TANZIA: Afisa wa TAKUKURU auawa

TANZIA: Afisa wa TAKUKURU auawa

duh... Ujinga umecost life ya mtu....Kwani kushangilia lazima kupigana risasi?

Vingi Viulizo.....

R.I.P Afisa Takukuru
 
uhai auwez kurudi tena,harafu ni bahat mbaya,ilikuaje akaifyatua,nina maswali mengi nikiwauliza mtaona mi ni police,ila huo ni uzembe
 
Takukuru wanaruhusa ya kutembea na silaha?

Raia wote wanaruhusiwa kutembea na silaha kwa masharti yaliyowekwa kisheria. Hitaji la kutembea na silaha ni kubwa zaidi katika taaluma zinazoitaji kujilinda kama vile biashara na uandishi wa habari. Wafanyakazi wa TAKUKURU wapo katika taaluma onayohitaji kujilinda. Lakini taarifa hii inatia shaka hapakuwa na bahati mbaya.
 
walikuwa kwenye sherehe au vitani? Shereheni na mabastola ya nini?
 
afisa wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa, takukuru amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na mtumishi mwenzake kwa bahati mbaya walipokuwa katika sherehe za kumuaga mwenzao katika hotel ya south beach iliyopo kigamboni jijini hapa dar es salaam. Risasi hiyo ilimpata mhanga huyo katika kichwa na kumuua hapohapo. Innalillah wayna ilahy rajiun

funguka chanzo nini hadi jamaa akawasha moto
 
It happens jamani manake hata mimi ilishawahi kunitokea bahati nzuri nilikuwa nimeelekeza chini

Mkuu.. Bunduki zote zinakuwa na safety pin.. Ikiwa off hata ufanye haiwezi hata ciku moja kufyatuka risasi.. Inapokuwa on ndo hapo ukigusa trigger kidogo ngoma inatoka.. Sasa ukisema it happens maana yake sio bahati mbaya.. Ni uzembe na makusudi maana ni lazima uliweka on kwa maana ya risasi zitoke.. Ndo ya Ditopile haya..
 
It happens jamani manake hata mimi ilishawahi kunitokea bahati nzuri nilikuwa nimeelekeza chini

kumbe na wewe takukuru eeh? Nna kesi na nyie, nitakusaka nikupe rushwa unisaidie kuimaliza shemeji.
 
Bahati mbaya?? Mpaka anaset bullet into chamber and pull the triger ni very sensitive process.....
 
Hiyo silaha alikuwa nayo mkononi au ilikuwa kwenye holster? Kama ni mkononi, inilikuwa yanini ilihali walikuwa kwenye sherehe? Na kama silaha ilikuwa kwenye holster iliwezaje kulenga kichwa? Ikumbukwe kuwa kama bastola ipo kwenye mfuko wake iwe kwapani au kiunoni, mdomo unaelekea chini.
 
Mkuu.. Bunduki zote zinakuwa na safety pin.. Ikiwa off hata ufanye haiwezi hata ciku moja kufyatuka risasi.. Inapokuwa on ndo hapo ukigusa trigger kidogo ngoma inatoka.. Sasa ukisema it happens maana yake sio bahati mbaya.. Ni uzembe na makusudi maana ni lazima uliweka on kwa maana ya risasi zitoke.. Ndo ya Ditopile haya..

si ndo mi nashangaa.....labda huenda wanapewa silaha bila mafunzo lakini otherwise ni maksudikally
 
Jamani afisa wa watu amepigwa na kitu chenye ncha kali kichwani kwa bahati mbaya!poleni sana wafiwa
R.I.P pccb officer
 
1. RIP !
2. Polisi wanasemaje: ni uzembe au mauaji yasiyokusudiwa?
3.Kama kawaida ni risasi iliyomuua au kitu chenye ncha kali ?
4 . Mtuhumiwa alikuwa na kibali cha kubeba silaha muda na mahali alipokuwa ?
5 Alikuwa amelewa au hajalewa?
6. Mtuhumiwa ana historia ya tabia gani hasi ?
7. Marehemu ameacha mjane au watoto ?
8. What is the way forward- mambo yataisha hivihivi au kuna hatua ambazo zinachukuliwa ?
 
Mmmmmhh!! Kweli ni majaliwaliwa yake MUNGU kuiona mwaka!

Uchunguzi wa kina inastahili!

Marehemu BWANA ampe pumziko la milele shambani mwake!
 
Chadema watakuwa wanahusika na walirusha kitu chenye ncha. Kali hewani.
Upumzike kwa hali uliyoiandaa ukiwa hai!!
 
Back
Top Bottom