The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Mimi nafikiri tumesema mengi sasa ni wakati wa JK kuact maana tangia amemteua uwaziri tena watu wanapiga kelele lakini kafunga masikio.
 
Kwa yote yasemwayo, Chenge ni mtu wa kusifiwa!!

Alipoingizwa kwenye List of Shame :- hakuhamaki, hakukanusha, hakutishia kwenda mahakamani, hakukosa usingizi, alire-tain post yake, hakwenda Maelezo kujieleza, na hata alipoulizwa juu ya hela zote hizo aliishia kudai hazihusiki na BAE!!

Huu ndio UJASIRI WA KUFISADI.

Siamini kuwa ali-engage a prominent Lawyer from USA kwa ajili ya vi-pound hivyo. Uwezekano mkubwa ni kwa ajili ya kulinda a diversified investments portfolio ambayo haijulikani.

By the way, fedha hizi zilioredheshwa kwenye daftari la Ofisi ya Maadili?
 
Niliwahi kusema kipindi cha nyuma kuwa huyu jamaa hafai hata kidogo. Niliwahi kumtaja yeye pamoja na wenzake kama Meghji, Mungai n.k. Sasa nafurahi kuona kuwa siri zake, moja baada ya nyingine zimeanza kulipuka. That's nice. Na bado, tunataka zote zitoke. Hawawezi kuigeuza nchi yetu kuwa kampuni yenye mashareholders wachache tu (i.e. wana mtandao). Nchi yetu ni mali ya kila raia halali wa nchi hii. Wasilete mchezo na kodi zetu. Watu tunakatwa kwenye mishahara mpaka tunatamani kulia. Ukija kwenye magari bado wanakata, ukienda kwenye fuel wanakamua, ukija kwenye kodi zingine, wanamaliza. Then ukigusa madini na neema nyingine wanajimegea wao na watoto wao. Mpaka waishe, mwaka huu.
 
Haya mambo ya kulindana, wakicheza na hao kina JK tunawang'atusha kwenye viti. Na hii ni kwa watu kusali usiku na mchana, kama hawajakosa hivyo viti, hatujui wananyang'anywa vipi na Mungu but I believe lazima kitokee kitu. Manake wameanzwa wengine then mwishoni kabisa anapatikana source au mzembe/wazembe walioachia kwa makusudi kabisa na kwa interest zao wenyewe, ufisadi ufanyike bila hofu.
 
Naomba kuwauliza ndugu zangu, kulikuwa na idea ya kumwandikia barua Fisadi Andy au Jak kuhusiana na hatua tunayotaka huyu fisadi achukue au achukuliwe, kulikuwa na hitimisho la ile suggestion?
 
Naomba kuwauliza ndugu zangu, kulikuwa na idea ya kumwandikia barua Fisadi Andy au Jak kuhusiana na hatua tunayotaka huyu fisadi achukue au achukuliwe, kulikuwa na hitimisho la ile suggestion?

Sijui hitimisho lilikuwaje lakini nafikiri JK haitaji kundikiwa barua kwa kuwa nina uhakika anaingia Boardin hapa na kuona maoni ya watu, unajua watu hawawezi kukulupuka na kuanza kumsema mtu furani bila kuwa na tetesindo maana waswahili wakasema "Kila lisemwalo lipo kama halipo basi laja" hatutaki tukimshauri akulupuke no he should take his time to investigate lakini la chenge lilikuwa wazi sana, kila mtu alikuwa analiona kama linavyooneka la Mkapa
 
Sijui hitimisho lilikuwaje lakini nafikiri JK haitaji kundikiwa barua kwa kuwa nina uhakika anaingia Boardin hapa na kuona maoni ya watu, unajua watu hawawezi kukulupuka na kuanza kumsema mtu furani bila kuwa na tetesindo maana waswahili wakasema "Kila lisemwalo lipo kama halipo basi laja" hatutaki tukimshauri akulupuke no he should take his time to investigate lakini la chenge lilikuwa wazi sana, kila mtu alikuwa analiona kama linavyooneka la Mkapa



Tuendelee kusema huku tukisubiria kuchukuliwa kwa hatua zinazostahili.
 
Uchunguzi wa nini tena wakati ushaidi umepatikana?. Wananchi wanatka kuona vitendo vinachukuliwa kwa watu kama hawa na akina Mkapa alike

Uchunguzi, i meant alivyopekuliwa nyumbani kwake na ofisini kwake,hio ni tosha hata kama ushahidi umeshapatikana...tayari kishadhalilishwa.
 
Yule mtu anaconfindance kubwa sana hataenda mahakamani wala hatafukuzwa kazi, na hamtamfanya kitu maana yeyey ni engineer wa ufisadi wote wa mkapa na pesa iliyomweka madarakani JK hivyo watamlinda kwa nguvu zote maana wakimwaga mboga yeye atamwaga ugali wakose wote.
 
Mtakuja sikia aliuza ngombe za urithi huko bariadi na kampuni aliyeuzia hizo ngombe waliweka hizo pesa kwenye ac yake huko uingereza
 
CHENGE MJUMBE WA KAMATI KUU YA CHAMA CHA MAPINDUZI NA MJUMBE WA KAMATI YA MAADILI YA CCM. Kamati ya Maadili ndiyo iliyopitisha waraka uliowasilishwa katika NEC ya Butiama iliyopaswa kujadili UFISADI wa EPA na Richmond????? Sasa ndio huyooooooooo!!!! Ataendelea katika kamati ya Maadili na Usalama ya CCM?
 
Waheshimiwa wana JF ni wakati muafaka sasa kwa watanzania kubadilika na kutumia taaluma zetu kutokomeza ufisadi huu.
Napenda kupata ushauli wa kisheria kutoka kwa wanasheria wetu, je hapa Chenge hana kesi ya kujibu? na kama ipo ni utalatibu upi utumike kumfikisha mahakamani hata kama ataendelea na wadhifa wake wa uwaziri? Kama mwananchi wa kawaida ninayo haki ya kumfunguria mashita kwa kuhujum uchumi wa nchi?
Naombeni mawazo yetu ili niweze kushugurikia huyu fisadi mkubwa.
 
CHENGE MJUMBE WA KAMATI KUU YA CHAMA CHA MAPINDUZI NA MJUMBE WA KAMATI YA MAADILI YA CCM. Kamati ya Maadili ndiyo iliyopitisha waraka uliowasilishwa katika NEC ya Butiama iliyopaswa kujadili UFISADI wa EPA na Richmond????? Sasa ndio huyooooooooo!!!! Ataendelea katika kamati ya Maadili na Usalama ya CCM?

Hili ndilo swali ninalojiuliza hapa mkuu halisi!
Kama Chenge ana nafasi kubwa hivi ndani ya ccm na wao ccm hawana cha kufanya dhidi yake, je kuna mtu bado anataka baraza hili liwe na imani na ccm kama chama?
 
Waheshimiwa wana JF ni wakati muafaka sasa kwa watanzania kubadilika na kutumia taaluma zetu kutokomeza ufisadi huu.
Napenda kupata ushauli wa kisheria kutoka kwa wanasheria wetu, je hapa Chenge hana kesi ya kujibu? na kama ipo ni utalatibu upi utumike kumfikisha mahakamani hata kama ataendelea na wadhifa wake wa uwaziri? Kama mwananchi wa kawaida ninayo haki ya kumfunguria mashita kwa kuhujum uchumi wa nchi?
Naombeni mawazo yetu ili niweze kushugurikia huyu fisadi mkubwa.

Mkuu Chibingwa wazo lako ni zuri sana lakini kumbuka "Pembe la ng'ombe halifichiki" Huko mahakamani utaenda kama nani, kama Chibingwa?
 
Ishitakiwe CCM kwa wananchi maana wao ndio mahakama ya mwisho kabisa, ukumbuke hata ukiamua kwenda mahakamani majaji waliteuliwa na wao hivyo kesi ya nyani uwezi kumpelekea Ngedere ukapona.
 
Ndugu wana JF hoja yangu ya msingi hapa ni Bwana Andrew Chenge "akaunti yake yake kukutwa na dola za kimarekani milioni moja"
- hii akaunti iko nje ya nchi
- iko katika visiwa visivyo maarufu saana duniani
- sheria zake za fedha ni dhaifu sana.
Sasa basi kwa wanasheria hatunahoja ya msingi hapa kushitaki Chenge atueleze au awaeleze watanzania hizo hele kazipataje na kwanini kaziweka nje ya nchi?
naombeni ushauri wenu wa kisharia tafadhari.
 
Ni kweli chibingwa inabidi wanasheria watusaidie, maana hii mijitu imezidi kuiba.
 

KUMBE KWELI KAZI IPO,YAANI DUH! VYOMBO VYETU VYA HABARI VIPO WAPI???? KWA HIYO HAPA NASHAWISHIKA NIWE NASOMA NEWS PAPER ZA NJE
NDIO KUNA HABARI NYINGI ZA KWETU ZA MUHIMU.

HAWA WATU KUMBE NI WAIZI EEEH YAANI SASA HAPO,MOYO UNANIUMA MNO MAANA HAWA WATU WAMEKUWA MASHETANI KABISA MAANA KUTOKANA NA MAMBO WANAYOFANYA KUNA WATU WANAJIUA KWA AJILI YAO KUTOKANA NA UGUMU WA MAISHA UNAO SABABISHWA NA HAWA VIONGOZI WETU.SASA HIYO ELA YA RADA JAMANI PESA YETU,
HAWA WATU WATA PIGWA NA LAANA JAMANI MAANA SASA HIVI WATU WENGI WANA JIUA KWASABABU YA UGUMU WA MAISHA SERIKALI IMEKUWA SIO MSAADA TENA JAMANI.

TUFANYE NINI NA SISI AKILI TUMEPEWA!!!??? KAMA WANAFANYA HIVI NA SISI TUFANYEJE ILI ELA ZETU ZIRUDI?
 
Back
Top Bottom