TANZIA: Afisa wa TAKUKURU auawa

TANZIA: Afisa wa TAKUKURU auawa

Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na mtumishi mwenzake kwa bahati mbaya walipokuwa katika sherehe za kumuaga mwenzao katika hotel ya South Beach iliyopo Kigamboni jijini hapa Dar es salaam. Risasi hiyo ilimpata mhanga huyo katika kichwa na kumuua hapohapo.

Innalillah wayna ilahy rajiun

[/LEFT]
Jamani kwenye sherehe ,tena sherehe za wakubwa kuna sababu gani ya kubeba silaha ,au walikuwa wanaenda kuwinda Ruaha National Park,sio bure kuna namna,na hiyo namna inaelekea kwenye mgongano wa kimasilahi
 
Kwa hiyo aliyeua amesamehewa?

Kiwango chako cha kuelewa ni cha fb, unategemea kupata majibu gani hapo!!! Tuhuma ya mauaji hata wiki moja haijaisha mtu unajiita ''GREAT THINKER'' unauliza swali la mtoto wa chekechea!!! naomba niishie hapo labda wako wenye majibu ya swali lako.
 
Naona mambo ya Marekani na uhuru wa silaha yameshahamia na kwetu.....huyo jamaa hakuanza kuua mamake nyumbani sababu wabongo kwa kuiga hawajambo....


Najua watakuja sema alikuwa napiga risasi juu kwa bahati mbaya risasi ikaenda juu kisha ikarejea chini na kumpata marehemu sehemu za kichwani...

Na Jeshi la polisi watasema lazima walipize kisasi
 
Kweli chuki mbaya.Hawa watu wa takukuru wameuana wenyewe kwa wenyewe kwenye pombe zao sasa mlitaka usalama wa taifa ukataze watu kunywa pombe.Mfumo kristo unawapunguzia watu uwezo wa kufikiri.Magufuli kaenda kwa Laila kenya kelele.Sasa mbowe kaenda kimyaaa.

Nafikiri utakuwa umepumua sasa
 
Maneno ya Mwanakijiji ni haya hapa chini:Mi sikuona maji taka hapa.

"Kwamba sasa afisa wa TAKUKURU Bhoke Ryoba ameuawa na "watu wasiojulikana" mbele ya kadamnasi ya watu inaendeleza kile ambacho wengine tumekisema kwa miaka sita sasa - kuna tatizo la msingi la muundo na utendaji katika Usalama wa Taifa. Ninakumbushia tu."

Sasa tafakari maneno yaliyo katika Blu na ujiulize ni mara ngapi matukio makubwa yamefanywa hapa Tanzania na yakawa yamefanywa na "watu wasiojulikana." Kesi inayoongelewa inahusu tukio kubwa ambalo limefanywa na watendaji katika Serikali, kuleta maana kuwa kuna criminals wapo ndani ya Serikali ya nchi yetu.

Criminals huwa hawaruhusiwi kufanya kazi katika serikali, na zuwio hili hufanywa na serikali makini kwa kufanya Vetting ya watendaji. Jukumu la Vetting ni jukumu la taasisi ya Data collection kuhusu watu wataofanya kazi zoooote katika serikali. Hata wafagizi lazima wawe vetted kwa sababu unaweza kusababisha shida kubwa sana katika serikali kutokana na kuweka criminal kwenye nafasi ya mfagizi kwenye ofisi ya serikali. Accurate Data Collection for Decision Making ni kazi ya Intelligence. Hapa Tanzania watu wa aina hiyo hatuna kwa sasa, and that should explain why very stupid decisions are made on occassions hapa nchini.

Hawa watu wasiojulikana walifikaje hapo kumuua afisa wa Takukuru bila kujulikana? Wewe unaona kuna maji taka katika hii hoja hapo? na unapata sababu kushangaa "sijui kama unafahamu majukumu ya usalama wa taifa? Si lazima kuchangia kila thread mkuu. Kama kitu hukielewi soma tu uelimishwe na wengine katika michango yao.
:smile:fuatilia update ya habari ya tukio hilo. sio kwamba wahusika hawajulikani mbona wanafahamika na wako mahabusu. tatizo mnadakia mambo bila kufanya tafiti!
 
Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na mtumishi mwenzake kwa bahati mbaya walipokuwa katika sherehe za kumuaga mwenzao katika hotel ya South Beach iliyopo Kigamboni jijini hapa Dar es salaam. Risasi hiyo ilimpata mhanga huyo katika kichwa na kumuua hapohapo.

Innalillah wayna ilahy rajiun

[/LEFT]

Ilikuwaje hadi silaha itolewe hadharani
 
:smile:fuatilia update ya habari ya tukio hilo. sio kwamba wahusika hawajulikani mbona wanafahamika na wako mahabusu. tatizo mnadakia mambo bila kufanya tafiti!

Asante kwa taarifa mkuu. Wasomaji wengi wa habari huwa tunatoa hukumu ya tukio kutokana na kile kinachojulikana awali, na hivi ndivyo wengi tulivyofanya katika tukio hili. Ukitaka kuliita hilo kudakia mambo uwe huru kufanya hivyo. Ila ujue ya kuwa katika kila habari ambayo wajuzi huita developing story huwa panakuwapo mambo mapya. Sidhani kama taarifa za awali zilikuwa na habari ya watu kuwa mahabusu. So? Asante kwa taarifa yako hii mpya ambayo sikuwa nayo awali. Nani yupo Mahabusu Mkuu? Ni mfanyakazi wa kitengo chochote cha Serikali? au ni raia kama mimi.... uchunguzi wa awali unasema nini kuhusu safety pin ya revolver kujiachia? na wanasema nini kuhusu pistol kutoka ilipokuwa na kuchagua kichwa cha marehemu badala ya mguu? You seem well informed. tujuze mkuu...
 
Hii ni murder case hakuna jingine pale. Manslaughter inaweza kuja baadaye baada ya uchunguzi wa kina kukamilika. Pistol unayo mfukoni kwenye koti au kiunoni ukiwa kwenye party. Unaamua kuichomoa kutoka sehemu hiyo uliyoihifadhi. Halafu unai cock (kupeleka risasi kwenya chamber tayari kwa mapambano. baada ya hapo unaelekeza mtutu kwa watu. Halafu unatoa usalaama wa triger (safety triger lock). Baada ya hapo unabonyeza hiyo triger ukiwa umeelekeza mtutu kwenye kichwa cha mtu (? rafiki yako) na risasi inafanya kazi yake kama ilivyoelekezwa. Halafu useme ni bahati mbaya risasi imetoka yenyewe tu toka mfukoni mwako na kumpata huyo jamaa kichwa (automatic head seeking missile/bullet). Haiwezekani kabisa. Hata hizi simu zetu za Kichina wanazosema ni fake (mimi siamini kama ni fake kwani zinafanya kazi vizuri tu na zinadumu muda mrefu) huwa hazijipigi tu zenyewe zikiwa mfukoni, sasa sembuse bastola hata kama ni feki ya Kichina inayotumiwa na TAKUKURU? Tena mtumiaji akiwa ni well trained person millitary wise? Hakuna jaji ambaye atamwachia kuwa hana hatia ya mauuaji ya kukusudia hata kama yule aliyemkusudia kumuua risasi ilimkosa na ikaenda kumuua mtu mwingine.


unachoongea ni kweli kabisa ila kwa TZ hii ni ngumu sana haki ya mtu kupatikana, tayari kuna habari kuwa marehemu aliuawawa na watu wasiofahamika walivamia sherehe amabao inasadikiwa ni vibaka, ´kwa hiyo kuna namna wanataka kuficha kuwa marehemu aliuawawa na mfanyakazi mwenzie either kwa makusudi au bahati mbaya.
Naipa pole sana familia ya marehemu Bhoke
 
sijaelewa kitu hapa

huyo dada alikua amelala na jamaa bichi au??

au ndio zile za kazi na dawa?
 
mkuu naamini unamjua mwanakijiji post zake.... mara nyingi ni za chuki na uchochezi ila wajinga wengi huwa wanamshabikia bila kujielewa.

haya hayajafika mlangoni kwako... hapo ndipo utajua nini kinaongelewa... rukaruka na kandya sana sasa ila law ya karma huwa haichezi mbali
 
Usalama wa Taifa unahusika vipi hapo? Unajuaje labda ugomvi wa mapenzi?

Aliyekwita mwanakijiji hakukosea.

Huwezi kuelewa uhusiano wake kama wewe uko kwenye kitengo cha kimachinga huko usalama wa taifa
 
Back
Top Bottom