Kwenye series ya LOST kuna mambo ya ajabu sana ndani ya kile kisiwa nikikumbuka nabaki kushangaa tu:
1. Kwanza kisiwa hakipo kwenye ramani. Yani unajikuta tu umetokea.
2. Ukiingia hamna kutoka. Japo watu baadae waliweza kutoka baadae.
3. Hauwezi kuumwa ukiwa ndani ya kisiwa.
4. Wanawake wote wanaopata mimba ndani ya kisiwa wanakufa.
5. Sheria za physics hazifanyi kazi kabisa mule ndani.. kwa mfano unaweza ukarusha jiwe juu likachelewa au likawahi kufika.
6. Kuna jamaa kazaliwa miaka ya 1800 lakini hazeeki.
7. Kuna huyo mtu ambae haonekani.
8. Kama ulikuwa unaumwa ugonjwa wowote ukiingia ndani ya hicho kisiwa tayari ushapona!
Hatari sana.. ongezea jambo lililokustahajabisha kwenye hii series kama umewahi kuicheki.