TANZIA: Afisa wa TAKUKURU auawa

TANZIA: Afisa wa TAKUKURU auawa

KAUMZA

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2010
Posts
699
Reaction score
241
Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na mtumishi mwenzake kwa bahati mbaya walipokuwa katika sherehe za kumuaga mwenzao katika hotel ya South Beach iliyopo Kigamboni jijini hapa Dar es salaam. Risasi hiyo ilimpata mhanga huyo katika kichwa na kumuua hapohapo.

Innalillah wayna ilahy rajiun
Ofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Bhoke Ryoba, amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na ofisa mwenzake wakati wakisherekea ufukweni mwa Bahari ya Hindi jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Afisa Uhusiano wa Takukuru, Ryoba alifariki dunia juzi baada ya kupigwa risasi.

"Tumekuwa tukipokea simu nyingi kutoka kwa watu wakihitaji kufahamu ukweli wa tukio la kupigwa risasi kwa mtumishi Bhoke Ryoba, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk. Edward Hoseah, anapenda kutoa ufafanuzi kuhusu tukio hili kwamba ni kweli alifariki dunia Jumamosi (juzi) usiku baada ya kupigwa risasi," ilieleza kwa kifupi taarifa hiyo

 
hiyo bahati mbaya inajua kulenga. R.i.p marehemu. mia
 
  • Thanks
Reactions: awp
Kichwani,kwenye sherehe,kwa bahati mbaya?
Ni uzembe mtupu na si ajabu huyo askari hajapata mafunzo ya siraha ,na kama alipata basi ni mzembe na hastahili kukaa na siraha,hv anajua thamani ya uhai wa mtu?
 
Mmnh, !!! maswali mengi kuliko majibu
 
Bahati mbaya kwa misingi gani? ina maana hiyo risasi imetoka yenyewe au mhusika kafyatua risasi? Nna maswali mengi kichwani mpaka nakosa majibu.

RIP afisa.
 
ilikuwaje
usalama wa bunduki unafunguliwa
risasi inaenda chemba
taiga anabonyeza
risasi inatoka
bahati mbaya kweli?
hafai kupewa au kumiliki siraha
uzembe wa hali ya juu

Kulenga majambazi inakuwa ngumu ila za bahati mbaya ndio zinafanya kazi
 
Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na mtumishi mwenzake kwa bahati mbaya walipokuwa katika sherehe za kumuaga mwenzao jijini hapa Dar es salaam. Risasi hiyo ilimpata mhanga huyo katika kichwa na kumuua hapohapo. Innalillah wayna ilahy rajiun

Mkuu ungetuambia anaitwa nani..., me nimepata jina moja anaitwa Bhoke na alikuwa na cheo cha mchunguzi wa kawaida.

RIP Bhoke
 
Uchunguzi wa kutosha ufanyike.
Mara nyingi hawa maaskari wanauana kwa kudhamiria.

Pumzika kwa amani marehemu.
Poleni wapendwa wake.
 
Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na mtumishi mwenzake kwa bahati mbaya walipokuwa katika sherehe za kumuaga mwenzao jijini hapa Dar es salaam. Risasi hiyo ilimpata mhanga huyo katika kichwa na kumuua hapohapo. Innalillah wayna ilahy rajiun

Bahati mbaya!

We ni mahakama?
 
It happens jamani manake hata mimi ilishawahi kunitokea bahati nzuri nilikuwa nimeelekeza chini

Hatukatai. Ila kwa bahati mbaya ya aina yako ina maana marehemu angekuwa amelala sakafuni au sijui amechuchumaa!
 
Back
Top Bottom