Serengeti fiesta 2014 special thread

Serengeti fiesta 2014 special thread

Im not platnumz' fan.
Lakini what happens now, isnt a new thing from watz.
We are like that.
Ukifanikiwa, watakuchukia tu.
Watajidai kuna sababu, lakini hakuna.
Hii ni sababu ya kwa nn wasanii wetu wanang'aa mmoja mmoja at a time.
We so blinded by jealousy that we cant see that we are killing everything we had!

Hapa akija mwingine lazma tumfanyie hayahaya mambo mpaka ashuke itakuwa furaha yetu
 
Jamaaan naombeni muiendeleze thread yenu hadi mwakani muda kama huu bila kuchoka hata pia team domo msikate tamaa hata mwakani mtanfunika tu Ally kiba 4real

Team Kiba 4real hapa
 
Yale yale ya Mwana FA na Lady jay dee.Bongo raha sana,ushabiku huu naufananisha ule wa siasa mkoa wa Mara,Vijana wakiamka tu kua tunataka Sisiemu utapenda siku wakiamkia Chadema mbona utashangaa mwenyewe.Mi Napenda muziki wowote wa msanii yeyote yule ulio vizuri,habari ya maisha ya mtu its out of my bussiness.Nawengi tunashabikia muziki kama mpira na vyama vya siasa vile.
Nakumbuka enzi za Mr Nice baada ya kushuka kimuziki hao hao mashabiki wa muziki wake ndo wakawa wakaanga sumu.
Hayati Kanumba nae wakamponda et hajui lugha ya malkia duh.
Hii ndo Tanzania ktk burudan..kuna watu hawalali wala hawali kisa anamfuatilia msanii fulani.
Principle ya Watanzania ni kwamba ukipanda juu lazma wakushushe
 
Wadau Diamond alisema kauli hiyo baada ya kuona Kiba alipewa promo ya muda mrefu kabla hajapanda stage, akapafom akapata nafasasi ya kupumzika na kuchange nguo. Akala promo nyingine tena 'THE RETURN OF THE KING'

AKAJIPANGA KWA MUDA MREFU , NDO AKAANZA PERFORM MWANA DAR.

SASA TUKIWEKA USHABIKI PEMBENI NI WAZI KABISA KIBA ALIKUA MORE RESPECTED THAN DIAMOND.

SASA WATU WALIO NDANI YA CLAUDS NDO WANAJUA NI WAPI DIAMOND AMEWAKOSEA CLOUDS.

KI UKWELI KABISA KWA HADHI YA DIAMOND YA SASA NA ALIVYOKUA TREATED. ITS NOT FAIR.
 
asante kiba umenitoa kimasomaso roho iliniuma sana dimond alivyokutusi eti yupo tayari kukusaidia nafikiri amejionea kua wewe inatakiwa umsaidie maana tayari kwisha habari yake

Yaani kiba amsaidie Dimond hahah....wakati hata hili shangwe analolipata ni kwaajili ana bifu na Diamond huyo alikiba wenu angekuwa na Bifu na Barnaba au Bob juniour angesahau hata kupata shoo
 
jamani mwacheni Daimond afanye yake na kiba afanye yake.mbona mnataka mmoja wapo ashuke.mie am happy kuona Daimond na kiba wote wapo juu.ntasikitika mmoja wapo akishuka.

Dimond ndo yupo juu...kiba labda tujifanye vipofu na viziwi ndo tutasema yupo level moja na Dimond
 
Angevaa mbowe anekiona cha mtema kuni wangemtafuta na vifaru
 
umeona afu watu wenyewe wabongooo
watoto waumavi maviniii
wanakushusha na kukupandisha on the spot
diamond aache dharau na mbwembwe zake

Amemdharau nani mbona tunamtaftia sababu tu Dimond kama tunamvhukia tukiri tunamchukia tu
 
Diamond ni msanii mwenye kipaji thabiti anastahili Sifa kwa hilo .

Tatizo lake amejisahau kuwa umaarufu alionao ndani na nje ya nchi unatokana na watanzania tena wengne wa kipato cha chini.

Style yake ya maisha imebadilika sana tangu amepata umaarufu

Anasa za wanawake anaowabadilisha kila siku na kujiita majina (km sukari ya warembo). Juzi tu amehonga gari ya kifahari kwa kimada wake.

Amefikia hata kuwadharau wale aliowakuta ktk mziki wengine walisaidia kumtoa, Bob Juniour, Ally Kiba. Kwa ufupi ni aina ya watu wasio na shukrani.

Tangu ameupata umaarufu na fedha akasahau kuwa pesa hiyo nying imetoka kwa watanzania wa maisha ya kawaida, Maneno ya kejeli yanaanza mara "sifanyi shoo ya Mil 2"
Mara kupanda ma private jet, kujipa vyeo ving, kuendekeza bifu nk.

HE HAS OUTSTANDING TALENT YES, BUY HE HAS 2B A BIT HUMBLE.

Kwanza anaonekana anadharau watanzania wote maskini.

Wacha wamzomee

Mafanikio yake lazima yamsogeze mbali na wale wa kipato cha chini kwa sababu hana tena kipato cha chini. Huwezi ukafanikiwa halafu just because kuna watu wapo chini ukayakataa mafanikio yako. Besides kuwa msanii ni package kubwa. Inabidi uwe kweli msanii. Sio kipaji, but everything bout you has to become your business. Sababu ya wengi hapo mwanzo kutokufanikiwa ni woga wa kubadilika. Wewe ni international musician, so itabidi uwe tu international. Hamna haja ya kuwataja ambao walifikiri kuwa chini ndo utapendwa na watu. Ona sasa wanaitwa wamefulia na wengi wamesahaulika. Watu hawataridhika kamwe. Kama umeamua kuwa mwanamziki kwa ajili ya kitaa chako sawa. Kama you are doing it to get yourself internationally, you gotta do what it takes.
 
Heri mpambano ungeisha Sare kama Yanga na Simba maana hii thread ilianza na mbwembwe nyingi.Naona mwisho watu wamekubali kilichotokea,Vipi TI kaomba kolabo kwa Diamond?

Subiria suprise
 
Jide alisema Clouds ni washen.zi lakini wao ndo walikuwa wanawakingia kifua.....vipi kibao kimawageukia??
 
Amemdharau nani mbona tunamtaftia sababu tu Dimond kama tunamvhukia tukiri tunamchukia tu

Wabongo ndio zetu kuwa- discourage wanaofanya vizuri , But the fact remain Diamond keshakuwa wa Kimataifa ! hizo kelele hazisaidii lol Nampenda Ali Kiba pia namshauri asipate Bichwa kisa kelele za wahuni Fiesta !
 
Back
Top Bottom