The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

In other words Chenge amekuwa detained UK?


Aahh, Icadon unakosea bana. Chenge anasaidia upelelezi, hajawekwa ndani. Wanaowekwa ndani ni vibaka wa Samora avenue, Mtaa wa Kongo na kule Mwananyamala.
Unamshushia hadhi huyu Mtemi wa Vijisenti, Chief Mnyantuzu!
 
kuwa washinikize kuundwa kamati ya Bunge kumchunguza Chenge na kazi zote alizofanya kama Mwanasheria Mkuu. Taifa lipewe tathmini ya kina ya yote aliyoyafanya ambayo yanaonekana wazi kuwa yalikuwa si kwa manufaa an masilahi ya Taifa bali ni Uhujumu kuangamiza Taifa.

Mkuu Kishoka,

Heshima mbele, unajua unahitaji kuziona hizi DVD za bunge, ndio utaelewa kuwa wabunge wetu wanachukua talking points zao nyingi sana kutoka hapa JF, yaaani haya yote uliyoyasema yamerudiwa na wabunge kama yalivyo kwenye mjadala wa Lowassa kujiuzulu, na exactly kama tulivyosema hapa,

Nimemalizwa na Ndesamburo, ambaye yeye amerudia maneno yote tuluyoyasema hapa kwenye topic ya viongozi wa China na sheria zao jinsi zilivyo kali, anawaaambia Lowassa na mafisadi wenziwe kuwa ingekuwa China wote wangepangwa mstari na kupigwa risasi kwenye public, kwa hiyo binafsi I am very much at peace kuwa hapa hatupotezi muda na sikutegmea kabisa of how much political influence sasa hivi JF tunai-command as far as hoja nzito is concerned.
 
Bado ninauliza,

extradition kati ya UK na TZ ilisainiwa lini/

je na sisi tukimtaka Hillary Benn watakubali kumtoa?


ES

huna haja ya kuedit kitu wewe weka mkanda kama ulivyo
 
Bado ninauliza,

extradition kati ya UK na TZ ilisainiwa lini/

je na sisi tukimtaka Hillary Benn watakubali kumtoa?


ES

huna haja ya kuedit kitu wewe weka mkanda kama ulivyo

Kwanini usimpigie Kikwete simu umuulize hilo swali?
Ama kwasababu Chenge yuko huko Uingereza and so unataka nini?
 
Ama ni kweli Chenge yuko huko Uingereza kutafuta kambi nyingine ya kujisafisha baada ya ile ya uzaramo na usukuma huko Mara VS Dar es salam?
 
Bado ninauliza,

extradition kati ya UK na TZ ilisainiwa lini/

je na sisi tukimtaka Hillary Benn watakubali kumtoa?


ES

huna haja ya kuedit kitu wewe weka mkanda kama ulivyo

GT naona unataka kutoka nje ya mada suala sio tukimtaka Hillary Ben,Swali ni lini Serikali yetu ilijaribu kumtafuta, achilia mbali kumuulizia mtu aliyedhulumu mali ya Wadanganyika?balali pia anahitaji extradition?
 
GT naona unataka kutoka nje ya mada suala sio tukimtaka Hillary Ben,Swali ni lini Serikali yetu ilijaribu kumtafuta, achilia mbali kumuulizia mtu aliyedhurumu mali ya Wadanganyika?balali pia anahitaji extradition?

Mweleze huyu maana naona inaelekea kisomo chake badala ya kumfanya awe na "Data" kimemfanya "Adate!"
 
interesting....unfortunately naona hatutaki kukubali kuwa hiii issue watakao faidika ni malawyers lakini hilo naona baadhi yenu hamtaki kulikubali kuwa they make a living out of legal loopholes

 
interesting....unfortunately naona hatutaki kukubali kuwa hiii issue watakao faidika ni malawyers lakini hilo naona baadhi yenu hamtaki kulikubali

Sasa si ndio maana!?
Hata kama na wewe ni lawyer kwanini usiwasiliane nae uende ukamwakilishe badala ya kujaribu kuhadaa wananchi?
 
...To me, hii kesi ya BAE/SFO inaonyesha wazi hata kama ni tuhuma, kuna ulazima wa Serikali na hasa Bunge kuunda tume/kamati ya Bunge kuchunguza kazi zote alizozifanya kwa niaba ya Serikali.

...washinikize kuundwa kamati ya Bunge kumchunguza Chenge na kazi zote alizofanya kama Mwanasheria Mkuu. Taifa lipewe tathmini ya kina ya yote aliyoyafanya...

Mchungaji, Jina lake lihimidiwe!

Mimi sipendi hizi kamati za Bunge. Ubaya wa kamati, kwanza, hazina nguzu ya kubana watu kisheria. Product yake, at the end of the day, ni mapendekezo tu. Mazao ya kazi ya kamati inategemea mapenzi, discretion, ya Rais kutekeleza mapendekezo. Na Kikwete anajulikana kwa kukalia ripoti. Ilikuwa ni bahati, bahati mno Kikwete kukubali Serikali yake ivunjwe na kamati ya Mwakyembe. Commentators wengi wamesema hii ilitokea kwa sababu Kikwete alikuwa anataka kubadilisha Waziri mkuu to begin with. Kuna kina Sitta mpaka uruke viunzi vyao kabla ripoti haijasomwa, na kina Pinda wako in charge pale Bungeni, watu ambao wamesha foreclose mashitaka ya kina Mkapa kabla hata hayajaletwa. Siku ikija ripoti, wataleta mizengwe tu.

Isitoshe, hizi kamati nazo saa nyingine zinakuwa extrajudicial. Mwakwembe kuna Due Process fulani alizipinda makusudi ili ripoti iwe nzito. Ki ufupi hakumsikiliza Lowassa. Ilikuwa sawa Lowassa kuondoka kwa sababu anajulikana sio msafi, lakini Mwakyembe, kubali usikubali, alimfanyia drive-by.

Tulazimishe vyombo vilivyopo, vyombo vinavyo bana Kisheria na vinavyo banwa na Sheria za Taratibu za Uchunguzi wa Jinai, ili tusitegemee discretion ya Kikwete, na Sitta na Pinda, kuleta mashitaka. Kamati haziwezi kushitaki mtu.

Zaidi ya Tume ya Kulinda na Kutetea wala Rushwa, na Tume mfu ya Maadili, kuna idara nyingine ya kujitegemea chini ya Hazina, Financial Intelligence Unit, ambazo zote zinatakiwa ziwe na nguvu kuzidi hizi kamati za discretion. Na tusisahau, at the end of the day ni kazi za Polisi, na Director of Criminal Investigation, na Director of Public Prosecution kuchunguza huu udhalimu.

Economic Crimes Act of 1984

21.-(1) The investigation of all economic offences reported to the police shall be conducted by police officers, with the assistance of such public officials or category of public officials as may be designated by the Directorof Public Prosecutions after consultation with the Director of Criminal Investigation


Kwa hiyo kazi za hii Mikamati na Mitume na mi Miidara na Wakurugenzi wote ni duplicate tu, na wanapoteza resources na focus.

Hizi Kamati na Tume Msalie Mtume sio za kuzitegemea hizi. Tuimarishe vyombo vya dola.
 
Mkuu, thank you so much for keeping us informed with those nyetis. If this is true then it is encouraging news as our efforts to fight mafisadi are showing positive results.

Mungu ibariki Tanzania na Watanzania wote wasiokuwa mafisadi.
 


je na sisi tukimtaka Hillary Benn watakubali kumtoa?

GT uko huko njia rahisi ni ku lobby hayo magazeti ya UK na ukamwaga data za huyo Hillary Benn. Usitegemee, na hili unalijua wazi kuwa hakuna nchi yeyote ya third world inaweza kukandamiza hawa ma G8 unless una visima vya mafuta
 
Aahh, Icadon unakosea bana. Chenge anasaidia upelelezi, hajawekwa ndani. Wanaowekwa ndani ni vibaka wa Samora avenue, Mtaa wa Kongo na kule Mwananyamala.
Unamshushia hadhi huyu Mtemi wa Vijisenti, Chief Mnyantuzu!

Videole viliteleza mkuu, I meant anaisaidia SFO...Ila mimi niko interested na baada ya uchunguzi kukamilika whats next, yatakuwa mambo ya amerudisha asilimia kubwa ya hela na tumuache mzee wa watu apumzike?
Kwenye hili na lile la Richmond nimewadharau kabisa PCCB...
 
Sasa UK kafikia wapi? Bellmarsh, Kensington au Nigerian Millionaire's row?


Nafikiri kwa kuwa bado yeye ni shahidi basi atapangishiwa hoteli za kawaida tu.

Jamaa wana pesa ya kulipia kila kitu katika masuala kama haya. Paundi ipo mkuu usiwe na wasiwasi.

Lakini angekuwa ni mtuhumiwa basi angefikia Paddington au Charing Cross ambavyo ni vituo vikuu kwa London kama pale Cetral yetu Dar.

Halafu Belmarsh ni kwa wale watu hatari kiusalama na ni jela, Kensington ni kwa bibi hakuna vurugu na hio ya mwisho...
 
Mkuu Es ahsante kwa point nyingi ulizoweka lakini kuna walakini kidogo!!!

Issue ya Chenge kwenda London haina uhusiano wowote na SFO. Narudia, Chenge yuko London kwa mambo binafsi na SFO walishamalizana naye.

SFO hawajaribu kuisaidia TZ in any way or shape, the investigation is against BAE only. The link to TZ ends with Vithlani and it is true Vithlani had some wire transfers to mzee wa Visenti na ndio sababu ya SFO kumkomalia. Now to prove that the said money was BAE money is where Chenge atatupiga goli sababu SFO hawatakuwa na maelezo kuhusu hela za Chenge wao watawabana BAE na corruption.

Now ni aibu kwa sisi watanzania na viongozi wetu kusema eti tunasubiri uchunguzi wa SFO?? This is insane!! SFO hawachunguzi kwa kina ni viongozi gani wa TZ walipewa rushwa, wao wanachunguza kama BAE walimpa rushwa Vithlani na yeye akawapa viongozi wa TZ. Wakiprove hilo, then wanawabana BAE.

Now link ya Vithlani to TZ leaders hilo swala lilitakiwa libebwe na Usalama, DCI, Mwanasheria Mkuu wa Tanzania, DPP na kamati za bunge.

Hapa tunachezewa shere!!

Ni hayo tu wakuu.
 
Sasa UK kafikia wapi? Bellmarsh, Kensington au Nigerian Millionaire's row?

None of those I'm afraid. A man of ways and means like Chenge will not accept anything less than a kingsize bed at Buckingham Palace to lay his one-million $$$ Harvard-educated ass. 😀
 
Back
Top Bottom