Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Ukificha ugonjwa, kifo kitakusema. Kutokana na kuwa katika kundi la mwisho katika vipengele mbalimbali vya maendeleo na utawala bora, ni sawa kusema “nchi yetu ni ya mwisho”. Kuwa katika kundi la wachache wa mwisho ni kuwa wa mwisho.

Kuna tatizo kubwa kwenye vita dhidi ya rushwa. Wanaotegemewa kuongoza hivyo vita, ni wale wale ambao wanapashwa kushambuliwa. “Adui” wa kweli katika vita dhidi ya rushwa hapa kwetu ni viongozi. Wataongozaje vita dhidi yao wenyewe? Ilibidi kuwe na chombo huru cha kupambana na rushwa. PCB iliyo ndani ya Ofisi ya Rais haiwezi kushutumu viongozi, hasa wale wakuu, kwani ni viongozi wao, na ni washirika wa wakubwa wao wa kazi.

Inatakiwa kuwe na chombo kinachoajibika kwa wananchi, kwa kupitia Bunge. Kuwe na kamati ya kikatiba ya uteuzi wa wakuu wa PCB (mpya), Polisi, Jeshi, Magereza na Mahakama. Viongozi hao wa kikatiba, wasiteuliwe na kufukuzwa kazi na Rais. Kwa njia hiyo wataweza kumchunguza hata Rais inapoonekana anavunja sheria.

Haiwezekani kuleta utawala bora wa kuridhisha na wa kisheria Tanzania bila kufanya mabadiliko makubwa katika katiba yetu. Bahati mbaya, wale tunaotegemea wakubali na kuongoza marekebisho hayo ya katiba wanapinga. Wanapenda tuendelee na hali ya sasa kwani wanafaidika nayo, na wanadiriki hata kuwadanganya wananchi kwamba tunafanya vizuri sana.

Wananchi waliosoma vizuri hawadanganyiki kiurahisi, lakini hali ya Elimu Tanzania ni duni sana. Ni rahisi sana kuudanganya umma wa Tanzania, na viongozi wetu wanaishi kwa hilo.

Waandishi wa habari waendelee kuwalimisha wananchi kwa kuandika ukweli, hata ule unaouma. Tuendelee kukazania Elimu kwa ujumla. Umma ulioelimika vizuri una nguvu za kujikomboa zisizo na kifani!
Augustine Moshi
 
Mgumu, miye sijabisha elewa nilichosema...wakati mwingine usiwe mgumu tu alimradi mgumu.
 
Maneno mazito haya . Kiliba hatayapenda maana yumo kwenye mkumbo
 
Tusikwepe issue hapa kwa kujaribu kujiliwaza eti kuna uongo ndani yake.Tatizo la Tanzania viongozi wake ni vijib.. vya western na haipigwi darubuni kama Nigeria au Zimbabwe na pia haijulikani sana kama Nigeria,Zimbabwe,Kenya au Somalia.Watanzania tunakuwa wepesi sana kukanusha mambo bila kujua ukweli. Pale Kigoma silaha zilikuwa zinapakiwa Kwenye meli za DRC usiku kwenda Kongo kwa usimamizi wa jeshi la wananchi wa TZ.Lakini mwandishi wa watu walikanusha ujumbe wa Darwin

Kwa ufupi tu hebu toeni mfano wowote wa mikataba ya ubinafsishaji,biashara au uuzaji wa makampuni ya umma ambayo haina ubadhilifu au rushwa!!!Tanzania inanuka rushwa pengine zaidi ya tunavyojua.
 
In Tanzania, we fight corruption with seminars
Karl Lyimo

In late 1995, the government-in-waiting in Dar es Salaam articulated a pledge to fight corruption. That was when then president-elect Benjamin Mkapa granted an interview to David Martin that was published in the Tanzanian English daily The Guardian.

Both Mkapa and Martin were accredited journalists of no mean repute in Tanzania. Mkapa went on to become president of the country (1995-2005). Martin was and remained the director of a renowned research organisation in Harare.

THAT INTERVIEW covered a wide range of issues. Mkapa said he would constitute a lean government of around 21 ministers and said he would sack any official perceived to be corrupt.

Neither of the pledges was kept.

The Mkapa administration eventually had around 50 ministerial appointees and none of his principal appointees who came to be perceived to be corrupt — and there were not a few — was ever brought to account.

What happened? I can't tell you that for certain. What I can say is that big government is still the name of the game in the post-Mkapa era: President Kikwete has 61 ministers. And, for all practical purposes, the war on corruption is still on the backburner — with the switch turned off.

How many principal officers of government have been prosecuted for graft in our time? This can only mean one of two things. Either our public officials are divine and above board in thought and deed, or there is a cover-up, with the government being unable or unready to wash its dirty linen in public.

Every president who comes on the scene pledges to fight corruption. But there are no casualties on the ground. Is the war being fought using blank ammunition?

The other day I read an interview in a local English weekly granted by Edward Hosea, the head of the Prevention of Corruption Bureau.

He was quoted as saying the government has reiterated its resolve to fight corruption at all levels, refuting claims that it still lacks the requisite political will.

IF THE government is doing so, then it must be a war of words, fought through documents, seminars and workshops, posters, the electronic media and via other theoretical fora. The government has already gone through a five-year National Anti-Corruption Strategy and Action Plan and has launched phase two of the same that will run from 2006-2010.

The plan "is seen as being a broader and inclusive structural and policy document on corruption. The document will provide a platform for dialogue among government institutions and other relevant authorities?"

How I long that the government and the people of Tanzania would put dialogue and policies and other theories aside and gird up for the real fight against graft.

Setting up integrity committees, a good governance co-ordination unit and an ethics secretariat is not going to root out corruption. The vice is already so institutionalised and systemic that nothing short of surgical action will do.

Fighting corruption is like fighting a malignant tumour. It calls for a total, concentrated war, that will hit at the head of the vice — the barracudas of corruption — not the small fry. In China, they shoot corrupt government officials at dawn. The least we could do here is take them to court or name, shame and sack them as we recover the monies from their ill-gotten wealth. Like a cancer, graft must be annihilated.

Karl Lyimo is a freelance journalist based in Dar.
 
Makada wa umri wangu na walionizidi wanakumbuka wakati wa enzi za TANU ilikuwa ni ada kwa wanachama na viongozi kabla ya mkutano wowote wa chama kuanza wajumbe waliohudhuria walitakiwa kwanza kusoma ahadi kumi za chama kwa ghaibu; soma zaidi: http://mjengwa.blogspot.com
 
Hay ni madai ya kweli jamani ? Ama ni mimi sijaelewa aina ya Demokrasi wanayo ongelea ?

Mwandishi Wetu
HabariLeo; Sunday,January 28, 2007 @00:05

TANZANIA imepanda chati katika kukuza na kuimarisha demokrasia na kujali haki za binadamu, imefahamika. Katika Afrika imekuwa nchi ya 20 kati ya nchi 53 ambazo zimechunguzwa kwa mwaka jana, huku ikiwa ya 95 duniani miongoni mwa nchi 151.

Taasisi ya Kufuatilia Viwango Duniani (WAO) katika taarifa yake inaonyesha Tanzania inaendelea kuwa miongoni mwa nchi zinazozingatia haki za binadamu na kudumisha demokrasia.

Mwaka 2000 Tanzania ilikuwa ya 117 duniani na mwaka 2005 ilikuwa ya 95. Katika Afrika kwa miaka hiyo ilikuwa ya 27 na 22. Taarifa hiyo inaeleza kuwa nchi ya kwanza duniani kwa mwaka jana ni Finland, ya pili Denmark na ya tatu ni New Zealand.

Mynamar ndiyo nchi inayotajwa kutojali haki za binadamu na kutokuwapo demokrasia duniani ikifuatiwa na Turkmenistan na Libya. Nayo Afrika Kusini ni ya kwanza katika Afrika na kufuatiwa na Mauritius na Ghana, huku Sudan, Zimbabwe na Libya zikishika ‘mkia’, kwa kutowatendea haki wananchi wao au wageni wanaotembelea nchi hizo. Hazina demokrasia pana inayoruhusu pia uhuru mkubwa wa kujieleza.

WAO yenye makao yake makuu London, Uingereza hufuatilia kila mwaka maendeleo ya ukuaji wa demokrasia na haki za binadamu katika nchi kwa kuzingatia namna zinavyoendesha uchaguzi, zinavyowatunza wafungwa, zinavyoruhusu uhuru wa kujieleza, na kukubali kukosolewa na wananchi wake bila ‘kuwaziba’ midomo.
 
2007-02-03 09:05:00
By Angel Navuri

United States Agency for International Development in Tanzania through the Millennium Challenge Account (MCA) Threshold Plan announced yesterday that it would start two-year training programme for Prevention of Corruption Bureau officials (PCB).

Briefing reporters in Dar es Salaam MCA Threshold Programme Coordinator Aaron Karnell said the training will be held in Dar es Salaam starting this month.

He said the objective of the programme was to reduce corruption in the country�s local districts and central government agencies.

It will emphasize prevention, oversight and deterrence of corruption. This would be accomplished by enhancing the capacity of the media by strengthening the role of parliament, engaging citizens groups and through sustained political support at senior levels of governance.

Karnell said PCB officials would be trained by New York City department of investigations.

Wanaokula Rushwa inabidi wakamatwe na wageni kama vile sisi wenyewe hatuwajui. Makubwa haya.
 
Mzee Es haandiki hivi na hata maelezo ya huyu jamaa yanatofautiana na yale ya awali aliyotoa mzee Es kuhusu balozi mahalu. Ila nina shaka sana na Mugongo Mugongo pamoja na kwamba sii kawaida ya mzee Es kuingia na jina bandia.
 
waungwana,

kwanini tunatumia sana hii luga ya kigeni (kiengereza) hapa kwenye JF bcoz si dhani kama wote ambao wanaangalia hii JF kuwa wanajua huu umombo; so naomba tutumie luga yetu ya Taifa (Kiswahili) - kwani faida kubwa itapatikana kwa wale wote ambao wanafatilia hizi habari.
 
waungwana,

nawaomba ingelikuwa busara zaid kama tungelitumia lugha yetu ya Taifa (Kiswahili) hapa kwenye JF yetu, kwani kwa mtazamo wangu si dhani kama wote ambao tunapata habari hapa JF kuwa nutajua Kiengereza.

Ukingatia kuwa JF ipo kwa ajili ya kuelimisha - na kupata habari ni haki ya kila mtu, so naamini kama tutatumia kiswahili faida kubwa itapatikana baada ya kupata faida hizo watu wachache

Thanx!!!
 
Wazo zuri sana lakini wakati mwingine ni vigumu kwa sababu ya kuwakilisha makala iliyoandikwa kwa lugha ya kiingereza. Nitajitahidi kuandika kwa kiswahili katika mada ninazotoa lakini kama ni habari ambayo naileta hapa ambayo imeandikwa kwa kiingereza siwezi kuitafsiri.

Napendekeza wale ambao kiingereza kinawapiga chenga wawe wanajitahidi kusoma hizo mada za kiingereza kwani zitawasaidia kuelewa na kufananisha na zile za kiswahili (kama habari zinahusiana).
 
Kwa mtazamo wangu, nchi yenye demokrasia angalau ya kweli (maana so far bado hatujui ni demokrasia ipi ndiyo ya kweli duniani), ni lazima iwe na nguzo nne za kuiendesha serikali yake, ningependa tuziangalie nguzo hizo na kuwepo au kutokuwepo nchini kwetu, yaani Tanzania, na faida na hasara zake:

Katika nchi yenye demokrasia ya kweli, au angalau, ni lazima kuwe na serikali yenye kutawaliwa kwa kutumia nguzo nne muhimu as a system,

1. System ya siasa ya kuichagua na kubadilisha serikali kwa njia ya uchaguzi ulio huru na wa haki.

2. Active participartion ya wananchi, kama raia wa nchi, katika siasa na civil life.

3. Ulindwaji wa haki za binadamu kwa wananchi na raia wote wa nchi.

4. A rule of law na procedure ambazo zina-apply equally kwa raia na wananchi wote.

Ningependa tuongelee each of these four elements au nguzo nne muhimu za maaana ya demokrasia, kwa kuzi-link na political situation nzima ya Tanzania, na pia obligations na requirements za wananchi wetu katika democrasia hiii.

Ahsanteni!
 
Kwa kuanza ninasema demokrasia ni lazima iwe njia ya wananchi kuchagua VIONGOZI wao wa vitengo vyote vya dola katika nchi yao, na kuwa-hold accountable kwa their policies na conduct au tabia zao wanapokuwa madarakani, na wananchi hao ndio wenye uamuzi wa mwisho wa kuwachagua WABUNGE, na RAISI wao, na wanafanya hivyo kwa kuchagua betweeen competing parties kwenye uchaguzi ulio huru na wa haki.

Je Tanzania hili linafanyika?
 
In order for the rulers of democracy to allow the expansion of democracy in any nation, I believe three factors must happen before wananchi can have sauti kubwa katika kuamua public affairs zao,

1. Internal conflicts

2. External Threats

3. National Unity na maendeleo.

Na haya hayajatokea deeply katika Tanzania, so this should explain why we are still limping on the democracy avenue!
 
Na haya hayajatokea deeply katika Tanzania, so this should explain why we are still limping on the democracy avenue!

Kwa kuwa tz ni nchi changa, sitegemei everything kuwa ok at this point, ila it might take up to generations and generations to come for democracy to work. Ndio maana mataifa makubwa yamechukua miaka hadi 200 kuwa katika proper position, sasa basi kinachotakiwa na sie ni kuendeleza mambo mzuri ili vizazi vyetu vya baadae viwe katika hali nzuri !

Inaweza ikatuchukua approximately miaka 25-40 kuwa na more democracy iwapo chama kimoja kitatolewa madarakani !!
 
Ndugu zangu wana JF,

Kwanza naomba kuweka wazi kuwa kamwe sikuwa na nia ya kumfunua ndugu yangu Mzee Es kama ndugu zangu kadhaa walivyotafsiri. Nia yangu ilikuwa kumtanabahisha kaka yangu Mzee Es kuwa kwa mtindo anaotumia ni wazi maisha bora kwa kila mtanzania hayatafanikiwa kamwe.

Huku nikijua kuwa ndugu yangu Mzee Es ni mwana wa tabaka tawala, nilichukua uamuzi wa kumtikisa kidogo nikijua kuwa kuamka kwake kutasaidia kundi tawala na watanzania kwa ujumla. Wapo wanaodai kuwa ili kukubalika ndani ya kundi ni lazima uimbe wimbo unaokubalika kwa "wenye nguvu" ndani ya chama. Lakini kwa ufuatiliaji wangu wa siasa za nchi yetu ni dhahiri siasa za "ukada pofu" hazina nafasi ndani ya kundi hilo la wateule kwa muda mrefu. Na yeye ni mwana kundi wa kizazi kipya kama mimi ingawa sio mwanakundi

Mfukuto kundini ni mkubwa na mfukuto wa kimawazo (ukitoa ule wa kimadaraka) unaoendelea ndani ya mioyo ya wanakundi ni dalili njema ambazo wanakundi vijana kama Mzee Es wakiamua kuthubutu kusema ukweli bila ya kutetereka, mambo yataanza kunyesha mstari wenye matumaini.

Nasema hivyo huku nikitambua mwenendo wa kundi tawala katika urithishaji wa majukumu nyeti kwa damu mpya ya tabaka tawala (wazungu wanaita reduplication of elite). Na mambo kama hayajabadilika bila ya kutarajiwa ni wazi ndugu yangu Mzee Es akiwa tayari kuchukua risk ( nasikitika kuwa nikubwa mno lakini) karibuni atasimikwa majukumu ya kuitetea nchi yetu kwa njia moja ama nyingine.

Tukija katika mada ya DEMOKRASIA NA TANZANIA YETU, ni wazi kuwa hadi sasa tupo njia panda. Ukiniuliza kama tumefanikiwa kuendeleza demokrasia nchini mwetu nitakwambia ndiyo, lakini ni demokrasia tata inayoamini ukiritimba wa chama kimoja (dominant party democracy).

Ni wazi kuwa hali hii inakidhi matakwa ya rafiki zetu katika unyang'au (partners in plundering-The Western powers) na vilevile maslahi ya tabaka tawala, vizazi vyao (kwa wakati huu) na wale mwalimu wangu Kamarade Chachage (najua amelala kwa furaha uko alipo akiamini kuwa Tanzania ipo katika mikono mizuri kwa sasa) aliowaita makuwadi wa soko huria ama utandawizi. Kwa ujumla demokrasia hii inakidhi maslahi ya Tanzania kama taifa kwa wakati huu (sio ujao).

Swali linakuja:
Je demokrasia hii inakidhi matamanio, maslahi na matakwa ya watanzania kwa ujumla? Hili ni swali gumu ambalo ningependa kuliacha wazi ili kila mtanzania mwenye upendo wa dhati na wala usio na chembe ya unafiki kwa Tanzania yetu (yaani watanzania kwa ujumla) ajiulize na kujitahidi kung'amua jibu sahahi.

Kuhusu swali la nini kinapaswa kifanyike kujenga UPINZANI MAKINI NA WENYE NGUVU nchini mwetu kama alivyouliza ndugu yangu Mzee Es katika "thread" tofauti na hii napenda kumjibu kwa ufupi sana kama ifuatavyo. Ili kufanikiwa hilo;

Ni mimi na wewe kuacha kujidanganya kuwa mfumo tulio nao sasa unaweza kubadilisha mambo katika nchi yetu.

Ni mimi na wewe kuacha kudanganyika na kile tunachokiita mafanikio ya wakati wa sasa ambayo tunayapata kutokana kuwa karibu na na waaminifu kwa "wenye inji" (kama alivyosema Mzee Mrema)

Ni mi na wewe kuacha kulalama kuwa upinzani ni mbovu wakati hatuko tayari kujitoa kuufanya uwe mzuri na makini na wakati mwengine kuwa mstari wa mbele katika kushabikia mambo ambayo yanadhoofisha huo upinzani kwa kuwakejeli wale waliothubutu kujitoa mhanga.

Ni mimi na wewe kuwa wakweli kwa taifa letu na kuacha kulalama kwa kificho na kuwa tayari kuita mavi ni mavi...

Kuhusu ndugu yangu anayedai kuwa NCHI YETU NI CHANGA kwa kweli hiyo lugha ilikuwa murwa enzi za Baba wa Taifa alipokuwa anajenga taifa letu lakini kwa miaka hii zaidi ya 40 hatuwezi kuendele kudai taifa letu bado ni changa. Ni uchanga gani huo wa miaka 40 na zaidi?

Ukweli ni kuwa tunashindwa kuwa na uthubutu wa kusema kawaida (business as usual) haiendelezi nchi bali unaendelze maslahi finyu ya sisi wachache tulio karibu na usukani wa nchi na hiyo sio sawaaaaaa kabisa

Inashangaza sana kuona kuwa watanzania wengi tulio katika tabaka la juu ama tunaojiona tuko karibu na tabaka la juu (masikini mwalimu huko alipo na na ulimbukeni huu wa matabaka haya) tunapenda kujidai kuumizwa na unyang'au unaoshamiri katika nchi yetu halafu tunakubali kuwa wanafiki hata pale Kiongozi wetu anapotusihi tuache unafiki.

Anayedai kuwa tusubiri miaka 20-40 ili tukue, hivi amesahau kuwa hata mwalimu aliambiwa hivyo hivyo wakati anawaongoza wazee wetu kudai uhuru katika miaka ya Hamsini?. Si bure wengine alikuwa nao wakaishia kumsaliti na kuwasaliti watanzania punde tulipopata uhuru.

Lakini zaidi ya hivyo ina maana tukae tusubiri hiyo miaka 20 hadi 50 ndio tupokee zawadi ya demokrasia tunayoiota ama tuifanyie kazi kuanzia sasa?

Lakini hivi kweli hali inaruhusu starehe hiyo ya kusubiri hiyo miaka ifike kwa spidi ya unyang'au inayoendela nchini mwetu na zaidi miongoni mwetu?

Swali kubwa la kujiuliza ni kuwa tutaendela kuwa na Tanzania yetu katika miaka hiyo 20 hadi hamsini ama tutakuwa kama wenzetu wanaotuzunguka ama hata wenzetu wa Somalia? Anyway labda hili haliwahusu wengi wali katika mtandao huu maana wao ni watu wa majuu…ulaya

Na zaidi kama tunashindwa kujikomboa sasa kutoka katika tufani tuyojijengea kwa madaha hivi sasa, ikifika miaka hiyo mazingira yatakuwa yanatoa mwanya wowote wa kufanya mabadilioko hayo?

Ndugu zangu, tumebarikiwa nchi yenye kila "potentials" za kuwa nchi nzuri na bora kwa kila mtanzania na hata asiye mtanzania. Kwa maajabu ya mungu ni kuwa hata kama tumekuwa tuanajitahidi kuibomoa kwa spidi kali bado mungu anatuonyesha upendo wake usio na kifani.

Tatizo ni kuwa kwenye miti hakuna wajenzi(tusubiri wakina nanihi waje kutujengea). Wengi wetu ama ni waoga wa mabadiliko ama hatutaki kuwa sehemu ya Tanzania iliyo njema kwa wote kama tunavyojifaragua humu ndani ya mtandao.

Tanzanianjema
 
Mzee ES,

Naomba niambatanishe hii habari kuhusiana na Makamu wa Raisi Dr. Shein. Ukweli ni kwamba kama Wabunge na Wafanyakazi wa Serikali watafuata ushauri wake, hiyo itakuwa njia pekee ya kuona kuwa Demokrasia itafanikiwa.

Wengi wenu mtafikiri habari hii inahusu Sheria pekee. Angalia msisitizo wake wa "separation of powers"! Meaning each branch of government should be independent and have powers to hold the other accountable without fear or intimidation!

Dr Shein stresses judicial independence​
DAILY NEWS Reporter
Daily News On Saturday; Saturday,March 24, 2007 @00:07
resize_image1.php
THE Vice-President, Dr Ali Mohamed Shein, opens a legal experts meeting in Dar es Salaam yesterday. Third right, is the Minister for Justice and Constitutional Affairs, Dr Mary Nagu. (Photo by Amour Nassor)THE Vice-President, Dr Ali Mohamed Shein, has reiterated the importance of adhering to the principle of separation of powers and independence of each of the three arms of government.

Opening a one-day conference on professional ethics in the legal profession in Dar es Salaam yesterday, Dr Shein said that the judiciary should be free from interference if it were to perform its constitutional role of reviewing actions taken by the government and its officials.

“An independent, impartial and informed judiciary therefore holds a central place in the realisation of a just, honest, open and accountable government,” said Dr Shein.

Dr Shein defined the legal profession as including lawyers, advocates and notaries, who should all “help to ensure that the judicial system functions properly,” he said.

Earlier, the Minister for Justice and Constitutional Affairs, Dr Mary Nagu, told the participants that the government was aware that salaries for public servants, including those in the legal sector, were small compared to those in the private sector.

“I wish to remind public servants, especially those in the legal sector, that the small incomes should never be the reason to compromise their ethical performance,” said Dr Nagu. adding that the government always tried to improve the welfare its workers.

The conference has drawn participants from different parts of the world in order to exchange, share information and learn ways to address issues of ethics and corruption in the legal sector.

Presenting a paper, the Director-General of the Prevention of Corruption Bureau (PCB), Mr Edward Hosea, said that the legal sector’s image was tainted by corruption and misconduct.

“Time has come to restore the image of the profession and its legal system by improving the legal conduct that has integrity,” stressed Mr Hosea. The meeting was organised by the Ministry of Justice and Constitutional Affairs and the German Agency for Technical Co-operation (GTZ).
 
TanzaniaNjema na Rev. Kishoka nadhani hapo juu nilishasema tz haiwezi kuwa na democracy kama ccm wapo madarakani 4 the fact kwamba hata ccm wenyewe hawana democracy ndani ya chama chao na ukiangalia viongozi wa ccm wapo tayari kufa kwa ajili ya chama kuliko kwa ajili ya nchi, mfano mzuri ni Mzee ES na mzee wake Mzee Malecela

Also, viongozi wetu wa sasa wapo kwa ajili ya wao wenyewe kitu ambacho kinakwamisha sana maendeleo na hivyo HAKI kutokuwepo, na kama haki hamna in most cases yaani hapo democracy haitokuwepo kamweeeee, kwanza kumnyima mwenzako haki yake "is not a democractic act", sasa sijui kwa nini viongozi wa tz kila kukicha wanaongelea kuhusu democrasia wakati wanajua itawabana !!
 
Back
Top Bottom