Mwafrika wa Kike
JF-Expert Member
- Jul 5, 2007
- 5,185
- 64
Jamani, mimi hizi tuhuma za ufisadi wa watu zimeshanichosha! Hivi ni wapi duniani zaidi ya Afrika ambapo serikali inakuwa na mafisadi na maskendo kibao halafu hakuna hatua zozote za maana zinazochukuliwa dhidi ya watuhumiwa? Hii haingii akilini kabisa hata kwa mimi mwenye akili ya wastani.
Hivi ni wapi duniani penye demokrasia ya kweli ambapo watu watakichagua chama kilichopo madarakani kuendelea kutawala huku viongozi wa serikali yake wakiendelea kuiba (allegedly) na kuitafuna nchi huku wananchi wake wengi wakiishi maisha ya kifukara? Hivi ni watu gani duniani wanaoweza kuwachagua viongozi ambao ni mafisadi na wasiotetea maslahi yao?
Nina mengi ya kusema na nimechoka kusikia watu wakituhumiwa kwa ufisadi na nimechoka kuona watu wakiendelea kuwapigia makofi na vigelegele mafisadi ambao hata hawawajali.
Aaaagh...nimechoka hata kuandika...
Ngabu,
inasikitisha sana lakini taratibu watu wanapata elimu na wanajifunza cha kufanya. Cha muhimu hapa kwanza ni kuwachukia hawa watu.
Mimi sicheki na mafisadi, siongei nao nicely wakati najua kuwa ni mafisadi this much. Call me Makathi lakini ninachukia hawa mafisadi with a passion.
Magazeti muhimu na makini kama Thisday na mengine yatawafuata hadi mwisho. Magazeti ya kiswahilil kama raia mwema, mwanahalisi na Tanzania Daima yataandika habari zao. Wananchi wakijua kila kinachofanyika watafanya the right thing inshallah!