLD imefanya malipo yamwisho 6 Juni 2006 ya Sh. 220,980,370. Hadi 31 Machi mwaka huu ilikuwa na akiba ya Sh. 1, 379,359,367.39.

Kiasi cha fedha kilicholimbikizwa kwenye akaunti za TANGOLD ambako wakurugenzi ni pamoja na Chenge na watumishi wengine wa serikali, zinalingana na kiasi ambacho serikali inapigia magoti kutoka kwa wafadhili.

Hivi sasa Chenge anachunguzwa na makachero wa Uingereza na Tanzania kuhusiana na uwezekano kuwa alipokea hongo katika biashara ya kununua rada ya kijeshi kutoka kampuni ya BAE Systems ya Uingereza.

Alipoulizwa kuhusu hali hii ya uchotaji fedha na ulimbikizaji nje, Dk. Willibrod Slaa, mbunge wa Karatu amesema, “kama hizi fedha ni za serikali kwa nini serikali igeuke ombaomba wakati zimelala benki?”

Kwa nini umma usiamini kuwa fedha hizo zimo mikononi mwa mtandao wa kifisadi, anahoji Dk. Slaa na kuongeza, “Kigugumizi cha serikali kinatoka wapi hapa wakati fedha hizi zinatosha kujenga madarasa 400 ya sekondari au wastani wa shule moja kwa kila mkoa.”


Follow the money....source http://www.halihalisi.co.tz/08/04/16/
 
Back
Top Bottom