Sofia Simba na Sakata la Mafisadi na Wapiganaji!

Sofia Simba na Sakata la Mafisadi na Wapiganaji!

hawa wapuuzi; yeye kasema kadi yake ni ya mwaka fulani, ya namba fulani imetolewa Kisutu; huyo mtu wa CCM anatakiwa kusema "hiyo kadi ni yauongo, kadi yenye namba hii haipo, na tawi la Kisutu halikutoa kadi hiyo tarehe na mwaka huo"...

Habari imekwisha; lakini katika wazimu wao wanataka mtu awapigie magoti, awalambe lambe, awamwagie maua na kuwaimbia wimbo wa CCM nambari one.
Sio kuwapigia magoti.
Ukweli ni kwamba, wana namba za kadi na majina yote ya wanachama wao mkoa wa Dar na jina la mengi halipo.

Kwa sababu yeye ni fisadi,inawezekana anakadi feki
 
Ahh!! Sio kundi la taarabu ni SEGERE maana Taarabu inachezwa ndani ya ukumbi mara nyingi lakini SEGERE popote yaani sisi ndio Wapiga kura SASA tunangoja nini jamani Si mmeona vituko vya viongozi? Haya Fikiria huyu Mh. Lion yaani amemwaga pwaaaa!! sasa wewe kazi kwako mimi kura yangu CHADEMA WEWE JE..................
 
KWELI MAGEZI(has no status)UMENENA JAPO UMEFIKA MBALI SANA KWA DEVALUATION YA MH WAZIRI SIMBA,
EEEEEEEEEH,HAYA NDO MAMBO YA KUANGALIA BW. JK PINDI TUTAKAPO MUONGEZEA MIAKA MINGINE 5.
HIVI JAMANI KUTEUA MTU KUWA WAZIRI KUNAHITAJI PHD? KUMJUA YUPI ANAFAA NA YUPI HAFAI, HEBU TUWE WAZALENDO WA KWELI VIONGOZI WA KIAFRIKA.

Nani alikwambia tuna mpango wa kumuongezea miaka mingine mitano? Ili afanye nini?
 
Mkuu umefika mbali sana na hizi comments na sijajua ni kitu gani kime prompt hizo personality attacks.Bangi ? Msanii ? anyway. Mie huwa nashauri watu ku dwell kwenye hoja na mimi mara zote nikiwa sina cha kujibu huwa naacha kuandika kuliko kumvamia mtu kwa matusi . I am not happy na hizi comments

Mods, Lunyungu is right!! huyu engineer hajafanya sawa...pls!!!!!!!
 
Mh Sophia aliwaambia wabunge wa kamati maalumu inayoongozwa na Mzee Ruksa kuwa hii nchi inayumbishwa na watu wanne ambao ni Speaker Sitta, Bernard Membe ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje ya Nchi, Rostam Aziz na Edward Lowassa. Alisema ni muhimu baada ya bunge kumalizika kamati ikawaita na kuwahoji na kuuliza wanaipeleka wapi nchi yetu.

Alitoa mfano wa mama Anna Kilango kuwa alishakutwa na madawa za kulevya nyumbani kwake kabla ya kuolewa na Mh Malecela.

Alihoji hela mfanyabiashara huyo anazotumia kuzunguka nazo nchi nzima eti vikoba zinatoka wapi? "Wanafikiri zinatoka mfukoni kwa Mengi, lahasha, pesa hizo zinatoka kwa mabalozi hivyo wajue wanashirikiana kuihujumu nchi."

Sophia alisema ukimfuatilia sana Mengi na utajiri wake utaona kuwa chimbuko lake ni hao hao wahindi anaowatuhumu kila kukicha huku akifikiri hatumjui kuwa yeye sio Mr. Clean hata kidogo.
Aliwaonya wabunge hao wajitenge na Mengi kwani anawapotosha kwa kiasi kikubwa.

Mtoa habari,
Asante kwa makala. Mie nina maswali kidogo hapa kama utaweza kumwaga habari zaidi itakuwa mswano sana sana.

1. Alisema nini juu ya Membe, Rostam Azziz na Lowassa zaidi ya hayo maneno?

2. Hii story ya mama Kilango kukutwa na Madawa ya kulevya ni ya kweli hii? Kama ni kweli basi huyu mama kweli alitumwa na mtu mmoja mkubwa sana maana hizi habari zitafumua siri nyingi sana Tanzania.

3. Hii ya Mengi kupata pesa kutoka nje ya nchi imeshaongelewa hapa JF kama sikosei. Kuna mtu mwenye habari zaidi? Nafikiri kidogo kidogo nchi itarudi kwa Watanzania wenyewe.

Kama huyu mama ndiyo BOSS wa vyombo vya usalama, na ana uwezo wa kwenda hadi ndani ya hizo ofisi na kusoma habari za ndani, basi anaweza kuwa anasema kweli, Na kama anadanganya, basi inatakiwa ahukumiwe kama JASUSI na apigwe risasi.
 
............Mzee Malecela siyo daktari wa mama Sofia kwahiyo mama Sofia anabaki kuwa mtu na akili yake timamu isipokuwa baada ya kumwaga radhi majuzi hapa kuna watu badala ya kujibu hoja wakaja na viroja na mipasho ya kinamama.

Pia tukubali kwamba kabla hata daktari hajatoa ushuhuda wake, ni watu wakawaida (majirani, marafiki, nk.) wanaogundua abnormalities na kumfikisha mtu kwa daktari.
 
Sio kuwapigia magoti.
Ukweli ni kwamba, wana namba za kadi na majina yote ya wanachama wao mkoa wa Dar na jina la mengi halipo.

Kwa sababu yeye ni fisadi,inawezekana anakadi feki



Hvi, mtu ukiwa na utajiri sasa hivi TZ maana yake wewe ni fisadi?

Halafu Samwel, kwa jinsi ninavyoijua hali ya TZ, ofisi za serikali tu zingine haziko "computerized", sasa niambie ofisi za CCM, tena tawi....watakuwa na mfumo mzuri wa kutunza kumbukumbu kweli? Mtindo wenyewe wa kuhifadhi kumbukumbu katika mafaili ya karatasi, hadi utafute jina la mwanachama ukalikosa na kuwa na uhakika kwamba kweli halipo ni kazi kubwa sana.

Simtetei Mengi, ila give the guy a break. Pia namshauri kama hawamtaki, si ahamie chama kingine? Au awe tu mwananchi asiyeambatana na chama chochote? Kwani lazima jamani?
 
Mkuu FMES,

Sijui una maana gani hapo juu? Shauri ya box kunibana, sijafuatilia huu mjadala zaidi ya mchango niliotoa siku ile thread hii ilipoanza.

Kuendelee kuandika majina ya watu wengine ambao hawahusiki na mjadala huu sidhani kama inasaidia kwenye utetezi wako.

Kuna tofauti kubwa kati ya kinachojadiliwa kwenye thread hii na hayo uliyoyaandika ya Mwakalinga. Waziri Sophia ametamka wazi mbele ya vyombo vya habari na mbele ya viongozi wa chama chake, hivyo kama madai yake ni ya uwongo kuna njia nyingi ambazo wahusika wanaweza kuzifuata kuhakikisha majina yao hayachafuliwi.

Hilo la Mwakalinga, linasemwa na wasanii, ambao wanajificha kwenye migomba kabla ya kutamka neno. Kama wanaamini hivyo waseme wazi kama alivyosema Simba naamini huyo Mwakalinga kesho yake atakuwa anapambana nao mahakamani.

Ni muhimu kuweka wazi kwamba ukiachia madai wanayotoa kupitia JF, hakuna kiongozi hata mmoja anayeweza kusimama kwenye vyombo vya habari akasema Mwakalinga kapewa milioni 400 na Lowassa maana hata hao wanaopenyeza hayo maneno wanajua hayana chembe hata ya ukweli na hawako tayari kuona wanaburuzwa mahakamani.

Mwisho, Mwakalinga hana nia wala sababu ya kufadhiliwa na mtu yeyote. Kama ni ubunge basi atajifadhili mwenyewe.

Nafikiri kwenye maandishi yako hapo juu humtendei haki Mwakalinga kwa kuweka statement kama hiyo ambayo inaweza kuwafanya watu ambao hawajafuatilia jambo kama hilo waamini kuna madai kama hayo yametolewa kiwaziwazi.

- Mkuu Mtanzania, kwa kawaida huwa nina tabia ya kukataa upuuzi regardless unaelekezwa kwa nani, samahani sana kama nimekukwa za na huo mfano wangu nia haikuwa kutomtendea haki Mwakalinga, nia na madhumuni ilikuwa kuweka wazi kwamba pamoja na kushuka sana kwa maadili ya uongozi Tanzania, haina maana wananchi wote pia tumeishiwa maadili, kuna ambao bado tunayo, tunayasimamia na tunayaishi, na tunazikataa kabisa hizi siasa za kwa kuwa mimi ni fisadi, basi ni lazima nihakikishe wote tunaonekana mafisadi,

- Hii tabia mpya iliyozuka ya viongozi uchwara na machangudoa kama Sophia, ya kuamka tu kuanza kuongea pumba bila facts, kwa Waziri Wa Ofisi Ya Rais anayesimamia Takukuru, anasimama mbele ya kamati muhimu kama hii ya Mwinyi na kujigamba kwamba CCM hakuna msafi, na kwamba Lowassa ni kiongozi bora na hana makosa yoyote, ni lazima wananchi wastaarabu kama mimi tuikatae na tutaikataa mpaka mwisho wa dunia.

- Katika kuongea siasa huwa tunatumia mifano yote ya kisiasa, Mwakalinga aliposhutumiwa hapa JF kuwa amepokea hela za Lowassa nilikuwa wa kwanza kusimama kama sasa kutaka facts, aliposhambuliwa tena hapa JF kwamba amepitia Monduli kwa Lowassa pia nilikuwa wa kwanza kudai facts kama ninavyodai facts kuhusu huu upuuuzi wa Sophia, na ahsante kwa kunikumbusha kwamba Sophia ameongea to the public, ninavyofahamu ni kwamba aliongea kwenye kamati tu, ambako hakuna waandishi wa habari wala vyombo vya habari, lakini nimekusikia sana mkuu na samahani sana mimi nilidhani kua hizi ishus zinafanana za kupakana matope,

- Again samahani sana na sitarudia tena mkuu, isipokuwa tu simtetei kiongozi yoyote, mimi huwa ninasimamia principle na sio watu fulani ukiwekwa ukweli sawa, lakini huu upuuuzi wa mitaani hapana bado hili taifa tupo wenye kusikia aibu, na kutumia commonsense as opposed na hawa kina Sophia,

- Again, Mkuu Mtanzania samahani sana kwa kukukwaza, my bad na it won't happen again, promise!


Field Marshall Es!
 
Mh! Jamani, lisemwalo lipo?

Sidhani kama huyu mama, pamoja na "uendawazimu" wake, atakurupuka tu na kutunga jambo kama hili. Lazima kwa wadhifa wake amezifuma hizi ishu mahali, na inawezekana hao anaopambana nao walikorofishana nae ndo akaamua kufumua mambo.

Sasa ndio naanza kujiuliza kwanini Mengi na Malecela waanze kumtangaza kuwa ni kichaa apimwe akili?....forgive me if this sounds like a conspiracy theory, but what if there's a plan to finish off this "Lioness"? Tusishangae tukasikia hali yake ya afya si shwari
 
I hate this tabia ya watanzania " aje ofisini kwangu ajitambulishe" hii statemet ni ya kimwinyi sana, kwani wanachama wengine wote anawajua, crazy!
 
SAY IT AGAIN: "Dr. Slaa for President 2010"

Sikonge,Ili tusonge mbele tunahitaji kuifanyia kazi hii signature yako,Period! Mengine yatafuatia baadae!
 
Haya jamani kwa sasa tumalize hii mipasho iliyoanzishwa na simba jike na tupange mikakati ya kuikomboa nchi hii.

Kwangiu mimi naona wote wanaorumbana ni vichaa tu, wanazidiana kidogo ukiangalia kwa jinsi wanavyotia watanzania umaskini, kwa kweli ukiwa na akili timamu sio lahisi kufanya haya wayafanyayo.

Simba ametusaidia kuvumbua watu akili kuwa kumbe sisiemu kuna viongozi vichaa ndiyo maana ya umaskini uliokithiri kwa watanzania hauishi na ni jukumu letu kuchagua viongozi wenye akil timamu na si hawa vichaa.

nawaombeni jamani tufunge hii mipasho kwa sasa
 
Mambo mazito haya.

Shalom, mbona kimya? Wamekukatia umeme na heater hazifanyi kazi (Baridi).

Njoo Sikonge tupate Maembe kwa wingi sana sasa hivi.

Ukitutafutia wawekezaji wawe wanatengeneza juice au kusindika itakuwa poa sana mwanangu (This is not a JOKE). Maembe ni mengi sana na mengi yanaharibika tu.

Naona mjadala unaishiaishia. Ila dalili za uchaguzi zinaanza kuonekana.

Mhhh, mwakani Tanzania inawaka moto. Siasa za kuchafuana mwakani zitakuwa zinatisha. Maadamu wote wameshajua jinsi mechi inavyochezwa, kazi ipo.

Mungu Ibariki Tanzania,
 
FMash
mmi simtetei S.Simba kwa manenu aliyoongea kutokana na yeye ni waziri. Nasimtetei mwana ccm yoyote kwa sasa, me nipo kando na ctaki hata kumtetea mmoja wao, kwani megundua wote ni wachafu, tofauti na wewe unae watetea kina Malecela waziwazi. Nakumbuka ,maneno ya mwalim sanaaa kwa sasa alivyokua akimuita JOHN.

- Tatizo lako sio anything, isipokuwa ni mimi, na mimi nimekuhakikishia mara nyingi sana kwamba huna ubavu wa kusimama na mimi either hapa JF, aua hata in the real life, JF ninakuja kukata ishus sijali upande wa pili upo wewe au anybody, ninachojali facts sasa wewe ukileta za kuleta mimi sina peremende ninakurudishia zile zile za kuleta, uchafu wa CCM au usafi wao mimi haunihusu, kwa sababu ninaamini kuwa kama CCM wote ni wachafu, basi wananchi wote wa Tanzania tuliowachagua kutawala for he last 47 years tunakuwa kama wao CCM, yaani wachafu 100%.

- Ya kumtetea Malecela hayo ni yako, mimi ninatetea principle which Malecela happened to be involved, meaning kwamba hata wewe ungekua involved ningefanya the same, lakini hii ni demokrasia una haki ya kufikiri anyways you want kuhusu ninachokifanya hapa, who cares anyways!

- Mwalimu alimuita Malecela muhuni, kwa tabia zetu za Kitanzania ikiwa na maana ana wanawake wengi, kitu ambacho na Mwalimu alikuwa nacho yaani wanawake wengi, unless una maana Mwalimu alikuwa na maana nyingine labda uiweke hapa, otherwise unahangaika bure ndugu yangu, ufisadi unakuwa established na facts sio midundiko na uchangudoa,

- Jeetu kama nilivyoambiwa na wahusika, hajawahi kuifadhili harusi wala kampeni ya urais wa Malecela, isipokuwa anaweza kuwa aliachangia kama wananchi wengine walivyomchangia, na kama alichanga hazikuwa hela za kutisha maana wangejua especially kampeni za urais ambapo ni shabibu na Abson ndio hasa waliotoa contribution kubwa sana kwenye kampeni yake, sasa unless Jeetu amewahi kuwa a proven fisadi before harusi na kampeni za urais 2005, kama Malecela na mkewe walipokea hela zake hata kama ni senti tano knowingly kuwa ni za kifisadi, then wanahitaji kutangulia Segerea now! na nitakuwa the first kudai hilo!

Otherwise, ninakubali kuwa Sophia anakuwa kichaaa na anahitaji kwenda Mirembe kutibiwa. Na wewe huwezi kunifanya anything hiyo nafasi nimekupa mara nyingi na bado siku zote nimeiacha wazi kama una ubavu anytime tukikutana bring it on sitishiki na hizo chuki zako wivu, ukileta matusi hapa nitakujibu 24/7 na wala sikuogopi pamoja na michezo yako mingi unayoifanya humu JF inayotakiwa kufanywa na watoto wadogo kuliko mtu mwenye PhD ya online na mtumzima mwenye mke na watoto, lakini ndio demokrasia na akili ni nywele, na mimi nitaendelea hapa JF na kusimamia principle bila kujali inamhusu nani.


FMEs!
 
Mambo mazito haya.

Shalom, mbona kimya? Wamekukatia umeme na heater hazifanyi kazi (Baridi).

Njoo Sikonge tupate Maembe kwa wingi sana sasa hivi.

Ukitutafutia wawekezaji wawe wanatengeneza juice au kusindika itakuwa poa sana mwanangu (This is not a JOKE). Maembe ni mengi sana na mengi yanaharibika tu.

Naona mjadala unaishiaishia. Ila dalili za uchaguzi zinaanza kuonekana.

Mhhh, mwakani Tanzania inawaka moto. Siasa za kuchafuana mwakani zitakuwa zinatisha. Maadamu wote wameshajua jinsi mechi inavyochezwa, kazi ipo.

Mungu Ibariki Tanzania,

Ha ha ha ha ha ha!

Usiongee na mimi mpaka ukapime mirembe. Sikonge=Simba
 
Halafu mnasema huyu mama kichaa!Huyu mama siyo kichaa huyu isipokuwa ameamua kumwaga ugali baada ya hao wanaojiita wapiganaji kumwaga mboga ili wakose wote.
Mkuu Wazalendo shukran mkuu.Kama una mengi zaidi ya hiki kikao tumwagie mkuu na sisi tufaidike
 
Kaaazi kweli kweli! Tanzania bila mafisadi, inawezekana!
 
Mkuu umefika mbali sana na hizi comments na sijajua ni kitu gani kime prompt hizo personality attacks.Bangi ? Msanii ? anyway. Mie huwa nashauri watu ku dwell kwenye hoja na mimi mara zote nikiwa sina cha kujibu huwa naacha kuandika kuliko kumvamia mtu kwa matusi . I am not happy na hizi comments

Umeonyesha ukomavu wa hali ya juu sana mkuu! Siku zote huwa najiuliza huyu ni Engineer wa matusi! Manake kwenye thread ya Uchaguzi serikali za Mitaa alichemka pia,Nashindwa kuamini kama huyu ni Baba/Mama wa familia.
 
Huyu mama asipuuzwe kwa 100%, haiwezekani kwamba eti yote aliyosema hakuna chembe ya ukweli kwa jambo hata moja! Anne Kilango mbona hajasema kwamba aliyosema Sofia Simba ni uwongo ila alisema ETI kwa nini hakuyasema muda huo wote! Kwa upande wa John Samwel Malecela naye hajakanusha zaidi ya kudai ETI Sofia Simba akapimwe akili! Remember you can extract sense out of nonsense!
 
Wakati malumbano mbalimbali yanaendelea kuhusu hoja alizotoa Mh Sophia Simba bado kuna mengi aliyoyasema ambayo bado hayako katika public forum.
Hizi ni habari za ndani zilizotujia.
Mh Sophia aliwaambia wabunge wa kamati maalumu inayoongozwa na Mzee Ruksa kuwa hii nchi inayumbishwa na watu wanne ambao ni Speaker Sitta, Bernard Membe ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje ya Nchi, Rostam Aziz na Edward Lowassa. Alisema ni muhimu baada ya bunge kumalizika kamati ikawaita na kuwahoji na kuuliza wanaipeleka wapi nchi yetu.
Waziri Sophia alisema kwa namna zote watu hawa ni wahusika wakuu wa mambo yanavyokwenda sasa hivi kwa hiyo kamati hiyo inayoheshimika iwaite watoe ufafanuzi na waseme wanataka kuifikisha nchi wapi.
Sophia alisema kundi la kina Spika lenye wabunge wanaojinadi kuwa vinara wa kupinga ufisadi wakiongozwa na mpendwa wao mfanyabiashara Reginald Mengi wenyewe sio wasafi hata kidogo.
"Hakuna mtu msafi pale, sema tu serikali ina namna ya kushughulikia mambo yake," alisema.
Alitoa mfano wa mama Anna Kilango kuwa alishakutwa na madawa za kulevya nyumbani kwake kabla ya kuolewa na Mh Malecela. Pia, Jeetu Patel ambaye anasemekana kuwa ni fisadi papa, aliwachangia harusi yao fedha nyingi sana, zaidi ya sh millioni mia mbili hivyo haelewi nani ni fisadi kweli - aliyetoa au aliyepokea.
Alisema Malecela alishajipanga kuwa rais wa Tanzania na mkewe first lady, na kwa kuwa hayo hayakutokea, kelele za mama Kilango sasa hivi ni hasira hizo.
"Ninawaeleza ninyi haya yote ili mnapofuatilia haya mambo ni vizuri mkajua chimbuko lake ili kuweza kuyapatia utatuzi," Sophia aliiambia kamati.
Alimgeukia pia kinara wa wapambanaji Reginald Mengi kuwa magazeti yake yamekuwa yakiandika habari za kuichafua serikali na chama cha CCM.
Alihoji hela mfanyabiashara huyo anazotumia kuzunguka nazo nchi nzima eti vikoba zinatoka wapi? "Wanafikiri zinatoka mfukoni kwa Mengi, lahasha, pesa hizo zinatoka kwa mabalozi hivyo wajue wanashirikiana kuihujumu nchi."
Aliongeza: "Tunafahamu mambo mengi kukaa kimya hakumaanishi hatujui kitu tuna vyombo vya dola vipo makini vina taarifa zote lakini kama serikali, tuna namna ya kushughulikia mambo kwani hii nchi inaongozwa na utawala wa sheria hivyo lazma sheria ifuate mkondo wake."
Sophia alisema ukimfuatilia sana Mengi na utajiri wake utaona kuwa chimbuko lake ni hao hao wahindi anaowatuhumu kila kukicha huku akifikiri hatumjui kuwa yeye sio Mr. Clean hata kidogo.
Aliwaonya wabunge hao wajitenge na Mengi kwani anawapotosha kwa kiasi kikubwa.
Alisema ujinga wa Mengi unaonekana pale anapojitahidi kila kukicha kujifananisha na rais. Anachofanya rais, na yeye eti anafanya. Rais Mengi huyo ameteuliwa na nani? Sophia aliuliza.

- Ndugu yangu mbona unahangika sana, unahngaikia nini hasa? kinachikuwsha ni nini hasa mkuu haya maneno unatunga tunga ili yakusaidie nini?

1. Sophia amemsifia Lowassa kuwa ni Mwanaume wa shoka na kwamba hajawahi kuona kiongozi safi na mchapakazi kama yeye, amesifia Rostam, Karamagi, na Makamba kwamba ni viongozi imara sana an wasafi na hasa Makamba kwamba anakiweka chama pazuri sana.

- Hayo ya viongozi wanne umeyatunga na kuyabandika tu hapo uonekane uko objective kumbe ni ayako ni ile ile tu kumchafua Malecela na mkewe, unachohangikia nini hasa mkuu?

2. Mama Kilango alikutwa na madawa ya kulevya na nani? kampeni zote za uchaguzi wapinzani wake wameshindwa kuyasema hayo, kwenye kampeni za urais Sophia alikuwa upande wa Mtandao kwa nini hakusema haya? Waziri wa Takukuru anashindwa nini kutoa ushahidi wa madai yake na kummaliza adui yake mkubwa Mama Kilango?

Unahangaika bure ndugu yangu, hutafanikiwa mafisadi Tanzania tunawafahamu na wanafahamika sana, hizi dataz ni zako sio za kutoka huko kwenye kamati na unapoteza muda wako bure tu even though ninajua kuwa una muda mwingi sana wa mchezo, lakini unahangaika bure! Kama Mama Kilango is too good kuuza madawa ya kulevya ni upuuuzi usio na mfano! kama wazazi wenu ni mafisadi na mmeshiriki kula hela zao za kifisadi poleni sana lakini sio wote ni lazima ni mafisadi, unahangaika bure tu mkuu!

- Hizi dataz ni zako wewe tu mkuu wala hazina anything to do na huko Dodoma! Unatengeneza kichwa cha habari cha kujaribu kuwamanilulate watu hapa JF waamini uko serious unajipa thakns mwenyewe, unahangikia nini rudi kule kwenye ile thread tumalizie ngoma uliyoianza mwenyewe! acha huu utoto JF is bigger than this foolishness!

FMEs!
 
Back
Top Bottom