BINARY NO
JF-Expert Member
- Dec 29, 2011
- 2,148
- 2,160
TANESCO Ilemela Mwanza ndo funga kazi... Rushwa imetamalaki kuna mzee mmoja alilipia mwezi wa 7 mwaka Jana ndo kafungiwa ijumaa hii iliyopita na apo walishamgonga 50,000 juzi kuwapigia wakashtuka kua duh mwezi wa saba ndo wakampigia kuja wanataka tena 30,000 ya rushwa ndo wamfungie.@TANESCO NYAKATO ni mabingwa wa kuomba rushwa ,yani kuunganisha umeme imekua kama hisani wakati ni haki yetu na tumelipia, Mimi unaingia mwezi wa 6 sasa sijaunganishiwa umeme tangu nilipie mwaka Jana mwezi wa 10,kuna boya wa hapo Nyakato anaomba rushwa ya laki 2 Ili nipatiwe huduma wakati nilishalipa 27 elfu. Poor Tanesco
Tatizo tulilonalo sasa ni Viongozi wetu kua km hawapo yani wameshakata tamaa... #Mh waziri January Makamba upole wako uliokithiri umelirudisha shirika letu hili kwenye rushwa ya kiwango cha lami.
Waziri Kelemani nadhani alikua MTU sahihi kwenye hili shirika kwani alikua anafuatilia mikoani na kwa mameneja wa kanda...Lakini sijawahi ona Makamba akifanya ziara zaa ufuatiliaji... Watu waamelipia tokea Mwaka Jana mwezi wa 10 mpaka Leo miezi 6 hakuna huduma ya umeme, Waziri yupo, RC yupo,DC yupo ata Meneja nae yupo lakini hakuna ufuatiliaji wowote.
Mbaya zaidi tunaona matajiri wakifungiwa Je hizo meter zinatoka wapi? Kongore kwa #Tanesco mkoa wa Mara kwa kuwamaliza wateja wenu wote waliolipia kabla ya 05/01/2022...
Kuna haja ya viongozi wakubwa wenye uchungu na nchi hii kufatilia kwa ukaribu hizi rushwa za Tanesco... Tunakukumbuka mh Waziri Kalemani kwa ufuatiliaji wako makini sasa nimepata picha kwann waTZ walikua ............