Series (Special thread)

Shemeji mtu mbona ameshakata moto Ile Siku BIANCA alipovamia dojo la muhuni
shemeji yake Jackal alikuwepo sema alikuwa mitungi akapigwa chuma na yule mwenzie Bianca😁
 
Wale wazee garini alikuwa amewasamehe bibi akajichanganya kumkita bisu la begani. Ukawa mwisho wao. Jackal hana huruma
 
Mbona kama bianca anamimba ?
Hii nadhani picha ya muda kidogo kabla au baada ya kuigiza. Maana mnaweza kumaliza kuigiza halafu mkaacha episodes zenu kwa wataalamu wa sauti, video n.k na mkasubiri kwa hadi mwaka ngoma ikipikwa studio
 
Maamuzi ya mtoto mkali Bianca kuingia katika nyumba ya Jackal akiwa hana backup ya kutosha ni maamuzi yaliyogharimu maisha yake na partner wake. Hata partner wake alionya kuhusu hatari ya maamuzi yale.

Unaingia kichwakichwa kwenye nyumba ya assassin mwenye uwezo kumnyutrolaizi mtu aliye umbali wa zaidi ya kilometa 3!?
 
Kitendo cha Bianca kumwita Jackal jina lake halisi (Duggan) ni kosa ambalo haliwezi kumuacha hai mbele ya selfish na emotionless guy like Jackal.

Nakubaliana na wewe kuwa maamuzi ya Bianca kuingia nyumbani kwa Jackal ni ya kipuuzi sana, achilia mbali wazo la kutaka kumtia nguvuni Jackal bila kumuua.
 
Shemeji mtu mbona ameshakata moto Ile Siku BIANCA alipovamia dojo la muhuni
shemeji yake Jackal alikuwepo sema alikuwa mitungi akapigwa chuma na yule mwenzie Bianca😁
🀣🀣🀣
Hii scene nimejikuta nimeisahau kabisa, nadhani ni masikitiko ya kumpoteza mtoto wa nguvu Bianca yamefanya nisahau kuhusu kifo cha shemeji.
 
Wale wazee garini alikuwa amewasamehe bibi akajichanganya kumkita bisu la begani. Ukawa mwisho wao. Jackal hana huruma
Daaah, ile scene ilinisikitisha sana mkongwe. Yule bibi hata sijui alikuwa anawaza nini?

Me nadhani baada ya mission yake ya mwisho mchizi moyoni mwake alishajiwekea nadhiri ya kuacha kuua, yule bibi amekuja kuharibu kila kitu, ndio maana baada ya kuwaua mchizi aliumia sana.

Season ya pili itatuletea Jackal katili zaidi, maana ukiongezea mama Carlito kumkimbia na yule mshua kumdhulumu malipo yake, Jackal wa season 2 atakuwa na kisirani hatari.
 
Yah hii inawezekana na hata jamaa atakuwa anajua πŸ€”
Mzee, Bianca anaponaje?
Hivi tumeona vizuri kweli eneo alilopigwa shaba Bianca!?
Bianca amepigwa shaba kwenye koo la hewa, shaba imetokea upande wa pili wa shingo, anaponaje!?

Na hata maongezi ya Osi na yule bi mkubwa msaliti mwishoni mwa episode ya 10 yanaonesha kuwa Vince na Bianca wamedanja.
 
Bianca alishakufa mana ule msemo wa tumuache aende Spain then sisi tutajua namna ya kudeal nae walijua tu tutamfahamisha mwamba na hatoweza kuwaacha salama this time.
Hapana, yule mshua ana tabia ya kumchukulia poa Jackal tangu series inaanza, yeye binafsi aliamini kuwa Bianca akipewa taarifa za mahali alipo Jackal basi anaweza kufanikisha kumuua Jackal. Lengo lake lilikuwa baada ya Bianca kumuua Jackal basi Bianca nae apotezwe hukohuko Spain.

Pia Zingatia, Bianca alipewa order ya kumuua Jackal, sio kumtia nguvuni, idea ya kumtia nguvuni Jackal ndiyo iliyomuua Bianca na ndio iliyofelisha mkakati wa yule mshua.
 
Kwenye muvies huwa wanapona 😁😁
 
Namuonea huruma huyo mzee. Anamwita Jackal eti ni loose end!! Yani jackal awe lose end kweli?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…