Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Mbinu yao ya kuruka ni kweli kama walivyoeleza lakini sijui kwanini nimejikuta nacheka tu ,kila mtu sasa anatoa hiyo mbinu na wakati jamaa ashadondoka.

Njia nzuri ni kusubiri tu gari isimame,mambo ya kuruka haya watu watakuja kutegua nyoga.

Ila yote kwa yote jamaa aliyetoa ule uzi ni bonge la comedian aloo
Wakati mwingine inatokea tu pale ambapo unataka ushushwe sehemu ambayo gari haitakiwi kushusha abiria. Mimi kuna siku niliwahi waomba Rungwe wanishushe Eso badala ya kwenda hadi Stendi Kuu wakaniambia pale hawaruhusiwi kushusha labda nikae mlangoni then watapunguza tu speed kidogo ili nishuke.

Na kweli walivyofika wakapunguza speed huyo nikaruka zangu wakatambaa uzuri sikuwa na mizigo nilikuwa na begi moja tu la mgongoni ndiyo maana hata nao walikubali vinginevyo ukiwa na mizigo hawakubali kukushusha sehemu kama hiyo maana hekaheka za kushusha mizigo yako inabidi gari isimame kabisa.

Sasa kwenye hizi daladala za mjini ndiyo kabisa imekuwa kama mazoea abiria kuomba kushushwa sehemu zisizoruhusiwa tena unaweza kuta ndiyo wengi kuliko hata wanaoshukia kwenye vituo rasmi. Watu tumeruka hadi kwenye treni ile ya mjini Gerezani-Pugu ambayo kuteleza na kukanyagwa mguu ni dakika sifuri sembuse magari.
 
Haha mimi nilicheka pale watu walivyokuwa wanamshauri akiruka anatakiwa atangulize mguu wa kushoto then afanye kama anakimbia hivi ndiyo hataanguka. Basi wengine wakawa wanasema hizo ni theory tu jaribu uone.

Ila comment iliyonichekesha kuliko zote jamaa mmoja alikuja akasema "ukikosea kuruka ni either ulambe lami au utembee speed ya subaru". Aiseee nilicheka hapo kwenye speed ya subaru maana hiko kitu kiliwahi nitokea.
 
Back
Top Bottom