TANZIA: Afisa wa TAKUKURU auawa

TANZIA: Afisa wa TAKUKURU auawa

Hakuingia kwenye mtego wa majambazi kweli huyu
maana hawa watu bwana
 
Uchunguzi umefanywa na taasisi gani mpaka kukonclude ni "bahati mbaya"?

Sent from my GT-P7500 using Tapatalk 2
 
Wafanyakazi wa TAKUKURU, aliyefyatua risasi, afisa wa TAKUKURU, aliyepigwa risasi kichwani, Afisa Mchunguzi wa TAKUKURU. Then bahati mbaya? Kusema kweli inaniwia vigumu sana kuamini kwamba ni bahati mbaya, uchunguzi wa kina ufanyike.

Inasikitisha sana, poleni wafiwa.
 
Ka nzi kanaonyesha marehemu alikuwa anatoka ndani ya maji wakati matakukuru wawili wakirushiana risasi kwa masihala na punde marehemu kupatwa na risasi ya paji la uso na kudondokea ndani ya maji. Kuna cover up inataka kufanyika kuonyesha marehemu alishambuliwa na majambazi
 
mpaka sasa ni mmoja kati ya hao matakukuru 'amekamatwa'. Marehemu alikuwa ameacha wageni na kwenda kuungana na wenzake kwa ajili ya kuwaaga matakukuru walioamishwa vituo.
 
wabongo wengi hawajui bunduki. wanadhani inafyatuliwa kama unavyowasha swichi ya taa ya umeme, yaani unabonyeza tu mara moja. bunduki ina hatua hizo alizotaja jamaa yetu hapo. Huwezi kuwa kwenye sherehe alafu una bunduki imefunguliwa usalama labda kama ulikuwa na kusudio la kuifyatua.

Nadhani budnuki hiyo ilikuwa ni bastola. Silaha za siku hizi, hapa naongelea bastola, si rahisi mno kupiga risasi kwa bahati mbaya kwa vile nyingi zina usalama zaidi ya mmoja, mara nyingi zinakuwa tatu. Ya kwanza ni ile ambayo unaifunga na kuifungua, ya pili ipo kwenye trigger (unahitaji nguvu kiasi ukivuta trigger kuiondoa hiyo kwa kubonyeza trigger) na ya tatu ikpo katika kitako cha bunduki (butt). Hiki unakiondoa kwa namna unavyoishikilia bastola, huwa unasukuma plate maalumu jinsi unavyoshikilia kile kitako kwa nguvu. Bila kufanya hivyo bunduki haitapiga risasi au risasi ita jam katika chamber.
 
niko hapa msibani ni simanzi. Marehemu anamtoto wa chini ya mwaka mmoja. Analia anamtaka *****. Usiombe.

Kumbe ni kweli mimi nilifikiri ni kama ile ya Mzumbe University Graduatioan ambayo baada ya page zaidi ya 10 za R.I.P tulikuja gundua kuwa ni uzushi. Msiba ni wapi, Na je seniority list kati ya marehemu na jamaa aliyevyatua kitu chenye ncha kali imekaa aje? SO SAD to both families
 
Mods, hapa siwaelewi. Ama mnamalizia Wikiendi!


Topic: Msiba: Afisa wa TAKUKURU auawa


icon1.png
Polisi, Jwtz wajeruhiwa na wacongoman ktk ziwa Tanganyika
 
Wanakwenda picnic na Ak 47 (silaha)? How?
 
Mkuu ungetuambia anaitwa nani..., me nimepata jina moja anaitwa Bhoke na alikuwa na cheo cha mchunguzi wa kawaida.

RIP Bhoke

kwaheri mpendwa eeeh.kapumzike kwa aman Mungu alipanga ufe kwa style hii kwa sabbu alikuwa na uwezo kw kukukinga lkn aliruhusu iwe
 
It happens jamani manake hata mimi ilishawahi kunitokea bahati nzuri nilikuwa nimeelekeza chini

Yaan bahati mbaya inakuja na aura???? Y did you target the earth surface then????

Haya maneno muwaambie wasiojua silaha kabisa........google on accidental bullet utajua uzembe ulioufanya
 
Yaan bahati mbaya inakuja na aura???? Y did you target the earth surface then????

Haya maneno muwaambie wasiojua silaha kabisa........google on accidental bullet utajua uzembe ulioufanya

alikuwa akitaka kupiga risasi hewani kutishia vibaka.
 
alikuwa akitaka kupiga risasi hewani kutishia vibaka.


So he released the bullet on sitting position while the deceased was standing...........

Unajua maana ya kupiga risasi hewani lakini.....upper arm na ribs zinakuwa katika angle gani??????
 
Hizi bahati mbaya ndizo zinazotumaliza,utasikia watu wanasema siku yake ilishafika kweliii????kila kitu kwetu ni bahati mbaya na utashangaa na wafanyakazi wenzake wakamtetea
 
Haka kataasisi kanatakiwa marekebiho ya haraka kabla mambo hayajawa mabaya zaidi
 
kweli siku yako ikifika imefika tuu, yani risasi ijipige yenyewe au ikupate wewe na ufariki? ishi kama hii ilimpata kijana mmoja musoma yeye alipigwa na rfk yake bahati mbaya wakati wanatest bastola aliyonunua(marehemu).

Please be careful na silaha
 
Takukuru wanaruhusa ya kutembea na silaha?

Mkuu Maafisa wa TAKUKURU (hasa wachunguzi) wanaruhusa ya kutembea na Silaha. Wakikubamba na rushwa ukaamua kutimua mbio, wanakuwasha risasi.
 
Hizi habari roborobo bana, tunashindwa tuchangie nini!
hebu uliyeleta uzi toa habari kamili! nashangaa comments kibao
wakati haina mashiko, very stupidi indid!
 
kweli siku yako ikifika imefika tuu, yani risasi ijipige yenyewe au ikupate wewe na ufariki? ishi kama hii ilimpata kijana mmoja musoma yeye alipigwa na rfk yake bahati mbaya wakati wanatest bastola aliyonunua(marehemu).

Please be careful na silaha

Hii ni murder case hakuna jingine pale. Manslaughter inaweza kuja baadaye baada ya uchunguzi wa kina kukamilika. Pistol unayo mfukoni kwenye koti au kiunoni ukiwa kwenye party. Unaamua kuichomoa kutoka sehemu hiyo uliyoihifadhi. Halafu unai cock (kupeleka risasi kwenya chamber tayari kwa mapambano. baada ya hapo unaelekeza mtutu kwa watu. Halafu unatoa usalaama wa triger (safety triger lock). Baada ya hapo unabonyeza hiyo triger ukiwa umeelekeza mtutu kwenye kichwa cha mtu (? rafiki yako) na risasi inafanya kazi yake kama ilivyoelekezwa. Halafu useme ni bahati mbaya risasi imetoka yenyewe tu toka mfukoni mwako na kumpata huyo jamaa kichwa (automatic head seeking missile/bullet). Haiwezekani kabisa. Hata hizi simu zetu za Kichina wanazosema ni fake (mimi siamini kama ni fake kwani zinafanya kazi vizuri tu na zinadumu muda mrefu) huwa hazijipigi tu zenyewe zikiwa mfukoni, sasa sembuse bastola hata kama ni feki ya Kichina inayotumiwa na TAKUKURU? Tena mtumiaji akiwa ni well trained person millitary wise? Hakuna jaji ambaye atamwachia kuwa hana hatia ya mauuaji ya kukusudia hata kama yule aliyemkusudia kumuua risasi ilimkosa na ikaenda kumuua mtu mwingine.
 
Back
Top Bottom