Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Miezi ya mwanzoni Mzee wa Richmonduli ama EL alikuwa anapita sana kwa wahindi na kuomba mapesa kwa njia hizo .Sasa sijui ni maandalizi ya Uchaguzi wa Urais wake au ilikuwa kuwaeleza kwamba yeye sasa ni namba 3 toka juu sielewi but his agents have been doing for sometime .Nia yao siijui wewe unasemaje ?Hata mzee Es aliwagi kupiga kelele juu ya move za Lowasa .
 
Tuangalie maana ya Rushwa kutoka PCB www.tanzania.go.tz/pcb/rushwa/maana/html

Rushwa imetafsiriwa kwa namna mbalimbali kama ifuatavyo:

1. Kamusi ya kiswahili sanifu imetoa maana ya rushwa kuwa ni fedha au kitu chochote cha thamani kinachotolewa na kupewa mtu mwenye madaraka ya jambo fulani ili apate kupendelea au kutoa haki kwa asiyestahiki. Rushwa inajulikana kwa maneno mengine kama; chai, chiriri, hongo, mrungula, ufisadi.

2. Taasisi ya maendeleo ya uchumi ya Benki ya Dunia (The Economic Development Institute of the World Bank) katika kitabu chake kilichoandikwa na Petter Langseth etal,’’National Intergrity system country studies” imetafsiri rushwa kuwa ni matumizi mabaya ya madaraka ya umma kwa faida binafsi. Pia inaainishwa kuwa rushwa inahusu tabia ya baadhi ya Watumishi katika sekta ya umma, Wanasiasa au Watumishi wa serikali ambavyo wanajihusisha kinyume na sheria kujinufaisha wao binafsi au ndugu zao kwa kutumia vibaya madaraka waliyopewa. Rushwa ipo katika namna nyingi kama vile: hongo, kujitwalia mali ya umma kwa matumizi binafsi, ubadhilifu wa fedha za umma.

3. Kamusi ya kiingereza ya oxford inatafsiri Rushwa kuwa ni upotovu au kuvunjika kwa maadili au uaminifu katika kutekeleza shughuli za umma kwa hongo au upendeleo.


Aina za rushwa
1.Rushwa ndogondogo...
2. Rushwa kubwa
Kundi hili linajumrisha viongozi na watumishi wa umma wa ngazi za juu ambao kuhusika kwao katika rushwa kunatokana na uroho na kujilimbikizia mali na fedha. Hawa ni wale ambao vipato vyao halali vinatosheleza mahitaji yao ya msingi na wana mali na fedha za kutosha. Kundi hili linatumia mbinu mbalimbali kudai na kupokea rushwa kama ifuatavyo: -

(i) Viongozi wanaopaswa kutoa maamuzi muhimu ya kitaifa huhongwa na wafanyabiashara hao; wanapeana madaraka ya wenyekiti au ukurugenzi katika Bodi za mashirika ya umma kwa upendeleo na bila ya kuzingatia ujuzi, uwezo na maslahi ya Taifa na wamekuwa wanaingilia shughuli za watendaji wakuu kufanya maamuzi kama ya kugawa maeneo ya uwindaji au maeneo ya ardhi yasiyoruhusiwa kisheria.

(ii) Watendaji wakuu wanapokea rushwa ili wakiuke kanuni na taatibu za kutoa zabuni, kutoa misamaha ya kodi mbalimbali na kuzingatia katika mikataba ya ujenzi na makampuni kwa ajili ya kazi za kitaifa bila kujali maslahi ya Taifa. Vilevile watendaji wakuu na maafisa watendaji wamekuwa wanaficha udhaifu wa viwango vya ujenzi na uhafifu wa vifaa au huduma na kuidhinisha malipo ili waweze kupata kamisheni na wamekuwa wanatoa nafasi za masomo nje ya nchi baada ya kupata chochote.

(iii) Wanasiasa hutoa rushwa kwa wajumbe wakati wa uchaguzi ndani ya vyama vya siasa au kwa wananchi katika chaguzi ili waweze kupigiwa kura au wananchi waweze kuwapigia kura wagombea wao.

(iv) Wabunge nao wamekuwa wanatoa rushwa kwa wapiga kura ili wachaguliwe, wamekuwa wanawasilisha madai ya uwongo kuhusiana na shughuli zao za ubunge, wanahonga waandishi wa habari ili waandike habari nzuri zinazowahusu na wamekuwa wanadai zawadi wanapotembelea viwanda vya umma na vya binafsi. Wabunge waliopo kwenye kamati mbalimbali za bunge huomba takrima, fedha taslimu na hulipiwa mahali pa kulala na wakuu wa mashirika au Idara wanazozishughulikia.


Kwa mantiki hiyo, hiyo nayo ni rushwa!
 
Lakini ni viongozi wangapi ambao hupewa ufadhili na wafanyabiashara au baadhi ya watu ukifichwa kama ushabiki na mapenzi? Madaktari wangapi hupewa "asante" na baadhi ya wagonjwa matajiri baada ya kunusuru maisha yao au ya wale wawapendao? Nakumbuka daktari mmoja ambaye alijengewa nyumba na mhandisi mmoja wa Kimarekani kule Mbeya baada ya daktari huyo kuokoa maisha ya mke wa mhandisi! Sasa sijui kama ile ilikuwa rushwa au asante tu!!
 
Hiyo ni rushwa ya wazi kaka. Hata kaika takrima haipo. Pia zawadi ni kufuru kuiitta hivyo.

Ni ufisadi mzee mwanakijiji
 
sasa viongozi wasipewe zawadi au misaada na wananchi wenzao au wapiga kura wao? Kama mtu akakutendea jambo na unauwezo wa kutoa shukurani kwa kutoa zawadi, bidhaa au huduma fulani ni kosa gani hilo?
 
Lakini ni viongozi wangapi ambao hupewa ufadhili na wafanyabiashara au baadhi ya watu ukifichwa kama ushabiki na mapenzi? Madaktari wangapi hupewa "asante" na baadhi ya wagonjwa matajiri baada ya kunusuru maisha yao au ya wale wawapendao? Nakumbuka daktari mmoja ambaye alijengewa nyumba na mhandisi mmoja wa Kimarekani kule Mbeya baada ya daktari huyo kuokoa maisha ya mke wa mhandisi! Sasa sijui kama ile ilikuwa rushwa au asante tu!!
Kwa mfano huu wa Daktari nafikiri hiyo ni zawadi au shukrani kwani walitoa baada au alimjengea baada na hakukuwa na mzingira yeyote ya kuomba kabla ya huduma na wala kurudi tena kuomba msaada baada ya kutoa au kujenga.
 
KNKCU, ila unafikiri huyo Mhandisi leo akipatwa na kaugonjwa na akaenda hospitalini kweli atasubiri kwenye foleni? au huo msaada wake umemnunulia ufunguo wa ofisi ya daktari wetu? Kama amemsaidia kumjengea nyumba Daktari huoni kuwa huyo Mhandisi anastahili angalau kidogo kupata kaujiko akifika ofisini kwa daktari ukilinganisha na sisi wengine ambao hata kufagia nyumba ya daktari hatujafagia?
 
KNKCU, ila unafikiri huyo Mhandisi leo akipatwa na kaugonjwa na akaenda hospitalini kweli atasubiri kwenye foleni? au huo msaada wake umemnunulia ufunguo wa ofisi ya daktari wetu? Kama amemsaidia kumjengea nyumba Daktari huoni kuwa huyo Mhandisi anastahili angalau kidogo kupata kaujiko akifika ofisini kwa daktari ukilinganisha na sisi wengine ambao hata kufagia nyumba ya daktari hatujafagia?
Hapa itategemea na msimamo wa huyo Daktari na lengo la huyo aliyejenga hiyo nyumba na kama alijenga kwa kushukuru hawezi kurudi na kutotaka kupanga foleni na kama Daktari hana tabia ya kupindisha sheria first come first to be saved then ataendelea na majukumu bila ya matatizo na kama kuna ambaye atahudumiwa bila ya kufuata utaratibu wowote ni yule wa emergency na hapa kama Daktari anajua kazi yake na muungwana atawaomba radhi wagonjwa waliotangulia kwa kuwafahamisha umuhimu wa kumuona huyu ambaye maisha yake yapo hatarini zaidi na wagonjwa wanakubali wanapoelezwa hali halisi na kuiona.Hapatakuwa na muingiliano wowote kwani wote walifanya kwa nia njema.Aliyetoa alitoa kwa nia njema na aliyepokea alipokea kwa njia njema.Kabla ya kutoa hakuombwa na kabla ya kupokea hakuomba.Rejea yule Waziri wako aliyepita kwenye yale maduka ya kina Bushiri et al.
 
kwa hiyo kama mtu hakuomba au kuonesha kuomba akapewa basi inawezekana isiwe rushwa...!!
 
kwa hiyo kama mtu hakuomba au kuonesha kuomba akapewa basi inawezekana isiwe rushwa...!!
MAELEZO YAKO HAPO ONGEZA NA HAKUJENGA MAZINGIRA AU MIANYA YAKUMFANYA MTU AMPE CHOCHOTE AU AMFANYIE CHOCHOTE KWA MINAJILI YA KUPEWA HUDUMA AMBAYO KWA MUJIBU WATARATIBU AU SHERIA ALITAKIWA AMHUDUMIE KAMA MOJA YA KUTIMIZA WAJIBU WAKE KIKAZI.
Hivyo kutokana na mfano wa Daktari ulioutoa hapo awali mazingira hayo yote yaliyoanishwa hapo juu hayakuwepo.Tena huyu Engineer ni Mgeni Ambaye hivi tunapoandika hapa huenda amesharudi kwao Marekani.Na huenda hategemei tena kupata huduma kutoka kwa huyo Daktari,Mazingira ya mfano wako yanashahabiana zaidi na Ahsante , Kushukuru au Zawadi.
 
MWJJ,
Just how hypothetical is this scenario?
On one hand it sounds sooo familiar..on the other hand, it leaves a lot of questions.
As I know it, and I have proof of it; viongozi wengi; and I dare say waliokuwepo katika awamu iliyopita walitumiwa vibaya sana na wafanyabiashara wakubwa kwasababu ulizozibainisha hapo...NJAA!
Ilifikia mahali maofisa wadogo wa TRA au Customs wanaogopa kukamata mali za watu fulani kwasababu mara watakapofanya hivyo jamaa anapiga simu kwa mkubwa, na bila aibu huyo mkubwa(waziri) anapiga simu kwa bosi wa huyo ofisa mdogo, as a result, wakati bado wako kwenye tukio na huyo mfanyabiashara, huyo ofisa mdogo wa TRA/Customs anapigiwa simu kuwa aachane na huyo jamaa mara moja. You can imagine the embarassment they 'boys' suffer
Hii ilikuwa kawaida, and if they are here and they are honest they will confirm this cos I know of some instances myself.
Hao mawaziri bahati mbaya sana bado wako kwenye chati, only that kale ka confidence kamepotea, and this is where I give credit to Jeikei..whatever poison he gave them in Ngurdoto made them wary...Jeikei's unpredictability has proved to be a positive thing in some areas..wale walafi wame-shrink kidogo. As a result, hata ile kiburi ya hao wafanyabiashara nayo imeshuka..Imebakia ya mpambe wa EL ambae analipiza kwa yale aliyokuwa akiyaona enzi hizo kwa wenzake!

So, is your case hypothetical, or, ni kwamba umepata data ambazo hazijakamilika ukaamua kuileta kama hypothetical case ili kuwa kwenye safe side?
 
kama mtu alifurahisha na huduma au kitu chochote ni bora akamwomba muhusika achague charity yeyote iliatoe hiyo ahsante au shukrani yake,baadala ya kumpa muhusika.kinyume cha hapo ni rushwa tu.
 
Mwendapole, the case is hypothetical to the extent that revealing the names and actual places where this incident occured would compromise the sources.. beyond that, it is hypothetical because i said so...
 
Well, that answers my question.
It also confirms my suspicion. It also shows that people knows a lot, and are not happy with what they know,but what can they do...the rich are getting richer while the poor are getting poorer..and the gap between the two is awesome...Pengine iko siku tutakuwa na responsible leaders (that is, when wishes will be horses)
 
Kwa kweli nakerwa sana na matangazo yanayorushwa na television ya taifa ya kupiga vita rushwa ambayo yameandaliwa na Taasisi ya Kupiga Vita Rushwa Tanzania. Hapo unaoneshwa traffic akisimamisha daladala halafu anapewa rushwa ya shs 5,000/= analiachilia. Au unaonyeshwa hakimu akimwachia mtuhumiwa baada ya kupewa rushwa ya kama shs 30,000 (kama niliziona vyema kwenye TVT) Vile vile, kuna nesi analazimisha rushwa itolewe ili mgonjwa apigwe X-Ray.

Kweli, hizi rushwa ndizo zinaonekana mbovu sana katika taifa na za kukemewa mpaka kwenye runinga? Mbona hamtuonyeshi mfano wa kigogo mmoja akiingia mkataba wa kuleta/kununua umeme Tanzania? Au wa kununua rada? Au kujenga twin towers za benki kuu? Hizi ni rushwa ambazo kila mtanzania, (pamoja na wewe unayetarisha matangazo hayo) ameathirika. Bei ya umeme imepanda, na kuna tetesi tena kuwa itapanda mwezi wa sita. Priorities zetu za kupiga rushwa ziko wapi? Mmewapigia kelele weee Hakielimu kuwa wanatoa matangazo ya kudhalilisha taaluma za wafanyakazi wa serikali, nanyi mmeanza kufanya hayo hayo. Lakini naamini kuwa mmeanza kufanya hivyo ili ku-divert attention ya wananchi kwenye hizo rushwa kubwa kubwa ambazo zinafanywa na viongozi wa serikali.

Haya, endeleeeni. Labda ndio the best approach. Mimi nayaunga mkono mawazo ya Doc. Mwakyembe wakati wa kujadili mswada wa kupiga vita rushwa.
 
?
Kwa kweli nakerwa sana na matangazo yanayorushwa na television ya taifa ya kupiga vita rushwa ambayo yameandaliwa na Taasisi ya Kupiga Vita Rushwa Tanzania. Hapo unaoneshwa traffic akisimamisha daladala halafu anapewa rushwa ya shs 5,000/= analiachilia. Au unaonyeshwa hakimu akimwachia mtuhumiwa baada ya kupewa rushwa ya kama shs 30,000 (kama niliziona vyema kwenye TVT) Vile vile, kuna nesi analazimisha rushwa itolewe ili mgonjwa apigwe X-Ray.

Kweli, hizi rushwa ndizo zinaonekana mbovu sana katika taifa na za kukemewa mpaka kwenye runinga? Mbona hamtuonyeshi mfano wa kigogo mmoja akiingia mkataba wa kuleta/kununua umeme Tanzania? Au wa kununua rada? Au kujenga twin towers za benki kuu? Hizi ni rushwa ambazo kila mtanzania, (pamoja na wewe unayetarisha matangazo hayo) ameathirika. Bei ya umeme imepanda, na kuna tetesi tena kuwa itapanda mwezi wa sita. Priorities zetu za kupiga rushwa ziko wapi? Mmewapigia kelele weee Hakielimu kuwa wanatoa matangazo ya kudhalilisha taaluma za wafanyakazi wa serikali, nanyi mmeanza kufanya hayo hayo. Lakini naamini kuwa mmeanza kufanya hivyo ili ku-divert attention ya wananchi kwenye hizo rushwa kubwa kubwa ambazo zinafanywa na viongozi wa serikali.

Haya, endeleeeni. Labda ndio the best approach. Mimi nayaunga mkono mawazo ya Doc. Mwakyembe wakati wa kujadili mswada wa kupiga vita rushwa.
Watayarishaji wa hayo matangazo ni nani? waombwe watayarishe na matangazo yanayohusu Rushwa kubwa kubwa kama za mikataba inayofanywa na viongozi na wahisani ,Bila ya kusahau viongozi na wawekezaji tena itolewe kwa Lugha zote mbili kiswahili na kiingerza ili jamii ifadike na ujumbe uwafikie na wahusika wasio wazawa.
 
Mwandishi Wetu
HabariLeo; Saturday,April 28, 2007 @00:02

Ni baada ya Sitta kumaliza suala la Mengi na Malima

Ndesamburo asema haamini kama uchunguzi utaachwa

TAASISI ya Kuzuia Rushwa (PCB) imesimamisha uchunguzi dhidi ya wabunge wanaotuhumiwa kula rushwa wakati wa kusikiliza shauri kati ya Mbunge wa Mkuranga, Adam Malima na Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi.

Mkurugenzi wa PCB, Edward Hosea jana alithibitisha taasisi yake kuacha uchunguzi huo baada ya Spika wa Bunge Samuel Sitta kutangaza kufunga mjadala kuhusiana na suala la Malima na Mengi.

“Spika mwenyewe ametangaza kufunga mjadala huo. Wewe unataka sisi tuendelee nalo la nini,” alisema Hosea alipoulizwa na HabariLeo kuhusu hatua iliyofikiwa na PCB katika uchunguzi wake.

Alisema kwa vile Sitta ameamua kufunga mjadala wa suala hilo, taasisi yake imeona hakuna haja tena ya kuendelea na uchun guzi wake, “Siyo sisi tuliofunga ila ni bunge lenyewe…Mjadala wa hilo umefungwa.”

Hosea ametangaza kufunga uchunguzi wa suala hilo wakati tayari alikwisha kuahidi kuwa taasisi yake ingewahoji wabunge wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge baada ya kikao kilichomalizika wiki iliyopita. Mkurugenzi huyo alitoa ahadi hiyo kabla ya tangazo la spika alilolitoa katika kikao hicho.

Hosea pia aliahidi kuwa wahusika wote katika sakata hilo wangehojiwa bila kujali cheo wala nafasi ya uongozi aliyonayo katika serikali. Tayari PCB ilishaanza kumhoji Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo ambaye ndiye mtu wa kwanza kutoa tuhuma hizo hadharani. Wakati Ndesamburo anatoa tuhuma hizo, alitangaza kujiuzulu ujumbe katika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa kile alichodai kubaini ufisadi kufanywa kwa wajumbe wa tume hiyo hivyo akahofu kutotendeka kwa haki.

Ndesamburo alidai Yussuf Manji kuwa ndiye aliyetoa rushwa hiyo. Mbunge huyo alidai pia kuwa tuhuma hizo aliambiwa na Mengi ambaye pia alipigiwa simu na Waziri Mkuu Edward Lowassa akimtaka afute shauri hilo kwa vile tayari walikwisha kuhongwa.

Kutokana na tuhuma hizo, Sitta aliamua kuikabidhi PCB kufanya uchunguzi wa tuhuma hizo baada ya kutolewa na mbunge huyo mtu mzima na mzoefu. Spika alisema tuhuma hizo haziwezi kupuuzwa hata kidogo kwa vile ni kosa la jinai ambalo mbunge hana kinga yoyote.

“Nimeikabidhi PCB ili uchunguzi ufanywe kubaini ukweli na hatimaye kuachia sheria ichukue mkondo wake,” alisema Sitta wakati akieleza sababu za kuiomba taasisi hiyo kuchunguza tuhuma hizo alizodai ni nzito kwa wabunge.

Kuonyesha kuwa hakuwa anatania, Ndesamburo amekuwa akiandika kitabu kuhusiana na namna Malima na Mengi walivyoshughulikiwa vibaya na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.

Ndesamburo alipotafutwa jana aeleze maoni yake kuhusiana na hatua ya PCB ya kufunga uchunguzi huo alishangaa kusikia kuwa PCB haitaendelea kuwahoji wabunge kuhusiana na tuhuma za kula rushwa. Ndesamburo alisema, yeye alishahojiwa na PCB hivyo alitarajia kuwa wahusika wengine wangehojiwa hata baada ya Sitta kusema kuwa suala hilo limekwisha.

Ndesamburo alisema anaamini suala hilo bado lipo hai kwani hata PCB yenyewe hawajamjulisha kuwa hawataendelea kuwahoji wabunge wengine hasa ikizingatiwa kuwa yeye alishahojiwa na PCB iliahidi kuwahoji baada ya kumalizika kwa kikao cha Bunge kilichomalizika wiki iliyopita.
 
Back
Top Bottom