Wakati malumbano mbalimbali yanaendelea kuhusu hoja alizotoa Mh Sophia Simba bado kuna mengi aliyoyasema ambayo bado hayako katika public forum.
Hizi ni habari za ndani zilizotujia.
Mh Sophia aliwaambia wabunge wa kamati maalumu inayoongozwa na Mzee Ruksa kuwa hii nchi inayumbishwa na watu wanne ambao ni Speaker Sitta, Bernard Membe ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje ya Nchi, Rostam Aziz na Edward Lowassa. Alisema ni muhimu baada ya bunge kumalizika kamati ikawaita na kuwahoji na kuuliza wanaipeleka wapi nchi yetu.
Waziri Sophia alisema kwa namna zote watu hawa ni wahusika wakuu wa mambo yanavyokwenda sasa hivi kwa hiyo kamati hiyo inayoheshimika iwaite watoe ufafanuzi na waseme wanataka kuifikisha nchi wapi.
Sophia alisema kundi la kina Spika lenye wabunge wanaojinadi kuwa vinara wa kupinga ufisadi wakiongozwa na mpendwa wao mfanyabiashara Reginald Mengi wenyewe sio wasafi hata kidogo.
"Hakuna mtu msafi pale, sema tu serikali ina namna ya kushughulikia mambo yake," alisema.
Alitoa mfano wa mama Anna Kilango kuwa alishakutwa na madawa za kulevya nyumbani kwake kabla ya kuolewa na Mh Malecela. Pia, Jeetu Patel ambaye anasemekana kuwa ni fisadi papa, aliwachangia harusi yao fedha nyingi sana, zaidi ya sh millioni mia mbili hivyo haelewi nani ni fisadi kweli - aliyetoa au aliyepokea.
Alisema Malecela alishajipanga kuwa rais wa Tanzania na mkewe first lady, na kwa kuwa hayo hayakutokea, kelele za mama Kilango sasa hivi ni hasira hizo.
"Ninawaeleza ninyi haya yote ili mnapofuatilia haya mambo ni vizuri mkajua chimbuko lake ili kuweza kuyapatia utatuzi," Sophia aliiambia kamati.
Alimgeukia pia kinara wa wapambanaji Reginald Mengi kuwa magazeti yake yamekuwa yakiandika habari za kuichafua serikali na chama cha CCM.
Alihoji hela mfanyabiashara huyo anazotumia kuzunguka nazo nchi nzima eti vikoba zinatoka wapi? "Wanafikiri zinatoka mfukoni kwa Mengi, lahasha, pesa hizo zinatoka kwa mabalozi hivyo wajue wanashirikiana kuihujumu nchi."
Aliongeza: "Tunafahamu mambo mengi kukaa kimya hakumaanishi hatujui kitu tuna vyombo vya dola vipo makini vina taarifa zote lakini kama serikali, tuna namna ya kushughulikia mambo kwani hii nchi inaongozwa na utawala wa sheria hivyo lazma sheria ifuate mkondo wake."
Sophia alisema ukimfuatilia sana Mengi na utajiri wake utaona kuwa chimbuko lake ni hao hao wahindi anaowatuhumu kila kukicha huku akifikiri hatumjui kuwa yeye sio Mr. Clean hata kidogo.
Aliwaonya wabunge hao wajitenge na Mengi kwani anawapotosha kwa kiasi kikubwa.
Alisema ujinga wa Mengi unaonekana pale anapojitahidi kila kukicha kujifananisha na rais. Anachofanya rais, na yeye eti anafanya. Rais Mengi huyo ameteuliwa na nani? Sophia aliuliza.