Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

TanzaniaNjema

Nakubaliana nawe kuwa katika nyakati hizi ambazo dunia iko katika mkondo wa mtandao na miundo mbinu, ni fikira za kijinga kusema kuwa ni lazima tusubiri miaka 50 au tupitie zama za mapinduzi ya kilmo, kisha ya viwanda, hata vita kuu mbili za dunia na vita Baridi kwa Tanzania na Afrika kuwa na mazingira bora ya demokrasia na ufanisi.

Ni upupu mtupu, ndio naonga kauli ya Dr. Sheni ambayo ni ya kimapinduzi na ni mawazo ya kipekee ambayo si kawaida kutoka kwa watawala wa Kiafrika.
 
Tanzanianjema,
Kwanza imenigusa sana kwamba ulikuwa mwanafunzi wa Prof. Chachage. I never met the man lakini katika nafasi ya kazi zangu tuliwahi kuzungumza mara kadhaa kwa simu na alikuwa mmoja kati ya Watanzania wachache niliowaheshimu. Having said that labda niongezee kuwa ningetamani kuona tuna Ma-Chachage hamsini au mia moja pale nyumbani na hasa katika nafasi za uongozi. Lakini unfortunately tulio nao ni wale aliowaita makuhadi wa utandawazi. Kwa muda mrefu sana CCM imekuwa the only party. Na inavyoonekana hivi sasa kuna waliotumia hiyo kwa manufaa yao wenyewe. Na unfortunately hao ndio sasa wamepenyeza kwenye nafasi za uongozi. Ni jambo la kusikitisha sana kumsikia Katibu mkuu wa chama akiwaambia wanafunzi kuwa ukijiunga na CCM utapata cheo cha ukuu wa wilaya etc. Hii ndiyo mindset iliyoenea katika CCM. Ukiwauliza CCM leo wanaamini kitu gani as far as itikadi is concerned watakuangalia kama wewe ndiye mwenda wazimu. Ndio maana unawakuta wote wanafukuzia kuuponda upinzani. CCM ya leo siyo TANU ya enzi za Mwalimu. Ukiwauliza ni kitu gani wanachomwenzi Mwalimu watakuambia umoja na mshikamano. But Mwalimu was bigger than that. Mwalimu contributed more than that. Mwalimu was anti-imperialist lakini hawa viongozi wa leo wa CCM wameukumbatia ubeberu ali mradi wanakula nao sahani moja. CCM leo imebaki a gargantuan mammoth without direction.Ukiniuliza kama kuna demokrasia leo Tanzania jibu langu ni hapana. Kuna utawala wa elites for the elites and the rich na hawa wanafanya kila mbinu kulinda nafasi zao kwa kutumia chama kinachoitwa CCM.
 
Striking the right balance between freedom and power is essential paradox of governing. Wa-Tanzania, ni lazima tusimamie sera ya kuwa na serikali ambayo itakuwa yenye ubano wa nguvu zake au madaraka yake kwa kukabidhi madaraka kwa majority will na uhuru wa binafsi.

Halafu pia ni vyema mara kwa mara tukawa na peaceful civil protests kwa ajili ya kuiamusha serikali isilale, kwa sababu ni muhimu that the tree of our liberty be refreshed from time to time, with the peaceful civil disobedience.

Ingawa pia ni muhimu kwa serikali kuwa na madaraka kamili ili kutimiza maamuzi yake ya kuwahakikishia wananchi wake political na economic well being, lakini ni vyema power hiyo ikawa limited, badala yake wananchi ndio wawe na maamuzi ya mwisho juuu ya their political and public policies kupitia kwa wawakilishi wao.

Tanzania tunajitahidi, lakini tatizp kubwa tulilo nalo bado ni wananchi wasioelewa, kwa maneno mengine bado tuna wananchi ambao bado hawana political knowledge ya kutosha, sasa ni wajibu wetu kama taifa kukazania elimu!
 
Mzee Jasusi,

Maneno mazito, kuna moja muhimu ambalo hata mimi linanichanganya, la CCM kuwakumbatia mabeberu na msimamo wa Mwalimu dhidi ya mabeberu, maana binafsi nilifikiri na I might be wrong kuwa hilo ndilo hasa liliomfanya Mwalimu aondoke mapema uongozini, kwa sababu alifikia mahali ambapo hakuwa na alternative baada ya Cold War kuisha, hapakuwa na pa kukimbilia tena kupata misaada iwapo angeendelea kukataa kuwakumbatia mabeberu au?


Na ninajua kuwa Mwalimu hata alipong'atuka, bado alikuwa anaendelea kushauri na hata kuiongoza CCM kwa pembeni, sasa what happened? maana alianza kuliona boti likitetereka na hasa kwenye hili la msimamo wa itikadi?

Ahsante Mzee!
 
Mabeberu ndo akina nani?
Una maana wawekezaji?

CCM inatakiwa kufuta yale maneno ndani ya katiba kwamba bado inajenga siasa ya ujamaa.

Wawekezaji tunawahitaji. Wenyewe pekee yetu tulishindwa kujenga nchi tangu tulipo watimua mwaka 1967 Azimio la Arusha

Au Vipi?
 
Haya yote uliyoyasema Mzee ES ndio tunayoyataka, lakini sio tuliyonayo! Sasa tufanyeje ili tuwe nayo, ndio issue nafikiri ya kujadili.

Kila nikifikiria jawabu, swali lingine linaibuka. Kwa mfano,kwa kuanzia lazima tuwe na strong civil society, lakini mbona tuna NGOs nyingi ambazo ni comformists na zimekuwa kitega uchumi tu cha watu wachache kwa ajili ya matumbo yao? Lazima tuwe na vyama vichache sana vya upinzania ambavyo vina viongozi ambao ni credible, daring and visionary. Lakini mbona wanasiasa wengi wazuri hawataki kujiunga na opposition parties Tanzania? Ok, labda wameridhika na status quo, kwa hiyo hawaoni haja ya mbadala, lakini mbona hawaishi kulalamika wakikaa pembeni kwenye kuchoma nyama na kula bia? Mbona manung'uniko ni mengi sana kutoka kila upande? Kila nikijiuliza haya maswali na nikilinganisha na nchi za wenzetu Afrika, sipati jawabu, kinachoendelea Tanzania. Kwa nini watanzania hawapendi kutoa mawazo yao in public lakini wanapenda kulalamika pembeni? Hili nimelishuhudia zaidi jana pale kwenye mkutano wa waTanzania Londona, wote waliunga mkono katiba isipokuwa mtu mmoja, lakini pembeni kati ya watu 15 niliongea nao, 11 waliiponda sana ile katiba! Najiuliza nanyi nawaulizeni tena, kwa nini watanzania hawawezi kutoa mawazo yao in public?

Very interesting debate I am reading with great curiosity.
 
Haki
Haki katika duru za siasa siyo kama ile ya watoto 5 kugawana zambarau 50 kwamba kila mtoto atapata 10.Haki katika nyanja za siasa ni kutii sheria na mamlaka.
Nani anaye tii sheria na mamlaka? Kila mwananchi. Kadiri ninavyo ijua sheria na katiba ya Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania watu wote wako chini ya sheria isipokuwa Raisi ambaye katiba inasema Hawezi kushitakiwa.
Kwa hiyo kama Sheria na Mamlaka zilizopo zina mushkeri hiyo ndo hoja ya kuiongelea na ndiyo hoja ya msingi kuliko kudai haki.

Kwa hiyo kuongelea haki katika siasa ni lazima twende kisengele nyuma mpaka kwenye chanzo. Katiba. Hii hali tunayoiita hakuna haki ni matokeo tu.

Kuendele kujadiri matokeo ni kujifunga kihoja na kuvaa mawani ya kiza. Tunabakia kuangalia kidonda na kusikitika badala ya kujiuliza donda limesababishwa na Nini ?Nani? kwanini?

Majibu ya maswali mengi tunayo jiuliza yapo ndani ya kuuelewa vyema utamaduni wa CCM kama kundi, kama chama na kama chama tawala.
Zaidi ni kuuelwa udhaifu wao.Hatutakiwi kucheza mbali na CCM hata siku moja.

Kama unapigana na jitu halafu kila ukirusha ngumi zinaishia kiunoni tu kwa vile wewe ni mfupi ni ujinga kuendele kuutafuta uso wa jitu ili uutandike.
Tafuta sehemu nyingine Nyeti kama P&*&#$#@ zake tandika.

Nyimbo wanazo imba CCM sisi hatutakiwi kuimba hata kidogo.
Hizi nyimbo zao za Demokrasia,Haki, Usawa, Uwazi, Kupambana na Rushwa, Sela hatutakiwi kuimba.

Tutunge nyimbo zetu wenyewe, hata kama zina maneno kama yao, halafu tuziimbe kwa melody ya kwetu.

Kwanza tujiulize tunataka nini?
Hivi tunachotaka ni Haki na Demokrasi tu?
Haki ni nini? Fedha?
Demokrosia? Kama ile ya akina Sokoreti wa Ugiriki ya kale au Hii tunayoiona hapa UESIEI?

Hata kama kuna utawala wa sheria haiwi bure bure na kulala lala bado lina kuwa ni suala la mapambano.Mbinde.

Ukiwa mbele ya JAJI kazi yako ya kwanza ni kutoa vielelezo vitakavyo kusaidia kujenga hoja ili sheria iwe upande wako.

Mahakamani watu hawalii lii wala kuonyesha simanzi ili sheria iwe upande wao ila wanasimama kidete na kutetea hoja zao kwa nguvu zote
 
Mzee Es:

Umezua mjadala muhimu sana-naomba watu waendelee kuijadili ile misingi minne uliyoitoa ambayo KATIBA yetu haina- Hivyo the bottom line i....tunahitaji KATIBA MPYA....nashangaa ile thread ya Katiba na ile ya Tanzania tunayoitaka zote zimewekwa kiporo......they are all related.....Tanzania tunayoitaka itatupelekea kuwa na New Vision wakati ile ya Katiba Mpya pamoja na hii ya kwako zitatupelekea kuwa na MFUMO MPYA WA UONGOZI na MAISHA wa kufanikisha hiyo DIRA MPYA.

Ila umesema unashangaa wakati CCM inakumbutia ubeberu Mwalimu alikuwa wapi- ukitaka kujua soma uongozi wetu na hatima ya Tanzania uk wa 28 na 67

Utagundua kuwa Mwalimu alishaikana misingi ya sera ambayo CCM ilianza kweneda nayo...alisema wazi CCM imecha Azimio la Arusha na imetupilia mbali sera ya ujamaa na kujitegemea na kwamba anasikitika kuwa bado viongozi wanapita klwa hila na janja janja wakiendelea kuwadanganya wananchi kwamba CCM anafuata siasa ya ujamaa na kujitegemea........

Mwenye ile nukuu atupe hapa..........

Tatizo si kufuata soko huria...tatizo ni kuwa tunafuata soko holela kwa kusukumwa na RUSHWA na Ubinafsi hususani wa WATAWALA!

Kwa hiyo hiyo misingi minne unayoisema imebomolewa katika kila kona...kwa maneno(kisera na kisheria) na kwa vitendo( kujiuza kwa mabeberu!)

JJ
 
Mzee Mnyika,

Heshima mbele, kidogo tu wakati bado naendelea kutafakri ya wajumbe huko juu na wewe pia, hicho kitabu Mwalimu alikiandika kwa ajili ya kumsaidia Mkapa ili awe rais,

kwa hiyo kwa maoni yangu kilikuwa ni kitabu cha kampeni spinning, hakukiandika Mkapa akiwa madarakani ambapo ndipo hasa mambo ya kukumbatia mabeberu au wawekezaji yalipokuwa yameshamiri!

halafu lets say alikemea kama unavyosema, je alitoa the alternative?
 
Mzee ES,
Si kweli kwamba Mwalimu aliandika kitabu hicho kumkampeinia Mkapa. Mkapa was not Mwalimu's 1st choice for 1995. Hata nimemsikia Mkapa mwenyewe akisema hivyo. Ni pale tu Salim alipokataa kuchukua forms (Mwalimu alisema Salim alitaka apewe uongozi kwenye sahani) ndipo walipoanza kutafuta altenative. Mwalimu aliandika hicho kitabu baada ya kuzuka kutokuelewana kwa hali ya juu kati yake na Mwinyi. Anyway hilo ni suala jingine kwa muda mwingine. Katika uwekezaji Mwalimu alitaka msisitizo uwe kwa wawekezaji wa ndani, lakini wenzake katika CCM waliona kuwa wawekezaji wa nje ndiyo "serious." Kauli hiyo ameisema Mkapa na sasa hivi anaitumia Mwuungwana. Mwalimu aliona madhara ya kutegemea sana uwekezaji wa nje, na baadhi ya madhara hayo tumeanza kuyaona sasa. Hata ukiangalia nchi zilizoendelea kupita sisi--Wamalaysia na sasa Wachina--kuna uwekezaji wa kigeni unaoenda sambamba na wawekezaji wa ndani. Kwetu hivi sasa hiyo si sera tena. Na msimamo wake katika madini unaufahamu. Lakini tunajua kinachofanyika hivi leo.
 
Mzee Jasusi,

Ninskusikia sana, lakini tunawezaje kuwa na wawekezaji wa ndani yaani wazawa wasiokuwa na hela? Maana hawa wazawa wanahitaji financial empowerment kutoka serikali yetu ambayo sio siri haina huo mtaji,

kwa mfano, niambie ukimpa mzawa kujenga bara bara itawezekana kweli? Sasa kama unayosema kuhusu msimamo wa Mwalimu on wawekezaji ni kweli na sina sababu ya kubisha knowing ukaribu wako naye, ninasema hakuwa realistic kwa sababu Wa-Tanzania hatukuwa prepared ku-deal na mambo mazito ya uwekezaji wa high levels, tulihitaji muda wa kujifunza toka kwa wageni na ndio maana tukaingia kwenye ubia na wageni,

Now siwatetei baadhi ya viongozi waliouvuruga kabisa huu mpango wa uwekezaji, lakini ninaamini kuwa mahali tulipo sasa na hiyo ishu nzima ni kwa sababu ya kutokuwa na alternative, kwani hayo ya Mwalimu ni theory tu yeye akiwa rais ni serikali ndiyo iliyokuwa inamiliki kila kitu na faida yake tukaiona, mbona Mwalimu asi-implement hizo idea akiwa madarakani? sio kwa sababu alijua kuwa haiwezekani?
 
Mzee ES,
You have asked a good question. Ni kweli Watanzania wengi hawana uwezo wa kumwaga mamilioni ya dollars katika investment. Mwalimu alishauri kuwepo mpango wa 50-50 au 40-60 kati ya wawekezaji na serikali yetu, na kwamba kila mwekezaji wa kigeni atafute local partner. Hili halikusikilizwa na Mwinyi, wala Mkapa. Kumekuwepo mifano ya wawekezaji wanakuja Tanzania bila hata senti tano mfukoni, somehow wanapata mikataba ya ajabu ajabu na baada ya muda wana mamilioni ya fedha. Kuna ile mindset kwamba a foreigner is a serious investor and not a local one. Mfano mwingine ni pale Mengi alipotaka kununua hoteli ya Kilimanjaro lakini akapigwa chenga akauziwa mwekezaji kutoka Uarabuni. Kuna mifano mingi tu. Katika madini kulikuwa hakuna lazima ya kuwakaribisha AFGEM kutuchimbia tanzanite, lakini leo wapo na wanachuma $500 million a year wakati Tanzania tunapata less than $20 million. Hivyo hivyo katika dhahabu. Hatujui Sinclair anachuma kiasi gani, na watu wanaendelea kuhamishwa kwenye mashamba yao ya miaka mingi ili "mwekezaji achimbe dhahabu." Ulimsikia Mwungana akimjibu yule dada kutoka Tarime katika ule mkutano mjini New York mwaka jana. We had altenatives but we have chosen the wrong one simply because, I believe, someone is making money when a foreign investor's deal goes through.
 
Salamu zenu waheshimiwa mabibi na mabwana!

Nimekaa hapa na nimejikuta maswali yakizidi kujipanga kichwani mwangu utadhani mtu anayepanga matofali ya kuchoma kwenye tanuru nje kidogo ya mji wa Iringa, pembezoni mwa barabara iendayo Mbeya! Na kwa kadiri ninavyofikiria najikuta nashindwa kupata jibu la uhakika na kitu hicho kinanitia hofu kuwa tusipoangalia tumeendelea kukubali rushwa ya aina hii kiasi cha kuifanya ni kawaida. Fuatilia kisa hiki:

Mheshimiwa akiwa amevalia nguo za kawaida, yeye na dereva wake anateremshwa karibu na Duka la Bw. Bushiri. Wapita njia wanamtambua kuwa huyo ni mheshimiwa fulani. Hana lengo la kununua kitu isipokuwa kusalimia wafanyabiashara wachache. Anaingia dukani na mwenye duka kumuona anaingiwa na kiwewe na kuanza kujibamiza kwa "mwenye nchi huyo"

"Mheshimiwa!! karibu karibu" Bw. Bushiri anasema huku akiteremka kwenye kiti chake kikubwa kilichoko kwenye kona ya duka hilo.

"Asante sana Bw. Bushiri, habari za shughuli bwana" Mheshimiwa akajibu huku akinyosha mkono wake ambao ulikuwa umenona utadhani wale 'kuku' wa Salanda huku vinyweleo vya ngozi yake vikiwa vinameremeta kwa mafuta aliyojimwagia.

"Ni njema tu mzee, tumebahatika nini kutembelewa na mtu mzito kama wewe" Bushiri hakuchelewa kuuliza kwani alijua mheshimiwa anapokuja kwenye duka lake huwa anataka kitu.

"Ah! kukusalimia tu bwana, unajua tena mihangaiko ya hapa na pale" Kwa soni za uongo mheshimiwa akamjibu, huku macho yake yakiangaza angaza kila kona ya duka hilo. Bushiri, hakuchelewa kuelewa nini kinaendelea. Akaamua kumkaribisha mheshimiwa ofisini kwake kwenye kona nyingine ya duka hilo ambapo watu wengine hawaruhisiwi kupita. Walipoingia ofisini baada ya kuulizana hali za watoto na wake zao, Bw. Bushiri akamuuliza mheshimiwa

"Sasa mzee, unahangaika nini tena"

"Bwana we, unajua tena nilitarajia mzee angeniteua kwenye kaposition fulani lakini hakufanya hivyo. Hata hivyo nimehakikishiwa kuwa kwenye next reshuffle naweza nikaukwaa na mimi. Sasa nikasema ni bora nianze kuwajua rafiki zangu ni nani bwana" Mheshimiwa akajibu kwa uhakika huku unono wa mashavu yake ambao uliunganika hadi kwenye shingo ukitingishika tingishika utadhani ng'ombe wa maziwa wa pale Kange, Tanga.

"swadakta! na marafiki zako tupo mzee" Bushiri alijigamba huku akijigonda kifuo kwa mkono wake kuonesha na yeye ni mmoja wa marafiki hao.

"Nashukuru Bw. Bushiri, sasa hivi nahangaika kuinua kile kibanda changu kule Mbezi, ila hali ngumu bwana" Mheshimiwa akasema kana kwamba kwa mzaha. Bushiri alitamani aanze kumuuliza "hali ngumu gani" anayozungumzia kwani akianza kumhesabia pesa ambazo mheshimiwa huyo na wenzake wanamegewa na nchi yao, basi maana ya "hali ngumu" haipo tena. Lakini hakuthubutu.

"Sasa mzee tatizo nini nini kwenye kibanda?" Aliuliza Bushiri kwa unyenyekevu.

"Cementi bwana bei ghali kweli na mabati ndio usiseme, ila ningependa kuweka vigae, ndio nahangaika hapo" Mheshimiwa akajibu.

"Sasa" Bw. Bushiri akadakia, "Mzee usiwe na wasiwasi, nitamtuma dereva siku ya jumamosi na mifuko 50 ya saruji na vigae 5000 hivyo vya kukusaidia kidogo" Alimalizia huku akiandika kwenye kijitabu chake cheusi ambacho kurasa zake nyeupe zimeanza kugeuka na kuwa za rangi ya udongo.

"hayo maneno sasa" Mheshimiwa akajibu huku akisimama kuagana na Bw. Bushiri.

"Mzee na wewe ukifika katika ufalme wako usitusahau mzee" Bw. Bushiri alisema kwa upole lakini akiwa anatoa ujumbe ulio dhahiri.

"Bila ya shaka, umenifaa leo, na siku moja nitakufaa bwana" Mheshimiwa alisema huku akimuelekeza dereva wake aliyekuwa bado anang'aa ng'aa macho kuwa muda umefika waondoke.

Walipotoka kwenye duka la Bw. Bushiri, waliendelea na 'kaziara' hako kafupi kwenye maduka ya Bw. Minja, duka la Mzee Sudi, duka la vifaa vya umeme la Patel na duka kubwa la samani la Bw. Abdalah Fundi lililoko eneo la Keko gerezani karibu na barabara ya kwenda Chang'ombe. Mwisho wa siku, Mheshimiwa alikuwa amepata ahadi ya saruji, vigae, mabomba ya maji, samani za ndani ya nyumba, mafjiri mawili, viyoyozi sita na mazuria toka Uchina. Aliporudi nyumbani mheshimiwa alienda kujipongeza kwenye Baa ya "Sisi kwa Sisi" iliyoko kwenye kona ya mtaa wake ambapo huko nako hata bia alipewa ya dezo!

Miezi sita baadaye, mheshimiwa wetu alikuwa anamalizia kujenga 'hekalu' lake kubwa eneo la Mbezi ya Kimara upande ule mwingine kutoka upande wa nyumba ya jenerali Musuguri. Ilikuwa baada ya mabadiliko ya mawaziri ya hivi karibuni Mheshimiwa akapewa na yeye unaibu wa wizara moja nyeti, na haikuchukua muda kwa yeye kuanza kuwarudishia fadhila wafadhili wake. Kwa vile sasa kaupata na ujiko mkubwa kidogo mheshimiwa wetu ameanza tena kufanya viziara vya hapa na pale kwa wafanyabiashara wa mikoani na pole pole ameanza kujenga "vibanda" vingine karibu kila mkoa katika mihangaiko yake ya kila siku, kwani "hali ngumu". Na wakati haya yote yanaendelea, mheshimiwa ameendelea kunawiri na kunenepa! Wale wafanyabiashara wote waliomsaidia sasa hivi wanaweza kupiga simu wakati wowote na kutaka hisani ya aina yoyote toka kwa Naibu Waziri na mara nyingi wanapata!

Mfano mzuri ni kuwa hivi karibuni Bw. Bushiri alikuwa afanyiwe uchunguzi na TRA lakini kwa neno zuri la Naibu Waziri uchunguzi huo umezimwa baada ya Bw. Bushiri kulipa kodi ya shilingi milioni moja tu wakati kodi aliyotakiwa kulipa kwa halali ilizidi shilingi milioni 40! Huu ndio uzuri wa "kujuana na mkubwa".

M W I S H O

Kikanusho: Kisa hiki ni cha kubuni. Mlingano wowote na watu, majina, au matukio halisi ni wa kinasibu. Haki zote za kunakili zimeachiliwa na M. M. Mwanakijiji



NB: Kisa hiki kinamhusu mheshimiwa mmoja tu kati ya wengi, kama wengi wanafanya tabia ya aina hii, athari zake ni kubwa kiasi gani? Je kuna ubaya wowote kwa viongozi kutafuta na kupokea zawadi za aina hii? Kama raia anataka kumsaidia kiongozi kuna kosa gani hapo? Je hii nayo ni rushwa, takrima, zawaida au ukarimu tu wa Watanzania? Maswali yameanza tena kichwani mwangu.
 
Hicho kisa hapo juu ni matukio ya RUSHWA tupu, rushwa ambayo inafanywa na kila kiongozi ndani ya serikali yetu na taasisi zake.

Ni ukweli unaowaacha utupu hawa wakubwa ambao wanatumia nafasi zao kama viongozi kupata mali bila kutoka jasho, maana uongozi Tz ni kuukata na kuishi vizuri.

Inanishangaza taasisi kama TAKURU yenyewe wafanya kazi wana mali zisizowiana na kipato chao na mlolongo unaendelea kuzunguka mfumo mzima ktk system. Kazimkweli kweli.

Mahekalu yaliyoko Msasani Peninsular, Mbezi Beach, Bahari Beach, na sasa yanayoota kama uyoga hapo Upanga na mengine mengi yanamilikiwa na hawa hawa ambao ndio wanadai kuliongoza taifa hili kutoka ktk umasikini.

TRA kama taasisi ya kukusanya mapato ingeainisha mpangilio wa kukusanya kodi kutoka kwenye pango za haya mahekalu kwani mengi yanakodishwa na wazungu kati ya $ 2,500 mpaka 4,500 kwa mwezi. Aidha, thamani ya mali iliyowekezwa - kwa mfano kama hekalu thamani yake ni Tsh million 500, inabidi kodi ya kipato hicho ilipwe regardless kimepatikana halali au kwa rushwa plus penalty calculated based on the age of this asset. WENGI WANAWEZA KUYAKIMBIA MAHEKALU YAO.

Hili ni zoezi lisilowezekana kwani hakuna atakaye mnyooshea mwenzie kidole!!

Bongo hii, ila wanakufa wanaviacha KAZI YA MUNGU HAINA MAKOSA!
 
Lakini wao wanasema ni shukurani ya wananchi kwao!!
Hii ni shukrani ya aina gani?kwanini asitoe shukrani kupitia kipato chake halali yaani mshahara na marupurupu anayoyapata kwa posho za safari,malazi na N.K
Kitendo cha kutumia dhamana ya uongozi aliyopewa na Wananchi kuwasaidia hao anaowaita marafiki zake kutolipa kodi na kulikosesha Taifa mapato ambayo ukusanywaji wake ungewasaidia watanzania wote si shukrani bali ni kulipa fadhila ambayo alipewa kwa kuweka rahani kauli ya kwamba karibu nitachaguliwa na nitakapochaguliwa kwenye huo wadhifa mpya nami nitawasaidia sasa kutokana na ahadi aliyoitoa ni dhahiri hata waliotoa msaada walitoa wakitumaini siku moja watapata malipo(Rushwa ili wafanikishe mambo yao kupitia huyo mheshimiwa) Na Hii rushwa ndiyo iliyomfanya Mheshimiwa afikie maamuzi potofu kwa kuwapigia simu watu wa TRA wamsamehe kodi Bw.Bushiri na kuliingizia Taifa hasara.Kama ingekuwa ni shukrani na si Rushwa basi Bw Mh .Waziri angetoa Fedha Mfukoni mwake na kumuongezea Bw.Bushiri ili alipe Kodi TRA na watanzania wote wafaidike,Lakini kilichojiri ni kuendelea kujinufaisha yeye na waliomfadhili kabla ya kupewa dhamana na kutumia dhamana hiyo kulitia hasara Taifa kwa kulikosesha mapato!
 
.............................
...................................................................................

Walipotoka kwenye duka la Bw. Bushiri, waliendelea na 'kaziara' hako kafupi kwenye maduka ya Bw. Minja, duka la Mzee Sudi, duka la vifaa vya umeme la Patel na duka kubwa la samani la Bw. Abdalah Fundi lililoko eneo la Keko gerezani karibu na barabara ya kwenda Chang'ombe.
.......................................................................
.......................................................................................


MKJJ
nnavyojua MINJA mwenziwe MINGE naona hujamuweka hapo.

halafu nnahisi huu ni uchokozi wa makusudi kwa akina mswahili, maana wote uliowataja hapo ni waakina mswahili.

japo umejificha kwenye mwamvuli wa kisa cha kubuni
 
Hapa naona tatizo kubwa ni kujipendekeza na kupenda vya dezo zaidi kuliko rushwa.

Huyu mheshimiwa anataka vya dezo, anataka ajenge majumba bila jasho.

Wenye maduka wanajipendekeza kwa wakubwa bila kujua kuwa ni wajibu wao kulipa kodi

Hao maafisa wa TRA nao wanajipendekeza kwa waziri. Badala ya kuheshimu sheria ya kodi na kufanya uchunguzi kwa mujibu wa sheria, wao wanamuogopa waziri.

Sasa inabidi wafanya biashara wajue sheria za nchi na watambue na kuona kuwa wana wajibu wa kulipa kodi.

Wafanyakazi wa serikali nao waanze kuheshimu kanuni na sheria zinazoongoza taasisi zao badala ya kuogopa wakubwa zao.

Kwa ilivyo sasa polisi akiamriwa kuua mtu anaweza akafanya huku akijua kabisa hakuna mtu mwenye haki ya kutoa uhai wa mtu.

Kujipendekeza na woga ni mdudu anayetutafuna sana katika ile nchi!
 
Back
Top Bottom