Imekuwa ni kawaida ya mbunge wa Mwibara mh Kangi Lugola kutembea na Ilani ya CCM mkononi mwake. Juzikati aliitwa na Takukuru kwa mahojiano na alipofika alilisalimia kundi la waandishi wa habari kwa kuwapungia kitabu cha ilani ya CCM.
Nitoe tu angalizo kama mh Kangi Lugola atapandishwa katika mahakama ya mafisadi basi kwa haraka sana chama kimzuie kupanda kizimbani na kitabu cha Ilani.
Haitaleta picha nzuri kwa wananchi endapo Ilani ya uchaguzi ya CCM itanajisiwa.
Huyu Kangi alisema hajawahi kuona Mtu Muongo Duniani kama Prof Assad, kisa waliulizwa MZIGO wa Uniform mliingiza kwa meli ipi onesheni bill of lading, Scanner za TPA mbona hazina record ya kupita mzigo huo, mbona Account ya Mzabuni haijawahi kutuma fedha nje kununulia mzigo huo
Kangi hakuwa Waziri wakati wa Sakata la Uniform lakin kama kawaida ya Mabaharia lazima wateteane akawatetea wenzie, la kwake wenzie wamejitenga wanamrushia Nanga ajiokoe kwa dhoruba ya Baharini badala ya Boya
Hatuwezi kwenda kwny Uchaguzi bila ya kutoa kafara watu waone Mahakama ya Mafisadi ikiwa kazin
johnthebaptist,
Shetani hawezi kwenda popote bila mapembe yake , atamuachia nani ?
Kingine ni hiki , mvunja ilani mkuu ni Magufuli , mbona hujawahi kumkoromea asivae sare za ccm ?
Ilani ya ccm aliyozunguka nayo Magufuli kuomba kura nchi nzima 2015 imeandika namna ya kuwasaidia watoto wa kike kurudi shule baada ya kupata mimba na kujifungua , mbona Magufuli hakuheshimu hilo ?
johnthebaptist, Mkuu niambie ni jizi gani kutokea chama cha upinzani kapandishwa mahakamani kwa kesi zenu za wizi. Majizi yote yanayopandishwa kizimbani yanaijua ilani ya CCM au wanayo mifukoni.
Mnamuonea wivu, mwenzenu kaisom a na kuitafsiri hadi ikamuwezesha kujipatia mabilioni. Mbinu zoooote za wizi zinapatikana kwenye kile kijitabu ndiyo maana anakithamini kwani kimemuondolea umasikini. Yule sasa ni bilionea siyo mwenzenu tena. Na kwa vile siku hizi mahakama zimepewa uwezo wa ku compromise na mafisadi atatoka tu kujilia mabilioni yake.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.