TANZIA: Afisa wa TAKUKURU auawa

TANZIA: Afisa wa TAKUKURU auawa

i love wild parties, lakini vitu vya moto vinatakiwa kutumika kwa uangalifu sana, si inatakiwa aelekeze juu sasa yeye alifanyaje? RIP afisa
 
Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na mtumishi mwenzake kwa bahati mbaya walipokuwa katika sherehe za kumuaga mwenzao katika hotel ya South Beach iliyopo Kigamboni jijini hapa Dar es salaam. Risasi hiyo ilimpata mhanga huyo katika kichwa na kumuua hapohapo. Innalillah wayna ilahy rajiun

Mmh...bahati mbaya?tena kichwani dah inahitajika maelezo ya ziada!RIP Afisaa
 
Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na mtumishi mwenzake kwa bahati mbaya walipokuwa katika sherehe za kumuaga mwenzao katika hotel ya South Beach iliyopo Kigamboni jijini hapa Dar es salaam. Risasi hiyo ilimpata mhanga huyo katika kichwa na kumuua hapohapo. Innalillah wayna ilahy rajiun
Yaani Mnaenda sherehe na Bunduki? Halafu sherehe yenyewe ya kuaga Mtu, wacheni maskaha bana.

Bunduki tokea lini ikashikwa wakati mdomo wake unaangalia juu? Jamaa walipanga kumwaga mkuu wao kwa kumla risasi ya kichwa.

Huyo aliye uwa ana cheo gani na amesha wekwa lupango?
 
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imethibitisha kuwa mtumishi wa taasisi hiyo, Bhoke Ryoba ameuawa kwa kupigwa risasi jana usiku.

"Tumekuwa tukipokea simu nyingi kutoka kwa watu mbalimbali wakihitaji kufahamu ukweli kuhusu tukio la kupigwa risasi kwa Mtumishi wa TAKUKURU - Bhoke Ryoba. Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Dkt. Edward Hoseah, anapenda kutoa ufafanuzi kuhusu tukio hili kwamba ni kweli Mtumishi Bhoke Ryoba amefariki dunia jana usiku - Jumamosi tarehe 22/12/2012 baada ya kupigwa risasi," imesema taarifa iliyotolewaleo na makao makuu ya TAKUKURU.

Taarifa hiyo imesema, uchunguzi wa Polisi kuhusu chanzo cha tukio hilo bado unaendelea.
 
Risasi za BAHATI MBAYA kwa kweli zinajua kulenga vichwa, dahhhh.....

Wanyamwezi tunaimba "Ohh Ohhh Nsasi zyabelwa mitwe..... Nsasi, ahhh, Nsasi, zyabela mitwe....." ambao ulikuja ukawa wimbo wa "ohh TANU/KANU yajenga nchi....." Aliimba Mirambo enzi zake miaka ya 1880's hadi leo.....

RIP Marehemu Takururu worker.
 
ilikuwaje
usalama wa bunduki unafunguliwa
risasi inaenda chemba
taiga anabonyeza
risasi inatoka
bahati mbaya kweli?
hafai kupewa au kumiliki siraha
uzembe wa hali ya juu

  • Bastola inalenga yenyewe kujielekeza kichwa cha mhanga huku mmiliki ameshika chupa ya bia hana habari bastola inafanya vitu vyake.
  • Mara mlio "Paaaaaaaaaaaa" Watu wote wanashangaa, bastola inamshitua mmiliki wake "ni mimi usishangae"
  • Anasema jamani ni bahati mbaya.
  • Sote tunaamini ni bahati mbaya.
 
Ofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Bhoke Ryoba, amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na ofisa mwenzake wakati wakisherekea ufukweni mwa Bahari ya Hindi jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Afisa Uhusiano wa Takukuru, Ryoba alifariki dunia juzi baada ya kupigwa risasi.

“Tumekuwa tukipokea simu nyingi kutoka kwa watu wakihitaji kufahamu ukweli wa tukio la kupigwa risasi kwa mtumishi Bhoke Ryoba, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk. Edward Hoseah, anapenda kutoa ufafanuzi kuhusu tukio hili kwamba ni kweli alifariki dunia Jumamosi (juzi) usiku baada ya kupigwa risasi,” ilieleza kwa kifupi taarifa hiyo.
 
Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi!
 
Rest In Peace, Bhoke mke wangu, nitakukumbuka daima ula ujue bado tuko pamoja.

Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na mtumishi mwenzake kwa bahati mbaya walipokuwa katika sherehe za kumuaga mwenzao katika hotel ya South Beach iliyopo Kigamboni jijini hapa Dar es salaam. Risasi hiyo ilimpata mhanga huyo katika kichwa na kumuua hapohapo.

Innalillah wayna ilahy rajiun

[/LEFT]
 
Five Ws + one H ziko wapi?
Who?-Bhoke Ryoba, Ofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru),
What?-amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na ofisa mwenzake
Where?-ufukweni mwa Bahari ya Hindi jijini Dar es Salaam.
When?- Jumamosi (juzi) usiku wakati wakisherekea
Why?-missing!
How?-Missing!

RIP Bhoke Ryoba!.
Kama ni ndugu na Ayoub-Pole Ayoub!.
P.
 
Hizi habari roborobo bana, tunashindwa tuchangie nini!
hebu uliyeleta uzi toa habari kamili! nashangaa comments kibao
wakati haina mashiko, very stupidi indid!

Mjanga punguza dharau basi na kebehi
 
Last edited by a moderator:
Yaani Mnaenda sherehe na Bunduki? Halafu sherehe yenyewe ya kuaga Mtu, wacheni maskaha bana.

Bunduki tokea lini ikashikwa wakati mdomo wake unaangalia juu? Jamaa walipanga kumwaga mkuu wao kwa kumla risasi ya kichwa.

Huyo aliye uwa ana cheo gani na amesha wekwa lupango?

alijisalimisha polisi baada ya tukio
 
Hii habari mbona ina utata. Mara mwenzake mara watu wasiojulikana..................!!!

Baadaye ofisa habari wa Takukuru Doreen Kapwani alifafanua kuwa ofisa huyo mchunguzi alifikwa na umauti wakati anajumuika na marafiki zake katika moja ya tafrija iliyokuwa ikifanyika katika eneo la Kigamboni.

Alisema akiwa katika hafla hiyo, ghalfa walitokea watu wasiojulikana na kumiminia risasi hadi kufa.

"Hawa watu walimvamia Ryoba aliyekuwa kwenye sherehe moja na kumshambulia kwa risasi na kisha wakatokomea kusikojulikana," alisema na kuongeza:

"Watu hao hawakutambulika kwa kuwa baada ya kutekeleza azma hiyo walitoweka haraka na kutokomea."

Alipotakiwa kueleza pengine kumekuwepo matukio yoyote katika siku za hivi karibuni yanayoweza kusababisha tukio hilo, Kapwani alijibu "ni mapema mno sasa kudadisi suala hilo."

Kapwani alisema Ofisi ya Takukuru kwa sasa haiwezi kueleza chochote kwani tukio hilo limeripotiwa polisi kwa uchunguzi zaidi.

Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleman Kova alipotakiwa kuelezea hatua zilizochukuliwa na jeshi hilo baada ya tukio hilo, alisema kuwa hangeweza kuzungumzia chochote kwa vile alikuwa nje ya ofisi.
 
Back
Top Bottom