Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,801
- 71,226
Nadhani wote sasa tumekwisha ona na kupata picha za mgogoro huu wa ubinafsishaji wa Bandari na mchakato mzima na jinsi habari za wajumbe wa Kamati ya Bunge ya miundo mbinu walivyosafirishwa kwa gharama za mamlaka ya Dubai na kupokea rushwa mbalimbali ikiwemo fedha kuzagaa.
TAKUKURU ambayo gharama zake kubwa za kuiendesha tunazitoa sisi lakini hakuna la maana kama hili wanashughulika bali wao wako busy na makarani wa mahakama, manesi na watumishi wadogo lakini wahujumu kama hao wabunge hawaguswi na wanakuja kutuharibia nchi.
Je, TAKUKURU ivunjwe na kuundwa chombo kipya au tufanyeje maana hawa wameshindwa.
TAKUKURU ambayo gharama zake kubwa za kuiendesha tunazitoa sisi lakini hakuna la maana kama hili wanashughulika bali wao wako busy na makarani wa mahakama, manesi na watumishi wadogo lakini wahujumu kama hao wabunge hawaguswi na wanakuja kutuharibia nchi.
Je, TAKUKURU ivunjwe na kuundwa chombo kipya au tufanyeje maana hawa wameshindwa.