Uchaguzi 2020 TCRA na Mitandao ya simu mtuombe radhi kwa SMS hii. Mmetoa namba za wananchi kwa wanasiasa? Mmefanya makosa makubwa!

Huu mchezo hawajaanza Leo, Vodacom na Airtel ndo zao. Wamempa access JPM ya database za wateja wao.

Natamani watu waende mahakamani kwa hili ili haya makampuni yalipishwe fidia ya kutosha.
Unataka watu ndo waende wakushtakie? Mtumeni lissu aende kama jambo dogo kama hilo nalo mnashindwa kufungua file, eti nyie ndo mnategemewa kuingia barabarani.
 
Huko ni kuingilia uhuru wa watumiaji wa simu, wanajua kabisa wateja wao watakuwa na itikadi tofauti kwanini watume meseji za kumpigia kampeni mgombea wa CCM?

Kuna wajinga watasema ni haki yao kwasababu CCM wamelipia, watambue CCM wamewalipa hao wenye makampuni ya simu hawajawalipa watumiaji, haya mambo ya kujipendekeza kwa CCM yakome, wanastahili kushtakiwa.
Natamani mnaopinga wote muhame nchi muende mkaishi Congo au muende Rwanda mkaishi huko kwa muda fulani.
 
Hili jambo ameniambia wife leo yeye ametumiwa tena limesomeka jina ambalo si lake.

Nikajisemea ole wao wanitumie msg kama hizi. Kwanza ni usumbufu na kutukosea adabu, hivi inakuwaje wanadhani ya kuwa kila mtu ni mpiga kura ? Sisi wengine tunakuwa na vitambulisho vya kupiga kura kuepuka usumbufu tu katika harakati zetu.
Ukitumiwa utafanya nini!!?
 
Huwa mnasoma Terms & Conditions za hiyo mitandao kabla ya kujiunga? Vipi privacy policy huwa mnasoma pia? Kila kitu wameandika kwenye zile karatasi za simcard na kwenye websites zao. Kitendo cha kununua simcard zao na ku-activate maana yake ume-AGREE terms na conditions zao so umekubaliana na meseji zozote za promo watakazokutumia.

NB: Kabla haujaenda kuwashtaki soma vigezo na masharti ya mtandao husika usije ukageuziwa kibao ukafungwa wewe badala ya kampuni.
True
 
Tulizeni munkar, leo mmepokea kutoka CCM ndio mnataka kwenda mahakamani afu wengine wanasema eti kapewa database :D

acheni utani, hizi meseji za matangazo zipo nyingi sana tu tunatumiwa za makampuni mbalimbali kila uchwao wakitusumbua tu.
 
Huwa mnasoma Terms & Conditions za hiyo mitandao kabla ya kujiunga? Vipi privacy policy huwa mnasoma pia? Kila kitu wameandika kwenye zile karatasi za simcard na kwenye websites zao. Kitendo cha kununua simcard zao na ku-activate maana yake ume-AGREE terms na conditions zao so umekubaliana na meseji zozote za promo watakazokutumia.

NB: Kabla haujaenda kuwashtaki soma vigezo na masharti ya mtandao husika usije ukageuziwa kibao ukafungwa wewe badala ya kampuni.
Mkuu haiko hivyo, taarifa zako zilizoko kampuni za simu ni siri ya wewe na kampuni.Taarifa hizo zikitolewa kwa mtu mwingine bila ridhaa yako ni kosa.Kampuni itatakiwa kutoa taarifa hizo serikali kwa special purpose.kilichofanyika ni makosa.Kitendo cha makampuni ya simu kutoa access ya database za wateja wao kwa wagombea urais au vyama vya siasa ni kosa.Nakuhakikishia kama customers wakalalamika kwa wingi wao na kufungua kesi ni shida
 
Tulizeni munkar, leo mmepokea kutoka CCM ndio mnataka kwenda mahakamani afu wengine wanasema eti kapewa database :D

acheni utani, hizi meseji za matangazo zipo nyingi sana tu tunatumiwa za makampuni mbalimbali kila uchwao wakitusumbua tu.
Haahaa mkuu hujui.bila database kutolewe hizo SMS zisingeingia kwa wateja kamwe.watalaamu wa it watakubaliana nami
 
Back
Top Bottom