The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Tuhuma za Chenge katika Gazeti la Guardian hizi hapa

BAE corruption investigation switches to Tanzania·

Ahsante sana kwa hii habari ndugu yangu Bubu Msemaovyo, ningependa kukuarifu tu kuwa habari hii tayari imeshawekwa kwenye ile thread ya Chenge basi Jiuzulu. Usivunjike moyo na endelea kutuletea habari nzuri kama hizi.
 
Kwa maneno na ndoto za kuitoa CCM madarakani sioni kama tutapata uhuru wetu.

Tanzania tulikwenda kupigana Msumbiji, Zimbabwe, A.kusini na kwingineko ili kuzigomboa nchi hizo na kusahau kwamba tunatakiwa kupigana ndani ya nchi yetu ili kupata uhuru wa kweli.
Nionavyo mimi ni kwamba sasa imefikia point ni bora kuanza kuchinjana kuliko kufanyana mabwege. Tuchukue sheria mikononi kuwashughulikia mafisadi wote kwani uwezo huo tunao. Mafisadi ni wezi kama wezi wengine ambao tunawapiga na kuwachoma moto, hivyo tunaweza kabisa kuwapiga na kuwachoma moto mafisadi moja badala ya mwingine. Sasa ni muda muafaka wa kuchukua silaha na kuingia mitaani maana serikali iliyopo madarakani ni bubu, kiziwi na kipofu.
 
kafara hiyoooooooooooooo inanukiaaaaaaaaaaaaaaa
yetu macho ............
bado machoni pa wazazi wangu nitamkumbuka na nkumpongeza daima DK SLAA MTU WA WATU....NANI ANGEJUA AU KUWEZA KUFICHU UFISIMAJI KAMA HUU KAMA SI KUANZA KWA HUYU JAMAAAAAAAA
WANA AMANI WOTE WAIPENDAO SHERIA YA BWANA WALA HAKUNA LA KUWAKWAZA..............
 
Jamani Kuna Tetesi Nimesikia Huko Dodoma, Nimesikia Kuwa Chenge Yuko Mbioni Kubwaga Manyanga Saa Yoyote (kujiuzuru)na Kwamba Tusikilize Muda Wowote Kuanzia Sasa Tutasikia Teyari, Na Kwa Sababu Hili Swala La Chenge Ni Kubwa Muungwana Ameamua Kuhairisha Safari Yake Ya Uk Na Kisha Kamtuma Shein.stay Tunned
 
Hapo awali kidogo yapata miaka miwili hivi ilianza kashfa ya Fredrick,mara mkubwa wake-Benjamini,ikafata ya Bank kuu na waliotajwa wakiongozwa na Daudi,Raisi kwenye tamko lake wakati akimwajibisha Daudi sehemu ya taarifa ilisomeka MHESHIMIWA RAISI AMEKASILRIKA NA KUSIKITISHWA SANA NA UBADHILIFU WA EPA waliotajwa na padr slaa,Richmond nayo ikaitikisa nchi na hatujaona hatua kutoka kwa wakubwa na wala hatujaskia kama pia Raisi alikasirika,ila inawezekana alimskitika swahiba wake kwa yaliyomkuta.Hili la Bwana Andrea sijui litakuwa na kishindo saana kimaamuzi,atakaa kimya kama wenzake na kama ilivyo ada ya wabongo watalisahau na hasa likitokea janga lingine kama hilo.Nafikiri sasa Daudi akirudi hapa dar yaweza wasimuguse kabisa.Kwenye hili mchungaji Kristofa sijamsikia labda anawasiliana na wanasheria wake kuona kama kuna kesi ya kujibu.Sijui tutafikiria kwa sauti mpaka lini

mungu wabariki watz
 
Pili kaona noma kuhusu maswali ya waamdishi wa habari kuhusu hiyo ishu ndo maana kakimbia

Mkuu kweli inawezekana Anaogopa kuadhirika. lakini si wananchi hata wa kule Mbeya walimutahadharisha kuhusu huyu FISADI?

Wanasema za Mwizi arobaini, huyu Mwizi ni lazima twende hata jimboni kwake kuhakikisha anaondoka na kukimbilia kule marta, au kwenye visiwa alikoweka mabilioni.

Inabidi anyanganywe Pass ili uchunguzi ufanyike alikopata hizo pesa.

Pamoja na kupewa Mlungura, Inawezekana anashirikiana na majambazi, maana mabenki yaliyovunjwa bongo na watu kutokomea ni mengi mno.
 
Chenge anarudi leo usiku au mapema alfajiri. Kuna kila dalili anaweza kuamua kuweka manyanga chini hasa baada ya kuambiwa uzito wa suala hili. Wanamsubiri mzee arudi tu.

thanks
 
Hivi karibuni tumesoma mengi kuhusu waziri Chenge ambaye amepatikana na mamilioni kwenye akaunti ya nje yaani off shore account. Sasa nimeanza kusikia tetesi mitaani (unproven)ya kuwa yuko chini ya ulinzi na anafanyiwa interrogation. Lakini official report zinadai yuko China na rais. Naomba mwenye data za uhakika atueleze waziri Chenge yuko kweli kwenye msafara?
(Natumaini nimeweka thread kwenye forum sahihi!)
 
Trivia

Heading imekaa kama "Arctic Monkeys to release third album this year"
 
Mimi nafikiri Chenge hana aibu angelikuwa na aibu angetangaza kabla hajarudi bongo. Bi Senti 50 ebu sema anatokea wapi maana nina hamu sana ya kumpokea Airport angalau nimpige picha tu huyo FISADI.
 
Hii inaweza kuwa hela ya IPTL, ndio maana kasema kuwa haihusiani na RADAR, na ndio maana kampasia Mtu wa TANESCO pia.Na Zingine za Meremeta
 
Hapa wa kushtakiwa ni CCM, kwa wananchi sio mahakamani!

Kitila, kuwashtaki kwa wananchi na hawa jamaa ambao ni wezi wa kura na pia vyombo vya dola vyote wamevithibiti sidhani kama kutasaidia lolote. Sasa hivi CCM wamehusishwa na wizi wa mabilioni ya BoT ambayo yaliingia kwenye chama hicho ili wazitumie kwenye uchaguzi mkuu wa 2005. Hii ni kwsi nzuri sana kuifungua kama tutaweza kujiorganize kama Watanzania walio ndani na nje ya nchi ili kujua ukweli hasa kuhusu mabilioni yaliyokupuliwa pale EPA na kuingia ndani ya mfuko wa CCM. Hili litaiabisha CCM zaidi na pia linaweza kabisa kufunua uozo mwingine mzito zaidi. Bank account zote za CCM zikaguliwe na vitabu vyao pia vikaguliwe ili kupata ukweli wa huu ufisadi wa EPA ambao wahusika hawajaguswa hadi hii leo.
 
UK pound 5 milion sawa karibu na US$ 12.5 milion.
New jersey US $1 milioni hapo bado uswiz,amstedam. duu

Watu kama hawa ni wakupiga risasi tu.
 
Da ebwana kweli Pembe la Ng'ombe halifichiki. Hii Mijamaa inamaana haina hata Haya halafu bado linang'ang'ania Madaraka. Tunakwenda wapi jamani? Mafisadi mmekula vya kutosha tunaomba Mtuachie Nchi yetu jamani. Na ninauhakika itakuwa pesa ya Rada tuu.
 
Mkuu Kakindomaster Anganza Kunyanganywa Vithlani Mpaka Uk Wanawaletea Ushaidi Mnashindwa Kumnyanganya Passport Ije Kuwa Huyu Mbongo Manzese Kwake Chooni...
Uushauri Tusiwe Na Pressure Ya Kutegemea Mapya...hakuna Kitakachofanyika Juu Yake Na Hakuna Kesi
 
Hii inaweza kuwa hela ya IPTL, ndio maana kasema kuwa haihusiani na RADAR, na ndio maana kampasia Mtu wa TANESCO pia.Na Zingine za Meremeta

Mkuu huyu jamaa usikute amechanganya kila Mkataba, sasa bomu limelipuka, mayai aliyotaamia naona sasa yanaelekea kuonekana, hiii issue ikifanywa vizuri sana inaweza kukamata wengi sana. Unaona na huyo wa tanesco, ingelikuwa serikali inafanya kazi(Siyo wale wale) tayari hapa tungerudisha mabilioni serikalini.

Lakini ujanja ujanja utasikia kajiudhuru wanachagua wakuu wa vitengo kuchunguza na ndio mwisho wa maneno.
 
Hili ndilo swali ninalojiuliza hapa mkuu halisi!
Kama Chenge ana nafasi kubwa hivi ndani ya ccm na wao ccm hawana cha kufanya dhidi yake, je kuna mtu bado anataka baraza hili liwe na imani na ccm kama chama?

CCM kukubalika bila kuburuza wananchi ni ndoto maana viongozi wao asilimia kubwa wana asili ya UFISADI, wale wazuri wote wamezuliwa mambo na kusongea mbali na chama.

SIfa nzuri ili uwe kiongozi wa CCM lazima upende UFISADI, Watanzania kweli tuna kazi.

Angalia nitaje wachache tu, RA, EL, CHenge, Karamagi, MKapa,hawa ndio tano bora....,

Hawa ndio walio na maamuzi ya chama wengine ni kunyosha mikono juu tu. Wakulu wana kazi ya kusafisha chama.
 
Back
Top Bottom