Mkuu FMES,
Sijui una maana gani hapo juu? Shauri ya box kunibana, sijafuatilia huu mjadala zaidi ya mchango niliotoa siku ile thread hii ilipoanza.
Kuendelee kuandika majina ya watu wengine ambao hawahusiki na mjadala huu sidhani kama inasaidia kwenye utetezi wako.
Kuna tofauti kubwa kati ya kinachojadiliwa kwenye thread hii na hayo uliyoyaandika ya Mwakalinga. Waziri Sophia ametamka wazi mbele ya vyombo vya habari na mbele ya viongozi wa chama chake, hivyo kama madai yake ni ya uwongo kuna njia nyingi ambazo wahusika wanaweza kuzifuata kuhakikisha majina yao hayachafuliwi.
Hilo la Mwakalinga, linasemwa na wasanii, ambao wanajificha kwenye migomba kabla ya kutamka neno. Kama wanaamini hivyo waseme wazi kama alivyosema Simba naamini huyo Mwakalinga kesho yake atakuwa anapambana nao mahakamani.
Ni muhimu kuweka wazi kwamba ukiachia madai wanayotoa kupitia JF, hakuna kiongozi hata mmoja anayeweza kusimama kwenye vyombo vya habari akasema Mwakalinga kapewa milioni 400 na Lowassa maana hata hao wanaopenyeza hayo maneno wanajua hayana chembe hata ya ukweli na hawako tayari kuona wanaburuzwa mahakamani.
Mwisho, Mwakalinga hana nia wala sababu ya kufadhiliwa na mtu yeyote. Kama ni ubunge basi atajifadhili mwenyewe.
Nafikiri kwenye maandishi yako hapo juu humtendei haki Mwakalinga kwa kuweka statement kama hiyo ambayo inaweza kuwafanya watu ambao hawajafuatilia jambo kama hilo waamini kuna madai kama hayo yametolewa kiwaziwazi.